Siri usiyoijua kuhusu ndoto na tafsiri zake

Siri usiyoijua kuhusu ndoto na tafsiri zake

Msaada mara nyingi sana naota nakemea pepo,wachawi,..Yani nasali na kukemea ndotoni ..hii inamaana gani?
Inamaanisha uko thabiti kiroho na moyoni mwako unamcha Mungu kuliko unavyojionesha kwa nje na katu usiwaambie watu wabaya juu ya ndoto kama hizi maana watataka kukudhuru, ushauri kama mazingira unayoishi siyo mazuri(yana inshu za kishirikina) vumilia tu maana huwezi dhurika au unaweza hama kuepuka kero nakwenda pengine.
 
Ni takribani mwezi sasa naota tu mambo ya kufanya mitihani shuleni ama chuo ilhalia nishamalizaga mambo ya elimu.

Mara ya kwanza kwanza nliona kawaida ila daah imekua too much karibu kila siku naota eidha najiandaa na pepa( hapa nakua na hofu kichizi lakin nkishaingia kwenye pepa narelax), nafanya pepa ( nikiota hivi huwa nakua nimeconcetrate kwenye pepa na mara nyingi nakua sina hofu) , au nshamaliza pepa ( hapa napo huwa panantesa kwasababu huwa naanza kukumbuka nilichoandika ambacho sijaandika yani sijakiota ila pia sijui kumbukumbu inatokaga wapi ila nakua sawa kua nlichoandika kina usahihi kwa kiasi chake na marafiki wengine wameenda opp na hapa nakua washkaji tunajadili tulichoandika.
Je, una jambo lolote ambalo limekufanya ukwame kimaisha au uhisi kaugumu fulani kutimiza ama kulitekeleza?
Je, huna kazi, umetingwa na pressure za majukumu au mafanikio ya kazini, unaandamwa na changamoto ngumu kuzitatua au unahisi siku hizi umekaa idle sana?
Chanzo cha ndoto zako kipo ndani ya hayo maswali endapo ukijitathimini vyema kuhusu hali yako kwa sasa ilivyo. Suluhisho lake ni subra na uvumilivu kama kipindi hiko ulivyoweza kuhimili mikikimikiki ya shule na majaribu yake hasa pressure ya mitihani na adhabu, kwan soon yatapita na hali ikishaimarika utashangaa utokaa uote tena ndoto za namna hiyo.
 
Nimeota Mdogo wangu alikua na matatizo kaandamwa na mikoani tukashauli aombewe badala yake yule Mchungaji akaanza kuniambea mimi nikakubali anscombe katikati ya maoni nikaanza kuwapiga mchungaji na wasaidizi wake nikawa kama mwehu hadi wakakosa nguvu
Dadayangu akaja ailipoona lile tukio akaomba waache kuniombea sababu niliwadharirisha wachungaji akaogopa wasije kunidhuru baada ya muda mfupi nikawa nimelala sifanyi chochote dadayangu akaanza kulia akahisi nimekufa

Ndoto yako inakulenga wewe kama kikwazo au chanzo cha matatizo yako mwenyewe hivyo angalia unapokosea narekebisha fikra juu ya mambo yanayokukwamisha kupiga hatua.
 
Nikumbukumbu tu za kawaida haina maana yeyote zaidi ya ubongo kurelax unless ikijirudia rudia
Mkuuu nimeota leo nipo shuleni kwetu niliposoma O level mara muda wa kunywa chai saa 4 nitoka na sahani kubwa imejaa mihogo ya kuchemsha ssa ni mingi sana nikakutana na wadada 2 nikawaambia njooo tule mihogo wakanibeza hatuli mikavu mie nikaanza kula mikavu nilikuwa na tu maji kidgo sana nikala mihogo kma kipande kdgo na maji yakaish du nikakutana na rafiki yangu simtaji jina
Nikamuambia mihogo mingi akasema njooo hapa wadau wengi nikaweka chini du hapo ndio nikastuka
JE MAAANA YAKE NINI?
 
Mkuu mtarimbo umekula kona ya wapi tena?Tafsiri yako inaeleweka vizuri sana sio ya kubabaisha haina makando makando.

Majibu yako yanarandana na uhalisia kabisa na unajibu vizuri mnoo..yaani unajikuta majibu unayatafuta Mwenyewe sababu unafundisha namna ya kutafsiri rudi tafadhali sisi wanafunzi wako tuko hapa tunakusubiri kwa hamu kubwa naona umetutelekeza.

Kama kuna watu wanakukosoa na kukukasirisha embu wapuuze tafadhali,wana wivu wa kike tu unawasumbua kama wangekuwa wanajua si tungeona hapa wakileta tafsiri nzuri zaidi zinazoeleweka kuliko wewe??

Njoo tafadhali Mkuu Mtarimbo.
 
Ndoto za maji huwa asilimia kubwa huwa ni za mafanikio,maji code yake ni mafanikio au maarifa au cheo au ukuu inaonesha utapitia kipindi cha mafanikio kwenye mambo yako ,na unatakiwa uwakumbuke ndugu zako pindi ukifanikiwa ,la sivyo ukienda kibinafsi hutafika mbali
Ndoto za maji zinajirudia sana kwangu, nimeota nimesimama Nataka kuvuka mto ghafla nikaanza kuona maji yanaongezeka yanajaa.
 
Ndoto za maji zinajirudia sana kwangu, nimeota nimesimama Nataka kuvuka mto ghafla nikaanza kuona maji yanaongezeka yanajaa.
Unaonywa usivuke mto kwa daraja au kuruka (wana wa israel waliyafes maji kwa uwezo wa Mungu)maana neema yako ya mafanikio umefunguka pita kwenye kile unachohofia sijui wewe una plan gan ila unaloliogopa kufanya ndio mafanikio yako yalipo.Mwisho unahitaji msaada wa Mungu sana omba sana
 
Mkuu nami nisaidie kutafsiri ndoto hizi:
1. Juzi kati niliota nimekutana na watu zaidi ya watatu niliosoma nao miaka 15 iliyopita, sura na majina yao havijapotea bado. Tukafurahi na kupiga picha ya pamoja.

2. Rafiki yangu alimpoteza mama yake mwaka jana mwishoni, baada ya miezi 2 kaota ndoto mama yake (marehemu) amepita akiwa ndani ya bus, rafiki yangu kaanza kumuita mama yake amsubiri waondoke nae, mama yake kamkatalia, bus likaondoka.

Asubuhi na mapema kanisimulia, na asubuhi ile alikuwa anasafiri hivyo kapanda gari mwendo wa kama km 1 gari likataka kupata ajali, Mungu ni mkubwa likajikita mahali, wote wakapona[emoji1431]

Je, ndoto hii iliashiria nini??
mtarimbo
 
[mention]mtarimbo [/mention] nina ndugu yangu (baba mkubwa) aliyenilea toka utotoni mpaka ukubwani lakini alifariki toka 2013.

1.Cha ajabu ni miaka imepita sasa lakini mara nyingi nimekuwa nikimuota kwenye ndoto zangu hata usiku wa kuamkia leo nimemuota na mara nyingi naota nipo kwenye nyumba yake ambayo tumekuwa tukiishi na familia yake japo kwa sasa nimeshahama nipo kwangu.

2. kuna kipindi nafikiri mwaka umepita sasa niliota kwamba amerudi licha ya kwamba kwenye hiyo hiyo ndoto ilikuwa inaonesha tulimzika hiyo 2013.

Naomba tafsiri mkuu.
 
Mkuu nami nisaidie kutafsiri ndoto hizi:
1. Juzi kati niliota nimekutana na watu zaidi ya watatu niliosoma nao miaka 15 iliyopita, sura na majina yao havijapotea bado. Tukafurahi na kupiga picha ya pamoja.

2. Rafiki yangu alimpoteza mama yake mwaka jana mwishoni, baada ya miezi 2 kaota ndoto mama yake (marehemu) amepita akiwa ndani ya bus, rafiki yangu kaanza kumuita mama yake amsubiri waondoke nae, mama yake kamkatalia, bus likaondoka.

Asubuhi na mapema kanisimulia, na asubuhi ile alikuwa anasafiri hivyo kapanda gari mwendo wa kama km 1 gari likataka kupata ajali, Mungu ni mkubwa likajikita mahali, wote wakapona[emoji1431]

Je, ndoto hii iliashiria nini??
mtarimbo
Mkuu ukiota huko na marafiki zako wa shule inaleta tafsiri ya kuna watu wako wa karibu ambao umewasahau inabid uanze kujenga nao mahusiano ya karibu maana wamebeba furaha yako ,huwez jua watakupa msaada gani kwenye matatizo yako
 
Kumuona mama ndotoni inamaana gani mkuu


Na kuonana na viongozi wa juu wa taifa inamaana gani mkuu
 
Mkuu ukiota huko na marafiki zako wa shule inaleta tafsiri ya kuna watu wako wa karibu ambao umewasahau inabid uanze kujenga nao mahusiano ya karibu maana wamebeba furaha yako ,huwez jua watakupa msaada gani kwenye matatizo yako

Asante sana, na hiyo ndoto ya 2?
 
AENDE MBELE ZA MUNGU KWANI MUNGU ANAKAA WAPI. TAFSIRI NDOTO SIO MNAVAMIA SIREDI HALAFU MNALETA INJILI HAPA. KWANI MAKANISA HAYAWATOSHI.
 
Kumuona mama ndotoni inamaana gani mkuu


Na kuonana na viongozi wa juu wa taifa inamaana gani mkuu
Kumuona mama ndotoni ina maana kila utakalopanga litanyooka. Kama ni marehemu kuna ujumbe mwema anakujulisha.
 
MSAADA PLEASE
Nilikuwa nasafiri kwenda mahali. Njiani nikamuota mtu ambae hatujawasiliana muda kidogo. Nimemuota mara mbili
Mara ya kwanza alikuwa anatembea usiku
Mara ya pili hivyo hivyo anatembea usiku nikawa namwambia usiende huko akawa hanisikii
JE HII NDOTO INA MAANA YOYOTE AU NI WENGE TU LA SAFARI?
Safari ni maisha kuna mtu anakuhusu anafanya au anaandamwa na Jambo lisilo jema unashauriwa kumwonya au kumshauri. Japo yaonekana ulishajaribu ukashindwa. Si lazima awe uliyemwona ndotoni ila mna ukaribu.
 
Asante mkuu na vipi kuona viongozi ndotoni mfano rais au pm
Kuona raisi maana yake kuna watu watakumbwa na dhoruba au madhara fulani kama hukumu ya mabaya waliyoyatenda. Wanakuhusu kwa namna moja au nyingine.
 
Kwanza nianze kwa kuelezea ndoto maana yake,

Ndoto ni mkusanyiko wa matukio ambayo binadamu huyaweka kichwani kwake ambayo humjia bila zuio (involuntary) kwenye ubongo wakati akiwa amelala,matukio haya huwa hayaeleweki na saa nyingine huwa kinadharia zaidi mfano kuota unapaa wakati kiualisia haiwezekani.

Kiujumla sayansi imeshindwa kuja na jibu kamili kuhusu ndoto ,na matokeo yake wameishia kutoa tafsiri hiyo .

Ukija kwenye dini ndoto huwa ndio njia maalumu ambayo ulimwengu wa Roho hutumia kuwasiliana na binadamu, hapa sasa ndio nataka tuanze.

Kibibilia Mungu hutumia matukio tuliyoyaifadhi au kumbukumbu za vitu tulivyoifadhi moyoni ,ili kutengeneza codes za mawasiliano kati yake yeye na sisi .

Sasa kuna mambo kadhaa ambayo huwa ukiota lazima ujue kufungua hizo codes ,ni maarifa rahisi ila inahitaji uwe mcha Mungu na mwerevu.

Mfano
1:Ukiota unapaa angani
Ndoto ya namna hii ukitaka kuifahamu lazima ujue kwa nini Mungu katumia anga,anga maana yake ni ulimwengu wa nuru ,ardhi ni ulimwengu wa giza ,hivyo ukiota unapaa ni taadhari kutoka kwa Mungu kwamba uache kutembea kwenye ulimwengu wa giza ,hamia ulimwengu wa nuru, nikuhakikishie ukifanya hivyo hutakaa uote tena kupaa sure.

2: Kuota unafanya mapenzi
Codes za ndoto hii ni mbili kulingana na mazingira yako,mfano ukiota unafanya mapenzi na ukiamka unajihisi mchovu na mara nyingine kama mwanaume unahisi umemaliza ,basis ujue kuna pepo wachafu wanakuchezea.

Ila ukiota unafanya mapenzi na ukiamka hakuna ishara yoyote nikimaanisha uchovu au uchafu basi ndoto hii huwa ni njema code ya mapenzi ni pesa maana ni kipi kinapendwa zaidi ya mapenzi kama si pesa hivyo ukiota unafanya mapenzi ni ishara ya kupata pesa, kama unayefanya naye humjui basi utapata pesa kwenye vyanzo usivyotarajia.

Kama umeota unafanya mapenzi na mtu unayemjua basi ujue utapata pesa zaidi kwenye vyanzo vyako vya kiuchumi unavyovijua.

3;Kuota uko darasani ,na kufanya mitihani
Hii ndoto code yake ni hivi jiulize ni nini hukupa wasiwasi kama kama kipindi uko shule hasa wakati wa mitihani kama kukosa pesa wakati wa matatizo, hivyo ndoto hii ukiota ni onyo kutoka ulimwengu wa roho kwamba kuna matatizo makubwa yatakujia na yanahitaji pesa hivyo unahitaji kuweka akiba ya pesa ,upunguze matumizi la sivyo hilo tatizo litakuaibisha.

4;Kuota kusalitiwa kimapenzi
Code yake ni hivi ni nini huumiza moyo na kuuvunja moyo kama usaliti wa kimapenzi? jibu ni msiba.

Hivyo kama umeota mwenzi wako anakusaliti na kiuhalisia si kweli basi ni ujumbe wa kifo kwa huyo uliyemuota either yeye, familia yake watakumbwa na tukio la msiba hivyo muombee huenda bado ulimwengu wa roho haujaidhinisha hilo janga.

Itaendelea kesho, pia ukumbuke somo la ndoto lilikuwapo tangu zamani Yusuph alisoma kupitia vitabu alivyoiba mama yake RHaheli wakati anatoka kwa baba yake aliyekua mganga na mtabiri alijulikana kama Laban, Danieli alisomea huko uajemi enzi za utumwa.

Na binadamu huota zaid ya ndoto 20 kwa siku ,ndoto yenye ujumbe huwa unaikumbuka vema na huwa inaushtua moyo.

Nyingine huwezi kuzikumbuka maana huwa kazi yake ni kuufanya ubongo ufanye kazi vizuri ,hivyo siyo ndoto zote ni ujumbe unatakiwa uwe mwerevu wa kusoma mazingira na hali yako.
Kuota moto unaunguza kanzu uliyoivaa kisha unaamua kuivua na unabaki na pensi maana yake nini? ......Na hali ya kuwa wala huwa siyo mpenzi wa kuvaa kanzu
 
Naota Mara nyingi Sana nipo juu ya jengo refu,mnara au mti..,wakati wa kushuka nashindwa ,nilitaka kudondoka tu nastuka.
 
Back
Top Bottom