Mkuu hapa ni jamii huru,sisi ni watu huru,unaweza kuweka hoja mezani tukaijadili ili tujifunze zaidi.Ndoa ni unnatural. Ipo against nature ya binadamu lakini acha nikae kimya na upendo feki wa wanandoa utamalaki kwenye hili jukwaa.
Ni muda ambao mtoto anakamilisha hatua za ukuaji wake kuanzia kulala,kunyonya,kukaa,kutembelea tumbo,kutambaa,kusimama,kutembea mpaka kukimbia na kuongea maneno kadhaa.
PESA ndio kila kitu
Wanawake wasikuizi bila pesa hayaendi wakuu, na hata kama huyo mwanaume anamaisha ya kawaida ila yupo na mwanamke ujue huyo mwanamke katoka either kwenye maisha ya shida au alikuwa single mother, kwa sikuizi kunakasumba unaenda ukweni kujitambulisha mama/baba mkwe anakuuliza unafanya kazi gani? Na ilitokea kwa kaka yangu hivyo sometimes unaweza jenga urafiki na huyo mwanamke baada ya kumuoa akawa nayeye analeta urafiki kinafiki tu.
Mi kunijambia hapana asee[emoji57][emoji57][emoji57]Hiyo sentensi ya mwisho imenichekesha sana...
Kweli kabisa unapoishi na mwenzi wako kirafiki unakuwa huru sana hata kuachia ushuzi mnapokuwa pamoja faraghani wala si issue kabisa.. yani mnaishia kuchekana tu
Mnaposema mwanamke bila hela sijui huwa mna maanisha nini hasa?kwamba utafute pesa ili umpe mwanamke?Wanawake wasikuizi bila pesa hayaendi wakuu, na hata kama huyo mwanaume anamaisha ya kawaida ila yupo na mwanamke ujue huyo mwanamke katoka either kwenye maisha ya shida au alikuwa single mother, kwa sikuizi kunakasumba unaenda ukweni kujitambulisha mama/baba mkwe anakuuliza unafanya kazi gani? Na ilitokea kwa kaka yangu hivyo sometimes unaweza jenga urafiki na huyo mwanamke baada ya kumuoa akawa nayeye analeta urafiki kinafiki tu.
Hapo kwenye mahari kuwa kipimo nakupinga dada,mahari mara nyingi huwa ina halalisha utumwa kwa mwanamke yaani mentality inakuwa kana kwamba umemnunua mwanamke,Hahahaaa uttoh2002 sasa unawekaje urafiki na mtu kakutoa kwenu unakula vizuri halafu anakuja kukutesa na njaa lakini?
Hapo ndio utajua mahari kabla ya ndoa ni moja ya vipimo vya kujua kama muoaji ana muwezo wa kutunza mke[emoji23][emoji23][emoji23]
Uwiii...ndo mtu ukajambe huko mbali maushuzi yako, lkn kunijambia hapana aseeKujamba sio tabia bali ni lazima.
Kufanya jambo la lazima mbele ya mwenza wako sio tabia mbaya
Sasa anauliza ili iweje? Yeye kapata mkwe basi wengine huwa wana nia nzuri wengine nia yao majukum ya familia wanayahamishia kwako endapo unakazi nzuri.Kwahyo wazaz kuuliza anafanya kazi gani ni kosa?
Yes[emoji13][emoji13][emoji119][emoji119]Hiyo sentensi ya mwisho imenichekesha sana...
Kweli kabisa unapoishi na mwenzi wako kirafiki unakuwa huru sana hata kuachia ushuzi mnapokuwa pamoja faraghani wala si issue kabisa.. yani mnaishia kuchekana tu
My kwema?Mi kunijambia hapana asee[emoji57][emoji57][emoji57]
Ni mojawapo ya tabia chafu
Wow nimewapenda buree, how i wish too🙏 ni raha sana kuwa na mtu mnayependana na ni rafiki, mnakua free hata kukosoana bila kuhofia amani kutoweka, maana ni marafiki mkiongea yanaisha and life goes on.Yaani ninavyoishi na mke wangu aisee naomba Mungu asiruhusu ibilisi kupita katikati hakika tutazeeka amoja.
Mtoa mada upo sahihi kabisa,maisha ya ndoa mkiishi kama marafiki maisha yapo simpo sana.
Tunataniana muda mwingi,na wakati wa kuwa serious tukiwa tunaongea pamoja mambo mhimu tunakuwa serious.Mke wangu ni mpole sana,mcheshi sana hajui kubishana na mume,hajui kujibu vibaya akiona una hasira pengine umevurugwa na mtu au kazini anakuuliza kwa upole sana na hupenda kusema "pole mume wangu","msamehe tu mume wangu"
Aisee huyu mwanamke naona Mungu ameamua kunipa kama zawadi,kwa miaka yote 8 niliyoishi naye sijawahi kumtilia mashaka kabisa kuhusu kuchepuka,sijawahi kuona hata sms yenye ukakasi simu zetu zipo huru sana kila mtu anashika simu ya mwenzake bila hiyana.
Maisha yetu ni sawa na mtu na mdogo wake maisha simple tu siyo masheria na masharti sharti yasiyo na umhimu wowote.
Nikisikia watu wanalalamikia mabalaa ya ndoa huwa nasikitika sana.
Hata ikitokea nikapewa nafasi ya kuoa upya mwanamke ninayemta bado nitamuoa tena mke wangu.
"Ngono ni kipengere kidogo sana kwenye ndoa"
Cc wee hujapata bado? [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Wow nimewapenda buree, how i wish too[emoji120] ni raha sana kuwa na mtu mnayependana na ni rafiki, mnakua free hata kukosoana bila kuhofia amani kutoweka, maana ni marafiki mkiongea yanaisha and life goes on.
Bado jamani, vipi kuna kaka yupo huko unipe pasi?😂Cc wee hujapata bado? [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Kwema dear, kerege wanasemaje?My kwema?
SUPPORTEDUmeshawahi kujiuliza kwa nini kuna jamaa mke wake unamuona wa kawaida sana lakini wanaishi kwa amani kabisa na wanapendana?
Ni kwa sababu wamekuwa marafiki ndani ya ndoa, siri ya rafiki hata awe mbaya kiasi gani hauwezi kuchagua sura yake akiwa mshkaji ndio mshkaji huyo.
Kuna watu wana marafiki ambao hawataki wenza wao wawe kama marafiki zao. Mtu ana rafiki mlemavu lakini hataki mwenza wake awe mlemavu, Mtu ana rafiki kipofu lakini hataki awe na mwenza kipofu, mtu ana rafiki mzee saana lakini hataki mwenza wake awe mzee.
Hii ni kwa sababu urafiki una nguvu ya kuwaunganisha watu kwa muda mrefu kuliko ngono yenyewe. Lakini pia jiulize kwamba mbona suala la urafiki inawezekana kuwa watu wa jinsia moja wakawa marafiki?
Kuonesha namna ambavyo urafiki una nguvu kubwa ya kuwaunganisha watu na kuwafanya waendelee kuwa wamoja. Mwanandoa mwenzio anapokuwa rafiki yako kuna uwezekano mkubwa sana wa nyinyi kuishi kwa muda mrefu katika ndoa yenu kwa sababu ndoa yenu imeunganishwa na jambo la urafiki ndani yake.
Urafiki una nguvu kuliko ngono ndio maana kuna talaka kwa wanandoa na wala hakuna talaka kwa marafiki. Kwa sababu marafiki hawatengani kwa sababu ya ugomvi bali wanatengana kwa sababu ya umbali ndio maana una washkaji zako wa shule hamjawahi kugombana ila kwa sababu ya umbali una washkaji wengine.
Lakini kwenye ndoa watu hawatengani hivi hivi tu lazima wakorofishane wengi wao ndipo waachane. Ngono unaweza kupata kwa siku moja lakini urafiki hauwezi kupata kwa siku moja. Hivyo mwanandoa usijisahau sana ukahisi kwamba ngono ndio ishu kubwa katika ndoa, bali urafiki hasa ndio jambo kubwa.
Wanandoa msiconcetrate kwenye ngono kwa sababu ngono sio ishu tenconcetrate katika mahusiano mazuri ya urafiki na mkeo. Kinachowatenganisha wanandoa ni mahusiano ya kingono na wala sio mahusiano ya kirafiki. Ngono katika ndoa ni dharura endapo utakuwa na hamu ndipo unamaliza haja zako,ila kuna mambo mengi ya kufanya na kujadili na rafiki yako wa ndoa ukiacha ngono.
Mahusiano yanayotegemea ngono hudumu kwa muda mfupi na kuishia kwenye michepuko,mahusiano yanayounganishwa na urafiki hudumu muda mrefu sana.
Mke/mume wako ndiye rafiki yako.