Siri ya Pinda kuongezwa kwenye ‘Kikosi Kazi’ ni wajumbe kuelemewa na hoja ya Katiba Mpya

Siri ya Pinda kuongezwa kwenye ‘Kikosi Kazi’ ni wajumbe kuelemewa na hoja ya Katiba Mpya

Kazi kubwa ya Kikosi Kazi cha Rais ni kupata maoni kuhusu kudorora kwa Hali ya Demokrasia nchini lkn yenyewe imejikita zaidi kwenye upatikanaji wa Katiba Mpya.

Baada ya Kikosi Kazi kupendekeza katiba isubiri hadi 2025 wajumbe waligawanyika kuna wanaotaka mchakato uanze sasa na kuna wanaosema usubiri.

Pamoja na hayo maoni mengi ya wadau wanaohojiwa na Kikosi Kazi yanapendekeza kuanza mapema kwa mchakato wa Katiba, wanadai kama hoja ni muda au gharama waendelee ilipoishia Tume ya Warioba, hoja ambayo wanaotaka katiba isubiri wameshindwa kuijibu.

“Kuna wakati Kikosi Kazi huwa kinaelemewa na hoja za wanaokuja kutoka maoni hivyo wanaamini uwepo wake na uzoefu wake utasaidia kuongeza utulivu.” Profesa Rwekaza Mkandara.

Pinda alizima hoja ya Zanzibar ni nchi au siyo nchi, kaletwa kujaribu kuzima hoja ya Katiba mpya ni sasa au isubiri baada ya uchaguzi, je atafanikiwa? yetu macho na masikio.
Wakati ukifika mtoto kutoka tumboni kwa mama ni lazima atoke. Whether no hai au mfu lazima atoke. Kama wakati wa katiba mpya umefika hakuna atakayezuia.
 
Kwa Pinda watakua wamekosea Sana kwa Sababu yeye mwenyewe anataka katiba mpya kwa nguvu Zote.
 

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Kazi kubwa ya Kikosi Kazi cha Rais ni kupata maoni kuhusu kudorora kwa Hali ya Demokrasia nchini lkn yenyewe imejikita zaidi kwenye upatikanaji wa Katiba Mpya.

Baada ya Kikosi Kazi kupendekeza katiba isubiri hadi 2025 wajumbe waligawanyika kuna wanaotaka mchakato uanze sasa na kuna wanaosema usubiri.

Pamoja na hayo maoni mengi ya wadau wanaohojiwa na Kikosi Kazi yanapendekeza kuanza mapema kwa mchakato wa Katiba, wanadai kama hoja ni muda au gharama waendelee ilipoishia Tume ya Warioba, hoja ambayo wanaotaka katiba isubiri wameshindwa kuijibu.

“Kuna wakati Kikosi Kazi huwa kinaelemewa na hoja za wanaokuja kutoka maoni hivyo wanaamini uwepo wake na uzoefu wake utasaidia kuongeza utulivu.” Profesa Rwekaza Mkandara.

Pinda alizima hoja ya Zanzibar ni nchi au siyo nchi, kaletwa kujaribu kuzima hoja ya Katiba mpya ni sasa au isubiri baada ya uchaguzi, je atafanikiwa? yetu macho na masikio.
Kupoteza fedha za umma bure. Kama ni katiba mbona zoezi lilishakamilika. Eti mtu anapendekeza tuanzie na pendekezo la tume ya warioba? Yale mabilioni wanasiasa walikula bunge la katiba nani atawajibika? Yafaa wanasiasa waache ujinga na ulafi. Wananchi watakufa na mtu huyu jk kwa ubadhirifu. Fedha zimeliwa kazi ilikamilika halafu mtu anasema zoezi lirudiwe ili wao wale tena fedha za umma🙄
 
Kazi kubwa ya Kikosi Kazi cha Rais ni kupata maoni kuhusu kudorora kwa Hali ya Demokrasia nchini lkn yenyewe imejikita zaidi kwenye upatikanaji wa Katiba Mpya.

Baada ya Kikosi Kazi kupendekeza katiba isubiri hadi 2025 wajumbe waligawanyika kuna wanaotaka mchakato uanze sasa na kuna wanaosema usubiri.

Pamoja na hayo maoni mengi ya wadau wanaohojiwa na Kikosi Kazi yanapendekeza kuanza mapema kwa mchakato wa Katiba, wanadai kama hoja ni muda au gharama waendelee ilipoishia Tume ya Warioba, hoja ambayo wanaotaka katiba isubiri wameshindwa kuijibu.

“Kuna wakati Kikosi Kazi huwa kinaelemewa na hoja za wanaokuja kutoka maoni hivyo wanaamini uwepo wake na uzoefu wake utasaidia kuongeza utulivu.” Profesa Rwekaza Mkandara.

Pinda alizima hoja ya Zanzibar ni nchi au siyo nchi, kaletwa kujaribu kuzima hoja ya Katiba mpya ni sasa au isubiri baada ya uchaguzi, je atafanikiwa? yetu macho na masikio.
CHADEMA imeshakufa tayari hata mambo wanayosema ni kama vile wapo ndotoni

Tokea lini ccm wakashindana wao kwa wao kuhusu katiba Mpya

Uchaguzi ujao hata kura moja hamtapata
 
Marekebisho yoyote ya Katiba yafanyike kwa kutumia Ile Katiba pendwa ya Warioba,maana ndo yalikuwa maoni halisi ya WENYE NCHI YAO(WANANCHI).Ile Katiba ya Hayati SITA Ichomwe Moto maana ilikuwa Ni kejeli kwa watanzania
Vema kabisa. Hata katiba ya warioba ipitiwe upya Kuna vipengele vyitakuwa vimepitwa na wakati.

Kama ipo kwenye document tunaomba ikatwe vipande vipande iwekwe au ifunguliwe web site ambayo itasajili wachangiaji kutokana na majina yao ya vitambulisho au namba za Nida I'll watu wachangie bila kebehi au kutukana. Watu watachangia siku hizi wapo kwenye mtandao.
 
Walichoridhiana.Lumumba na Ufipa ndio Komredi Chongollo kakiwasilisha kwenye Kikosi kazi cha Prof Mkandalla na Zitto Kabwe

Usiwe mgumu kuelewa. Chigolo kakiwakilisha chama Cha Mapinduzi. Maongezi ndio kwanza yameanza baina ya ccm na CHADEMA
 
kazi ipo bora ingekuwa kibarua tungelipwa kutwa lakini kazi lazima ukopwe nguvu zako mpaka mwisho wa mwezi!
binafsi nawahurumia vijana kiufupi watawala hawawapendi na hawako tayari kuwaandaa kushika nchi bali wamejipanga kuendelea kuwapa nchi watoto wao na vizazi vyao hata kama damu itamwagika huo ndio ukweli.
na kwa kufanya hivyo wameamua kuwafanya vijana wengi wawe wajinga kwa kuhakikisha wanawajibu maswali magumu kwa majibu rahisi.
  • hebu fikiria kama biashara za umachinga zinalipa kwanini watoto wao hawazifanyi
  • kama boda boda inalipa kwanini watoto wao hawafanyi
  • na kama mziki unalipa ushawahi kuwaona na watoto wao wakiwa wanamuziki
  • zindukeni vijana shauri zenu mkizubaa ukubwani mtakosa hekima na mtatawaliwa milele na umaskini hautaondoka kwenu.
Wanajifanya kuwa na hati miliki ya hii nchi. Keki ya taifa haigawanywi sawa sawa
 
Kupoteza fedha za umma bure. Kama ni katiba mbona zoezi lilishakamilika. Eti mtu anapendekeza tuanzie na pendekezo la tume ya warioba? Yale mabilioni wanasiasa walikula bunge la katiba nani atawajibika? Yafaa wanasiasa waache ujinga na ulafi. Wananchi watakufa na mtu huyu jk kwa ubadhirifu. Fedha zimeliwa kazi ilikamilika halafu mtu anasema zoezi lirudiwe ili wao wale tena fedha za umma🙄

Mchakato ulifia njiani haujaisha. Ndio maana wanataka kuanzisha mchakato mpya.
 
Sasa mtu kama Pinda anaushawishi gani huyu kwa jamii?
Pinda alikuwa waziri mkuu wa VascoDagama ambaye ndio muhusika mkuu wa kuihujumu rasimu ya katiba ya Warioba!! Asije a kaleta upuuzi wa boss wake wa kutaka kuanza mchakato mpya ili Ikifika 2025 wawe hawajafanya kitu ili uchaguzi ufanyike kwa kutumia katiba ya sasa!! Hizo ni mbinu za Kikwete ili Hangaya aendelee 2025 na yeye afanikishe mishe mishe zake!!
 
CHADEMA imeshakufa tayari hata mambo wanayosema ni kama vile wapo ndotoni

Tokea lini ccm wakashindana wao kwa wao kuhusu katiba Mpya

Uchaguzi ujao hata kura moja hamtapata

Be realistic kura moja ndio Nini?. Usiangalie Mambo ya CHADEMA angalia uhitaji wa katiba mpya.
 
Mchakato ulifia njiani haujaisha. Ndio maana wanataka kuanzisha mchakato mpya.
Mchakato ndio ulikuwa umefika ukingoni wakati ulipohujumiwa na mafisadi!! Mpaka leo hawajasema kwanini walihujumu!! Kazi iliyobakia ilikuwa ndogo sana na hapo ndio wanatakiwa wamalizie sio kuanza upya!
 
Marekebisho yoyote ya Katiba yafanyike kwa kutumia Ile Katiba pendwa ya Warioba,maana ndo yalikuwa maoni halisi ya WENYE NCHI YAO(WANANCHI).Ile Katiba ya Hayati SITA Ichomwe Moto maana ilikuwa Ni kejeli kwa watanzania
Nakazia ✍️✍️✍️
Na hii post iwekewe 'lamination' kabisaa!

Mapendekezo ya Katiba ya mh. Warioba yalipatikana kwa weledi mkubwa kutoka Kwa wananchi, tena kwa gharama kubwa..

Hizi kelele zingine kama Katiba Pendekezwa ya Bunge la Katiba la hayati Sita na hiyo sijui Kikosi kazi cha Mukandala ni muendelezo wa ghilba, hila, utapeli, ufujaji wa fedha za umma (ufisadi) na kupotezeana muda🙄 Kwa lengo la kuchelewesha Katiba Mpya
 
CHADEMA imeshakufa tayari hata mambo wanayosema ni kama vile wapo ndotoni

Tokea lini ccm wakashindana wao kwa wao kuhusu katiba Mpya

Uchaguzi ujao hata kura moja hamtapata
Mkuu topic ni Pinda kuongezwa sio Chadema.
 
Mbowe alisema CCM na Chadema ndio vyama vikuu vya siasa nchini hivyo watakaa na kutoa mapendekezo yao

Wazo la Katiba mpya ni la Chadema sasa unadhani nani kalipeleka kwenye Kikosi kazi cha Prof Mkandalla na Zitto Kabwe?
Kikosi Kazi kimeundwa tangu 2021 Chadema haikuwemo, hadidu za rejea hazikutolewa na Chadema kwanza haihusiki na hicho kikundi.
 
Kikosi Kazi kimeundwa tangu 2021 Chadema haikuwemo, hadidu za rejea hazikutokewa na Chadema kwanza haihusiki na hicho kikundi.
Chadema imeingia kwenye Kikosi kazi cha Prof Mkandalla na Zitto Kabwe kupitia Maridhiano ya Ikulu

Inaweza kukuta hata Pinda kapendekezwa na Mbowe
 
Back
Top Bottom