Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Inamaana hujui ndiye amesababisha haya yotekwa lipi tena mkuu? Funguka
Wenye,kaskazini,mashariki,magharibi na kusini,usipo nielewa hapo usiniulize tena.Wakubwa gani hao?
Bila kufukua makabuli nchi hii itakushinda tu..."Mtukufu" alisha sema hafukui makaburi,hivyo tutawalipia wale wezi wa Lumbesa za Stanbic bank
Sahihi yupo kwenye baraza haaah hii nchi bwana....Jaribuni kumkumbuka jamaa aliyehutubia wazee wa CCM na kuwadanganya kuwa fedha ya ESCROW sio pesa ya Tanesco na akapigiwa makofi mengi sana, halafu wakapunguza bei na baadae uchaguzi ukafuata, sasa wameshinda hawana shida tena wacha tuisome namba
Mwombeeni awaweke ndaniNaomba muniombee kwa mungu, je wewe unawasaidiaje hao, wakati hutaki hata kutaja jina ESCRO!!!
Tulia kidogo tutaanza kuimba wimbo mmoja kama nchi.Wale mliokuwa mkiimba nyimbo ya wapinzani kuisoma namba naomba mje tena mkaimbe kale ka wimbo
Mzimu wa watu wa kale,bunge lingefanya kikao maalumu ili tujue ukweli kuhusu IPTL na jinsi ya kumaliza unyonyaji mamboleo.IPTL Mzimu unaoitafuna Tanzania,Bila shaka mwenye hili dubwasha ni yule mkuu wa dunia.Piga kelele ujuavyo lipo tu. tusipoangalia litakuwepo vizazi na vizazi.pumbavu sana.
wazo zuri tu. wao wakale wapi? nasikia hata Yale majenerator ya Kinyerezi ni yakwao.Wanajamvi amani iwe kwenu
Kwa maoni yangu kutokana na Tanesco kukabwa koo kisheria na standard charted bank ya Hong kong juu ya IPTL kuhusu malipo ambayo ni mzigo mkubwa mno kwa wananchi wanyonge hivyo ili kukwepa hilo, Serikali iitangaze mufilisi jina la Tanesco kwa hisa zote 100% na kuanzisha taasisi ya uzalishaji nguvu za umeme Tanzania kwa share mpya na kuchonganisha ushindani hilo linaweza kusaidia kisheria kuwepa limzigo likubwa mno na kusaidia wananchi, maana sasa Tanesco inabanwa sana na wale wa kule mbali kwa mikataba ilioingia bila kustukia harufu ya baadae
Mpaka waondoe sheria ya monopolistic ambayo inaibeba Tanesco.
Manyag'au CCM,wamegawana pesa na nyingine wakapeleka kwenye kampeni halafu wanyonge wanalipia walaaniwe Muhongo na CCM yake.