Siri ya upendo anaooneshwa Rais Samia katika ziara mikoani ni uchapakazi wake

Siri ya upendo anaooneshwa Rais Samia katika ziara mikoani ni uchapakazi wake

Maryam Malya

Senior Member
Joined
Nov 29, 2021
Posts
116
Reaction score
260
Na Chacha Wangwe Jr

Maelfu ya watanzania wanaojitokeza kumlaki Rais Samia Suluhu Hassan katika ziara yake Mikoani ni jambo la kuvutia lakini inapaswa ieleweke kuwa haya ni matokeo ya uchapakazi wake. Tuangazie mambo machache yanayopelekea Rais Samia kupendwa sana Mkoani Kigoma na Kagera;

1. Katika kipindi cha kuanzia April 2022 hadi Octoba 2022, serikali imeweza kuzindua miradi ya maendeleo ipatayo 1293 inayogharimu fedha za walipa kodi zaidi ya Bilioni 650. Mikoa ya Kagera na Kigoma ni sehemu ya wanafaika wa miradi hii inayolenga kustawisha maisha ya wananchi.

2. Ahadi yake ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo kama vile ujenzi wa Hospitali ya kanda, Chuo cha Ufundi Stadi na Huduma Burugo, Kituo kikubwa cha Umeme Mpomvu, na kiwanda cha kusafisha dhahabu Geita.

3. Kwa kipekee ahadi yake ya kuhakikisha watanzania wote wanapata umeme wa uhakika kwa kuzindua miradi sita ya umeme na kwa mara ya kwanza kuzima majenerata na kuiunganisha Kigoma katika gridi ya Taifa ambapo wananchi zaidi ya 10,000 watapata umeme wa uhakika.

4. Miradi inayogusa wananchi moja kwa moja kama vile Skimu ya maji Kakonko, Uzinduzi wa Hospitali ya Wilaya Kakonko, uzinduzi wa Barabara ya Kabingo yenye urefu wa takribani KM 50 iliyojengwa kwa kiwango cha lami na Barabara ya kidahwe yenye urefu wa KM 63 nayo pia ikiwa imejengwa kwa kiwango cha lami.

5. Kwa kipekee Rais Samia ametekeleza ahadi kwa wanakigoma kwa kuzindua Jengo la wagonjwa wa dharura (EMD). Hospitali ya Rufaa ya Maweni Kigoma inaendelea kuboreshwa kwa kasi ambapo mpaka sasa inaweza kutoa huduma za CT SCAN na hivyo kuepusha wagonjwa kusafiri umbali mrefu kufuata huduma.

Licha ya mambo mengi yanayowagusa wananchi wa kawaida kama vile ruzuku ya mbolea kwa wakulima, Elimu bure, Mikopo ya wanafunzi, mpango wa BIMA kwa wote, Rais Samia anaendelea kutekeleza miradi muhimu itayo huisha uchumi wa Kigoma na Mikoa ya jirani kwa kutoa fedha za uboreshaji wa Bandari zilizomo Mkoani Kigoma.

MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU MMBARIKI RAIS WETU

#SisiTumekubali #MamaYukokazini
 
Licha ya kwamba umeandika ukweli, lakini bado watakuja chawa wa yule muomba hifadhi wa canada wapinge ulichoandika hapa, tena bila fact yoyote.
 
Umesahau na FREE SPEECH. Yule Mwendazake hakutaka akosolewe. Kutwa kuwaandama watu kwenye social media na vijiwe wanaomsema Rais. Ila Samia kaachia mumseme mnavyotaka. Hana shida kwa kuwa ni Uhuru wa kikatiba
 
She is
Na Chacha Wangwe Jr

Maelfu ya watanzania wanaojitokeza kumlaki Rais Samia Suluhu Hassan katika ziara yake Mikoani ni jambo la kuvutia lakini inapaswa ieleweke kuwa haya ni matokeo ya uchapakazi wake. Tuangazie mambo machache yanayopelekea Rais Samia kupendwa sana Mkoani Kigoma na Kagera...
 
She is
Na Chacha Wangwe Jr

Maelfu ya watanzania wanaojitokeza kumlaki Rais Samia Suluhu Hassan katika ziara yake Mikoani ni jambo la kuvutia lakini inapaswa ieleweke kuwa haya ni matokeo ya uchapakazi wake. Tuangazie mambo machache yanayopelekea Rais Samia kupendwa sana Mkoani Kigoma na Kagera...
 
FfWs9PTXgAALegV.jpg

Rais Samia Suluhu alipokelewa kwa kishindo kwasababu wanakigoma wamefanyiwa maendeleo mengi ambayo hawakuwai kuyapata toka uhuru uanze kama umeme wa uhakika.

FfXoPqhXEAEXAas.jpg
 
Samia suluhu Hassani Ni zawadi kwetu watanzania tunayopaswa kujivunia na kuiheshimu maana viongozi aina yake Hawazaliwi kila Siku Na hawapatikani kila nchi
 
Na Chacha Wangwe Jr

Maelfu ya watanzania wanaojitokeza kumlaki Rais Samia Suluhu Hassan katika ziara yake Mikoani ni jambo la kuvutia lakini inapaswa ieleweke kuwa haya ni matokeo ya uchapakazi wake. Tuangazie mambo machache yanayopelekea Rais Samia kupendwa sana Mkoani Kigoma na Kagera;

1. Katika kipindi cha kuanzia April 2022 hadi Octoba 2022, serikali imeweza kuzindua miradi ya maendeleo ipatayo 1293 inayogharimu fedha za walipa kodi zaidi ya Bilioni 650. Mikoa ya Kagera na Kigoma ni sehemu ya wanafaika wa miradi hii inayolenga kustawisha maisha ya wananchi.

2. Ahadi yake ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo kama vile ujenzi wa Hospitali ya kanda, Chuo cha Ufundi Stadi na Huduma Burugo, Kituo kikubwa cha Umeme Mpomvu, na kiwanda cha kusafisha dhahabu Geita.

3. Kwa kipekee ahadi yake ya kuhakikisha watanzania wote wanapata umeme wa uhakika kwa kuzindua miradi sita ya umeme na kwa mara ya kwanza kuzima majenerata na kuiunganisha Kigoma katika gridi ya Taifa ambapo wananchi zaidi ya 10,000 watapata umeme wa uhakika.

4. Miradi inayogusa wananchi moja kwa moja kama vile Skimu ya maji Kakonko, Uzinduzi wa Hospitali ya Wilaya Kakonko, uzinduzi wa Barabara ya Kabingo yenye urefu wa takribani KM 50 iliyojengwa kwa kiwango cha lami na Barabara ya kidahwe yenye urefu wa KM 63 nayo pia ikiwa imejengwa kwa kiwango cha lami.

5. Kwa kipekee Rais Samia ametekeleza ahadi kwa wanakigoma kwa kuzindua Jengo la wagonjwa wa dharura (EMD). Hospitali ya Rufaa ya Maweni Kigoma inaendelea kuboreshwa kwa kasi ambapo mpaka sasa inaweza kutoa huduma za CT SCAN na hivyo kuepusha wagonjwa kusafiri umbali mrefu kufuata huduma.

Licha ya mambo mengi yanayowagusa wananchi wa kawaida kama vile ruzuku ya mbolea kwa wakulima, Elimu bure, Mikopo ya wanafunzi, mpango wa BIMA kwa wote, Rais Samia anaendelea kutekeleza miradi muhimu itayo huisha uchumi wa Kigoma na Mikoa ya jirani kwa kutoa fedha za uboreshaji wa Bandari zilizomo Mkoani Kigoma.

MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU MMBARIKI RAIS WETU

#SisiTumekubali #MamaYukokazini
Rais Samia Suluhu amefanya maendeleo makubwa kigoma tena yanayomgusa direct mwananchi kwaiyo wanakigoma walikua na kila sababu ya kumpokea kwa shangwe
 
Siku za hivi karibuni kumezuka nyuzi na I'd mbali mbali za wachumia tumbo zilizotumwa kusafisha njia kuelekea 2025......lakini tunachoowaambia ni kwamba mambo yapo bayana na wananchi wataamua......
 
Back
Top Bottom