Sisi ambao hatutekwi na Wahubiri Waongo wa Miujiza ndiyo hatuna Akili au waliotekwa nao ndiyo hawana kabisa Akili?

Fuatilia chimbuko la dini zote utajua
Tumedanganywa kwa Muda Mrefu sana. Kama Mungu angekuwa Ana Dini Pasingekuwa na Dini Tofauti tofauti zinazotofautiana

Ukiona Hivyo Hakuna Mungu hapo Bali ni Binadamu na Vitu vingine vinachanganya Kichwa chako ili viweze Kukutawala

Hakunq Mungu Mwenye Dini Tofauti tofauti unazoziona Leo hii . HAYUPO
 
Labda nikuulize swali haya uendelee kutafakari
1. Je unajivunia kuwa Roman catholic au kuwa Kwa Yesu Kristo?
2. Wewe ni mkristo au mkatholic?
3. Je Roman Catholic itakupeleka mbinguni?
4. Je siku ya hukumu kuna swali Mungu atakuuliza kuhusu ulipokuwa ukiabudu na kusali?
 
Wewe una matatizo yako binafsi, viongozi wakubwa wote wa Tanganyika wamelelewa na kukuzwa na KANISA TAKATIFU KATOLIKI LA MITUME.

Sio haya makanisa ya mifukoni mwa watu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mbele za Mungu hakuna kitu kinachoitwa eti kiongozi mkubwa yeye anataka tumuabudu ktk roho na kweli sio hayo masanamu na marozali ya kipepo hayo
 
Eebwana wee!. Naomba uniambie unaelewa nini kuhusu Mungu na Yesu Kristo? Kwa nini unasali?
 
Naamini katika kusaidia yatima,wajane na wahitaji( maskini na wagonjwa). Sadaka zangu ninaenda huko sio Kanisani.
Unafanya vyema. Kanisani kwenu mna raslimali zozote za kanisa labda? Kanisani kwenu pia kuna wajane na yatima? Huwa mnawahudumiaje?
Kanisalni kwenu mna vyombo vya kuhubiria? Mnavipataje na mnavitunzaje?
Kanisani kwenu kuna watu mmeajiri mfano walinzi, wafanya usafi, watu wanaokaa kanisani kwa masuala ya utawala labda. Hao watu huwa mnawahudumia namna gani kama wapo?
Sijajua kanisa unaloshiriki. Ningependa pia kujua mna makanisa mangapi ya aina hiyo na huwa mnayaanzisha namna gani?
Unajua kushirikishana ni kuongezeana maarifa. Naomba unisaidie.
 
Inawezekana sisi Wakatoliki hatuna akili! Yaani tungeenda kwa hao Manabii na Mitume kuchukua maji, mafuta, chumvi, vitambaa na sabuni za upako; muda huu huenda na sisi tungekuwa ni matajiri kama hai wenzetu!
 
Mkuu, andika neno: 2Timotheo 3:1-5 halafu search.
Utaona mambo!
 
Naomba unijibu swali langu mjomba.. Hadithi hizi kila mtu anaweza kuwaza atakavyo. Kama wewe unamwamini Yesu Kristo, jibu swali langu.

Ukiwa kanisani kama unasali, huwa mnatumia kitabu gani au mnautaratibu gani ambao hauhusishi mwanadamu yeyote?

Habari za Sodoma na Gomora wewe umezijuaje?
 
Sadaka siyo mali ya padri inakwenda jimboni na kutolewa kwa utaratibu maalum tofaut na walokole sadaka anachukua mchungaji anafanya anavotaka
Nani alikwambia kuwa sadaka siyo mali ya padri? Kama si mali yake zimewahi kurudi kwa waumini ? Unajua padri analipwa ngapi kwa mwezi,hizo siminary ninyi wakatoliki munasoma bure? Je hizo hospitali munatibiwa bure kwa kuwa ni sadaka zenu haziingii kwenye mfuko wa mtu?
 
Naamini katika kusaidia yatima,wajane na wahitaji( maskini na wagonjwa). Sadaka zangu ninaenda huko sio Kanisani.
Wewe una akili Timamu. Binadamu tusaidiane wenyewe kwa wenyewe. Mungu haitaji sadaka yako wala Dhabihu yako. Maana Yeye si Kiumbe Kama Wewe.

Yeye alikuumba Akakuweka Duniani yeye amekamilika katika kila Kitu, Kwahiyo haitaji Chochote kutoka Kwako.

Hizo sadaka wanazotoa Huko walishashindwa Kuthibitisha zinamfikiaje Mungu wamebaki ku Assume tu Mambo na Kumpamba Mungu
 
Nimeshakujibu. Mungu hayupo Hivyo

Mungu haitaji Sadaka yako Yeyote. Ushajiuliza Sadaka Inamsaidiaje Mungu unapoitoa.

Mungu ni Mkamilifu Haitaji sadaka Yako maana Yeye Si Kiumbe Kama Wewe ulivyo. Hizo sadaka na Dhabihu zinaishia Hapa Hapa Duniani kwa Binadamu Wenzako unaowapa kwa Kutokujua kwamba Wameweka Misingi hiyo ili wawatawale Akili zenu.

Maana Hata Kwenye Biblia Sadaka za Agano la Kale si Sadaka za Agano Jipya. Mungu wa Agano la Kale hafanani kitabia na Mungu Wa Agano jipya
 
Naamini katika kusaidia yatima,wajane na wahitaji( maskini na wagonjwa). Sadaka zangu ninaenda huko sio Kanisani.
I wish Ulimwengu mzima ungekuwa na mtazamo huu. Dunia pangekuwa sehemu salama sana. Lakini walio wengi ambao hawajitambui ndio wameshatekwa na makanjanja wachache. Mtu anaamini amnyime msaada jirani yake ambae ni maskini ila ampelekee kanjanja fulani huko kanisani huku akimuaminisha ataingia uzima wa milele na huyo anaekwambia hivyo hataki kujishughulisha anakutegemea wewe uende ndio ale na kubadilisha magari. Ujinga hautoisha daima
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…