Uchaguzi 2020 Sisi sio wajinga, Ulipochukua tu madaraka ukaanza na kubomoa nyumba zetu!

Uchaguzi 2020 Sisi sio wajinga, Ulipochukua tu madaraka ukaanza na kubomoa nyumba zetu!

Wakati pekee wa kila mtza kulipiza kisasi ni October 28 nje ya hapo ni hadi 2040 miaka 20 mbele ndo atatoka madarakani,atatumia kisingizio cha miradi atawale milele rejea kauli za Ndugai na wapambe wake.
 
Hela zilizochangwa kwa wahanga bukoba ni nyingi sana kuliko ukarabati alioufanya nyingi zimepigwa zingetosha kuwajengea nyumba za kisasa wahanga wote na chenji ingebaki. Hivo atueleze zipo wapi zingine mbona yaliyofanyika ayaendani na pesa zilizochangwa. Arudishe chenji
 
Mkuu pole sana
Kwa uliyotaja yanafikirisha yanaumiza ni wachache watakuelewa
Napata wakati mgumu kujiuliza kwa nini wengine wanaona ni Heri akaendelea kutukanyaga
Ni heri wataadharishwe pia ili wakiumizwa wasimlilie mtu
 
SISI SIO WAJINGA.

Ulipochukua tu madaraka ukaanza na kubomoa nyumba zetu katika bonde la Msimbazi. Bila huruma ukatuacha tumelala nje na watoto wetu. Ulidhani tutahama mjini lakini sisi bado tupo.

SISI SIO WAJINGA.

Ulipokuwa unapanua barabara ya Ubungo - Kibaha ukabomoa nyumba zetu. Mbunge wetu Mnyika aliomba utulipe fidia ukampinga mbele yetu. Lengo lako tufe masikini lakini kwetu sisi maisha yanaendelea.

SISI SIO WAJINGA.

Hukutaka tuwaone wawakirishi wetu, wakiwakirisha matatizo yetu Bungeni. Ulisema gharama za kurusha matangazo Live ni kubwa. Lakini leo hii unatuomba tufungue TBC tukuangalie ukikata mitaa kuomba kura.

SISI SIO WAJINGA.

Baada ya kuwa tumefanya kazi kwa miaka 40 na tumebakiza miezi 3 tustaafu ukatufukuza kazi kwa kisingizio cha vyeti feki. Ulidhani tutakufa kwa njaa lakini Mungu anatupigani bado tunaishi.

SISI SIO WAJINGA.

Tulipopata tetemeko la ardhi Watanzania wenzetu walituchangia pesa nyingi lakini wajanja wakatafuna. Ulipokuja Bukoba tulidhani utatutetea wanyonge badala yake ukatusimanga na kutukumbusha majanga ya Ukimwi, MV Bukoba kwamba yote yanatupiga sisi. Sasa nasikia unakuja kuomba kura kwetu! Je, ni kweli wewe utakanyaga Bukoba?

SISI SIO WAJINGA.

Tulipokuwa tuna njaa. Njaa iliyotokana na ukame. Tukakuomba msahada wa chakula. Hii sio kwako tu, hata Serikali zilizopita zilitusaidia tulipokumbwa na ukame. Lakini ulitujibu kwa kejeli na kiburi cha hali ya juu. Eti tusikuombe chakula, Serikali haina shamba. Leo hii unakuja tena kuomba kura?

SISI SIO WAJINGA.

Tukaenda Mtwara kulima korosho. Ukatuma askari wako wakatunyang'anya korosho halafu wakadai tuwaonyeshe mashamba yetu. Mbona wanaolima Mahindi, Pamba, Mpunga, n.k. hamuwaulizi mashamba yao? Ukasema hao askari watabangua korosho kwa meno ili kila Mtanzania atapata kilo 2, lakini hatujapata mgao.
Sasa nasikia unakuja kuomba kura! Labda uishie Nangurukuru kwa sababu.

SISI SIO WAJINGA.

Tumeitumikia nchi yetu kwa bidii kubwa. Tumefanya kazi kwa uzalendo mkubwa, huku tukipokea mishahara kidogo. Leo hii tumestaafu, tupo nyumbani miaka ikikatika. Lakini hutaki kutulipa mafao yetu. Bila aibu unakuja kutuomba kura tena?


#SISI_SIO_WAJINGA.
Usilie kamanda!
Lisu atarudisha vyeti feki.
 
Siko tayari kuona tunanunua ndege za mizigo angali kuna watanzania hawana uhakika wa maji safi.

Sisi sio wajinga, kura kwa Tundu Lissu
Kweli kamanda!

maana tulipokuwa hatununui mindege tulikuwa na uhakika wa maji safi.
 
Ulitaka uachwe unaishi bonde la msimbazi kama chura? Ili mafuriko yawe yanafunika nyumba yako ili upige mbizi ukiwa umelala!

Ulitaka watu waliojenga kwenye hifadhi ya barabara walipwe? Huku walishaenda mahakamani na kushindwa kesi?

Ulitaka madalali wa zao la korosho wawapunje bei wakulima? Mbona wakulima wamelipwa na hawalalamiki?

ulitaka watu waliofoji vyeti walipwe wakati walifanya kosa la jinai? Na mh rais akawasamehe maana walitakiwa pamoja na wewe mfungwe kwa kuiibia serikali.
 
Wewe na wenzako wanaoshabikia huu upuuzi ulioandika ni wajinga na wapuuzi kabisa. Ulitaka uachwe unaishi bonde la msimbazi kama chura? Ili mafuriko yawe yanafunika nyumba yako ili upige mbizi ukiwa umelala! Ulitaka watu waliojenga kwenye hifadhi ya barabara walipwe? Huku walishaenda mahakamani na kushindwa kesi?..
Hao waliofanya kosa la jinai miaka yote mbona products walizozitoa mlizpokea na mnaendelea kuzitumia?

Mbona hamkuziita ni za jinai?, mbona mpka leo mjomba wangu anadai zaidi ya milion sita za Korosho alizotapeliwa? ,mbona mahakama iliweka zuio na katazo la kubomoa nyumba za watu ila shetani wenu akakataaa kwa kuwa kaikalia mahakama?

Mbona huelezei kuhusu kuwakashifu watu waliopata majanga tena makubwa na kuwadhulumu ungekuwa wewe ingejisikiaje?.tanua ubongo wako ufikirie zaidi.
 
Back
Top Bottom