Uchaguzi 2020 Sisi sio wajinga, Ulipochukua tu madaraka ukaanza na kubomoa nyumba zetu!

Wakati pekee wa kila mtza kulipiza kisasi ni October 28 nje ya hapo ni hadi 2040 miaka 20 mbele ndo atatoka madarakani,atatumia kisingizio cha miradi atawale milele rejea kauli za Ndugai na wapambe wake.
 
Hela zilizochangwa kwa wahanga bukoba ni nyingi sana kuliko ukarabati alioufanya nyingi zimepigwa zingetosha kuwajengea nyumba za kisasa wahanga wote na chenji ingebaki. Hivo atueleze zipo wapi zingine mbona yaliyofanyika ayaendani na pesa zilizochangwa. Arudishe chenji
 
Sasa hiyo ndege ya mizigo si ndiyo itakayoleta fedha za kuchimba visima upate maji safi maana huna utamaduni wa kulipa kodi.
Ndege ya mizigo itabeba raslimali zetu kuzipeleka kwa mabeberu
 
Mkuu pole sana
Kwa uliyotaja yanafikirisha yanaumiza ni wachache watakuelewa
Napata wakati mgumu kujiuliza kwa nini wengine wanaona ni Heri akaendelea kutukanyaga
Ni heri wataadharishwe pia ili wakiumizwa wasimlilie mtu
 
Usilie kamanda!
Lisu atarudisha vyeti feki.
 
Siko tayari kuona tunanunua ndege za mizigo angali kuna watanzania hawana uhakika wa maji safi.

Sisi sio wajinga, kura kwa Tundu Lissu
Kweli kamanda!

maana tulipokuwa hatununui mindege tulikuwa na uhakika wa maji safi.
 
Ulitaka uachwe unaishi bonde la msimbazi kama chura? Ili mafuriko yawe yanafunika nyumba yako ili upige mbizi ukiwa umelala!

Ulitaka watu waliojenga kwenye hifadhi ya barabara walipwe? Huku walishaenda mahakamani na kushindwa kesi?

Ulitaka madalali wa zao la korosho wawapunje bei wakulima? Mbona wakulima wamelipwa na hawalalamiki?

ulitaka watu waliofoji vyeti walipwe wakati walifanya kosa la jinai? Na mh rais akawasamehe maana walitakiwa pamoja na wewe mfungwe kwa kuiibia serikali.
 
Hao waliofanya kosa la jinai miaka yote mbona products walizozitoa mlizpokea na mnaendelea kuzitumia?

Mbona hamkuziita ni za jinai?, mbona mpka leo mjomba wangu anadai zaidi ya milion sita za Korosho alizotapeliwa? ,mbona mahakama iliweka zuio na katazo la kubomoa nyumba za watu ila shetani wenu akakataaa kwa kuwa kaikalia mahakama?

Mbona huelezei kuhusu kuwakashifu watu waliopata majanga tena makubwa na kuwadhulumu ungekuwa wewe ingejisikiaje?.tanua ubongo wako ufikirie zaidi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…