Sitosahau safari yangu ya Lindi iliyojaa maumivu na tabu nzito

Sitosahau safari yangu ya Lindi iliyojaa maumivu na tabu nzito

Hii chai, maeneo ya Stand, kibaka hawezi kuwa na ujasiri sijui wa kunificha chin ya gari kukungoja wewe usiye na hela, na vyeti vya nini.

Inawezekana ni kweli ila umeongeza uongo mwingi, sehemu hii ya Vibaka imeharibu uhalali wa andiko lako kwa 100
Kwanza vibaka hawana akili ndio maana wakapewa hilo jina fikra zao ni kuwa wakichukua vyeti wanajua pesa nitatoa tu, ukweli wa mm kutokuwa na pesa niliujua mm tu wao hawakuamini maana wanajua huyu mtu kukubali si rahisi kwani wa ngapi wanaforce mpaka wanapata pesa?.
 
-----SEHEMU YA TATU - - - -

Konda wa bus la MASHALAH alipotangaza kituo yule jamaa aliekanyaga samaki zangu akasogea mbele bus likasimama jamaa akashuka. Nikiwa nimeinama chini nikijikuta nadondosha chozi huku namkumbuka mama alikuwa akiniambia "Mwanangu mpwayungu village kabla hujafanya maamuzi fikiri kwanza". Maamuzi niliyokurupuka Kuanza safari ya kwenda kilwa ilihali mm sio mmakonde wala mmwera nasina ndugu wala kibarua cha kwenda kufanya maamuzi haya yaliniweka kwenye wakati mzito sana. Ghafla mama wa samaki akafika nikasikia sauti nikiwa nimeinama inasema "kaka samahani naomba 2000 nataka kushuka" lakini kwa kuwa nilikuwa kwenye msongo mkubwa wa mawazo wa kupotelewa pesa plus njaa sikuweza kumjibu zaidi ya kukaa kimya nikiwa nimeinamia siti, yule mama nikasikia analalama we mkaka nataka kushuka mbona hunijibu nataka pesa yangu aliongea kwa sauti ya radi yenye mrindimo nadhani alikuwa mndengereko wa rufiji huyu. Ilinibidi niamke kukumbana na fedheha nikamjibu kuwa mama sio tu 2000 hapa sina hata Mia pesa zangu zote sizioni maana zilikuwa kwenye pochi. Yule mama nikaona ameshika kola yangu nilikuwa nimevaa Shati jeupe akasema hunijui sikujui nilikupa samaki wakiwa wazuri naomba pesa yangu natafuta riziki sikuja kuimba injili.

Aliponishika Ile kola yule babu wa pembeni yangu nikaona anamuongelesha kilugha sikuelewa ni lugha gani baada ya maongezi mengi yenye kerere nikaona yule babu kaingia mfukoni akampa mama wa samaki shilingi 1000 nasio 2000 yule mama alipopokea nikaona kaachia Shati langu akachukua beseni kwa hasira akaenda kukaa mbele karibu na dreva pale chini yake huwa hakunaga kiti ila unaweza kaa pia hususani hawa wachuuzi wa kupanda na kushuka. Yule babu akiniambia kijana kuwa na Amani nimempa pesa yake nikasema asante sana halafu nikakaa kimya. Bus likiwa kwenye mwendo kasi huku upepo unapukuta kufungua dirisha niangalie nje nikaona kumbe usiku umeingia. Nikasema hapa nikikaa kimya sitapata msaada wowote ikabidi nimwambie mzee tuliekuwa tumekaa nae hali halisi, yule mzee akanipa pole Kisha nikamwambia mm huku niendako ni mgeni sina mtu yoyote ninae mjua nimekuja kutafuta maisha. Yule mzee akasema hata yeye anaenda kwa mtoto wake ameoa juzi Kati kwahiyo anaenda kuwasalimia na kule ni mgeni pia ila ingekuwa ni somanga angeongea mengine. Nikasema hapa nimebugi hii safari ni ngumu kuliko ya wana wa Israel kuitafuta kanani.

Saa mbili usiku tukaingia stend ndogo hivi niyavumbi nikasikia konda anasema haya jamani wa kilwa kivinje teremkeni. Yule mzee akaniaga akashuka nikabaki peke angu. Nikiwa Sina hata Mia mfukoni saa mbili na nusu usiku bus likaiacha kilwa kivinje safari ya kuelekea kilwa masoko ikaanza. Nikawa najiuliza ivi nikishafika pale stend halafu naelekea wapi usiku huu, Shati lenyewe yule mama alilikunjakunja kalipaka mishombo ya samaki limechafuka siwataniona kibaka?. Nikasema sawa wacha tufike itafahamika tu maadam niendako ni watanzania wenzangu. Saa tatu na nusu hivi tukaingia kilwa masoko nandomwisho wa safari. Pale Kuna bodaboda nyingi vijana wa pale hawalali wakajazana kwenye mlango wa bus kutafuta abiria mkono uende kinywani, nikashuka nikapewa begi langu kwenye buti nikalibeba, bodaboda kila baada ya dakika mbili wanakuja vipi bro boda nawajibu Sina haja ya usafiri lakini wanarudi tena kuniuliza mwishowe nikatoka kwa mguu pale stend nikajisogeza pembeni kidogo nikakuta Kuna prutable wanacheza hapo ikawa kama ni saa nne na nusu hivi.

Nikiwa na begi langu kama mkimbizi mida ya saa tano yule mwenye prutable akaja akasema jamani nafunga nendeni mkalale, nikasema hapa sasa kazi ipo, nikaona wale vijana wanapita Kwangu kuniuliza tena kama ni abiria nikawa na jitahidi kuwa jibu kistaarabu kwamba siendi kokote ila ingekuwa kwetu mpwayungu wangeshapokea matusi, mwishowe wote wakaondoka. Sasa tukabaki mimi na yule mwenye prutable japo niliona ana kibanda cha vinywaji pia maana alikuwa anafunga. Anataka kuondoka tu nikamuwahi akasema wewe nani nikajieleza matukio yote yaliyotokea yule kijana akasema hapana siwezi kukupa msaada wowote maana saizi binadamu tumegeuka nyoka. Ikabidi aniache tena akasema nitoke pale sehemu yake ya kazi kwa ajili ya usalama wa mali zake. Ikawa ni saa sita usiku giza tororo Sina PA kwenda Sina hata Mia njaa inanipukuta, usingizi nikawa Sina kabisa kutokana na mashambulizi ya misukosuko.

Nikaona kukaa maeneo yale hapafai Sasa naenda wapi?? Kwa mbali nikasikia mziki unaunguruma nikasema huko huko naenda nikafata Ile sauti Kuna barabara ya mchanga ikawa inaenda mpaka kwenye huko mziki kumbe Kuna disco na watoto wa kike mle japo siwezi Sema ni watoto wakali maana hata hamu ya kuangalia Kuna nini humo sikuwanayo kabisa. Ile nafika tu disco ikawa imezimwa nikaona lundo la watu wa naondoka na vidada poa ila kwa muonekano vile vidada poa vimekubuhu vimefanya sana umalaya kimboka vikichuja vinaenda huko pembeni ya mji kuwa kamata maboya. Kila mtu alikuwa ananishangaa jinsi nilivyo maana wanajiuliza huyu wa wapi usiku huu na mbegi nzito halafu Shati haitamaniki sura ngeni?. Saa saba kamili kwenye Ile disco hapa kuwa na mtu tena. Sasa tukabaki mm na wale wahudumu wa ule ukumbi wa disco nikawafata nikawaambia maswahibu yangu wakasema msaada peke watakaonipa nikunipeleka kituo cha polisi maana pale naweza Pata pakujistiri.

Nikasema kwani kituo cha polisi Kuna vitanda vya kulala wageni, wakacheka kidogo huku wakiendelea kupanga maspika yao na manyaya Kisha wakajibu kuwa polisi hawawezi kukosa pakukuweka maana ni binadamu kama mm, ila wao kunipokea ngumu kwa sababu juzi Kati Kuna tukio kubwa lilitokea la mtu kuuawa kwenye njumba yake kwahiyo polisi kila siku wanasisitiza tusipokee wageni ambao hatuwafahamu. Nikaona kwenda kuomba msaada polisi huo ni uongo ngoja niendelee kuwashawishi tu. Nikawaambia kama hawana Imani na mimi nitawakabidhi hata vyeti vyangu vya shule bado walikataa wakafunga wakaondoka nikabaki peke angu. Ikawa ni saa saba na nusu hivi. Giza likawa totoro sauti pekee nilizoziskia ni za chura kwenye madibwi na bodaboda za wahuni wasiolala usiku.

Kukaa pale niliogopa sana maana lile eneo limejitenga nikasema hapa nirudi stend nilipotoka, nikafika stend Ile kufika tu Kuna vijana watatu nikakuta wamekaa kwenye bench moja hivi pembeni ya barabara ya lami karibu na stend nikasema hapo powa ngoja niende tupige story mpaka asubuhi. Nilipo fika nikasalimia wakasema mbona upo na begi usiku nikasema kawaida tu ila asubuhi nataka niende Dar kwa hiyo nasafiri ~niliwadanganya maana sio kila mtu wa kumwambia unayoyapitia kwa mda huo utaonekana mwehu angalia na nature ya Eneo. Kuna kijamaa flani hivi ni cheupe kirefu kiasi afu chembamba kikaja pale kikasema oya huyu Nani mazee mbona sura ngeni wakamjibu lakini kile kijamaa nikishari sana nadhani kakajua huyu nimeokota Leo. Kuna jamaa mmoja umri umeenda kiasi akasema mwache unamuhoji wa nini kila mtu na maisha yake. Yule jamaa akavutwa pembeni na hiki kushkaji kigomvi akapewa nadhani ilikuwa bangi Ile jamaa nikasikia anasema shukurani mtu wangu ngoja nikalale. Kumbe aliambiwa chukua bangi huyu mtu tuachie kwa nilivyohisi.

Wakabaki watatu Sasa hawa wote nilikuja kugundua ni vibaka wanaosumbua mji baadae nitaeleza. Kile kijama kikaja kilikuwa na bodaboda mbaya zaidi haina plate number. Kakasema ebu nitoe buku ten nakurudishia. Nikajisemea moyoni kumbe huku pesa ni rahisi kiasi hiki? Yani hata simjui tayari nimpe pesa lakini kwa kuwa nimejua hawana Nia nzuri ngoja tuone. Nikasema Sina hata Mia jamaa wenzake wawili wakakaa nyuma yangu wakasema nyie ndo wezi mnakuja kilwa kuiba mnatoroka usiku huu saa saba Kuna bus gani la Dar ebu fungua Hilo beg. Nikafungua begi haraka maana sura zao hata maongezi yalibadilika ghafla, nilitamani mda huo hata Gari ya polisi ipite lakini Hola sikuskia hata sauti za pikipiki. Majamaa wakasachi begi walipoona hamna kitu wakaona vyeti vyangu vya form 4 na form six. Kile kijamaa kikawaambia oyaaaa chukua hivyo vyeti pesa atatoa. Niliposkia hivyo nikasema bora mniue cheti hakitoki Ile nashangaa nikaona kile kijamaa kimetoa kisu kikasema hiki kisu kina rangi gani nikajibu haraka nyekundu. Kikasema basi hatuogopi kukutoboa macho maana sisi hatuui sisi tunakupa ukilema tu. Jamani watu wa kilwa mtanisamehe ila mna roho mbaya Sana.
Ile nataka kuzuia begi langu kile kijama kikasogeza kisu kwenye jicho langu.

....... I naendelea........
Kwann usingeenda kwa mwenyekiti
 
------SEHEMU YA SITA - - - - - -

Nilipoangalia mazingira ya yule jamaa mlevi nikaona amekojoa maeneo yale na yale maboksi ya kulalia yamekojolewa, kwa kuwa nilikuwa na usingizi sana nasiwezi kulala kwenye michanga ilinibidi nichague Kati ya haya "kulala kwenye mikojo au kutokulala kabisa".. Nikasema mm nalala maana hakuna namna Ile navua begi mgongoni niliweke ndani nakuta limefunguliwa zipu na baadhi ya documents zilizokuwa kwenye bahasha ikiwemo vyeti vya shule na cha kuzaliwa hamna pamoja na nguo zilizokuwa juu hakuna pia. Hali hii iliniokoa kulala kwenye mikojo maana nilikosa usingizi moja kwa moja huku nikijisemea moyoni mpwayungu village umekwisha. Nilisogea pembeni kidogo tu nikaka chini kama gunia puuuh! Nilitulia kama dakika kadhaa huku sijui hatima yangu maana mambo yalishaharibika. Ikawa kumepambazuka ni saa kumi na moja sasa wengine wanaenda kuswali wengine wanaletwa stend kwenda Dar na maeneo mengineyo. Sasa lile jamaa Levi lililokuwa linatoa mizigo likiwa nyuma ya bus kule nikasikia linatukana, oyaaa mpumbav gani huyu ametupatupa manguo yake huku niliposkia tu nilizunguka chapu kufika pale dah [emoji22] sikuweza kuamini kuo zangu zipo pale japo zimekanyagwa hazitamaniki pamoja na bahasha ya vyeti vyangu, kumbe kipindi tunapigana na wale vibaka zile kurupushani zilifanya zipu ya begi ijifungue nguo na vitu vingine vikadondoka nakwakuwa tulikuwa kwenye body defense hakuna aliyejali wala kuona nguo na vyeti vikidondoka mpaka wale wahuni wanakimbia kwenda kujificha Mungu aliepusha hawakuviona pia.

Ikawa asubuhi saa kumi na mbili watu wa Kawa wengi kiasi mazingira hayo, wauza supu na Chai, shoe shine, bodaboda, abiria, waenda kazini, wasio na kazi, wafanyabiashara na wachuuzi, kila Aina ya kundi mji ulionekana. Kuji kujitazana uso ni mchafu suruwali chafu Shati ndousisema tena ilikuwa nyeupe Ikawa haina rangi, maeneo ya shingo nilichubuliwa na yule kibaka mwingine na kucha zake nikawa nina michirizi tu usoni, nguo zangu za kubadilisha zimekanyagwa ni chafu, sina simu, Sina hata Mia, Sina ninaemjua, tumbo halina kitu kabisa. Ajabu ni kuwa kila aliepita karibu yangu hakuacha kunitazama huku wengine nilisikia wanasema "" WANAJIFANYAGA MATAHILA KUMBE USALAMA WA TAIFA "" nikijisemea kumbe mpaka sasa muonekano wangu nishakuwa kama chizi? Sikuweza kulaumu maana kwa muonekano kiukweli hakili yangu haikuwa Sawa tena nilikuwa nimechafuka kupita maelezo halafu nina njaa nikawa kama natetemeka na wakiona ule mtetemo mpaka mdomo unavibrate halafu nipo rafu kwanzia unyayo mpaka nywele automatically wanajua ni Chizi.

Sasa vikwazo vyote vya kuitwa punguwani nikageuza kuwa fursa. Nilienda kwa mama mmoja hivi anauza chai na tangawizi mm nikaenda kukaa bila kusalimia njaa imeniponda kwelikweli. Sasa wateja waliokuwa pale mmoja wao akamaliza kunywa akampa mama 2000 akarudishiwa 1200 nadhani alikunywa Chai ya 800 lakini yule jamaa hakupokea chenji akasema mpe huyo kijana Chai kwenye hiyo chenji iliyobaki. Yule mama akatabasamu akasema Sawa lakini huku mm nikijifanya sijui chochote vinginevyo watajua naekti. Shukurani za pekee mungu ampe utajiri yule jamaa lakini Uhuni alionifanyia yule mama muuza Chai sitasahau maana katika 1200 ilobaki alinipa maandazi mawili tu na Chai ambapo jumla ni kama 600 tu. Nikijisemea moyoni huyu alieninunulia Chai sio mzawa, wazawa ni huyu mama wanaroho ya nyoka tena wanaweza kukuua. Kwakuwa nilikuwa mgeni na hali ya kimwili mda huo sikuweza kuleta ligi maana ingekuwa vituko.

Nikanywa Chai inaisha yote ila niliona mabadiliko nikawa najihisi niko Sawa. Akili ya kupotelewa na fedha ikarudi tena nikaona ni bora hili swala mda huu nilipoti office za bus. Kwakuwa nipo hapohapo nikaingia ndani nilipo fika pale nikamkuta yule mlinzi, mkaka mmoja anakatisha tiketi na wateja. Mwonekano wangu uliwafanya hata wasinifatilie kwani walijua huyu sio mteja ni tahila, nikasikia yule mkatishatiketi anamwambia mlinzi ebu mtoeni huyo nje nilistaajabu kwakweli kwahiyo yule mlinzi Kwakuwa nimemsumbua tangu usiku hakunitoa kwa upole tena ila ilikuwa ni shuruti naukizingatia amri ni ya boss hataki kibarua kiote nyasi. Kulikuwa Kuna rungu pembeni akashika nakunikong'ota begani na mgongoni akanipiga tanganyika jeck uelekeo ni nje tena mbali na mazingira yale huku nikisikia sauti za watu jamani mwacheni tu, mwacheni jamani hata sisi hatujui kesho yetu, hata wewe unaweza kuwa chizi mda wowote huku mlinzi akisema hili limenisumbua tangu usiku.

Akaenda kunisukuma kandokando ya dampo moja hivi lipo sokoni, pale stend na soko LA kilwa vimepakana tu. Nikakaa kidogo nikasema ivi ni kweli au illusion??. Haya matukio niyakweli? Nikasema hapana let me be serious. Sasa nikaamka kwenye lile dampo nikaenda tena kwenye zile office kufika pale kumbe yule mlinzi akawa ametoka kidogo nikaingia yule jamaa alienifukuza akataka kuleta za kuleta nikamwambia nina yanayonisibu nahitaji kuzungumza na office nikaona mwarabu mmoja hivi yeye alikuwa dreva kipindi nakuja kilwa akasema ebu mwacheni aongee. Nikajisemea moyoni "this is the golden chance Iam going to talk each and every thing". Nilitiririka nikaeleza Sakata la wallet nikaja la vibaka na chanzo cha Kuja kilwa kimsingi ilinibidi niwe muwazi. Yule mwarabu na wengine pale walinipa pole nyingi sana, kwa Mara ya kwanza namuona mwarabu mwenye utu.

Wote nikasikia kumbe ni mkaka na hakili zake tu jamani. Yule mwarabu akasema kijana swala la kupoteza wallet yako ndani ya bus letu pole sana ila sisi hatuwajibiki kwa hilo kwasababu hatuwezi kulinda kitu ambacho hatujakabiziwa. Wallet ipo kwenye mfuko sisi ofisi tunaionaje? Kwahiyo sisi hatuhusiki ila chakukusaidia wewe nenda kituo cha polisi utapata msaada. Nilichoka sana uso ukawa mzito saizi mama aliefiwa na mtoto wake wa pekee. Sina hili wala lile nikaona yule mwarabu kaingiza mkono mfukoni kachomoa 20000 akanipa akasema niondoke au wanisaidie kunipeleka polisi kama sipajui mm nikawaambia nitaenda mwenyewe, Ile nataka kuondoka pia Kuna mama mmoja hivi nadhani alikuwa abiria akasema kaka chukua hii elfu kumi itakusaidia nilimpa asante nyingi sana ila siku piga goti. Ikabidi hivyo hivyo nilivyo nikapotea mazingira yale Ile pesa ikiwa imewekewa ulinzi wa kiwango cha pentagon.

Nilikuwa mchafu sana utofauti wa mimi na nguruwe ni majina tu ila mwonekano ulikuwa similar, nikaona sio ustarabu kukaa hivi ngoja nitafute chaka la kusafisha ngozi yangu money can't make me disrespected nikazunguka nyuma kidogo Kuna kigest flani hivi kufika pale nikanawa kwa maji tiririka huku wahudumu wakinishangaa mwingine akasema mwacheni tu anawe mikono yake jamani akimaliza tutabadilisha maji. Yani natia kinyaa kiasi cha wao maji yatakayobaki kwenye ndoo watamwaga [emoji22]. Nikaenda walipo nikawaambia uhalisia mm sio chizi Ikabidi ni waambie mkasa wa usiku wakacheka wakasema pole mkaka tusamehe tukajua mengine. Nikawaambia kama naweza Pata msaada wakuoga wakasema Sawa nikaonyeshewa Bafu nikapewa kipande cha sabuni ya Eva nikaoga. Nguo zangu nikabadilisha nikachukua ambazo chache hazikudondoka usiku ule wa purukushani ila zimejikunja sana wale wadada wakacheka afu wakaniambia nizivue wa nipigie pasi. Niliflahi kwa kweli niliwapa wakazinyoosha nikavaa nikiwa nimeng'aa.

------inaendelea usichoke - - - - -
 
------SEHEMU YA SITA - - - - - -

Nilipoangalia mazingira ya yule jamaa mlevi nikaona amekojoa maeneo yale na yale maboksi ya kulalia yamekojolewa, kwa kuwa nilikuwa na usingizi sana nasiwezi kulala kwenye michanga ilinibidi nichague Kati ya haya "kulala kwenye mikojo au kutokulala kabisa".. Nikasema mm nalala maana hakuna namna Ile navua begi mgongoni niliweke ndani nakuta limefunguliwa zipu na baadhi ya documents zilizokuwa kwenye bahasha ikiwemo vyeti vya shule na cha kuzaliwa hamna pamoja na nguo zilizokuwa juu hakuna pia. Hali hii iliniokoa kulala kwenye mikojo maana nilikosa usingizi moja kwa moja huku nikijisemea moyoni mpwayungu village umekwisha. Nilisogea pembeni kidogo tu nikaka chini kama gunia puuuh! Nilitulia kama dakika kadhaa huku sijui hatima yangu maana mambo yalishaharibika. Ikawa kumepambazuka ni saa kumi na moja sasa wengine wanaenda kuswali wengine wanaletwa stend kwenda Dar na maeneo mengineyo. Sasa lile jamaa Levi lililokuwa linatoa mizigo likiwa nyuma ya bus kule nikasikia linatukana, oyaaa mpumbav gani huyu ametupatupa manguo yake huku niliposkia tu nilizunguka chapu kufika pale dah [emoji22] sikuweza kuamini kuo zangu zipo pale japo zimekanyagwa hazitamaniki pamoja na bahasha ya vyeti vyangu, kumbe kipindi tunapigana na wale vibaka zile kurupushani zilifanya zipu ya begi ijifungue nguo na vitu vingine vikadondoka nakwakuwa tulikuwa kwenye body defense hakuna aliyejali wala kuona nguo na vyeti vikidondoka mpaka wale wahuni wanakimbia kwenda kujificha Mungu aliepusha hawakuviona pia.

Ikawa asubuhi saa kumi na mbili watu wa Kawa wengi kiasi mazingira hayo, wauza supu na Chai, shoe shine, bodaboda, abiria, waenda kazini, wasio na kazi, wafanyabiashara na wachuuzi, kila Aina ya kundi mji ulionekana. Kuji kujitazana uso ni mchafu suruwali chafu Shati ndousisema tena ilikuwa nyeupe Ikawa haina rangi, maeneo ya shingo nilichubuliwa na yule kibaka mwingine na kucha zake nikawa nina michirizi tu usoni, nguo zangu za kubadilisha zimekanyagwa ni chafu, sina simu, Sina hata Mia, Sina ninaemjua, tumbo halina kitu kabisa. Ajabu ni kuwa kila aliepita karibu yangu hakuacha kunitazama huku wengine nilisikia wanasema "" WANAJIFANYAGA MATAHILA KUMBE USALAMA WA TAIFA "" nikijisemea kumbe mpaka sasa muonekano wangu nishakuwa kama chizi? Sikuweza kulaumu maana kwa muonekano kiukweli hakili yangu haikuwa Sawa tena nilikuwa nimechafuka kupita maelezo halafu nina njaa nikawa kama natetemeka na wakiona ule mtetemo mpaka mdomo unavibrate halafu nipo rafu kwanzia unyayo mpaka nywele automatically wanajua ni Chizi.

Sasa vikwazo vyote vya kuitwa punguwani nikageuza kuwa fursa. Nilienda kwa mama mmoja hivi anauza chai na tangawizi mm nikaenda kukaa bila kusalimia njaa imeniponda kwelikweli. Sasa wateja waliokuwa pale mmoja wao akamaliza kunywa akampa mama 2000 akarudishiwa 1200 nadhani alikunywa Chai ya 800 lakini yule jamaa hakupokea chenji akasema mpe huyo kijana Chai kwenye hiyo chenji iliyobaki. Yule mama akatabasamu akasema Sawa lakini huku mm nikijifanya sijui chochote vinginevyo watajua naekti. Shukurani za pekee mungu ampe utajiri yule jamaa lakini Uhuni alionifanyia yule mama muuza Chai sitasahau maana katika 1200 ilobaki alinipa maandazi mawili tu na Chai ambapo jumla ni kama 600 tu. Nikijisemea moyoni huyu alieninunulia Chai sio mzawa, wazawa ni huyu mama wanaroho ya nyoka tena wanaweza kukuua. Kwakuwa nilikuwa mgeni na hali ya kimwili mda huo sikuweza kuleta ligi maana ingekuwa vituko.

Nikanywa Chai inaisha yote ila niliona mabadiliko nikawa najihisi niko Sawa. Akili ya kupotelewa na fedha ikarudi tena nikaona ni bora hili swala mda huu nilipoti office za bus. Kwakuwa nipo hapohapo nikaingia ndani nilipo fika pale nikamkuta yule mlinzi, mkaka mmoja anakatisha tiketi na wateja. Mwonekano wangu uliwafanya hata wasinifatilie kwani walijua huyu sio mteja ni tahila, nikasikia yule mkatishatiketi anamwambia mlinzi ebu mtoeni huyo nje nilistaajabu kwakweli kwahiyo yule mlinzi Kwakuwa nimemsumbua tangu usiku hakunitoa kwa upole tena ila ilikuwa ni shuruti naukizingatia amri ni ya boss hataki kibarua kiote nyasi. Kulikuwa Kuna rungu pembeni akashika nakunikong'ota begani na mgongoni akanipiga tanganyika jeck uelekeo ni nje tena mbali na mazingira yale huku nikisikia sauti za watu jamani mwacheni tu, mwacheni jamani hata sisi hatujui kesho yetu, hata wewe unaweza kuwa chizi mda wowote huku mlinzi akisema hili limenisumbua tangu usiku.

Akaenda kunisukuma kandokando ya dampo moja hivi lipo sokoni, pale stend na soko LA kilwa vimepakana tu. Nikakaa kidogo nikasema ivi ni kweli au illusion??. Haya matukio niyakweli? Nikasema hapana let me be serious. Sasa nikaamka kwenye lile dampo nikaenda tena kwenye zile office kufika pale kumbe yule mlinzi akawa ametoka kidogo nikaingia yule jamaa alienifukuza akataka kuleta za kuleta nikamwambia nina yanayonisibu nahitaji kuzungumza na office nikaona mwarabu mmoja hivi yeye alikuwa dreva kipindi nakuja kilwa akasema ebu mwacheni aongee. Nikajisemea moyoni "this is the golden chance Iam going to talk each and every thing". Nilitiririka nikaeleza Sakata la wallet nikaja la vibaka na chanzo cha Kuja kilwa kimsingi ilinibidi niwe muwazi. Yule mwarabu na wengine pale walinipa pole nyingi sana, kwa Mara ya kwanza namuona mwarabu mwenye utu.

Wote nikasikia kumbe ni mkaka na hakili zake tu jamani. Yule mwarabu akasema kijana swala la kupoteza wallet yako ndani ya bus letu pole sana ila sisi hatuwajibiki kwa hilo kwasababu hatuwezi kulinda kitu ambacho hatujakabiziwa. Wallet ipo kwenye mfuko sisi ofisi tunaionaje? Kwahiyo sisi hatuhusiki ila chakukusaidia wewe nenda kituo cha polisi utapata msaada. Nilichoka sana uso ukawa mzito saizi mama aliefiwa na mtoto wake wa pekee. Sina hili wala lile nikaona yule mwarabu kaingiza mkono mfukoni kachomoa 20000 akanipa akasema niondoke au wanisaidie kunipeleka polisi kama sipajui mm nikawaambia nitaenda mwenyewe, Ile nataka kuondoka pia Kuna mama mmoja hivi nadhani alikuwa abiria akasema kaka chukua hii elfu kumi itakusaidia nilimpa asante nyingi sana ila siku piga goti. Ikabidi hivyo hivyo nilivyo nikapotea mazingira yale Ile pesa ikiwa imewekewa ulinzi wa kiwango cha pentagon.

Nilikuwa mchafu sana utofauti wa mimi na nguruwe ni majina tu ila mwonekano ulikuwa similar, nikaona sio ustarabu kukaa hivi ngoja nitafute chaka la kusafisha ngozi yangu money can't make me disrespected nikazunguka nyuma kidogo Kuna kigest flani hivi kufika pale nikanawa kwa maji tiririka huku wahudumu wakinishangaa mwingine akasema mwacheni tu anawe mikono yake jamani akimaliza tutabadilisha maji. Yani natia kinyaa kiasi cha wao maji yatakayobaki kwenye ndoo watamwaga [emoji22]. Nikaenda walipo nikawaambia uhalisia mm sio chizi Ikabidi ni waambie mkasa wa usiku wakacheka wakasema pole mkaka tusamehe tukajua mengine. Nikawaambia kama naweza Pata msaada wakuoga wakasema Sawa nikaonyeshewa Bafu nikapewa kipande cha sabuni ya Eva nikaoga. Nguo zangu nikabadilisha nikachukua ambazo chache hazikudondoka usiku ule wa purukushani ila zimejikunja sana wale wadada wakacheka afu wakaniambia nizivue wa nipigie pasi. Niliflahi kwa kweli niliwapa wakazinyoosha nikavaa nikiwa nimeng'aa.

------inaendelea usichoke - - - - -
Kwanini kipindi una minguo michafu na una muonekano wa chizi hukubadilisha nguo ili uitengeneze muonekano mzuri ili hata ukitaka kuongea na watu wakuone sio chizi ila ukaamua uje kubadilisha baadae ulipoenda kuoga? Huoni kwamba unaondoa hisia za waodhani hii ni stori ya kweli kwa huko kupanga kwako matukio?
 
Nyizi kama hizi zilipotea sana humu, [emoji22] nakumbuka stori kama hizi alikuwa nazo KITOABU, na jamaa mmoja nime msahau jina alisafiri kwenda South Africa [emoji1221] miaka hiyo aka kutana na pisi kali Tshepiso kama sija kosea [emoji38] yaani Jf kuna raha sana.
 
Kwanini kipindi una minguo michafu na una muonekano wa chizi hukubadilisha nguo ili uitengeneze muonekano mzuri ili hata ukitaka kuongea na watu wakuone sio chizi ila ukaamua uje kubadilisha baadae ulipoenda kuoga? Huoni kwamba unaondoa hisia za waodhani hii ni stori ya kweli kwa huko kupanga kwako matukio?
Madafaka. Ndio uquote uzi wote
 
Nyizi kama hizi zilipotea sana humu, [emoji22] nakumbuka stori kama hizi alikuwa nazo KITOABU, na jamaa mmoja nime msahau jina alisafiri kwenda South Africa [emoji1221] miaka hiyo aka kutana na pisi kali Tshepiso kama sija kosea [emoji38] yaani Jf kuna raha sana.
Umemsahau HOLY HOLM na mkaka wa mzee Nchibaronda
 
Back
Top Bottom