Sitosahau siku niliyotishiwa bunduki na baba!

Sitosahau siku niliyotishiwa bunduki na baba!

Mtoto sio kupiga tu mpe na elimu ya maisha pia ndio elimu bora kuliko zote.

Wazazi weeeeengi hawakai na watoto wao, kuwapa nasa za ukweli wa maisha. Unaweza kudunda mtoto ukaishia kumtengenezea nidhamu ya uoga tu, awapo na wewe heshima za kifalme ila usipokuwepo anakua muhuni huni tu.

Lazima umsome mtoto wako tabia zingine ni za kurithi huenda hata ametoa kwako DNA zinasoma hivi vitu pia, hivyo lazima umsaidie kuondokana nazo.

Ukweli usiofichika wa kifalsafa mlezi mzuri ni baba, ila mama ni huruma na mapenzi, akikuchapa baada ya muda anaanza kukuchombeza polee mwanangu usirudie tena ehh... Ila baba anakufokonyoa na hamsemeshani mpaka kesho na amri za kikamanda kamanda tu.

Nakumbuka baba aliwahi kunipiga kofi moja hilo aisee nilihisima zimeruka huko kichwani,.. kama dakika 5 hivi sikua najielewa nini kimetokea. Ndio ilikua mara ya kwanza kunipiga kutoka najitambua.
 
Mkuu sioni kama kuna kitu cha kulipiza hapo, na inabidi umuombe mzee wako akufundishe kuwa na strength aliyonayo. Kilichotokea ni kwamba mzee wako aliona huyo jamaa ni mjinga kama wajinga wengine na ndio maana hakuangaika nae. Unadhazani kwa umri aliofikisha amesha tukanwa na wangapi?
Mambo mengine ni kuyadharua tu, ukilipiza na wewe unaonekana ni mjinga pia.

Perfect sana!
 
Watoto wa mboga 7 fc ni changamoto.

Mboga 7 hata si issue kivile when it comes kwenye malezi ya mtoto/watoto, hasa nyakati hizi!!

Karibu uswahilini tunakoshindia ugali tembele kutwa nzima mara moja...saa kumi jioni!!

Panya road wanatoka familia zipi kwa asilimia kubwa?!?

A Human is a complex being!
 
pole mkuu watu wa Dini wanasema samehe Saba mara sabini
Ila kwangu ukinifanyia ubaya mara Moja nakulipa mara Saba yake
Ila Mimi nakuapia hiyo jamaa ningemlia taiming ningemgonga vitasaaa mpaka maji aite mma pumbaf Hawa jamaa ukiwachekea Sana wanajitoaga ufahamu na kujiona malegend hivi
Narudia huyo boya angemtukana mshua wangu pale pale angechezea kipigo Cha mbwa Koko Tena kile Cha kustukiza anatolewa roki Kama general Mo Power!

Maajabu ni kwamba ungepigwa wewe mpaka uchakae!

Haijalishi action ya mtu kwako ama mbele yako, kikubwa ni Re-action yako kwao!
 
Afya ya akili ni tatizo kubwa sana bongo maana wengi hukuzwa wakiamini matumizi ya nguvu ndio njia pekee ya kumshape mtoto. Mwisho wa siku tunapata watu ambao kimaisha wapo fresh ila kihisia na kiakili wameathirika sanaa na hawajui

unashangaa upo kwenye usafiri wa umma au popote pale, unakuta kitu kidogo tu, mtu anapanic na kuvimba kuwa "atapigana". Yaani mtu anategemea misuli zaidi maana ndo ina nguvu ila kihisia na kiakili mwepesi sana



Pengine 90% of us ni Sadists due to the nature of our up bringing!?

Na hiki ndio kikwazo chetu halisi?? Is this the root of our selfishness?!?
 
Wazee wengi kujitafutia matatizo unamkokia mwanao silaha[emoji1787][emoji1787][emoji1787]ikichomoka utaiambia nini jamuhuri
nilimuona baba mkatili sana, sikuwa karibu naye kabisa
 
Mtoto sio kupiga tu mpe na elimu ya maisha pia ndio elimu bora kuliko zote.

Wazazi weeeeengi hawakai na watoto wao, kuwapa nasa za ukweli wa maisha. Unaweza kudunda mtoto ukaishia kumtengenezea nidhamu ya uoga tu, awapo na wewe heshima za kifalme ila usipokuwepo anakua muhuni huni tu.

Lazima umsome mtoto wako tabia zingine ni za kurithi huenda hata ametoa kwako DNA zinasoma hivi vitu pia, hivyo lazima umsaidie kuondokana nazo.

Ukweli usiofichika wa kifalsafa mlezi mzuri ni baba, ila mama ni huruma na mapenzi, akikuchapa baada ya muda anaanza kukuchombeza polee mwanangu usirudie tena ehh... Ila baba anakufokonyoa na hamsemeshani mpaka kesho na amri za kikamanda kamanda tu.

Nakumbuka baba aliwahi kunipiga kofi moja hilo aisee nilihisima zimeruka huko kichwani,.. kama dakika 5 hivi sikua najielewa nini kimetokea. Ndio ilikua mara ya kwanza kunipiga kutoka najitambua.
kwahiyo mzee wako alikupiga banzi mara moja ukazimia! 😆😆
 
The fact that you remember it...in details kama hivi, it means it made a Dent in the Line of your life!

Hilo ni kovu!

The good part is you decided to embrace it positively. Safi!
makovu kwa mwanaume ni kawaida sometimes, positive optimism ndiyo kitu muhimu when it comes to family matter
 
Ilikuwa hivi...
Muda mrefu sana yapata miaka 10 hiyo siku nilikuwa nacheza pool table mtaani, huo mchezo unaitwa "shamkware." Ni kamari na una majina mengi sana huu mchezo pia mnaweza cheza watu wawili au zaidi.

Katika kucheza na kupiga mahesabu makali mwisho wa game mshindi nlikuwa mimi. kwenda kuchukua pesa nlizoshinda ghafla muona baba ananitazama kwa ukali kinoma!
ikanibidi niiache ile pesa niondoke kinyonge nikijua tayari umeshakuwa msala!

Kurudi nyumbani dakika tano nyingi baba naye huyo! nilipigwa kila aina ya kipigo, ngumi, makofi, mateke na mkanda mwisho wa siku akachukua bunduki aina ya gobole na kulikoki kuelekeza kwangu...! akanipiga mkwara mzito sana na kusema "nitakuua nikikuona unacheza michezo ya kipuuzi na sioni faida ya kuwa na kijana mjinga ndani ya nyumba yangu."
niliogopa sana na tangu hiyo siku mpaka kesho pool table sina mzuka nao kabisa.

Baba amenipa vitu bora maishani, muda wake, kujali kwake na upendo wake. Nafurahi sana kuwa nae katika maisha yangu.

He is my superman.
Nia yake ilikuwa nzuri, japo imefanikiwa kwako lakini njia aliyoitumia kutishia kukuua ni mbaya Sana. Usije ukaitumia hii njia kwa mwanao. Inawea kusababisha madhara makubwa
 
Nia yake ilikuwa nzuri, japo imefanikiwa kwako lakini njia aliyoitumia kutishia kukuua ni mbaya Sana. Usije ukaitumia hii njia kwa mwanao. Inawea kusababisha madhara makubwa
nimekuelewa sana 🙏🏾
 
Pengine 90% of us ni Sadists due to the nature of our up bringing!?

Na hiki ndio kikwazo chetu halisi?? Is this the root of our selfishness?!?
kwa asilimia kubwa, kulelewa with emptiness of love or the one expressed in a wrong form

Japo sometimes kuna wale hufanya hivyo lakini bado hurudi nyuma na kuwawekea mazingira bora watoto wao. Kila kitu ni kizuri kikiwa na mipaka na kiasi
 
nafikiri afya ya akili Tanzania sio ugonjwa, wengi tumeathirika na hatujitambui
na mbaya zaidi tunaamini ni kawaida hadi pale zinapokuja impact ya hicho kitu mfano mtu akichukua maamuzi ya kujidhuru au kujiua wakati ni kitu kingepatiwa ufumbuzi kwa kuongea tu
 
Back
Top Bottom