Sitosahau UKIMWI ulichofanya mtaani kwetu. Nyie watu wa mapenzi kuweni makini

Sitosahau UKIMWI ulichofanya mtaani kwetu. Nyie watu wa mapenzi kuweni makini

Nakumbuka mitaa ya Kinyanambo mafinga tuliosoma huko ila hapakuwa na pisi
Umekaa mitaa choka sana sisi tulifikia mtaa unaitwa pipeline ndo kulikuwa uzunguni nyumba zina angalizika kwa mbali mwaka 96 nyumba nzuri kidogo na vihela kiukweli vilikuwepo tulitoka navyo dar vya uamisho wa maza tukapanga pipeline

baadae ndo tukamia huo mtaa wa mikosi wenye jina la herufi tu 2003...... mtaa wa kishua sana miaka hiyo ndo majanga yalipo anzia ... na kwanini nilijua majirani zetu wanakufa kwa ukimwi mama angu alikuwa nurse so alikuwa anapiga story tunasikiliza pia alikuwa anawauguza wakiwa hoi pale mafinga hospital...

pamoja na u unurse wake ukimwi ulikuja kum bamiza RIP my mumy...sitosahau ulivyoniangalia those dying eyes my god niliumia mara mwisho na kuniambia napenda harufu(perfume nilipaka) yako mwanangu nikasema bye ukajibu bye ndo maongezi yetu ya mwisho i will always love you ...leo naandika haya tribute yako pia kuwaasa wengine.... nikapanda basi la abc kurudi dar nikijua sito kuona tena ..kweli baada week tatu kaka angu alinipigia simu kusema mama is no more....

Tulificha kifo cha kusema kafa tu kwa presha ila ilikuwa AIDS .... hata wanangu nitakuja kuwasilimua hii story ya ule mtaa na hakuna hata sehemu.nimedanganya wala kusingizia maana maza alikuwa nurse so alijua hali za watu wengi wakilazwa

Mbaya zaidi mwaka 99 waliweka hodi maalumu la watu wa HIV so ukiwa huna hela afu una ukimwi unasekwa huko nadhani ile hodi walikuja kuivunja kuondoa unyanyapaaa ilikuwa chini kabisa kule

Nimesimulia story asilimia 5% tano tu ya majanga nilishuhudia mafinga why niliyajua mengi nilikuwa mtoto wa nurse tena mtoto pendwa.....

Asanteni wadau uzi wangu umesomwa na watu wengi naamini umetoa elimu kubwa kuhusu hili gonjwa ..

Wengine wanasema bora ukimwi kuliko kansa...ni hivi ukiwa na ukimwi hata kansa unapata kiu rahisi mno yaani ukimwi ni kama boss la magonjwa yote linapiga simu moja kansa njoo mara moja inakuja....likiamua kumwite chawa wake TB fasta tu.... bado kijana wake mkanda jeshi

Ukimwi ni boss wa magonjwa ukiamua inaweza sema basi tumvuruge awe kichaa unakuwa kichaa madaktar wanajua hili yaani ninaposema UKIMWI ni boss la magonjwa yote namaanisha linaweza sema tuletee vidonda tu utapata hadi ufe

Hizo kansa kwa watu wenye ukimwi ndo nyumbani maana boss wao ukimwi si anakuwepo ndani utashangaa unapata kidonda hakiponi then kansa

AIDS SIO MCHEZO
 
Kuna Mwalimu mmoja pale UD kwenye kota za Walimu alikuwa anakula kuku na mayai yake.

Alibahatika kupata Mabinti mapacha na walipoanza kupevuka tu aliwatenganisha kila mmoja kulala kwenye chumba chake, kumbe Lizee lilikuwa linakula zamu kwa zamu kwa hao Mabinti zake mbali na Mkewe.

"Mficha maradhi kifo humuumbua" hatimaye Doto alipata mimba, Mama Mzazi alipoona tu dalili zote ilibidi ambane Bintiye kwa maswali mengi kutaka majibu ya aliyemsababishia ujauzito, ingawa Binti alijitahidi sana kuficha ila mwishowe ilibidi amtaje Baba yake Mzazi ndiye mwenye ujauzito huo.

Mama akapandwa na presha ya ghafla ila alipomwambia Mumewe alikataa kata kata, Doto alianza kliniki na ndipo ilipobainika ana umeme alipokuwa anakaribia kujifungua, Kulwa naye ilibidi akapime baada ya kujua Mdogo wake Doto ana umeme halikadhalika naye alikutwa kaukwaa umeme. Mama Mzazi aliposikia hizo habari za umeme kwa Binti zake alipandwa na presha kubwa hadi kuzidiwa hatimaye Baba ilibidi atoroke kabisa home kujitenga na maswahibu hayo.

Mama Mzazi alifariki kwa presha, Baba Mzazi alichanganyikiwa naye hakukaa zaidi ya miaka miwili akavuta, Watoto mapacha walibaki Yatima wakiendelea kuishi kwa matumaini.

Dunia hadaa walimwengu Shujaa [emoji25]

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
dunia hii ina.mambo hata shetani atakataa hakueatuma kufanya hivyo
 
Verse 1

Nasikia raha jinsi nilivo star

Ni zaidi ya Robert De Niro

Nini top in Dar

Najukikana dunia nzima

Na kila kona hua natajwa langu jina

Sio tu watu wazima hadi watoto

Majina mengi a.k.a moto

A.k.a umeme a.k.a miwaya

A.k.a ngoma nzito isiyo na dawa

Ayaaaaah

Lakini sina ubaya

Na sibagui nchi za Africa nchi za Ulaya

Ni wengi tu nshawaondoa duniani

Na wengi bado nawatesa vitandani

Acha idadi kubwa ambao wapo safarini

Sijali mtoto wa kishua au unapoa uswahilini

Si mshajua nachozungumzia nini?

(UKIMWI UKIMWI UKIMWI)

Yeah a.k.a mimi

Natesa sana napokuingia mwilini

Akina gono kaswende wote baba yao mimi

Amini mi ndo kubwa la maadui

Na leo nakuja kwako usizuge kama hunijui

Halaa

RIP Genius CowBama
 
Kuna kijiji kimoja mkoa wa Kagera watu walikuwa na tabia ya kumegeana wake. Ngoma ilikuja ikaingia katika hiyo chain. Iliwatafuna wale wazee ni balaa. Ilikuwa inadondosha mmoja baada ya mwingine.

Hii kitu hapa Mkoa wa Njombe wilaya moja inaitwa Makete! Walikuwa na michezo ya kurithi Wajane na kulana wake na waume za watu! Walipukutika balaa
 
Sio mafinga tu HIV vijijini mkoa wa mara pia napo ipo ya kutosha

Nilienda huko kwa kazi ya mkataba hii miradi ya wadau wanao support wanaoishi na HIV aisee

Nimekoma kwenda huko katu sirudii

Binafsi nimetumia pep mara 2 pia nimezika wengi tu na kushuhudia vijana wadogo sna wakiteseka na hilo gonjwa
 
Mkuu tunapozungumzia ukimwi ishu hapa sio kufa, ila ishu ni kufa na ukimwi. Mtoa mada kana sentence anasema "kama hujawahi kumuona au kuuguza mgonjwa wa ukimwi huwezi kuelewa vizuri"
Ah kama mateso mbona watu wanateseka na cancer kisukari n.k.
 
Sio mafinga tu HIV vijijini mkoa wa mara pia napo ipo ya kutosha

Nilienda huko kwa kazi ya mkataba hii miradi ya wadau wanao support wanaoishi na HIV aisee

Nimekoma kwenda huko katu sirudii

Binafsi nimetumia pep mara 2 pia nimezika wengi tu na kushuhudia vijana wadogo sna wakiteseka na hilo gonjwa
Vijana pale kati panatuita jamani acheni tuu tufe na huu utamu wa mbususu
 
Kuna mwalimu mmoja wa kike (RIP) tukiwa tunakaa kota, siku za mwisho mwisho wa uhai wake alitoka nje ya nyumba yake mida ya saa 2:30 usiku hana nguo mwilini, akawa anazungumza kwa sauti kubwa,"vijana njooni muone jinsi ninavyoteseka. Msiache tamaa ziwaponze, mtakufa. Mimi nitakufa sio muda mrefu, njooni mjionee ninavyoteseka". Alikaa kama miezi 2 hivi akaaga dunia akiwa kwao Mbeya. Hiyo ilikuwa mwaka 2009 hivi
Daaah [emoji25]

Sent from my SM-G800F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom