Sitosahau yaliyonipata kijijini Kwamsisi

Sitosahau yaliyonipata kijijini Kwamsisi

Jina langu ninaitwa Soka (sio jina halisi) na kwetu ni huko Moshi uchagani. Nilisoma kwa shida na kufanikiwa kupata elimu ya Sekondari na kisha kujiunga na mafunzo ya ualimu katika chuo cha Marangu na kuhitimu kwa kutunukiwa Daraja A. Baada ya kuhitimu nilipangiwa kituo cha kazi ni huko Kwamsisi mkoani Tanga katika shule ya msingi Kwamsisi.

Nilivyofika nilishangazwa sana na mazingira ya shule na kijiji kwa ujumla. Kwanza nilipokelewa na wazee wa kijiji walio nionya sana kuhusu kile kijiji, wakaniambia niwe makini. Mzee mmoja aliyejitambulisha kama mzee Kingalu akanipatia kipande cha mfupa na kuniambia kuwa ni lazima nilale nacho ili niweze kuwa salama.

Niliogopa sana, nilipelekwa kwenye nyumba ya walimu ilikuwa ni nyumba ya bati iliyojengwa kwa kuta za miti na kusilibwa vizuri kwa udongo pia iliezekwa kwa bati. ilikuwa ni nyumba yenye hadhi kwa eneo hilo kwani asilimia kubwa ya nyumba za pale kijijini zilikuwa ni nyumba za udongo na kuezekwa na nyasi.

Siku ya kwanza nilipoingia shuleni ili niweze kutambulishwa nilishangazwa sana na mazingira yalivyokuwepo. Wanafunzi walikuwa ni wengi mno na walimu tulikuwa watano tu, ilikuwa ni mimi na mwenzangu wa kike tulioripoti ndani ya wiki hiyo pamoja na walimu wengine watatu akiwemo mzee mmoja mstaafu aliyeombwa kuhudumu hapo shuleni.

Siku niliyoripoti walimu wenzangu walinishangaa na kunionya kuwa kama sikuwa na kinga yoyote basi hapo kijijini sito paweza. Mimi niliwajibu kuwa siamini kabisa kwenye nguvu za giza na ninaimani kwa Mwenyezi Mungu kuwa ndiye atakaye nisaidia kwani mimi ni mkristo Mkatoliki. Nikatambulishwa mbele ya wanafunzi na mimi nikajitambulisha.

Siku hiyo nilifanya maandalizi kadhaa kwa ajili ya kipindi na kisha kuanza kazi yangu ya kufundisha. Siku za mwanzo nilishangazwa na umakini wa wanafunzi darasani, wengi walikuwa wakinitazama kwa makini na wengine walikuwa hawaongei wala kujibu chochote hata ukiwauliza maswali wakati wa kipindi, nilikuja kugundua kumbe walikuwa ni kama wamelala huku wakiniangalia kwa sababu ilikuwa hata nikiwashtua kwa kuwatingisha walibaki wakinitazama tu!

Nyumba yangu niliyopewa na uongozi wa Kijiji ilikuwa pembezoni kidogo na eneo la shule, na kama mnavyojua mazingira ya kijijini, nyumba ilikuwa pembezoni mwa kijiji. Siku moja nilivyokuwa nikirudi kutoka kazini, mtaani wakazi wengi walikuwa wakinitolea macho ya mshangao kama vile walikuwa wakinitamani sikuelewa hawakuniongelesha kwa lolote na nilivyo wasalimia wengi wao hawakunijibu walibaki tu wakinitazama! Niliwaona baadhi yao wakininyooshea vidole kama vile wanaelekezana kitu, mimi nilitembea haraka haraka kuelekea yalipo makazi yangu.

Nilifika nyumbani kwangu, vile naufungua tu mlango nilishangazwa kuona mnyama kama panya akitoka ndani ya nyumba yangu kwa kasi kubwa sana kupitia mlango mkuu wa kuingilia sebuleni, alikuwa amebeba mfupa! Nilishtuka sana baada ya kuingia chumbani kwangu na kuukosa ule mfupa niliopewa na mzee Kingalu, nikatambua kwamba uliondoka na yule panya niliyepishana naye pale mlangoni.

Nilivyofika ndani kwangu nikafanya utaratibu wa kuandaa chakula na baada ya kula nikajipumzisha kitandani na kupitiwa na usingizi totoro. Nilishtuka niliposikia jina langu likiitwa, "Soka! Soka!" hapo kijasho chembamba kikanitoka na nilipotazama mlangoni ulikuwa ni mwanga mkali sana na sikuweza kuona kitu chochote nikafikiria ni nani huyo aliyekuwa akiniita kisha nikaisikia tena ile sauti, na mara hii kwa mtetemo.

"Wewe ni mgeni hapa kijijini Kwamsisi, ila umewakasirisha wavyele(wazee wa kimila) kwani ulijiwekea zindiko la mfupa bila ruhusa ya wavyele. kwa hiyo mambo yatakayo kupata ni makubwa mno!"

Mimi nikawajibu kuwa ule mfupa nilipewa tu na mzee Kingalu na wala yeye hakuniambia kama ni zindiko hata hivyo jana nilivyo rudi kutoka kazini sikuukuta ule mfupa kwa hiyo kama ni zindiko mimi sina. Yule mtu akacheka sana na kuniambia kuwa yule panya niliyemuona sio panya wa kawaida bali ni mtaalamu wa kutegua mabomu ya kichawi, kisha ile sauti ikapotea na hapo mimi nikashtuka kutoka usingizini. Nilihisi kuwa huwenda ikawa ni ndoto tu iliyokuwa ikinisumbua japokuwa nilikuwa naogopa sana nilichukua biblia yangu nikalala nayo huku nikisali rozali.

ITAENDELEA...
Bantu Lady hivi ushapita hapaa??? Aaliyyah njoo uone mambo ya mwalimu soka hukuuu!
 
Jina langu ninaitwa Soka (sio jina halisi) na kwetu ni huko Moshi uchagani. Nilisoma kwa shida na kufanikiwa kupata elimu ya Sekondari na kisha kujiunga na mafunzo ya ualimu katika chuo cha Marangu na kuhitimu kwa kutunukiwa Daraja A. Baada ya kuhitimu nilipangiwa kituo cha kazi ni huko Kwamsisi mkoani Tanga katika shule ya msingi Kwamsisi.

Nilivyofika nilishangazwa sana na mazingira ya shule na kijiji kwa ujumla. Kwanza nilipokelewa na wazee wa kijiji walio nionya sana kuhusu kile kijiji, wakaniambia niwe makini. Mzee mmoja aliyejitambulisha kama mzee Kingalu akanipatia kipande cha mfupa na kuniambia kuwa ni lazima nilale nacho ili niweze kuwa salama.

Niliogopa sana, nilipelekwa kwenye nyumba ya walimu ilikuwa ni nyumba ya bati iliyojengwa kwa kuta za miti na kusilibwa vizuri kwa udongo pia iliezekwa kwa bati. ilikuwa ni nyumba yenye hadhi kwa eneo hilo kwani asilimia kubwa ya nyumba za pale kijijini zilikuwa ni nyumba za udongo na kuezekwa na nyasi.

Siku ya kwanza nilipoingia shuleni ili niweze kutambulishwa nilishangazwa sana na mazingira yalivyokuwepo. Wanafunzi walikuwa ni wengi mno na walimu tulikuwa watano tu, ilikuwa ni mimi na mwenzangu wa kike tulioripoti ndani ya wiki hiyo pamoja na walimu wengine watatu akiwemo mzee mmoja mstaafu aliyeombwa kuhudumu hapo shuleni.

Siku niliyoripoti walimu wenzangu walinishangaa na kunionya kuwa kama sikuwa na kinga yoyote basi hapo kijijini sito paweza. Mimi niliwajibu kuwa siamini kabisa kwenye nguvu za giza na ninaimani kwa Mwenyezi Mungu kuwa ndiye atakaye nisaidia kwani mimi ni mkristo Mkatoliki. Nikatambulishwa mbele ya wanafunzi na mimi nikajitambulisha.

Siku hiyo nilifanya maandalizi kadhaa kwa ajili ya kipindi na kisha kuanza kazi yangu ya kufundisha. Siku za mwanzo nilishangazwa na umakini wa wanafunzi darasani, wengi walikuwa wakinitazama kwa makini na wengine walikuwa hawaongei wala kujibu chochote hata ukiwauliza maswali wakati wa kipindi, nilikuja kugundua kumbe walikuwa ni kama wamelala huku wakiniangalia kwa sababu ilikuwa hata nikiwashtua kwa kuwatingisha walibaki wakinitazama tu!

Nyumba yangu niliyopewa na uongozi wa Kijiji ilikuwa pembezoni kidogo na eneo la shule, na kama mnavyojua mazingira ya kijijini, nyumba ilikuwa pembezoni mwa kijiji. Siku moja nilivyokuwa nikirudi kutoka kazini, mtaani wakazi wengi walikuwa wakinitolea macho ya mshangao kama vile walikuwa wakinitamani sikuelewa hawakuniongelesha kwa lolote na nilivyo wasalimia wengi wao hawakunijibu walibaki tu wakinitazama! Niliwaona baadhi yao wakininyooshea vidole kama vile wanaelekezana kitu, mimi nilitembea haraka haraka kuelekea yalipo makazi yangu.

Nilifika nyumbani kwangu, vile naufungua tu mlango nilishangazwa kuona mnyama kama panya akitoka ndani ya nyumba yangu kwa kasi kubwa sana kupitia mlango mkuu wa kuingilia sebuleni, alikuwa amebeba mfupa! Nilishtuka sana baada ya kuingia chumbani kwangu na kuukosa ule mfupa niliopewa na mzee Kingalu, nikatambua kwamba uliondoka na yule panya niliyepishana naye pale mlangoni.

Nilivyofika ndani kwangu nikafanya utaratibu wa kuandaa chakula na baada ya kula nikajipumzisha kitandani na kupitiwa na usingizi totoro. Nilishtuka niliposikia jina langu likiitwa, "Soka! Soka!" hapo kijasho chembamba kikanitoka na nilipotazama mlangoni ulikuwa ni mwanga mkali sana na sikuweza kuona kitu chochote nikafikiria ni nani huyo aliyekuwa akiniita kisha nikaisikia tena ile sauti, na mara hii kwa mtetemo.

"Wewe ni mgeni hapa kijijini Kwamsisi, ila umewakasirisha wavyele(wazee wa kimila) kwani ulijiwekea zindiko la mfupa bila ruhusa ya wavyele. kwa hiyo mambo yatakayo kupata ni makubwa mno!"

Mimi nikawajibu kuwa ule mfupa nilipewa tu na mzee Kingalu na wala yeye hakuniambia kama ni zindiko hata hivyo jana nilivyo rudi kutoka kazini sikuukuta ule mfupa kwa hiyo kama ni zindiko mimi sina. Yule mtu akacheka sana na kuniambia kuwa yule panya niliyemuona sio panya wa kawaida bali ni mtaalamu wa kutegua mabomu ya kichawi, kisha ile sauti ikapotea na hapo mimi nikashtuka kutoka usingizini. Nilihisi kuwa huwenda ikawa ni ndoto tu iliyokuwa ikinisumbua japokuwa nilikuwa naogopa sana nilichukua biblia yangu nikalala nayo huku nikisali rozali.

ITAENDELEA...
Naomba usiendeleze hii story kwani ni ya kusadikika
 
Jina langu ninaitwa Soka (sio jina halisi) na kwetu ni huko Moshi uchagani. Nilisoma kwa shida na kufanikiwa kupata elimu ya Sekondari na kisha kujiunga na mafunzo ya ualimu katika chuo cha Marangu na kuhitimu kwa kutunukiwa Daraja A. Baada ya kuhitimu nilipangiwa kituo cha kazi ni huko Kwamsisi mkoani Tanga katika shule ya msingi Kwamsisi.

Nilivyofika nilishangazwa sana na mazingira ya shule na kijiji kwa ujumla. Kwanza nilipokelewa na wazee wa kijiji walio nionya sana kuhusu kile kijiji, wakaniambia niwe makini. Mzee mmoja aliyejitambulisha kama mzee Kingalu akanipatia kipande cha mfupa na kuniambia kuwa ni lazima nilale nacho ili niweze kuwa salama.

Niliogopa sana, nilipelekwa kwenye nyumba ya walimu ilikuwa ni nyumba ya bati iliyojengwa kwa kuta za miti na kusilibwa vizuri kwa udongo pia iliezekwa kwa bati. ilikuwa ni nyumba yenye hadhi kwa eneo hilo kwani asilimia kubwa ya nyumba za pale kijijini zilikuwa ni nyumba za udongo na kuezekwa na nyasi.

Siku ya kwanza nilipoingia shuleni ili niweze kutambulishwa nilishangazwa sana na mazingira yalivyokuwepo. Wanafunzi walikuwa ni wengi mno na walimu tulikuwa watano tu, ilikuwa ni mimi na mwenzangu wa kike tulioripoti ndani ya wiki hiyo pamoja na walimu wengine watatu akiwemo mzee mmoja mstaafu aliyeombwa kuhudumu hapo shuleni.

Siku niliyoripoti walimu wenzangu walinishangaa na kunionya kuwa kama sikuwa na kinga yoyote basi hapo kijijini sito paweza. Mimi niliwajibu kuwa siamini kabisa kwenye nguvu za giza na ninaimani kwa Mwenyezi Mungu kuwa ndiye atakaye nisaidia kwani mimi ni mkristo Mkatoliki. Nikatambulishwa mbele ya wanafunzi na mimi nikajitambulisha.

Siku hiyo nilifanya maandalizi kadhaa kwa ajili ya kipindi na kisha kuanza kazi yangu ya kufundisha. Siku za mwanzo nilishangazwa na umakini wa wanafunzi darasani, wengi walikuwa wakinitazama kwa makini na wengine walikuwa hawaongei wala kujibu chochote hata ukiwauliza maswali wakati wa kipindi, nilikuja kugundua kumbe walikuwa ni kama wamelala huku wakiniangalia kwa sababu ilikuwa hata nikiwashtua kwa kuwatingisha walibaki wakinitazama tu!

Nyumba yangu niliyopewa na uongozi wa Kijiji ilikuwa pembezoni kidogo na eneo la shule, na kama mnavyojua mazingira ya kijijini, nyumba ilikuwa pembezoni mwa kijiji. Siku moja nilivyokuwa nikirudi kutoka kazini, mtaani wakazi wengi walikuwa wakinitolea macho ya mshangao kama vile walikuwa wakinitamani sikuelewa hawakuniongelesha kwa lolote na nilivyo wasalimia wengi wao hawakunijibu walibaki tu wakinitazama! Niliwaona baadhi yao wakininyooshea vidole kama vile wanaelekezana kitu, mimi nilitembea haraka haraka kuelekea yalipo makazi yangu.

Nilifika nyumbani kwangu, vile naufungua tu mlango nilishangazwa kuona mnyama kama panya akitoka ndani ya nyumba yangu kwa kasi kubwa sana kupitia mlango mkuu wa kuingilia sebuleni, alikuwa amebeba mfupa! Nilishtuka sana baada ya kuingia chumbani kwangu na kuukosa ule mfupa niliopewa na mzee Kingalu, nikatambua kwamba uliondoka na yule panya niliyepishana naye pale mlangoni.

Nilivyofika ndani kwangu nikafanya utaratibu wa kuandaa chakula na baada ya kula nikajipumzisha kitandani na kupitiwa na usingizi totoro. Nilishtuka niliposikia jina langu likiitwa, "Soka! Soka!" hapo kijasho chembamba kikanitoka na nilipotazama mlangoni ulikuwa ni mwanga mkali sana na sikuweza kuona kitu chochote nikafikiria ni nani huyo aliyekuwa akiniita kisha nikaisikia tena ile sauti, na mara hii kwa mtetemo.

"Wewe ni mgeni hapa kijijini Kwamsisi, ila umewakasirisha wavyele(wazee wa kimila) kwani ulijiwekea zindiko la mfupa bila ruhusa ya wavyele. kwa hiyo mambo yatakayo kupata ni makubwa mno!"

Mimi nikawajibu kuwa ule mfupa nilipewa tu na mzee Kingalu na wala yeye hakuniambia kama ni zindiko hata hivyo jana nilivyo rudi kutoka kazini sikuukuta ule mfupa kwa hiyo kama ni zindiko mimi sina. Yule mtu akacheka sana na kuniambia kuwa yule panya niliyemuona sio panya wa kawaida bali ni mtaalamu wa kutegua mabomu ya kichawi, kisha ile sauti ikapotea na hapo mimi nikashtuka kutoka usingizini. Nilihisi kuwa huwenda ikawa ni ndoto tu iliyokuwa ikinisumbua japokuwa nilikuwa naogopa sana nilichukua biblia yangu nikalala nayo huku nikisali rozali.

ITAENDELEA...
we ni mwongo na lengo lako ni kukashifu jamii za watu. Jamii nyingi zimehamia hizo wilaya za Handeni na Kilindi hakuna huo upumbavu unaouzungumza wewe. Na uache mambo ya kitoto.
 
SEHEMU YA 3

Mwalimu mkuu alituita kikao kilikuwa ni kikao kizito kujadili ujumbe ulioletwa na mzazi mmoja kwenye karatasi iliyokuwa imefungwa kwenye bahasha ya khaki alionekana kuwa akitetemeka na hakuwa sawa kisaikolojia, mimi nilikuwa ndio kwanza nikisahihisha madaftari huku nikibadilishana maongezi na mwalimu huyu wa kike aliyetokea kuwa karibu sana na mimi nilishtuka kumuona mwalimu mkuu akiwa kwenye hali ile.

"Walimu habari za mchana?" Tulikuwa walimu wanne wote tulitahamaki na hakuna hata mmoja aliye jibu wote tulikaa kimya. Siti akajibu, "nzuri." Sauti yake ikasikika kwa wote nasi tukarudia tena "nzuri." "Inaweza kuwa ni nzuri kwenu au la mmejibu kwa mazowea tu lakini kuna vita kali sana inayoendelea kati yetu haswa kwa nyinyi walimu wageni, inaonekana mmeshindwa kabisa kuheshimu wazee wa kijiji hiki, mzee Sa-Masimba ameleta barua hii amemtuma mwanaye ailete barua hii imenitisha kidogo kuisoma japo sijaielewa lakini ina alama ya damu.

"Alama ya damu?!" wote tulihamaki. "Ndio ni damu ya halisi kabisa ni kidoti kimewekwa juu ya bahasha kikiwa kimechovywa kama na kidole cha mkono, inaonekana kuna mtu anawindwa hapa je ni nani anayewindwa na kwanini?" alihoji mwalimu mkuu.

Barua ilisomeka, "Ndugu mwalimu mkuu hongera kwa kupata wafanyakazi wapya lakini sidhani kama vijana hao uliwafunza juu ya mila za kwetu, kuheshimu wazee na kuto jiingiza kwa namna yoyote na mipango ya kujaribu kupambana na wazee wa kimila, kama hiyo haitoshi kutengeneza wigo na kujiona kuwa huingiliki kwetu sisi tunahesabia kwamba ni dharau. Kama wameshindwa kutuheshimu japo kwa salamu mpaka kufikia hatua ya kupambana na sisi ki chwawi hakika hatuta waacha salama." ilimalizika shemu ya barua hiyo.

Nakumbuka siku hiyo tuliwaruhusu wanafunzi mapema sana ilikuwa kama mchana wa saa nane hivi. Mimi nilijua fika ndiyo mlengwa mkuu hivyo niliogopa sana tulitembea mpaka kwenye nyumba ya Mzee Samasimba tulivyo karibia tu tulipiga magoti huku tukitembea kwa magoti mpaka tulipoufikia mlango wa nyumba yake, mwalimu mkuu akiwa ametangulia mbele. Mzee mwenyewe hatuku mkuta basi wakatumwa watoto kwenda kumwita alikuja huku akiwa amevaa msuli wake kiunoni aliambatana na vijana wengine wawili mmoja alimtazama sana Siti kisha akaendelea mpaka wakaingia ndani mzee alisimama pale nje mkewe akamletea kigoda(kiti cha kukalia), akakaa kutusikiliza.

Mwalimu mkuu alikuwa ametangulia mbele aliongea naye kwa lugha ya Kizigua na mwisho aliinama sana huku akimwomba msamaha. Kwakweli nikiri wazi kwamba sikuwahi kushuhudia mchawi akiabudiwa kama siku hiyo, huyu mzee inasemekana alikuwa moja kati ya wazee wenye kauli sana pale kijijini, mambo mengi yalikwama endapo tu yeye asinge shirikishwa na kukubaliana. Ilifika zamu yangu ya kumwomba msamaha kwani tulimwendea kwa zamu, niliinama na kupiga magoti na kusema shikamoo mzee Masimba mimi ni mgeni hapa kijijini naomba unisamehe kama nilikukwaza kwa namna yoyote, sikumpa mkono kama wenzangu walivyofanya niliogopa kuchukuliwa nyota.

Tuliondoka baada ya kupakwa usembe(unga mweupe) usoni na kichwani na wale vijana wake, tulidhalilishwa sana siku hiyo hamna siku nilichukia kazi hii ya ualimu kama siku hiyo tulirudi nyumbani kila mtu akiwa kimya hamsemeshi mwenzake, nilitembea huku nikiwa na mawazo mengi macho yangu yakitazama chini huku machozi yakinilengelenga. "Kwanini binadamu anaabudiwa kama Mungu!" niliwaza moyoni ilikuwa yapata majira ya saa kumi nambili jioni ikikaribia saa moja usiku, nilishtuka kumuona Siti akiwa amenishika bega la kulia kwa nyuma niligeuka na kumtazama.

"Kwahiyo ndio unaenda nyumbani, uende salama ila uwe makini, hapa ndio Kwamsisi uache ubrazameni uheshimu watu." Kumbe ile hali yangu ya kujitengetenga na kutosalimia watu iliwaudhi wengi pia kujiweka karibu na mzee Kingalu ilikuwa ni hatari kwangu niliogopa kuiendea ile njia inayokwenda nyumbani, nilipokumbuka lile jicho alilonikata mzee Masimba nilipogoma kumpa mkono wa msamaha kwa kuwa sikutaka kushikana mkono na mchawi. Basi nikajua kuwa usiku huo lazima atanijilia nyumbani kwangu.

ITAENDELEA...
Hatariii nanusuu!!

Naendelea kusoma 🙇
 
Back
Top Bottom