Sitosahau yaliyonipata kijijini Kwamsisi

Sitosahau yaliyonipata kijijini Kwamsisi

SEHEMU YA 4

"Sitti sikuachi tuondoke wote." "Hapana kwanini unanifuata unadhani kwamba mzee atanielewa?" Mzee akimaanisha yule mganga mkuu anayekaa naye pale nyumbani, mueleze matatizo yangu huwenda akanisaidia. "Unadhani basi ninaimani sana na mambo haya ya kishirikina?" Sitti alijifanya kwamba hana imani sana na waganga lakini mimi moyoni mwangu nilijua fika kwamba yeye anaweza kunisaidia juu ya jambo hili kwa hivyo nilikata shauri la kumfuata mpaka pale alipokuwa akiishi. Kagiza ndio kalikuwa kakianza kuingia na unavyojuwa hali kijijini giza linawahi kuingia haraka na usiku huwa ni mrefu na wa kutisha mno.

Nilimshika Sitti mkono mpaka pale alipokuwa akiishi tulifika ilibidi aniache nje kwanza barazani ili aende akaongee na yule Mzee Mganga. Ni mganga aliyekuwa maarufu sana hapo kijijini sito mtaja kwa jina ili kuficha hadhi yake lakini kila siku hayakuacha kupaki magari yasiyopungua matano ya wateja waliokuwa wakihitaji huduma yake, nilifika nikasikia kuna mteja alikuwa akimalizia kumtibu niliketi barazani kwenye benchi na mara kidogo niliitwa na kuingia ndani, Siti alinitambulisha na baada ya utambulisho niliona yule mganga akitazama kwenye kioo chake na kisha baadaye akaongea kwa upole.

"Kuna watu wanakufuatilia, na hata hapa ulipo wapo mimi nimewaona?" "Wako wangapi?!" niling'aka kwa mshtuko. wapo wawili nilihisi huwenda kuwa ni wale vijana wa mzee Samasimba ndio wametumwa kunifuatilia, ni kweli Mganga alinieleza kuwa hao vijana wametumwa na mzee fulani ambaye hato mtaja jina na lengo lao ni kuangalia nyendo zangu na kisha kumpelekea yule mchawi taarifa. "Wewe huwezi kuwaona kwasababu huna nguvu za kuwaona," alisema kwa upole na kwa utulivu mno.

Nilikuwa nipo ndani kwenye chumba maalum cha uganga, koroboi iliyokuwa hapo chumbani ndiyo iliyokuwa ikitoa mwanga kwa wakati ule. Chumba kilitapakaa harufu ya udi ambapo mganga alikuwa ndio kwanza anaanza kupandisha maruhani yake alisimama akaanza kutetemeka mwili mzima mithili ya mtu aliyepigwa na shoti ya umeme. "Enyi wazee na mizimu ya wakulu njooni mumuokoe huyu m'bwanga, asije kudhulika na walimwengu wenye roho mbaya. aliongea kwa sauti kali sana kisha kuchukua tunguli yake akiisha kuitikisa sana akaipuliza na hapo ikatokea sauti kama ya filimbi. Aliizungusha kichwani kwangu na kuniwekea kichwani kwa dakika kadhaa kisha kuitoa na kuivaa shingoni kwani ilikuwa na ukamba wake.

Huyo mganga alikuwa amejifunga kaniki kwa mtindo wa lubega tu na kiunoni alifunga mkanda wa shanga za makombe ya baharini. Chumba chake kilijaa zana za kazi basi alichukua kikamba kama bangili yenye mafundofundo akanifunga mkononi ilikuwa ni kama hirizi ndogo, kisha akanipaka dawa kidogo kutoka kwenye ile tunguli na kunishika mkono kutoka nje huku akiwa ameshikilia pembe ndefu pamoja na mwengo (kama mkia wa ng'ombe) alizunguka nyumba mara nyingi huku akiimba na kisha akaniambia nimfuate nyuma twende nyumbani kwangu kuzuza. (kukagua usalama wa nyumba yangu).

Nilimfuata nyuma alikuwa akikimbia kwa kasi japo sio sana, niseme tu labda ni kile kihirizi alicho nifunga ama ile dawa aliyonipaka usoni kwani kuanzia hapo nilianza kuona mambo ya ajabu mno na yakutisha. Niliweza kuona mwanga kama vile kuna taa za umeme kijiji chote pia mandhari ya kijiji ilibadilika ikawa ni yakuvutia mno ni kama vile macho yangu yalipigwa kiini macho. Niliwaona watu wakiwa katika maumbo ya ajabu ajabu wengine wakitembea huku wakiwa uchi wa mnyama!

Kila tulikopita niliona vitu ambavyo nisingeweza kuviona kwa macho ya kawaida wale vijana walikuwa wakitufuatilia kwa nyuma baada ya muda sikuwaona tena. Tulitembea usiku na baadaye kuingia kwenye njia ya kuelekea mashambani ni njia ya mkato kuelekea nyumbani kwangu lakini njia hii hupitia kwenye makaburi ya kijiji. Ghafla nilimuona yule mganga akipunguza mwendo na hapo akatembea kwa mwendo wa kunyata, alinisubiri mimi nilikuwa nyuma nikimfuata, jasho lilikuwa limenitoka mpaka kulowesha nguo yangu ya ndani, niliingiwa na woga mkubwa. Alinishika mkono tukatembea kidogo kuyakaribia makaburi tukachuchumaa chini ya mbuyu, nilistaajabu nilicho kiona.

Mwanga mkali wa moto uliokuwa umekokwa hapo makaburini wachawi walikuwa wakicheza kwa furaha huku wakiuzunguka moto ule. Mara nikamuona Mzee Samasimba akija huku akiwa amepanda juu ya mnyama fisi, wote walitulia kumsikiliza, niliwaona pia wale vijana waliokuwa wakitufuatilia wakiwa pamoja naye. Aliongea mengi ambayo sikuyasikia kwani alitumia lugha ya asili (kizigua) mwisho nilisikia jina langu na la Mzee Kingalu yakitajwa mara nyingi sana sikuelewa lugha iliyokuwa ikitumika nilimuona yule Mzee akilia sana huku akiongea kwa uchungu. Ijapokuwa alikuwa akiheshimika na wachawi wenzake lakini safari hii ilionekana kama aliudhika mno.

Wachawi hawana kazi, maranyingi hutafuta visababu tu ili kuanzisha ugomvi, ni watu wanaopenda kuheshimiwa na kuabudiwa kama Mungu bila kujua kwamba hapa duniani tunapita tu. Ndivyo ilivyokuwa kwa jamii ile niliyo kutana nayo amahakika nilijuta sana kuifahamu jamii ile na tamaduni zake. "Hapa ndipo sherehe na vikao vya kichawi hufanyika, inaonekana leo hawatokula nyama ya mtu ila kuna mtu wanamtafutia sababu, ni ama wewe au mzee Kingalu lakini mwenzako ni gwiji wa mambo haya wewe pangupakavu tia mchuzi watakuramba kama karata!" alisema yule mganga kwa sauti ya kunong'ona mwisho aliniambia tuondoke tunaondokaje aliniambia nimshike upindo wa ile kaniki na mara tukatokea mbele ya nyumba yangu.

"Kwa leo hatutoweza kufanya hili zoezi, lala kesho ukitoka kazini upitie nyumbani." Akimaanisha zoezi la kukagua nyumba na kuizindika, sikumjibu nilielekea mlangoni kwangu, niliufungua mlango na kuingia ndani kisha kuwasha kibatari nilipakaa ile dawa niliyopewa jana na mzee Kingalu utosini ilinisaidia kuzuia nguvu za kichawi, lakini ile hirizi niliyopewa na Mganga wala sikuivua. Nilizima kibatari na kulala ilikuwa yapata majira ya saa sita usiku. Niliomba pakuche haraka ili niwe salama. Sikusikia tatizo lolote kwa usiku huu ila baadaye nilisikia sauti ya bundi akilia juu ya bati langu alilia sana mpaka nikapitiwa na usingizi nilimsikia akilia kwa mbali na kupotea.

ITAENDELEA...

Sitosahau yaliyonipata kijijini Kwamsisi-5
 
SEHEMU YA 3

Mwalimu mkuu alituita kikao kilikuwa ni kikao kizito kujadili ujumbe ulioletwa na mzazi mmoja kwenye karatasi iliyokuwa imefungwa kwenye bahasha ya khaki alionekana kuwa akitetemeka na hakuwa sawa kisaikolojia, mimi nilikuwa ndio kwanza nikisahihisha madaftari huku nikibadilishana maongezi na mwalimu huyu wa kike aliyetokea kuwa karibu sana na mimi nilishtuka kumuona mwalimu mkuu akiwa kwenye hali ile.

"Walimu habari za mchana?" Tulikuwa walimu wanne wote tulitahamaki na hakuna hata mmoja aliye jibu wote tulikaa kimya. Siti akajibu, "nzuri." Sauti yake ikasikika kwa wote nasi tukarudia tena "nzuri." "Inaweza kuwa ni nzuri kwenu au la mmejibu kwa mazowea tu lakini kuna vita kali sana inayoendelea kati yetu haswa kwa nyinyi walimu wageni, inaonekana mmeshindwa kabisa kuheshimu wazee wa kijiji hiki, mzee Sa-Masimba ameleta barua hii amemtuma mwanaye ailete barua hii imenitisha kidogo kuisoma japo sijaielewa lakini ina alama ya damu.

"Alama ya damu?!" wote tulihamaki. "Ndio ni damu ya halisi kabisa ni kidoti kimewekwa juu ya bahasha kikiwa kimechovywa kama na kidole cha mkono, inaonekana kuna mtu anawindwa hapa je ni nani anayewindwa na kwanini?" alihoji mwalimu mkuu.

Barua ilisomeka, "Ndugu mwalimu mkuu hongera kwa kupata wafanyakazi wapya lakini sidhani kama vijana hao uliwafunza juu ya mila za kwetu, kuheshimu wazee na kuto jiingiza kwa namna yoyote na mipango ya kujaribu kupambana na wazee wa kimila, kama hiyo haitoshi kutengeneza wigo na kujiona kuwa huingiliki kwetu sisi tunahesabia kwamba ni dharau. Kama wameshindwa kutuheshimu japo kwa salamu mpaka kufikia hatua ya kupambana na sisi ki chawi hakika hatuta waacha salama." ilimalizika shemu ya barua hiyo.

Nakumbuka siku hiyo tuliwaruhusu wanafunzi mapema sana ilikuwa kama mchana wa saa nane hivi. Mimi nilijua fika ndiyo mlengwa mkuu hivyo niliogopa sana tulitembea mpaka kwenye nyumba ya Mzee Samasimba tulivyo karibia tu tulipiga magoti huku tukitembea kwa magoti mpaka tulipoufikia mlango wa nyumba yake, mwalimu mkuu akiwa ametangulia mbele. Mzee mwenyewe hatuku mkuta basi wakatumwa watoto kwenda kumwita alikuja huku akiwa amevaa msuli wake kiunoni aliambatana na vijana wengine wawili mmoja alimtazama sana Siti kisha akaendelea mpaka wakaingia ndani mzee alisimama pale nje mkewe akamletea kigoda(kiti cha kukalia), akakaa kutusikiliza.

Mwalimu mkuu alikuwa ametangulia mbele aliongea naye kwa lugha ya Kizigua na mwisho aliinama sana huku akimwomba msamaha. Kwakweli nikiri wazi kwamba sikuwahi kushuhudia mchawi akiabudiwa kama siku hiyo, huyu mzee inasemekana alikuwa moja kati ya wazee wenye kauli sana pale kijijini, mambo mengi yalikwama endapo tu yeye asinge shirikishwa na kukubaliana. Ilifika zamu yangu ya kumwomba msamaha kwani tulimwendea kwa zamu, niliinama na kupiga magoti na kusema shikamoo mzee Masimba mimi ni mgeni hapa kijijini naomba unisamehe kama nilikukwaza kwa namna yoyote, sikumpa mkono kama wenzangu walivyofanya niliogopa kuchukuliwa nyota.

Tuliondoka baada ya kupakwa usembe(unga mweupe) usoni na kichwani na wale vijana wake, tulidhalilishwa sana siku hiyo hamna siku nilichukia kazi hii ya ualimu kama siku hiyo tulirudi nyumbani kila mtu akiwa kimya hamsemeshi mwenzake, nilitembea huku nikiwa na mawazo mengi macho yangu yakitazama chini huku machozi yakinilengelenga. "Kwanini binadamu anaabudiwa kama Mungu!" niliwaza moyoni ilikuwa yapata majira ya saa kumi nambili jioni ikikaribia saa moja usiku, nilishtuka kumuona Siti akiwa amenishika bega la kulia kwa nyuma niligeuka na kumtazama.

"Kwahiyo ndio unaenda nyumbani, uende salama ila uwe makini, hapa ndio Kwamsisi uache ubrazameni uheshimu watu." Kumbe ile hali yangu ya kujitengetenga na kutosalimia watu iliwaudhi wengi pia kujiweka karibu na mzee Kingalu ilikuwa ni hatari kwangu niliogopa kuiendea ile njia inayokwenda nyumbani, nilipokumbuka lile jicho alilonikata mzee Masimba nilipogoma kumpa mkono wa msamaha kwa kuwa sikutaka kushikana mkono na mchawi. Basi nikajua kuwa usiku huo lazima atanijilia nyumbani kwangu.

ITAENDELEA...
Taabu yote hiyo ya nini siku hiyo hiyo ningesepa na kuwaachia kijiji chao.
 
Kuna watu wana kera sana humu ..... story ya mwingine wew una kereka na nni ..... tuache sisi wengine tumesha kubali kudanganywa si basi .... nyuzi zipo nyingi kuna mtu kakulazimisha kusoma .....inonekqna unapenda otherwise usinge fuatilia episode ya kwanza hadi hapa .....
 
SEHEMU YA 4

"Sitti sikuachi tuondoke wote." "Hapana kwanini unanifuata unadhani kwamba mzee atanielewa?" Mzee akimaanisha yule mganga mkuu anayekaa naye pale nyumbani, mueleze matatizo yangu huwenda akanisaidia. "Unadhani basi ninaimani sana na mambo haya ya kishirikina?" Sitti alijifanya kwamba hana imani sana na waganga lakini mimi moyoni mwangu nilijua fika kwamba yeye anaweza kunisaidia juu ya jambo hili kwa hivyo nilikata shauri la kumfuata mpaka pale alipokuwa akiishi. Kagiza ndio kalikuwa kakianza kuingia na unavyojuwa hali kijijini giza linawahi kuingia haraka na usiku huwa ni mrefu na wa kutisha mno.

Nilimshika Sitti mkono mpaka pale alipokuwa akiishi tulifika ilibidi aniache nje kwanza barazani ili aende akaongee na yule Mzee Mganga. Ni mganga aliyekuwa maarufu sana hapo kijijini sito mtaja kwa jina ili kuficha hadhi yake lakini kila siku hayakuacha kupaki magari yasiyopungua matano ya wateja waliokuwa wakihitaji huduma yake, nilifika nikasikia kuna mteja alikuwa akimalizia kumtibu niliketi barazani kwenye benchi na mara kidogo niliitwa na kuingia ndani, Siti alinitambulisha na baada ya utambulisho niliona yule mganga akitazama kwenye kioo chake na kisha baadaye akaongea kwa upole.

"Kuna watu wanakufuatilia, na hata hapa ulipo wapo mimi nimewaona?" "Wako wangapi?!" niling'aka kwa mshtuko. wapo wawili nilihisi huwenda kuwa ni wale vijana wa mzee Samasimba ndio wametumwa kunifuatilia, ni kweli Mganga alinieleza kuwa hao vijana wametumwa na mzee fulani ambaye hato mtaja jina na lengo lao ni kuangalia nyendo zangu na kisha kumpelekea yule mchawi taarifa. "Wewe huwezi kuwaona kwasababu huna nguvu za kuwaona," alisema kwa upole na kwa utulivu mno.

Nilikuwa nipo ndani kwenye chumba maalum cha uganga, koroboi iliyokuwa hapo chumbani ndiyo iliyokuwa ikitoa mwanga kwa wakati ule. Chumba kilitapakaa harufu ya udi ambapo mganga alikuwa ndio kwanza anaanza kupandisha maruhani yake alisimama akaanza kutetemeka mwili mzima mithili ya mtu aliyepigwa na shoti ya umeme. "Enyi wazee na mizimu ya wakulu njooni mumuokoe huyu m'bwanga, asije kudhulika na walimwengu wenye roho mbaya. aliongea kwa sauti kali sana kisha kuchukua tunguli yake akiisha kuitikisa sana akaipuliza na hapo ikatokea sauti kama ya filimbi. Aliizungusha kichwani kwangu na kuniwekea kichwani kwa dakika kadhaa kisha kuitoa na kuivaa shingoni kwani ilikuwa na ukamba wake.

Huyo mganga alikuwa amejifunga kaniki kwa mtindo wa lubega tu na kiunoni alifunga mkanda wa shanga za makombe ya baharini. Chumba chake kilijaa zana za kazi basi alichukua kikamba kama bangili yenye mafundofundo akanifunga mkononi ilikuwa ni kama hirizi ndogo, kisha akanipaka dawa kidogo kutoka kwenye ile tunguli na kunishika mkono kutoka nje huku akiwa ameshikilia pembe ndefu pamoja na mwengo (kama mkia wa ng'ombe) alizunguka nyumba mara nyingi huku akiimba na kisha akaniambia nimfuate nyuma twende nyumbani kwangu kuzuza. (kukagua usalama wa nyumba yangu).

Nilimfuata nyuma alikuwa akikimbia kwa kasi japo sio sana, niseme tu labda ni kile kihirizi alicho nifunga ama ile dawa aliyonipaka usoni kwani kuanzia hapo nilianza kuona mambo ya ajabu mno na yakutisha. Niliweza kuona mwanga kama vile kuna taa za umeme kijiji chote pia mandhari ya kijiji ilibadilika ikawa ni yakuvutia mno ni kama vile macho yangu yalipigwa kiini macho. Niliwaona watu wakiwa katika maumbo ya ajabu ajabu wengine wakitembea huku wakiwa uchi wa mnyama!

Kila tulikopita niliona vitu ambavyo nisingeweza kuviona kwa macho ya kawaida wale vijana walikuwa wakitufuatilia kwa nyuma baada ya muda sikuwaona tena. Tulitembea usiku na baadaye kuingia kwenye njia ya kuelekea mashambani ni njia ya mkato kuelekea nyumbani kwangu lakini njia hii hupitia kwenye makaburi ya kijiji. Ghafla nilimuona yule mganga akipunguza mwendo na hapo akatembea kwa mwendo wa kunyata, alinisubiri mimi nilikuwa nyuma nikimfuata, jasho lilikuwa limenitoka mpaka kulowesha nguo yangu ya ndani, niliingiwa na woga mkubwa. Alinishika mkono tukatembea kidogo kuyakaribia makaburi tukachuchumaa chini ya mbuyu, nilistaajabu nilicho kiona.

Mwanga mkali wa moto uliokuwa umekokwa hapo makaburini wachawi walikuwa wakicheza kwa furaha huku wakiuzunguka moto ule. Mara nikamuona Mzee Samasimba akija huku akiwa amepanda juu ya mnyama fisi, wote walitulia kumsikiliza, niliwaona pia wale vijana waliokuwa wakitufuatilia wakiwa pamoja naye. Aliongea mengi ambayo sikuyasikia kwani alitumia lugha ya asili (kizigua) mwisho nilisikia jina langu na la Mzee Kingalu yakitajwa mara nyingi sana sikuelewa lugha iliyokuwa ikitumika nilimuona yule Mzee akilia sana huku akiongea kwa uchungu. Ijapokuwa alikuwa akiheshimika na wachawi wenzake lakini safari hii ilionekana kama aliudhika mno.

Wachawi hawana kazi, maranyingi hutafuta visababu tu ili kuanzisha ugomvi, ni watu wanaopenda kuheshimiwa na kuabudiwa kama Mungu bila kujua kwamba hapa duniani tunapita tu. Ndivyo ilivyokuwa kwa jamii ile niliyo kutana nayo amahakika nilijuta sana kuifahamu jamii ile na tamaduni zake. "Hapa ndipo sherehe na vikao vya kichawi hufanyika, inaonekana leo hawatokula nyama ya mtu ila kuna mtu wanamtafutia sababu, ni ama wewe au mzee Kingalu lakini mwenzako ni gwiji wa mambo haya wewe pangupakavu tia mchuzi watakuramba kama karata!" alisema yule mganga kwa sauti ya kunong'ona mwisho aliniambia tuondoke tunaondokaje aliniambia nimshike upindo wa ile kaniki na mara tukatokea mbele ya nyumba yangu.

"Kwa leo hatutoweza kufanya hili zoezi, lala kesho ukitoka kazini upitie nyumbani." Akimaanisha zoezi la kukagua nyumba na kuizindika, sikumjibu nilielekea mlangoni kwangu, niliufungua mlango na kuingia ndani kisha kuwasha kibatari nilipakaa ile dawa niliyopewa jana na mzee Kingalu utosini ilinisaidia kuzuia nguvu za kichawi, lakini ile hirizi niliyopewa na Mganga wala sikuivua. Nilizima kibatari na kulala ilikuwa yapata majira ya saa sita usiku. Niliomba pakuche haraka ili niwe salama. Sikusikia tatizo lolote kwa usiku huu ila baadaye nilisikia sauti ya bundi akilia juu ya bati langu alilia sana mpaka nikapitiwa na usingizi nilimsikia akilia kwa mbali na kupotea.

ITAENDELEA...
Mmmh noma sana
 
Usiporejea ntakukutukana kila siku!
Mim nlienda kumzoa mume wangu huko kwa msisi eneo linaitwa BICHWA NG'OMBE alikaa miezi miwili hajarejea alifuata mbao.
Nikamkuta anaishi na kibibi kuliko mama yake.
Ishukuriwe damu ya YESU
Chang'ombe but bichwa ng'ombe hakuna jina hilo
 
Ila mazingira ya kazi za walimu ni shida sana. Mzee wangu ashawahi tegewa radi kwenye majukumu yake huko vijijini.
Mzee wangu alikuwa mwalimu kuna wakati alihamishiwa katika shule moja Morogoro vijijini huko ndanindani.. ile shule ilikuwa na walimu wawili tu.!! Historia yapale wanasema iIlikuwa akiongezeka mwalimu wa3 basi anakufa. Na wakati mzee anaenda kuripoti shuleni akakuta kuna mwalimu amezikwa kama miezi mi3 nyuma. Nayeye alivyohamia pale hakuchkua hata zaidi ya mwaka akafariki..!
 
Hii story haina ukweli wote. Kama yalikutokea ni kwa kiasi kidogo tu. But hiyo barua inaonesha kabisa ni uongo wa kutunga. Wewe umetumwa unataka kutuharibia jina letu la Tanga.

ni vizuri muwe mnakuwa wakweli kama hadithi ni ya kutunga ukisema umetunga wala haipunguzi wasomaji. Si lazima useme ni kweli yametokea.

nimekuja baada ya walaji kulalamika pia unawapa tu episode tufupi tufupi sana. Ukaamua kunywa chai.... Episode.

ukawa unawaza episode. Nyie walimu si mna muda mwingi tu wa kupumzika? Hebu kaa andika episodes ya ukweli ndefu kutoka posta hadi angalau Bunju.
Andika Kwa Maandishi Ya Kawaida Sisi Sio Vipofu.
Unsubscribe Kama Hujapenda Hii Story
 
Back
Top Bottom