Siwezi kuandamana hata siku Moja ni ujinga

Shooter Again

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2022
Posts
5,603
Reaction score
9,263
Yaani Mimi niandamane nipigwe risasi nife nizikwe nioze eti kisa Kuna mizee ambayo yenyewe enzi zao yalikua yamezubaa nchi ikatafunwa Sasa hivi yanasema vijana wa gen z andamaneni kwajili ya tanzania mnaumwa nyie wazee pambaneni na hali zenu kama maisha yamekua magumu kwenu hamna kijana ataemwaga damu yake Kwa ajili yenu lnatakiwa nyie ndio mfe mapema Ili vijana tuishi Sasa nashangaa mpaka Leo mpo hai wajinga nyie nione tena mnaweka vi nyuzi vyenu uchwara humu Kila mtu afe kivyake maana hata huyo mbowe na chama chake anaejifanya mpinzani ndio walewale
 
ila Hersi akiondolewa madarakani utaandamana!
 
Mkuu punguza Hasira.

Msalimie jirani yako Tu usimlie mikausho.
 
Sawa sawa,bora uendelee kuandamana kwa ajili ya kina mondi konde gang
Kama akitua unaenda kuwapokea Airport

Ova
 
Kuandamana Bongo wote tuingie front kuanzia waTz waliokufa na kuzikwa mwaka 1961 up to date, vikongwe, wazee, wanaume wanawake viwete hadi vipofu
Kiufupi home wabaki watoto chini ya miaka 10 tu

Hakuna cha Gen Z au A wote ni nchi yetu na uzembe wa wazee kama Tate Mkuu RRONDO ndio umetufikisha hapa
 
Unajidanya tu ,siku ya kufa na aina ya kifo ilishapangwa kama ni risasi, ugonjwa , ajali n.k so kama ni risasi hajalishi upo kwenye maandamano au la utalamwa ,hivyo hivyo kama ni ugonjwa, ajali n.k
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…