Siyo lazima kila alama ya mvuka kwa miguu (zebra) dereva wa gari asimame, Sheria ifumuliwe imepitwa na wakati

Siyo lazima kila alama ya mvuka kwa miguu (zebra) dereva wa gari asimame, Sheria ifumuliwe imepitwa na wakati

Tatizo hata wavuka barabara nao hwajitambui, gari inasimama mtu anaendelea ongea na simu, wanapita wachache akiona wamevuka na yeye ndo anataka vuka
Wengine huwekwa chambo na askari ili kukuchomesha then wanakawiwa ganji,
Yaani jaamaa anakuwa anamtayme dereva na kuchomeka mguu, au kuingia wakati gari ikipita ili mbele trafiki anakwambia mbona unataka kugonga watu kwenye zebra,
 
Bro sheria haipo, lakini sheria iko wazi kumwachia trafiki ombwe LA mamlaka ya kipolisi kumdhibiti dereva asitoroke!
Moja ya njia hizo ni kuchomoa funguo, kushikilia leseni, kung'oa vibati vya plate namba. Na sheria IPO kimya kuhusu maamuzi hayo mabovu ya askari!

Tena wanaweza kukubambikia na kosa jingine la ukaidi na ulitaka kuwagonga walipokuamuru hukutii!

Wakakusweka ndani maana sheria imenyaza kimya juu yao!
Ndiyo maaana nasema TUFUMUE HII SHERIA YA BARABARANI IMEPITWA NA WAKATI IMEKAA KIKORONI SANA!
Basi kama haujui trafiki wengi wamepata matatizo kwa hilo unalolizungumza brother...
 
Usilete hisia kwenye mambo yanayohitaji sheria, hakuna dereva asiyepisha LA sivyo kila siku tungesikia vifo vya watembea mguu,

Tunachosema hapa, hizo zebra hata kama hakuna MTU wa kuvuka, ukipita trafiki anakukamata ,
Traffic wa wapi wanaokukamata hata kama hakuna watu?
 
Tena inatakiwa iongezewe mkazo na faini yake iwe juu zaidi, kwenye zebra unatakiwa usimame hakuna namna ,sehem ya wavuka kwa miguu siku zote inatakiwa iheshimiwe
 
Una hoja.. Kwenye zebra hakuna mtu anaetaka kuvuka, ukipita bila kusimama, li askari linakwambia mbona hukusimama kwenye zebra, ni upuuzi tu.
Angekuwepo mtu anataka kuvuka sawa, sasa hakuna mtu bado nisimame tu, haileti mantiki.
 
Ukikamatwa kwa sababu hakuna mtu wa kupita jua wewe sio dereva hata walivyokua wanakamata kipindi hawajakatazwa tuliwatafsiria hiyo sheria kuwa mpaka wawepo watu wa kupita sio unasimama tu unasimama ili iweje bara bara pamoja na alama zake inaongea nilipiata bara bara moja huko Arusha ya East Afrika wamechora naruhusiwa kulipita gari lingine ila sehemu ni hatarishi waliochora walikosea kwa hiyo sio unachoona Road kipo sawa jiongeze pana dereva mmoja Lori broke zimefeli badala ya kuliacha lipite alikua anasimamia sheria ni Mungu ndio alimuokoa maana alikoswa koswa sana baada ya kusimama tukamwambia ukifata sheria sehemu ya ajali utakufa jamaa anapiga honi yupo mteremkoni anakomalia sheria...mimi hata kwenda kuhakiki barua sijui Polisi mambo ya vyeti niligoma hakuna sheria hiyo na niliwaambia kila kitu kipo kwa mujibu wa sheria sio Utashi wa IGP leo kipo wapi yaani kila kitu watoe wao harafu tena nikahakiki kwao huko huko si ujinga huo...
Inawezekana una hoja ila hueleweki kwa sababu ya uandishi wako mbovu!
 
Tena inatakiwa iongezewe mkazo na faini yake iwe juu zaidi, kwenye zebra unatakiwa usimame hakuna namna ,sehem ya wavuka kwa miguu siku zote inatakiwa iheshimiwe
Ndugu yangu kuna barabara zinabebra nyingi kuliko watu, ebu waza hakuna watu wavukaji theni dereva asimame kila sehem!

Hata watembea kwa miguu haohao wakipanda daladala linalosimama kila kituo huanza kulalamika hii inaonesha jinsigani siyo kila sehem lazima kusimama hata kama hakuna watu!

Lakini sheria IPO kimya ndiyo maana askari anaweza kumuandikia dereva akiamua na hakuna kitu atamfanya maana sheria inamlinda askari kufanya hayo hata kubambika makosa
 
Ni kweli lakini na madereva pia mnazipuuza sana hizo sheria.
Kivipi lete hoja ..ingekuwa madereva wanapuuza hivi huko barabarani si kila siku watu wangegongwa?
Kwanini utazame kosa moja la miaka mitano na usione ibora wa madereva kila siku?
 
Kwenye zebra azima usimame utaki kanunue ndege fullstop, maana usiposimama au kupunguza mwendo na wa nyuma yako nae ataosha vile vile sasa watu watavuka saa ngapi , slow down unapokaribia zebra cheki kushoto kulia ukivuka osha
 
Wewe ni dereva au abiria?
Ninaendesha gari kwa zaidi ya miaka 20 na nimezunguka Tanzania nzima sijashuhudia hicho ulichoandika. Wewe kwa vyo vyote vile una-over speed (unaendesha kasi zaidi ya speed inayoruhusiwa) mjini.
 
Habari

Tunaongozwa na sheria zilizo expire muda wake!

Iko haja sheria ya usalama barabarani ifanyiwe marekebisho kwani ilitungwa zamani enzi hizo Tanzania hatukuwa na barabara za lami na magari ya kutosha!

1. Siyo kila zebra lazima mwenye gari asimame hata kama hakuna mtu,
lakini baadhi ya Trafiki waliowrngi huitumia sheria hii vibaya kujinufaisha na kubambikia watu!

Hii yote inawezekana kwasababu sheria inawalinda trafiki kumkandamiza dereva! Hivyo hiyo sheria imepitwa na wakati kuwepo sasa!

Kama nchi sasa tunatakiwa tuwe na zebra za aina tofauti kuliko sasa vibao vyote ni black and White!

Nashauri Kuwekwe sheria mpya kwa vibao vya alama za wavuka kwa miguu iwe kama ifuatavyo!

1. Zebra za mistari nyekundu na nyeupe hiyo viwekwe kwenye vivuko vya watembea mguu kuonesha ni lazima kwa dereva kusimama (Lazima); na mara nyingi vibao hivyo vitawekwa kwenye maeneo mhimu tu ya msongamano! (Hii itamuamrisha dereva lazima kusimama kupisha watembea kwa miguu)

2. Zebra za mistari nyeupe na kijani itumie kuonesha utahadhari lakini hii iwe rasmi kwa wote kwa mtembea kwa miguu kuonesha atavuka endapo tu kukiwa salama!
(Hii itamuelekeza mtembea kwa miguu kuvuka kwa tahadhari kwa usalama wake)

Je, Endapo kuna kosa na dereva hakubaliani na kosa hilo sheria inasemaje kuhusu adhabu?

Kwa sheria ya sasa kwakweli ni mbovu mno, Endapo traffic akiamua kumbambikia kosa dereva ambalo hakubaliani nalo, huwa kuna fomu maalum ya kujaza na dereva kusaini ili kwenda mahakamani!
Na kama itakuwa hivyo lazima chombo cha moto anachoendesha dereva kishikiliwe police hadi pale mahakama itakapoamua!
Sasa chukulia mfano: dereva anakwenda mbeya, halafu kakamatwa chalinze kwa kosa ambalo hakubaliani nalo, inabidi Apache gari hapo chalinze hadi pale mahakama itakapoamua ( Hii sheria ya muundo huu haitekelezeki na sijui waliotunga walikuwa na akili gani)

Nashauri, endapo kuna mazingira ya dereva kutokubaliana na kosa, uwekwe utaratibu wa kuchukua maelezo ambayo yanakuwa kwenye karatasi kaboneted, polisi aandike maelezo yake, pia dereva naye aandike palepale maelezo yake pasipo kushurutishwa, halafu nakala ya juu achaniwe dereva apewe ili akaripoti kwenye kituo cha polisi kilichokaribu naye ndani ya siku 7 baada ya tukio, then ipangwe Sikh ya kusikiliza hiyo kesi online kupitia ofisi za police traffic na iamuriwe baada ya kusikiliza pande zote (dereva na traffic )

Kwa dereva ambaye hatakwenda kuripo kwa ajili ya kesi hiyo aandikiwe faini kwa maana kesi itakuwa imesikilizwa kwa upande mmoja!

Hii italeta nidhamu kwa trafiki wanaobambikia watu makosa kwasababu, endapo kutakuwa na malalamiko mengi ya dereva kutokubaliana na kosa kwenye database ya polisi na ikionesha trafiki yule yule kufanya kosa kwa wengi basi ASKARI huyo aondolewe barabarani!

Zipo sheria nyingi sana za kufumua lakini kiufupi sheria ya usalama barabarani ifumuliwe!

Usipokuwa mvumilivu barabarani kwa sasa unaweza piga trafiki kwa jaziba barabarani kumbe yeye hana hatia Bali anasimamia sheria mbovu ipasavyo kwa maslahi yake!
Rules are rules! Without rules we are all savages.
 
Ndugu yangu kuna barabara zinabebra nyingi kuliko watu, ebu waza hakuna watu wavukaji theni dereva asimame kila sehem!

Hata watembea kwa miguu haohao wakipanda daladala linalosimama kila kituo huanza kulalamika hii inaonesha jinsigani siyo kila sehem lazima kusimama hata kama hakuna watu!

Lakini sheria IPO kimya ndiyo maana askari anaweza kumuandikia dereva akiamua na hakuna kitu atamfanya maana sheria inamlinda askari kufanya hayo hata kubambika makosa
Kuna zebra zilizochorewa Horizontal solid line ukifika pale unatakiwa usimame kuwe na mtembea kwa miguu au kusiwepo , ni lazima usimame, na kuna zile zebra ambazo zimechorwa tu pale unatakiwa upunguze mwendo hata kama hamna mtu hutakiwi kupita na speed 80kph unatakiwa upunguze mwendo pita na speed ambayo ikitokea chochote unaweza kusimama mara moja vinginevyo unatakiwa kupigwa faini kwa kosa la reckless driving

Trafiki kapewa hayo mamlaka ya kukuandikia faini ikiwa utaendesha bila tahadhari.
 
Kwenye zebra azima usimame utaki kanunue ndege fullstop, maana usiposimama au kupunguza mwendo na wa nyuma yako nae ataosha vile vile sasa watu watavuka saa ngapi , slow down unapokaribia zebra cheki kushoto kulia ukivuka osha
Slows down ndicho madereva hufanya speed ya 10kmh pasipo na watembea kwa miguu lakini bado askari anakamata na kusema kwanini hujasimama? Swali sheria inamteteaje dereva hapo akiandikiwa faini?
 
Kuna zebra zilizochorewa Horizontal solid line ukifika pale unatakiwa usimame kuwe na mtembea kwa miguu au kusiwepo , ni lazima usimame, na kuna zile zebra ambazo zimechorwa tu pale unatakiwa upunguze mwendo hata kama hamna mtu hutakiwi kupita na speed 80kph unatakiwa upunguze mwendo pita na speed ambayo ikitokea chochote unaweza kusimama mara moja vinginevyo unatakiwa kupigwa faini kwa kosa la reckless driving

Trafiki kapewa hayo mamlaka ya kukuandikia faini ikiwa utaendesha bila tahadhari.
Maeneo yote yenye zebra ni makazi ya watu na speed inayoruhusiwa si zaidi ya 50Kph, sasa hiyo 80kph ni wapi?
 
Slows down ndicho madereva hufanya speed ya 10kmh pasipo na watembea kwa miguu lakini bado askari anakamata na kusema kwanini hujasimama? Swali sheria inamteteaje dereva hapo akiandikiwa faini?
Uongo tena wa mwaka!
 
Back
Top Bottom