Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 48,475
- 70,102
Ukiyasikiliza maelezo ya Bashe katika tuhuma za maamuzi na kutolewa vibali vya biashara ya kuingiza sukari yana walakini mwingi na kuacha maswali zaidi
1. Ni kweli Bashe anayo mamlaka ya kujifanyia maamuzi tu kwamba nchi ina dharura ya upungufu wa sukari yanayompa mamlaka ya kutofuata taratibu za manunuzi wakati huo ?
Kama waziri anayo mamlaka hayo inabidi yaondolewe au yawekewe utaratibu maalumu usioacha mashaka, sio sahihi kumpa waziri mmoja mamlaka makubwa hivyo.
2.Kwa nini wakati huo Bashe anafanya haya maamuzi ya kwamba nchi ina uhaba wa sukari na vuwanda vya sukari vimeshindwa kuingiza sukari kutoka nje hivyo kuhitajika maamuzi ya dharura wizara yake ya Kilimo au ya biashara haikuwa inatoa taarifa rasmi kwa umma?
Je, Bashe alipeleka taarifa rasmi kwenye kamati husika za bunge kuhusu jambo hilo?
3.Kwa nini viwanda vyote vya sukari vilishindwa kuingiza hata kilo moja ya sukari kadri ya vibali vyao walivyoomba na kupewa? Huku sio sawa na kula njama za kuhujumu uchumi na hivyo kuhitajika kuwajibishwa mahakamani kwa makosa ya uhujumu uchumi?
Yani Bashe anasema viwanda vyote vilishindwa kuingiza sukari hata kilo moja ikabidi wizara wachukie taratibu nyingine halafu inaisha tu hivyo?! Hivi ndivyo biashara ya sukari inavyosimamiwa na wizara yake kwamba hakuna uwajibikaji?
1. Ni kweli Bashe anayo mamlaka ya kujifanyia maamuzi tu kwamba nchi ina dharura ya upungufu wa sukari yanayompa mamlaka ya kutofuata taratibu za manunuzi wakati huo ?
Kama waziri anayo mamlaka hayo inabidi yaondolewe au yawekewe utaratibu maalumu usioacha mashaka, sio sahihi kumpa waziri mmoja mamlaka makubwa hivyo.
2.Kwa nini wakati huo Bashe anafanya haya maamuzi ya kwamba nchi ina uhaba wa sukari na vuwanda vya sukari vimeshindwa kuingiza sukari kutoka nje hivyo kuhitajika maamuzi ya dharura wizara yake ya Kilimo au ya biashara haikuwa inatoa taarifa rasmi kwa umma?
Je, Bashe alipeleka taarifa rasmi kwenye kamati husika za bunge kuhusu jambo hilo?
3.Kwa nini viwanda vyote vya sukari vilishindwa kuingiza hata kilo moja ya sukari kadri ya vibali vyao walivyoomba na kupewa? Huku sio sawa na kula njama za kuhujumu uchumi na hivyo kuhitajika kuwajibishwa mahakamani kwa makosa ya uhujumu uchumi?
Yani Bashe anasema viwanda vyote vilishindwa kuingiza sukari hata kilo moja ikabidi wizara wachukie taratibu nyingine halafu inaisha tu hivyo?! Hivi ndivyo biashara ya sukari inavyosimamiwa na wizara yake kwamba hakuna uwajibikaji?