SMS zinatupunguzia wanaume pointi tatu muhimu

SMS zinatupunguzia wanaume pointi tatu muhimu

Ferruccio Lamborghini

JF-Expert Member
Joined
Apr 15, 2020
Posts
1,667
Reaction score
2,595
Usiku kwenye daladala, saa ya simu yangu inaonyesha ni saa 4:47. Najilazamisha kuacha kusinzia, mara nasikia sauti za wanawake wawili wakizungumza viti vya nyuma yangu… stori zao zinanisaidia kukimbiza usingizi wangu.

Nasikia mmoja anamwambia mwenzake; “basi wakati namalizia kuosha vyombo akaja, eti ananiuliza vipi sasa? Nikajifanya sijui kinachoendelea, nikamuuliza vipi kuhusu nini? Akanambia nilichokuomba mchana, nikamuuliza kipi? Yaani nilikuwa najifanya kama vile nimesahau kila kitu, sikumbuki chochote.

“Basi akajizugisha zugisha pale ndio akanambia, nilikuomba namba yako. Nikamuuliza ya nini? Akanambia maswali gani hayo, nikamwambia si namba yangu, nitakupaje bila kujua ya nini. Akanambia kuna vitu nataka tuongee. Nikamwambia si uviongee hapa hapa. Akaniuliza kwani tukiongea kwenye simu kuna shida gani? Na mimi nikamuuliza kwani tukiongea hapa hapa huku tunaonana uso kwa macho kuna tatizo gani?

“Akaishiwa maneno, akanambia haya, nimeshindwa mimi, akaondoka.”

Nikiwa kwenye kiti changu nikajikuta natamani kugeuka kuwatazama hawa wanawake wawili angalau nijue wanaonekanaje, lakini tatizo ni kwamba, kama ningefanya hivyo ingeonekana wazi kwamba nawasikiliza na mimi nilikuwa sitaki tufikie huko nikaamua kujituliza, nikaishia kutengeneza picha ya namna walivyo nikitumia sauti zao na aina ya mazungumzo waliyokuwa wanayaongea kwa sauti bila soni kwenye usafiri wa umma.

Basi nikasikia yule mwanamke mwingine akicheka, yule msikilizaji; “He he heeee! Umemkomesha. Yaani hiyo ndio dawa ya vijanaume vya siku hizi. Vinapenda penda lakini havijui kutongoza, yaani tangu zimekuja simu na meseji wanaume hawajiamini kabisa kuongea mubashara. Wanakimbilia kuomba namba ya simu ili watume vimeseji vyao vya ajabu ajabu.”

Mwenzake akadakia; “Na emoji za kopa kopa.” kisha wote wakacheka kwa sauti utasema kwenye gari hakuna abiria wengine.

Ukiachana na kukosa aibu kiasi kwamba wanaweza kuongea mazungumzo ya aina hii kwenye usafiri wa umma, kitu walichokuwa wanakiongea huenda kina ukweli, wanaume siku hizi hatujiamini sana, hatujui kucheza na maneno kabisa, hususan uso kwa uso.

Ndiyo, tunajua vigori wenyewe siku hizi hawaelewi maneno makavu, kama ni mwanamume suruali utaimba mashairi yote, kuanzia ya hayati Sheikh Shaaban Robert mpaka ya William Shakespeare hutopata kitu, lakini hiyo haitunyimi uhuru wa kuonyesha makali yetu ya kusimama uso kwa uso na mrembo na kumuelezea yaliyojaa kwenye mtima wako.

Unajua uzuri wa kurusha makombora uso kwa uso ni kwamba ukikutana na kichwa ngumu anakuzodoa unaondoka umenywea, lakini bado ndani unajiona kidume. Na hiyo kuzodolewa ndio vijana siku hizi wanachoogopa, ndio maana wanakimbilia kuomba namba za simu, ili hata wakizodolewa iwe kwa njia ya meseji haiumizi kama ya ana kwa ana. Ebu tuache woga bwana.

©Mwananchi
 
Nako 2 nako wana wimbo wao sehemu ya shairi inasema "hatutaki namba tunahitaji kuchapana" dawa ya hawa pisi unamchana direct to the point kuwa nataka tunyanduane kama Kuna mengine yatafuata tutajua mbele, hiyo namba anakupa ili kuarrange game
 
Kaniuliza kama nina demu nikamwambia sina/
Anahisi ashaniona sehemu tatizo kanisahau jina/

Unaitwa nani? Ncha Kali
Unaishi wapi? Ghetto
Kazi yako nini? Mpishi

Domo linakuwa zito niongee kipi cha maana!
Kivipi nimkazie jicho wakati mtoto kasimama!
Au nijikombee maujiko kwamba sitaki kujuana?
 
Ukweli ni kwamba mishipa ya aibu za wanawake wengi imeshakatika unaongea na. Mtoto mzuri ana kwa ana anakukazia macho hawezi hata kuyalegeza anakuskiliza kwa makini mpaka mwamba unaanza kujistukia tayari uwoga unakuvamia mdogo unaisha maneno ukimya unakitawala na aibu juuu sasa mpira unakuwa umesogea kwake anaanza kukuzodowa na kukutolea kauli mbovu mnyamwezi unaamuwa kusepa hili ni moja.

Mbili ni hivi mazingira huwa yantufanya tukose kujiamini mtoto mzuri umekutana naye kwenye daladala au uchochoroni imagine umekuna na mtoto mzuri umetana naye lets say bar or lounge hivi kwa jinsi mvinyo na maneno matamu yanayotoka kinywani mwakao yatakunyima point.

Tatu sometime jaribu kutumia vitu kinachoweza kukutowa aibu story fupi kuna jamaa tulikuwa tumekaa naye jamaa ni mtumiaji wa marijuana mzuri kabisa ghafla akakipata katoto kazuri jamaa akakifuata na kuanza kuzoza mara wakaja pale tulipokuwa tumekaa jamaa aakaanza kushusha makombora yule jamaa nilimuona kma mchawi maana zilishuka kombora namuona binti akaanza kulegea taratibu.
 
Kaniuliza kama nina demu nikamwambia sina/
Anahisi ashaniona sehemu tatizo kanisahau jina/

Unaitwa nani? Ncha Kali
Unaishi wapi? Ghetto
Kazi yako nini? Mpishi

Domo linakuwa zito niongee kipi cha maana!
Kivipi nimkazie jicho wakati mtoto kasimama!
Au nijikombee maujiko kwamba sitaki kujuana?
Laiti usinizingue kihivyo simuachi huyu kimwana,unaonekana muhenga ndugu, ifike mahali ufe sasa umshaishi vya kutosha
 
Laiti usinizingue kihivyo simuachi huyu kimwana,unaonekana muhenga ndugu, ifike mahali ufe sasa umshaishi vya kutosha

Dadadeeki nikifa leo haya maisha nayadai kinyama, ndo kwanza yameanza kunilipa juzi juzi tu… ila naamini nipo kipindi cha pili (second half![emoji22])
 
  • Usiku kwenye daladala, saa ya simu yangu inaonyesha ni saa 4:47. Najilazamisha kuacha kusinzia, mara nasikia sauti za wanawake wawili wakizungumza viti vya nyuma yangu… stori zao zinanisaidia kukimbiza usingizi wangu.

Usiku kwenye daladala, saa ya simu yangu inaonyesha ni saa 4:47. Najilazamisha kuacha kusinzia, mara nasikia sauti za wanawake wawili wakizungumza viti vya nyuma yangu… stori zao zinanisaidia kukimbiza usingizi wangu.

Nasikia mmoja anamwambia mwenzake; “basi wakati namalizia kuosha vyombo akaja, eti ananiuliza vipi sasa? Nikajifanya sijui kinachoendelea, nikamuuliza vipi kuhusu nini? Akanambia nilichokuomba mchana, nikamuuliza kipi? Yaani nilikuwa najifanya kama vile nimesahau kila kitu, sikumbuki chochote.

“Basi akajizugisha zugisha pale ndio akanambia, nilikuomba namba yako. Nikamuuliza ya nini? Akanambia maswali gani hayo, nikamwambia si namba yangu, nitakupaje bila kujua ya nini. Akanambia kuna vitu nataka tuongee. Nikamwambia si uviongee hapa hapa. Akaniuliza kwani tukiongea kwenye simu kuna shida gani? Na mimi nikamuuliza kwani tukiongea hapa hapa huku tunaonana uso kwa macho kuna tatizo gani?

“Akaishiwa maneno, akanambia haya, nimeshindwa mimi, akaondoka.”

Nikiwa kwenye kiti changu nikajikuta natamani kugeuka kuwatazama hawa wanawake wawili angalau nijue wanaonekanaje, lakini tatizo ni kwamba, kama ningefanya hivyo ingeonekana wazi kwamba nawasikiliza na mimi nilikuwa sitaki tufikie huko nikaamua kujituliza, nikaishia kutengeneza picha ya namna walivyo nikitumia sauti zao na aina ya mazungumzo waliyokuwa wanayaongea kwa sauti bila soni kwenye usafiri wa umma.

Basi nikasikia yule mwanamke mwingine akicheka, yule msikilizaji; “He he heeee! Umemkomesha. Yaani hiyo ndio dawa ya vijanaume vya siku hizi. Vinapenda penda lakini havijui kutongoza, yaani tangu zimekuja simu na meseji wanaume hawajiamini kabisa kuongea mubashara. Wanakimbilia kuomba namba ya simu ili watume vimeseji vyao vya ajabu ajabu.”

Mwenzake akadakia; “Na emoji za kopa kopa.” kisha wote wakacheka kwa sauti utasema kwenye gari hakuna abiria wengine.

Ukiachana na kukosa aibu kiasi kwamba wanaweza kuongea mazungumzo ya aina hii kwenye usafiri wa umma, kitu walichokuwa wanakiongea huenda kina ukweli, wanaume siku hizi hatujiamini sana, hatujui kucheza na maneno kabisa, hususan uso kwa uso.

Ndiyo, tunajua vigori wenyewe siku hizi hawaelewi maneno makavu, kama ni mwanamume suruali utaimba mashairi yote, kuanzia ya hayati Sheikh Shaaban Robert mpaka ya William Shakespeare hutopata kitu, lakini hiyo haitunyimi uhuru wa kuonyesha makali yetu ya kusimama uso kwa uso na mrembo na kumuelezea yaliyojaa kwenye mtima wako.

Unajua uzuri wa kurusha makombora uso kwa uso ni kwamba ukikutana na kichwa ngumu anakuzodoa unaondoka umenywea, lakini bado ndani unajiona kidume. Na hiyo kuzodolewa ndio vijana siku hizi wanachoogopa, ndio maana wanakimbilia kuomba namba za simu, ili hata wakizodolewa iwe kwa njia ya meseji haiumizi kama ya ana kwa ana. Ebu tuache woga bwana.

GAZETI MWANANCHI"
 
Mimi siogopi kabisa na naenjoy kutongoza rekodi yangu ni kumtongoza koplo wa polisi aliekuja kusimamia mtihani wangu wa kidato cha sita nkisubiri kwenda kufanya dissection ya mende
Yes nlimtongoza akiwa amebeba sub machine gun yake half magazine..
Mara ya mwsho nlitongoza kiziwi kwenye basi ya abood nlikua nkiongea anasmile tu kumbe anisikiii
 
Mimi siogopi kabisa na naenjoy kutongoza rekodi yangu ni kumtongoza koplo wa polisi aliekuja kusimamia mtihani wangu wa kidato cha sita nkisubiri kwenda kufanya dissection ya mende
Yes nlimtongoza akiwa amebeba sub machine gun yake half magazine..
Mara ya mwsho nlitongoza kiziwi kwenye basi ya abood nlikua nkiongea anasmile tu kumbe anisikiii
😁😁😁 Daah. JF is never boring. Where we dare to talk openly.
 
Back
Top Bottom