View attachment 1848831
View attachment 1848927
View attachment 1848950
Soko Kuu la Kariakoo jijini Dar es Salaam linaungua moto usiku huu huku jitihada za kuuzima zikiendelea.
Akizungumza na Mwananchi kwa simu, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla amethibitisha tukio hilo.
Makalla ambaye yuko kwenye eneo la tukio, amesema; “Ni kweli soko linaungua na tuko hapa tunapambana kuuzima moto”
Amesema moto huo umeanza kuwaka Saa 3:30 na chanzo bado hakijajulikana.
“Moto umeanza kama nusu saa iliyopita, tupo kwenye eneo tunapambana kuuzima” amesema Makalla ambaye hakutaja chanzo cha moto huo.