Sokoine University of Agriculture (SUA) special Thread

Siasa na kujipendekeza,elimu ya vitendo imepungua,kudahili wanafunzi wengi kuzidi uwezo,kile ni chuo cha kilimo chenye eneo kubwa la wazi linalofaa kwa kilimo ila halitumiki.
Elimu ya juu hatulimi mashamba makubwa. Just some potions for assessment mnatakiwa kujua hilo.
 
 
Mkuu Mukimbiri umenikumbusha mbali, herberium tuliandaa na lecturer mmoja alikuwa anaitwa Dr Mnyanziza, kama unamkumbuka.
 
Mkuu Mukimbiri umenikumbusha mbali, herberium tuliandaa na lecturer mmoja alikuwa anaitwa Dr Mnyanziza, kama unamkumbuka.
Simkumbuki. Sisi tulifanya na Prof. Temu. Ilikuwa ile ya kukausha na moto lakini majani yasiungue. Ilikuwa mnapeana zamu kulinda herbarium. Wakati nimejipumzisha kidogo jamaa wakaniita kwamba herbarium yangu inaungua. Kilichomoka speed hadi nikapoteza simu.
 
Du! Pole sana mkuu. Sio kwa mchomoko huo aisee. Sisi kipindi kile mfumo wa ukaushaji wa majani likuwa tofauti....ulikuwa unaweka mmea kwenye file na ku-press na kifaa fulani hivi unauacha unakauka wenyewe taratibu.
 
Ni kwa ajili ya kupanulia ujenzi wa chuo na lingine linatumika kama puffer zone inayotenganisha mashamba ya wenyeji.
Duh sua lini ikawaza kupanua ujenzi?
Njoo hapa mazimbu uone maajabu.
 
Duh sua lini ikawaza kupanua ujenzi?
Njoo hapa mazimbu uone maajabu.
Ujenzi utapanuliwa tu hapo baadaye, hasa idadi ya kozi itakapoongezeka. Badala ya kuja kuwahamisha wananchi, watatumia ardhi yao bila tatizo.
 
Najua kile kitaasisi hakifai kuendesha elimu nchini,wabaki na kufanya tafiti za kilimo na wanyama wao tu,hapo 100%,ulishaona chuo kikuu hakina ramani?,nenda sua haipo ramani.

Kuna postgrad student wao atanipa docs za mambo yanayofanyika pale yakikiuka taratibu za kielimu miaka ya karibuni hii,akinipa nitayaweka wazi hapa kwa TCU,wizara ya elimu na serikali kwa ujumla.
 
 
Chuo kigumu sana, yaani ukiingia SUA utasoma tu utake usitake, mkionekana wanafunzi mnazurura sana basi ujue mnajitafutia balaa za assignment na test za kila jumapili ili mtulie kusoma.
 
Chuo kigumu sana, yaani ukiingia SUA utasoma tu utake usitake, mkionekana wanafunzi mnazurura sana basi ujue mnajitafutia balaa za assignment na test za kila jumapili ili mtulie kusoma.
Jamani acheni uongo,hivi mnaongelea Sua ipi nyie watu?
Mimi ninaijua sua kwa kukaa morogoro miaka zaidi ya 7,,

Kuna elimu inatolewa ni miyeyusho tu.
Sua ya sasa ni tofauti na miaka kikiwa chuo cha kilimo,sasa hivi ni chuo cha kisiasa,na hizi sifa za uongo zimefanya wale viongozi wamejisahau.

Labda uje useme ni kozi zipi,ila kama ni za huku mazimbu tusidanganyane wandugu.
 
Hebu tumwagie nondo mkuu. Inaonekana una nondo za kutosha kuhusu elimu inayotolewa SUA kwa sasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…