Ndondocha mkuu
JF-Expert Member
- Feb 17, 2014
- 2,490
- 2,965
- Thread starter
-
- #41
Hahahaha, Mkuu maisha yanamengi, nazan tapeli anagonga GAMBE leoHuyo bodaboda Happ atawakumbuka wanaosema wafunge vifaa maalumu kufuatilia vyomba vyao sipati picha jamaa anahali gani usk huu huenda akisikia hata honi anatoka kuangalia km jamaa karudisha chombo
Poleni! Mlikwenda kutembezwa kwa gharama kubwa.Mh hawa watu ni hatari.
Nilikua nashinda kijiwe kimoja hivi cha kuuza maua. Siku hiyo akaja jamaa akauliza bei ya maua akatajiwa akasema atakuja kesho yake, alitaka maua ya zaidi ya laki 2.
Kesho akaja huku akiwa amekodi kirikuu kabisa, basi akatoa 20 kama tip ya vijana kumbebea maua. Tumemaliza akasema inabidi twende naye kwake ili tumshushie, tukakubali. Pesa ya maua akasema anaenda kuitoa benki Mlimani City.
Njiani akamwambia dereva wa kirikuu ampe laki 4 akamtumie mkewe akifik Mlimani akishatoa pesa atamrudishia. Dereva akajibu ana laki 2 tu, mshua wa maua akajibu ana laki jamaa akasema agewe tu hiyo hiyo.
Akaomba simu ya mshua wa maua ili atumie kuandika namba pembeni, mshua akatoa. Simu ilikua Hauwei Y6 Pro (at that time ilikua ni bonge la simu). Alivyogewa akashuka akaingia money shop akarudi tukaendelea na safari. Simu hajarudisha hapo
Kisha ikaja mada ya video ya mfanyakazi akimkanyaga mtoto na abuse kibao, mada ilivyopamba moto dereva kirikuu akasema halafu ninayo kwenye simu, mnunua maua akasema hebu nione. Akagewa simu akaangalia kisha akabaki nayo pia. Hii ilikua Tecno sikumbuki aina gani.
Tulivyofika Mlimani jamaa akashuka, akaingia ndani mule watu tukawa nje tunamsubiri. Baada ya muda kupita mshua wa maua akasema ebwana tuingie ndani tumshtue kua muda unaenda, jamaa alisema anaingia CRDB. Wakaingia, baada ya muda wanatoka wanasema mshkaji hayupo.
Kwa jinsi alivyo nadhifu na mchangamfu kumuwazia utapeli haikua rahisi, mshua wa maua akasema pigeni namba yangu, tunapiga simu haipatikani tukajaribu na ya dereva kirikuu ikawa haipatikani.
Jibu tukawa tushapata. Mshua wa maua anataka kumpiga dereva kirikuu akisema kashirikiana na yule bwana. Mwisho kila mtu akaamini kua ndiyo kashalizwa. Dereva kirikuu akasema hapa hapandi mtu gari langu maua yenu nayatupa. Katika ile 20 tukampa 5 ndiyo akakubali kuturudisha kijiweni.
Ukiwa masikini wa pesa hujiamini.Nahisi ni ile kuona mtu bado mpo naye na mnaenda kwake hivyo utaipata muda wowote au kuhofia kuonekana huna imani na mtu ambaye huko benki atatoka na zaidi ya laki 5.
Haaaaaahaaaaa jamaa umenchekesha kishenzi uulizaji wako hadi mtu ataogopa kusema yeye yuko wapi hapo!View attachment 1482604
Halafu huyu si mtoto kabisa...!
Kijiwe chenu kinaajirije watoto wadogo, afu we ndiye yupi hapo...
HahahaaHaaaaaahaaaaa jamaa umenchekesha kishenzi uulizaji wako hadi mtu ataogopa kusema yeye yuko wapi hapo!
Boda boda pengine kapata kwa mkopo au kujibana mpaka kakonda..leo anaibiwa mchana kweupe..akitoka hapo usishangae na yeye anakuwa katili ... ..maana machungu yake..dah aisee hapo kwa style hiyo hutoki lazima utabananishwa ukutani,roho inaniuma sana kwa huyo boda boda najaribu kuvaa viatu vyake da naona vinanipwaya sana
Nacheka utafikili mazuri lakini moyoni inauma mkuu achaHuyo bodaboda Happ atawakumbuka wanaosema wafunge vifaa maalumu kufuatilia vyomba vyao sipati picha jamaa anahali gani usk huu huenda akisikia hata honi anatoka kuangalia km jamaa karudisha chombo
Hiyo ni hadithi nyingine. Hebu tiririka hapa jamvini.Amtafute yule aliyeibiwa ng'ombe Mwanza
mpe pole huyo jamaa aiseeWakuu habarini za Mda Huu, Nina Kisa kimoja leo kama mnavyojua baada ya kumaliza Chuo Basi tunavyosubiri milioni Basi tunatafuta Buku.
Jana majira ya saa 4 Asubuhi nikiwa katika kijiwe changu cha kuchimba mchanga mgumu alitokea mteja mmoja aliyekua kavalia nadhifu sana akiwa ameshuka bodaboda kama abiria, kutokana na njaa niliyonayo ilibidi nimfate haraka nikijua labda Ni boss anaejenga apartment hapa mjini Basi amekuja kuchukua mchanga angalau trip 10.
Nikweli niliongeanae akasema anataka mchanga trip 4, na Bahati Nzuri kulikua na gari kubwa inamaliza kubeba mchanga trip ya mwisho Basi wakakubaliana na dereva ambebee mchanga wake Huku Mimi nikiongezewa dau toka 60000-70000 kwa trip.
Vijana walianza kupakia mchanga kwa kasi sana, Huku boss akiwa pembeni Kuna bucha akiagiza Nyama kg1 na baada ya hapo alimuomba pikipiki yule boda aliyekuja nae( ambae walionekana kuchangamkiana) Ili boss apeleke mboga nyumbani fasta sana Huku akidai atest isije ikawa kasahau kuendeshea.
Vijana wa kazi walimaliza kazi Huku tukimsubiri boss apande mbele Ili Twende location turudi kupakia tena, tulisubiri kwa Nusu saa Hakuna mtu, tukasema labda anasubr iive ale lakini mbaka sa 6 Hakuna mtu, tukamuuliza dereva boda kwani ulimtoa wapi huyo mtu, akadai walijuana Jana yake na alimtembeza Jana yake kutwa Huku akiwekewa mafuta ya 30,000.
Tulimuiliza unakujua kwake? Alijibu nilimpeleka sehem akanionyesha nyumba yake kwa mbali, tulimwambia aende lakini ALIPEWA JIBU kua hawamjui mtu huyo. Kijana alianza kuona mkojo unauma, kiungwana nilimuonesha choo.
ALISEMA amenunua pikipiki shilingi milioni 2 na Laki 3, wiki iliyopita, alionekana kuchanganyikiwa sana, Kuna mengi ya kujifunza. Kuhusu mchanga ilibidi tupeleke sehemu Yakwanza Huku bei ikishuka hadi 50,000.
Wanajf, usimuamini mtu KIZEMBE KIZEMBE. Bola Wali Nyama kuliko Walimwengu.
Karibuni kwa mchanga mgumu songea.
0738853634
Sahh mkuuBoda boda pengine kapata kwa mkopo au kujibana mpaka kakonda..leo anaibiwa mchana kweupe..akitoka hapo usishangae na yeye anakuwa katili ... ..maana machungu yake..
kwanini stori za DUDE ameacha kuigiza??Sijui kwanini wakati story inaendelea sura ya DUDE imenijia[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23].
Una uhakika hakuwa dude huyo jamaa???
Anasema hawakwenda sawa na wasafitv,itakuwa maswala ya mkikataba na mshiko.si unajua kazi ile ilikuwa hot sana.Hivi
kwanini stori za DUDE ameacha kuigiza??
Mkuu ina maana DUDE ameshindwa kutafuta mdhamini mwingine?Anasema hawakwenda sawa na wasafitv,itakuwa maswala ya mkikataba na mshiko.si unajua kazi ile ilikuwa hot sana.
Ulivyocheka dudu haikuchomoka kweli kwenye ngwengede.Nimecheka km fala hadi nliyelala nae anashangaa
Mkuu inaweza kua hakumjazia kwa mara mojaStory tamu.....
Huyo dogo wa boda boda alipigwa pikipiki ya aina gani? Maana umesema ilikunywa mafuta ya 30k! Tank yake sio mchezo.
Tuwasiliane Mkuu, Upo kama unaelekea Ruvuma,mtoa madahapo naona umefanikiwa kupiga picha na picha ya raisi vp songea mchanga unapatikana maeneo naitaji
KaribuTuwasiliane Mkuu, Upo kama unaelekea Ruvuma,