Soma unaweza jifunza kitu: Jinsi graduate nilivyopoteza 1.8M niliyoitafuta kwa jasho

Soma unaweza jifunza kitu: Jinsi graduate nilivyopoteza 1.8M niliyoitafuta kwa jasho

Pole mm pia iliwahi nitokea 5M ilipotea hivyo hivyo

Sent from my TECNO W4 using JamiiForums mobile app
Mkuu mbaya zaidi kwangu kueleza wenzangu ikawa shida, nikasema nani ataniamini nilikaa nalo moyoni Siku moja nikaamua kuwaeleza wenzangu na manager wangu.
Asee manager aaliwaka vibaya sana na kunitolea kauli ambazo sio nzuri.
Haya mambo kabla hajakukuta unaweza hisi MTU alifanya kusudi na nimejifunza staff wenzio mnacheka nao vizuri ila Siku yakukute ni wewe na Mungu wako.
 
Pole Sana mwanangu yote hayo ni ktk pilika pilika za kijikwamua magraduate mi nakumbuka nshatoaga 1m kwenye biashara iliyokua inantia hasara nikafanya maamuzi ya pupa ikapigwa yote na mshkaji wangu kabisa Yani machimboni huko...

Cha muhimu piga moyo konde na uamke kwa hasira zaidi ya ulizokua nazo kizitafuta
 
Mie niliibiwa kwenye daladala 6.4 M mwezi uliopita tena ya Ofisi,nikitembea nahisi moyo unachomoka nikikaa nahisi hivyo hivyo ni mateso ambayo sijawi kuyapitia toka kuzaliwa kwangu.
Pole sana mkuu ila next time tujitahidi kupunguza risks 6M unapanda daladala? Si bora hata uchukue bajaji ama Uber tusilaumu sana ilikua siku yako tu yakufundishwa na ulimwengu. Pole
 
Kwenye harakati za utafutaji kupoteza ni sehemu ya maisha.

Jambo la msingi ni kupambana kupunguza risk za kupoteza.

Mimi nilifanya kazi za usiku, nikakusanya zaidi ya 1M nikaenda kulima mihogo huku Kibiti. Haikurudi hata 100.

So, ni kawaida tu.
Nini kilitokea mkuu? Nguruwe walofanya ya nini?
 
Wapendwa wanajf habari za usiku,

Leo akili imetulia nimeona nitoe simulizi fupi ya jinsi nilivyoweza kupoteza tsh 1.8M.

Mara baada ya kugraduate pale SUA na (BSC GM) na kushindwa kupata temple nilijichanga katika kazi mbalimbali kama nyuzi zangu baadhi za nyuma zilivyoelezea mishemishe zangu ikiwemo shughuli za mchanga,tofali na tuition centre.

Kwa mwaka 2020 nilifanikiwa kukusanya kiasi cha shil milion 2 na laki 4 na niliamua hii pesa isikae benk tu kwavile bado naendelea kufight na mambo mengine bas niliamua kufanya biashara ya bodaboda.

Nilinunua bodaboda iliyokaribia kuisha kwa mkataba kwa tsh1l 1.8M na kumkabidh mtu aendeshe kwa makubaliano tuliyoafikiana. Nilkua namfaham lakini nilikua simjui sana kiundani na ndugu zake sana nilikuwa siwafaham sana.

Nadiriki kusema nimeweza kupewa mrejesho wa sku 10 pekee na mda huu navyoongea zimepita takribani wiki 3 sijaweza kuonana wala kuwasiliana na dereva wangu, polisi nimeripoti kwa kufata taratibu lakin sion matumaini ya kupata chombo changu, sijui mwenzangu ni mzima au ameaga dunia, nimejarbu kufatilia watu wake imeonyesha ni mhamiaj katika maeneo ya mkoa niliopo.

Nawaza sana, nimeweza kupoteza pesa niliyoitafuta kwa jasho sana ndani ya mwaka mmoja, nikiri sikuweza kulala kwa siku 2 mfululizo, Nimeamini hii dunia haina huruma.

Kuna muda nawaza ile ela bola ningeweka tu ,kuna muda nawaza sana nikiona mtu anaongelea pesa tu nawaza zile pesa zangu, nmebaki na kias cha laki 5 kwenye akaunt yangu nawaza lini nitafika tena kwenye milioni mbili na laki 4.

Kuna muda hua nawaza sana nikifikiria njia ngumu nilizoweza kupata hii pesa ,na njia rahs ilivyoweza kupotea hii pesa,kuna muda niliona haya maisha hayana maana, na kupitia huu mkasa i was so harsh, niliweza had kuseparate na mtu wangu ,ok ni hayo tu nimeona nishare nanyi wakubwa.

Muwe na usiku mwema.

Pole sanaa ndugu amini usiamini anaekuibaia anakuongezea utajiri, ngoja nikupe short yangu kidogo nipo kwa taasisi ya umma flani basi kuna kazi ikatokea ya kutengeneza madirisha ya ofisi ikatoka kama 2 mil kwaajili ya kazi hiyo. Sasa pale mtaani kuna mwana nilimzoea ana kijiwe chake ni fundi fundi mara nyingi alikuwa ananilalamikia kuhusu kazi basi nikaona nimuunganishe kama kawaida.

Ofisi yetu huwa ina tabia ya kukuamini mtumishi, unapewa hela yote kajingaike nayo nikamkumbuka jamaa nikamuunganisha jamaa akaomba hela robo tatu afuate material nikampa akafuata akarudi na material chache kazi ikaanza. Ebwanaee sujui alipatwa na nini jamaa kanikimbia bwanaee na madirisha sikupata msala ukawa wangu boss wangu haeliwi anataka pesa au madirisha mwaka sasa nimetoka kukopa kwa taasisi moja kwa riba chafu nimelipa madirisha yote jamaa mwaka hajaonekana na wala sijui yuko wapi ila process zote nilifuata mikataba na rb ninayo natembea nayo, Mungu si athumani ipo siku tutakutana kinachoniuma sio kuniibia bali kupotezewa credibility pale ofisini sipewi deal tena. Usikate tamaa hadi leo nalipa deni kwa hiyo taasisi. So usife moyo hatujakatwa mikono
 
Pole sanaa ndugu amini usiamini anaekuibaia anakuongezea utajiri ngoja nikupe short yangu kidogo nipo kwa taasisi ya umma flani basi kuna kazi ikatokea ya kutengeneza madirisha ya ofisi ikatoka kama 2mil kwaajili ya kazi hiyo sasa pale mtaani kuna mwana nilimzoea ana kijiwe chake ni fundi fundi mara nyingi alikuwa ananilalamikia kuhusu kazi basi nikaona nimuunganishe kama kawaida ofisi yetu huwa inatabia ya kukuamini mtumishi unapewa hela yote kajngaike nayo nikamkumbuka jamaa nikamuuonganisha jamaa akaomba hela robo tatu afuate material nikampa akafuata akarudi na material chache kazi ikaanza ebwanaee sujui alipatwa na nini jamaa kanikimbia bwanaee na madirisha sikupata msala ukawa wangu boss wangu haeliwi anataka pesa au madirisha mwaka sasa nimetoka kukopa kwa taasisi moja kwa riba chafu nimelipa madirisha yote jamaa mwaka hajaonekana na wala sijui yuko wapi ila process zote nilifuata mikataba na rb ninayo natembea nao mungu si athumani ipo siku tutakutana kinachoniuma sio kuniibia bali kupotezewa credibility pale ofisini sipewi deal tena . Usikate tamaa hadi leo nalipa deni kwa hiyo taasisi. So usife moya hatujakatwa mikono
Pole sana mkuu
 
Back
Top Bottom