Soma upate mawili matatu: Mhitimu mambo ninayopitia kipindi hiki katika harakati zangu

Nimeona mapito yako ila nakuashauri jambo moja “dogo” tu: badilisha jina unalotumia. Amini usiamini limechangia fate yako. What you think you’re is what you will be.
 
Unashindwa nini kuandika maneno kwa ufasaha, ni nini maana ya neno Kaxhkaxh na wewe utajiita msomi?
 
Yeah sifa ya mtoto wa kiume ni kugangamala!! Piga kaziii mzee.
Naona kitu kimepigwa Futo, hapo goma ni iende irudi, piga chepe kaka hakuna kulaza damu, nakua nafarijika sana kuona wanangu na nyie mnapiga kazi bila hiyana.

Binafsi nilipiga sana hizo kazi miaka michache iliyopita,pesa ya inapatikana sana humo ila ndo vile tu hakuna kucheka na kima.
 
Ukiamua kustick kwenye jambo moja stick huko huko, acha kuhangaika kama ngedere anayerukia matawi
Hivi nyie huwa mnaongelea jamii za aina gani? Ujue kuna mambo ukiyajua uhalisia wake huwezi kusema kitu kama hii, unataka kuniambia kuwa jamaa hana Focus kweli?
Unaujua msoto mkuu?,yani unataka jamaa afocus katika kuanzisha may be shule yake wakati huo awe anakufa njaa mtaa eti kisa tu yeye kafocus katika kuanzisha shule ambayo hajui hata pesa ya dawati moja ataipata lini na wakati huo inampasa akatafute pesa ya kula,n.k.

Acha Mwamba ajichange pesa za kujikimu maisha yake kwanza then hayo mambo ya FOCUS yatakuja baadae.
 
hatutofautiani sana
 
Degree zinawaaibu sana Graduates, walioishia lasaba wanaona wakishindwa maisha sawa ila wakimuona Graduate kashindwa maisha hawamuelewi wanampiga pressure za kila namna I.e kasoma lakini anamaisha kama sisi.
Hii point hii. Ni utamaduni wa watanzania. Angalia diaspora vs waliopo Bongo. Mtu aliye diaspora akionekana ana maisha magumu watu wengi hawamuelewi na wanamcheka ila aliye Bongo anaonekana kuwa ana haki ya kuwa na maisha magumu.
 
Hizo ndizo kazi za kiume lazima ukaze "tigo" pamoja na pumbu,naamini hata ukimpata demu unapiga show zetu za kinorth Korea.
Pambana hadi dakika ya mwisho sio wengine ana kidigrii hataki kazi za kutumia nguvu kisa yeye msomi.
Bongo kama huna connection na huna bahati lazima tigo ilowe jasho ili upate pesa hata kama ukitaka kupakuliwa.
 
Achaa tu hilii life liitwe life mm Siku naoa baada ya kumaliza chuo rafiki angu aliyeishia la saba alinichangia laki mbili na kunipa BMW lake buree kama gari ya bibi na bwana harusi .wakati huo mm naunga unga tu mtaani mpaka nika amua kuoa ilii maisha yaendelee sababu huwezi subr ajira kwa miaka zaidi ya mitano ndo uanze maisha ya familia .ilaa nashukuru mungu Leo sio sawa na Jana .nakushukuru Sana'a rafiki anguu uliyefeli darasa la saba ukaanza biashara ya samaki .

Sent from my TECNO CF7 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu uko kwenye a very right track, as long as umeshaanza hiyo Channel ya michanga komaa nayo aibu weka pembeni..

Kikubwa Fanya hiyo kazi kwa bidii kubwa na malengo makuu. Huku ukiweka akiba. Soma mazingira yote na fursa mbali mbali siku kiasi kikiongozeka kitumie kama mtaji aidha kuipanua biashara ya mchanga au kuongeza biashara nyingine.

Unaweza kuanziasha hata kijiwe cha kuuza mchanga Wa madebe kwenye maeneo yanayokuzunguka, watu watakucheka Ila baadaye watakuelewa. Hapo hapo uza mpaka sementi ya kupima kwa makopo au kilo na kokoto.. Ukiweza anzisha kimradi kidogo tu cha kutengeneza roovers zile za ukutani, mtaji ukiongezeka nunua vibao gonga hata tofali uwe unauzia wahitaji wadogo wadogo.. Lengo lako kuu iwe ni kukua kila siku.

Utatoboa, utatoboa amini amini nakuambia.. Nimepitia the same path unayopita sasa hivi.
 
Shukran
 
Tatizo lako unaangalia macho ya watu jichanganye wakikushangaa na wewe washangae. Kwa mfano ulipojificha ticha mkuu asikuone huenda anajua wewe ni kichwa ungeongea nae angekupatia ata connection private school ila wewe unajificha. Futa kwanza idea ya watu watanionaje maana ukiwa na hio hautakaa ufanikiwe ata ukipewa connection
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…