General Nguli
JF-Expert Member
- Apr 22, 2022
- 1,190
- 2,508
Acha nikae karibu na huu uzi...Kuna la kujifunza kwa wale ambao bado hatuja jipata.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kampuni nyingi za bongo laptop, simu,Ipad wanatoza kwa PC siyo cbm.Vitu kama laptops, computer displqy unaweza safirisha kwa meli na inakuwa kwa cbm!?
Ingia Insta page ya silent utakuta mawasiliano yao chati nao Kwa whatsup, watakutumia address zao za china inakuwa kama business card, supplier akikuuliza do you have a shipping agent in china? Unamjibu ndiyo harafu unamtumia hiyo business card kama ilivyo, Kwa hiyo baada ya wewe kulipia mzigo ndiyo anaupeleka kwenye warehouse za silent zilizopo china.mkuu, hivi nawasialiana au najiunga vipi na hawa shipping agents kama Silent ocean,? Ili niwatumie
Supplier akifikisha mzigo wako atapewa risti inayothibitisha kuwa mzigo wako umepokelewa na atakutumia kwenye page ya Alibaba mliyokuwa mnachati naye wakati wa manunuziMkuu kuna kitu nahitaj unifahamishe nitajuaje yakwamba agent ashapokea mzgo
Mzigo ukifika utapokea ujumbe kwenye simu yako kuwa mzigo umeshawasili na kukutaka ufanye malipo na baada ya hapo unaenda kwenye warehous(godown) la kampuni uliyosafirishia kuchukua mzigo wako ukiwa na nakala za risti za malipo na risti ile uliyotumiwa na supplier alipofikisha mzigo wako(rist ya mzigo kupokelewa china kwenye godown unaonyesha kwa kutumia simu yako kama uliyotumiwa na supplier)unafuata bandarini mwenyewe au unaletewa ulipo?
Hii ndiyo maana ya china, hizo bei ni halisiZile bei ndogo kwa Tanzania shilling je ni sahihi au wana namna
Uzi poa sana kaka, ziko site nyingine zenye bei chini ya Alibaba kama 1688, Pinduoduo n.kNingependa kutoa somo la bure kwa wale ambao wanawaza jinsi gani wanaweza kuanza kuagiza bidhaa kutoka china.
Bidhaa hizi ni za jumla kwa ajili ya biashara.
Utaagiza moja kwa moja kutoka kwa wazalishaji.
Kupitia uzi huu utaweza kuona bei halisi za bidhaa pamoja na kujua ni jinsi gani utasafirisha mpaka mzigo unakufikia ulipo.
Pia utafahamu ni kwa namna gani utamtambua mzalishaji gani wa bidhaa utaweza kumtumia na yupi sio salama kumtumia.kuokoa pesa zako zisipotee.
Haya yote utaweza kuyafanya kupitia simu yako ya mkononi.
Niamini mimi haya mambo yanawezekana huhitaji mtu wa kukushika mkono zaidi ya huu mwongozo.
Watu wanapiga pesa kwa kuagiza bidhaa kupitia mtandaoni tu bila hata ya kukanyaga china.
Bidhaa utakayouziwa bongo 80,000 - 100,000.Jua mfanyabiashara huyo kainunua china 20,000 - 30,000.
View attachment 2945112
Bei ya china
View attachment 2945113
Bei ya Kuuzia Tanzania
Ijapokuwa kuna gharama za usafiri ila haiwezi zidi 15,000 mpaka 20,000 kwa kila blender.. hapo utaona gharama mpaka inamfikia mkononi mfanyabiashara ni 35,000 mpaka 40,000.
Ingia alibaba fanya utafiti wa bidhaa mbalimbali naamini huwezi kosa idea ya nini utaweza kuagiza na kuanza kuuza kwa faida nzuri.
Hata kama huhitaji kwa sasa embu download hii application, ufanye japo research ya kujua bei za bidhaa zipo vipi huko viwandani na huku masokoni wanauzaje.
Chunguza bidhaa zinazouzika mtandoni au madukani kisha jaribu kuja kuangalia viwandani china wanauzaje..kisha ujionee ni kwa jinsi gani watu wanapiga faida ndefu.
Tena kwa mikoani ndio usiseme.Kama mtu akinunua mzigo kariakoo anapata faida jee akiagiza kutoka china moja kwa moja itakuwaje?
HATUA YA KWANZA
1.Download application ya alibaba kupitia playstore au appstore.
Hiki ni zoezi rahisi tu.Ingia play store kwa wale wa android na appstore kwa wale wa iphone.
Application inaitwa alibaba
View attachment 2945124
Kisha idownload hakikisha unajisajili kupitia email ambyo ipo active kwenye simu yako na pia utakapohitajika kuweka namba ya simu weka namba ambayo ipo active kwenye simu yako.
ili watakapohitaji kufanya verification email na simu yako ziwe active kwa zoezi hilo.
Hatua hii ni fupi sana. Achana na taarifa za biashara wewe weka tu taarifa zako binafsi kisha anza kuperuzi..
Baada ya kujisajili unaweza kuamua kubadili fedha itakayoonekana kweny bidhaa ili uweze kupata picha ya bei kwa pesa yetu ya Tanzania.
Chini kulia kuna neno alibaba bonyezahl hapo kisha juu kulia utaona USD sasa ibonyeze kisha tafuta pesa ya tanzania TZS ili bidhaa zote zionekane kwa bei ya tzs
View attachment 2945131
Baada ya hapo unaweza sasa kuanza kutafuta bidhaa.
Kuna aina kuu mbili za utafutaji ningekushauri uanze nazo
.Kutafuta bidhaa (product)
.Kutafuta mzalishaji wa hiyo bidhaa (Supplier/manufacturer)
View attachment 2945132
Hapo juu utaona nimeandika hand bags halafu juu yake kuna maneno mawili products na manufacturers
Hapo juu nimechagua products ndii maana unaziona bidhaw mbalimbali na bei zake.
Ukichagua products wanakuletea bidhaa tu na ukichagua manufacturers wanakuletea viwanda/wauzaji wa hizo bidhaa tu.
Ili kama utataka kuona wauzaji uweze kuangalia bidhaa zao mbalimbali zinazohusiana na bidhaa uliyochagua.
Hapa chini nimechagua manufacturers/supplier utaona wananiletea majina ya viwanda au wauzaji wa aina hizo za bidhaa
View attachment 2945137
MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KATIKA KUMCHAGUA SUPPLIER MZURI
1.Hakikisha ana alama ya verified (angalia picha hapo juu)
2.Mbele ya neno verified kuna miaka ambayo yupo katika mtandao wa alibaba.Kuanzia miaka 2 na kuendelea si mbaya ila angalia sifa ya 3 kujiridhisha zaidi
3.Angalia review (wanunuzi wanamzungumziaje huyu muuzaji)
hili ni muhimu pia.
View attachment 2945145
View attachment 2945146
Review itakusaidia kupata picha ya jinsi mzalishaji huyo au msambazaji anavyohudumia wateja wengine au ubora wa bidhaa yake..
Kitu kingine ni Trade Assuarance. Hii ni huduma ya alibaba ambayo pesa yako inakuwa haiend moja kwa moja kwa muuzaji mpaka alibaba watakapo kuridhisha kuwa hauna malalamiko yoyote juu ya muuzaji huyo.
View attachment 2945148
Unaweza muuliza huyo muuza kupitia chat now hapo kama ana support trade Assuarance.
Kitu unachotakiwa kufanya utakapo jiridhisha na bidhaa husika ni kubonyeza hiyo chat now ili uweze kuchat na muuzaji kabla hamjakubaliana kufanya malipo.
Unaweza muuliza wanaweza kuuuzia bidhaa ngapi kama MOQ (minimum order quantity) yaan idadi ndogo wanazoruhusu mtu kununua kutoka kwao.
Wapo wafanyabiashara wanaruhusu bidhaa kuanzia 10 wengine kuanzi 100 wengine 5 au hata 1.
Sasa ipo hivi ikiwa unataka ujihakikishie ubora wa bidhaa yaan uipate kwanza 1 ujiridhishe zaidi ongea na huyo suppier akutumie sample 1 ya bidhaa yao kwa njia ya ndege ili ukiipata hiyo bidhaa utajiri dhisha na kuamua kununua bidhaa nyingi zaidi kwa ajili ya biashara.
Hii itakusaidia kujiondoa katika riski ya kuagiza mzigo mkubwa ambao ukifika utajutia kwa kuwa haukidhi vigezo vyako.
Japo bei ya bidhaa ya sample 1 huwa kubwa kidogo ila ni bora zaidi kwa kuwa unajiridhisha kwa mara ya kwanza kujua ubora wa bidhaa.View attachment 2945152
Ukisha fanya resarch yako ya kutosha na ukaona umejiridhisha na bidhaa na bei na idadi ya bidhaa unazohitaji.
Mambo ya muhimu ya kuzingatia maana hapo ni bei ya bidhaa huko china.
unatakiwa ujue huu mzigo kuusafirisha mpaka unakufikia gharama yake ni kiasi gani na utatumia muda gani mpaka kukufikia?
Kuna mizigo unaweza safirisha kwa ndege hiu unawahi kufika inaweza chukua siku 7 tu kulingana na ratiba za ndege.
mizigo hii hupimwa kwa uzito kgs.
Ukishajua uzito wa bidhaa zako unawasiliana na agent wa kukusafirishia mzigo na kumueleza uzito na aina ya mzigo wako ili akupe bei kwa kilogram 1 ni kiasi gani.
Kuna mzigo inabidi uusafirishe kwa meli hii mizigo hupimwa mwa ujazo wa mita CBM (Cubic Metres) yaani urefu * upana * kimo vyotr katika metres.
Hapo unaweza muuliza muuzaji wako huu mzigo una CBM ngapi ukiufunga pamoja.
Muuzaji akikupa CBM nenda kwa agent wako wa kusafirsha mzigo akupe gharama kulingana CBM ya mzigo wako.
Baada ya kuona gharama za mzigo pamoja gharama za usafirishaji unazimudu.
Ndio unaweza kumwambia akuandalie payment link.
Hii ni link maalum ambayo ukiibonyeza inakuletea gharama za kulipia oda yako.
View attachment 2945166
Utaona hapo baada ya kukubaliana na supplier gharama akanipa hiyo link ya kulipia.
Ambayo inahitaji nilipe initial deposit 50% kisha wakimaliza kuandaa mzigo wangu nawamalizia 50% kisha wanatuma.
Hiyo link ukiibonyeza inakupeleka kwenye aina za malipo uchague
Mimi nachaguaga paypal kwakuwa nimeiunga na bank account yangu.
yaan haina longolongo zaidi ya verification ya simu yangu tu.
paypal itanionesha kiasi nacholipia katika usd na kiasi kinachokatwa katika account yangu ya TZS.
View attachment 2945170
Ukibonyeza agree & pay now hakikisha kiasi hicho kipo kwenye account yako.
Hapo malipo yataenda alibaba na supplier atapata taarifa na kuanza kushughulikia oda yako kulingana na makubaliano.
Hakikisha umempa supplier wako address ya agent ambaye atakusafirishia mzigo.
Supplier atapeleka mzigo kwa agent na baada ya hapo ni kazi ya agent kukuletea mzigo wako hapa Tanzania.
Maagent wapo wengi kuna silent ocean, mapembelo cargo, tosh cargo kuna shamwaa n.k.
watafute maagent hawa kisha wakupe address zao za huko china ili supplier apelek mzigo wako kwao.
View attachment 2945177
Hizo ndio hatua utakazohitajika kufuata ili kuweza kuagiza mzigo wako kutoka kwa wazalishaji china mpaka kukufikia Tanzania.
Ubarikiwe sana kiongozi kwa bandiko hiliNingependa kutoa somo la bure kwa wale ambao wanawaza jinsi gani wanaweza kuanza kuagiza bidhaa kutoka china.
Bidhaa hizi ni za jumla kwa ajili ya biashara.
Utaagiza moja kwa moja kutoka kwa wazalishaji.
Kupitia uzi huu utaweza kuona bei halisi za bidhaa pamoja na kujua ni jinsi gani utasafirisha mpaka mzigo unakufikia ulipo.
Pia utafahamu ni kwa namna gani utamtambua mzalishaji gani wa bidhaa utaweza kumtumia na yupi sio salama kumtumia.kuokoa pesa zako zisipotee.
Haya yote utaweza kuyafanya kupitia simu yako ya mkononi.
Niamini mimi haya mambo yanawezekana huhitaji mtu wa kukushika mkono zaidi ya huu mwongozo.
Watu wanapiga pesa kwa kuagiza bidhaa kupitia mtandaoni tu bila hata ya kukanyaga china.
Bidhaa utakayouziwa bongo 80,000 - 100,000.Jua mfanyabiashara huyo kainunua china 20,000 - 30,000.
View attachment 2945112
Bei ya china
View attachment 2945113
Bei ya Kuuzia Tanzania
Ijapokuwa kuna gharama za usafiri ila haiwezi zidi 15,000 mpaka 20,000 kwa kila blender.. hapo utaona gharama mpaka inamfikia mkononi mfanyabiashara ni 35,000 mpaka 40,000.
Ingia alibaba fanya utafiti wa bidhaa mbalimbali naamini huwezi kosa idea ya nini utaweza kuagiza na kuanza kuuza kwa faida nzuri.
Hata kama huhitaji kwa sasa embu download hii application, ufanye japo research ya kujua bei za bidhaa zipo vipi huko viwandani na huku masokoni wanauzaje.
Chunguza bidhaa zinazouzika mtandoni au madukani kisha jaribu kuja kuangalia viwandani china wanauzaje..kisha ujionee ni kwa jinsi gani watu wanapiga faida ndefu.
Tena kwa mikoani ndio usiseme.Kama mtu akinunua mzigo kariakoo anapata faida jee akiagiza kutoka china moja kwa moja itakuwaje?
HATUA YA KWANZA
1.Download application ya alibaba kupitia playstore au appstore.
Hiki ni zoezi rahisi tu.Ingia play store kwa wale wa android na appstore kwa wale wa iphone.
Application inaitwa alibaba
View attachment 2945124
Kisha idownload hakikisha unajisajili kupitia email ambyo ipo active kwenye simu yako na pia utakapohitajika kuweka namba ya simu weka namba ambayo ipo active kwenye simu yako.
ili watakapohitaji kufanya verification email na simu yako ziwe active kwa zoezi hilo.
Hatua hii ni fupi sana. Achana na taarifa za biashara wewe weka tu taarifa zako binafsi kisha anza kuperuzi..
Baada ya kujisajili unaweza kuamua kubadili fedha itakayoonekana kweny bidhaa ili uweze kupata picha ya bei kwa pesa yetu ya Tanzania.
Chini kulia kuna neno alibaba bonyezahl hapo kisha juu kulia utaona USD sasa ibonyeze kisha tafuta pesa ya tanzania TZS ili bidhaa zote zionekane kwa bei ya tzs
View attachment 2945131
Baada ya hapo unaweza sasa kuanza kutafuta bidhaa.
Kuna aina kuu mbili za utafutaji ningekushauri uanze nazo
.Kutafuta bidhaa (product)
.Kutafuta mzalishaji wa hiyo bidhaa (Supplier/manufacturer)
View attachment 2945132
Hapo juu utaona nimeandika hand bags halafu juu yake kuna maneno mawili products na manufacturers
Hapo juu nimechagua products ndii maana unaziona bidhaw mbalimbali na bei zake.
Ukichagua products wanakuletea bidhaa tu na ukichagua manufacturers wanakuletea viwanda/wauzaji wa hizo bidhaa tu.
Ili kama utataka kuona wauzaji uweze kuangalia bidhaa zao mbalimbali zinazohusiana na bidhaa uliyochagua.
Hapa chini nimechagua manufacturers/supplier utaona wananiletea majina ya viwanda au wauzaji wa aina hizo za bidhaa
View attachment 2945137
MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KATIKA KUMCHAGUA SUPPLIER MZURI
1.Hakikisha ana alama ya verified (angalia picha hapo juu)
2.Mbele ya neno verified kuna miaka ambayo yupo katika mtandao wa alibaba.Kuanzia miaka 2 na kuendelea si mbaya ila angalia sifa ya 3 kujiridhisha zaidi
3.Angalia review (wanunuzi wanamzungumziaje huyu muuzaji)
hili ni muhimu pia.
View attachment 2945145
View attachment 2945146
Review itakusaidia kupata picha ya jinsi mzalishaji huyo au msambazaji anavyohudumia wateja wengine au ubora wa bidhaa yake..
Kitu kingine ni Trade Assuarance. Hii ni huduma ya alibaba ambayo pesa yako inakuwa haiend moja kwa moja kwa muuzaji mpaka alibaba watakapo kuridhisha kuwa hauna malalamiko yoyote juu ya muuzaji huyo.
View attachment 2945148
Unaweza muuliza huyo muuza kupitia chat now hapo kama ana support trade Assuarance.
Kitu unachotakiwa kufanya utakapo jiridhisha na bidhaa husika ni kubonyeza hiyo chat now ili uweze kuchat na muuzaji kabla hamjakubaliana kufanya malipo.
Unaweza muuliza wanaweza kuuuzia bidhaa ngapi kama MOQ (minimum order quantity) yaan idadi ndogo wanazoruhusu mtu kununua kutoka kwao.
Wapo wafanyabiashara wanaruhusu bidhaa kuanzia 10 wengine kuanzi 100 wengine 5 au hata 1.
Sasa ipo hivi ikiwa unataka ujihakikishie ubora wa bidhaa yaan uipate kwanza 1 ujiridhishe zaidi ongea na huyo suppier akutumie sample 1 ya bidhaa yao kwa njia ya ndege ili ukiipata hiyo bidhaa utajiri dhisha na kuamua kununua bidhaa nyingi zaidi kwa ajili ya biashara.
Hii itakusaidia kujiondoa katika riski ya kuagiza mzigo mkubwa ambao ukifika utajutia kwa kuwa haukidhi vigezo vyako.
Japo bei ya bidhaa ya sample 1 huwa kubwa kidogo ila ni bora zaidi kwa kuwa unajiridhisha kwa mara ya kwanza kujua ubora wa bidhaa.View attachment 2945152
Ukisha fanya resarch yako ya kutosha na ukaona umejiridhisha na bidhaa na bei na idadi ya bidhaa unazohitaji.
Mambo ya muhimu ya kuzingatia maana hapo ni bei ya bidhaa huko china.
unatakiwa ujue huu mzigo kuusafirisha mpaka unakufikia gharama yake ni kiasi gani na utatumia muda gani mpaka kukufikia?
Kuna mizigo unaweza safirisha kwa ndege hiu unawahi kufika inaweza chukua siku 7 tu kulingana na ratiba za ndege.
mizigo hii hupimwa kwa uzito kgs.
Ukishajua uzito wa bidhaa zako unawasiliana na agent wa kukusafirishia mzigo na kumueleza uzito na aina ya mzigo wako ili akupe bei kwa kilogram 1 ni kiasi gani.
Kuna mzigo inabidi uusafirishe kwa meli hii mizigo hupimwa mwa ujazo wa mita CBM (Cubic Metres) yaani urefu * upana * kimo vyotr katika metres.
Hapo unaweza muuliza muuzaji wako huu mzigo una CBM ngapi ukiufunga pamoja.
Muuzaji akikupa CBM nenda kwa agent wako wa kusafirsha mzigo akupe gharama kulingana CBM ya mzigo wako.
Baada ya kuona gharama za mzigo pamoja gharama za usafirishaji unazimudu.
Ndio unaweza kumwambia akuandalie payment link.
Hii ni link maalum ambayo ukiibonyeza inakuletea gharama za kulipia oda yako.
View attachment 2945166
Utaona hapo baada ya kukubaliana na supplier gharama akanipa hiyo link ya kulipia.
Ambayo inahitaji nilipe initial deposit 50% kisha wakimaliza kuandaa mzigo wangu nawamalizia 50% kisha wanatuma.
Hiyo link ukiibonyeza inakupeleka kwenye aina za malipo uchague
Mimi nachaguaga paypal kwakuwa nimeiunga na bank account yangu.
yaan haina longolongo zaidi ya verification ya simu yangu tu.
paypal itanionesha kiasi nacholipia katika usd na kiasi kinachokatwa katika account yangu ya TZS.
View attachment 2945170
Ukibonyeza agree & pay now hakikisha kiasi hicho kipo kwenye account yako.
Hapo malipo yataenda alibaba na supplier atapata taarifa na kuanza kushughulikia oda yako kulingana na makubaliano.
Hakikisha umempa supplier wako address ya agent ambaye atakusafirishia mzigo.
Supplier atapeleka mzigo kwa agent na baada ya hapo ni kazi ya agent kukuletea mzigo wako hapa Tanzania.
Maagent wapo wengi kuna silent ocean, mapembelo cargo, tosh cargo kuna shamwaa n.k.
watafute maagent hawa kisha wakupe address zao za huko china ili supplier apelek mzigo wako kwao.
View attachment 2945177
Hizo ndio hatua utakazohitajika kufuata ili kuweza kuagiza mzigo wako kutoka kwa wazalishaji china mpaka kukufikia Tanzania.
Da nakazia hapo🙏Naomba kujua jinsi ya kujiunga PayPal na account yangu ya bank
Mkuu unaonekana uko legend mwaga Michele kidogo au tuje inboxUzi poa sana kaka, ziko site nyingine zenye bei chini ya Alibaba kama 1688, Pinduoduo n.k
Kwa products zenye quality uhakika, mtu anaweza check taobao.
Tatzo la site nyingi zenye bei nzuri, zina tumia kichina tupu..so uta hitaji translator….
Lakini kwa kuanzia, hapo si pabaya….
Mtu ukijimudu pia ni vyema ukafika china mwenyewe….kule utakuta pia baadhi ya bidhaa bei ni hata nusu ya hizi za alibaba na sites nyingine… issue n upatkanaji wa masoko….wabongo wengi hawatoi code….
Pia masoko yako mbali mbali sana….so uta hitaji mtu wa kukuguide….mimi niliemda kichwa kichwa, nikapoteza mwezi mzima hola….ila round 2 ikabidi nipate mchina, mambo ndo nika yafurahia.
Tukaze wakuu….ukimaster hizo site, unaweza save pakubwa sana, ukicompare na kununua hapa bongo.
NB: Zipo baadhi ya products tayar wachina wana agents bongo…so ukienda hawato kuuzia…. Ni vyema kujua pia hilo, usije fata hewa.
Tuendelee peana nondo.
Nilinunua mzigo wa 1. 2M ila almost mzigo wa 600,000 ni substandard na overpriced kwa bei niliyonunulia. Ingawa kwa kulazimisha nitauza hivyohivyo kurudisha gharama ila hela yangu imelala.Uzi safi
Beba maarifa ila usihadaike na urahisi wa bei.
Fanya utafiti wa kutosha, ingia youtube angalia reviews za hizo bidhaa haswa za umeme.
Kuna watu wengi wamepata hasara kwa kukurupuka, wachina nao ni washenzi, inabidi uwe mshenzi zaidi ili kulijua soko, na bidhaa zako.
Mfano mdogo tu blender aliyotolea mfano mleta uzi, nazifahamu vyema ni takataka, ni mbovu kupindukia zinakufa hovyo, na yote hayo ni kwasababu mchina katumia material zisizokidhi viwango na hivyo kupelekea gharama kuwa chini, kwasababu yeye hajali ikija kukufia huku TZ kama ela yako anakua keshaitafuna kitambo na huna cha kumfanya unabaki na mzigo wa mali mbovu, inabidi na wewe ujenge uhasama na wateja wako maana zitawafia na jina litachafuka.
Pole sana bingwa, ndio unazidi kukomaa kadri unavyoumia ndio unaimarika, utakua bora zaidi kadri unavyosonga.Nilinunua mzigo wa 1. 2M ila almost mzigo wa 600,000 ni substandard na overpriced kwa bei niliyonunulia. Ingawa kwa kulazimisha nitauza hivyohivyo kurudisha gharama ila hela yangu imelala.
Huu mzigo uliokuwa sawa unaenda vizuri. Suppliers wengine wakengefu. Suppliers wasio wa Aliexpress na Alibaba ni wazuri zaidi.
Niliagiza uko sababu MOQ ni ndogo, nilikuwa nataka vitu vidogo ambavyo kwingine mpaka niagize pisi nyingi.
Gharama kama nafuu sana kwa bongo ungenumua lwa kiasi gani?Ni projector ya 35USD na shipping wamenipa 25USD jumla 60USD.
Asante kwa hii experience yako mkuuUzi poa sana kaka, ziko site nyingine zenye bei chini ya Alibaba kama 1688, Pinduoduo n.k
Kwa products zenye quality uhakika, mtu anaweza check taobao.
Tatzo la site nyingi zenye bei nzuri, zina tumia kichina tupu..so uta hitaji translator….
Lakini kwa kuanzia, hapo si pabaya….
Mtu ukijimudu pia ni vyema ukafika china mwenyewe….kule utakuta pia baadhi ya bidhaa bei ni hata nusu ya hizi za alibaba na sites nyingine… issue n upatkanaji wa masoko….wabongo wengi hawatoi code….
Pia masoko yako mbali mbali sana….so uta hitaji mtu wa kukuguide….mimi niliemda kichwa kichwa, nikapoteza mwezi mzima hola….ila round 2 ikabidi nipate mchina, mambo ndo nika yafurahia.
Tukaze wakuu….ukimaster hizo site, unaweza save pakubwa sana, ukicompare na kununua hapa bongo.
NB: Zipo baadhi ya products tayar wachina wana agents bongo…so ukienda hawato kuuzia…. Ni vyema kujua pia hilo, usije fata hewa.
Tuendelee peana nondo.