Somo la 'Historia ya Tanzania' alilotaka Magufuli lasitishwa

Magufuli alikuwa sawa, achaneni kupinga kila jambo:

Tuachane na mtaala wa kikoloni tufundishe watoto wetu historia yetu na ya mababu zetu, tamaduni zetu, mila zetu, ili tukuze uzalendo kwa vizazi vya sasa na vijavyo
Hakuna haja ya kufundisha historia kwa Kiingereza,
Magufuli alikuwa sawa, Profesa Ndalichako harakisheni huo mtaala mpya
 
imagine unafundishwa historia ya mkwawa kiingereza[emoji16][emoji16],sijui ukasimulie wazungu ama!!!
 
Mnamjua mkoloni wewe hata miaka 30 hujatimizi!
 
Uzalendo ni nini?
 
sasa next uzeni ndege mgharamie mswada wa KATIBA yenu mpya! chenj itakayobaki fanyeni semina elekezi namna bora ya kufanya siasa..
 
Vijana wa kijiweni hawajui thamani ya historia. Yawezekana wanaopinga mtaala wa historia ya Taifa hawajui chimbuko la familia zao na tamaduni. Upumbafu na Ulofa
 
Hayati magufuli naona kaangukia pua tena

Somo la historia ya Tanzania lasitishwa

Katibu mkuu wizara ya elimu amesema syllabus hiyo imesitishwa haraka na haitafundishwa kokote.

Source ITV news
Ila maguguli ujue madktari wangechukua kichwa chake wakafanyie uchunguzi ili wajue kama alikua na akili za namna gani,inaweza kutusaidia kuongeza mapato ya nchi pale Makumbusho!
 
Huo mtaala unamsaidia nini kijana baada ya kumaliza elimu yake?

Tafuteni mmabo ya muhimu hata fani za ufundi ndio ziwe za lazima katika ulimwengu huu historia inamchango mdogo sana kwenye maisha ya kila siku.

Kuna SoMo la historia shuleni bado mnatka kulazimisha kuongeza na lingine kwanini msiboreshe hilohilo lililopo mashuleni ikawa mwaka mzima au miwili mtu anasoma historia ya Tanzania kwanini iwe mtu anasoma miaka yote ya shule kwa content ipi ya hiyo historia yetu na itasaidia nini mtu kujikwamua kwenye hili tatizo la ukosefu wa ajira?

Pia hao wataalamu wa kufundisha hiyo historia ya Tanzania mmewaandaa? Swala la mtaala Lina taratibu zake yaani mnataka hiyo historia ifundshwe na watu amabao hat Wao hawajaijua hiyo historia?
 
Hilo SoMo halina umuhimu wowote kwa sababu sioni utofati wake na historia inayosomwa shule ya msingi, zaidi sana ni kuongezea watoto wetu mzigo wa masomo yasiyo na ulazima. Nilichogundua hiyo historia ya Tanzania ulikua imelenga kuwasifu viongozi wa fisiemu na si vinginvyo.
 
Ni upumbavu tuu kuwaza kufundisha Historia kwa kiswahili kuwa utafanikisha jambo lolote la maana wakati somo la kiswahili wanafunzi wanafeli vibaya
 
Yaani hadi Professor Ndelichako anamsaliti Magufuli? Kweli?

Ni Magufuli aliyemuinua Professor Ndelichako kutokea benchi, akampa ubunge wa bure na zawadi ya uwaziri, leo hii bila aibu anaizika legacy ya Magufuli kirahisi.

Nimeamini adui wa mtu ni watu wa karibu yake. Magufuli alizungukwa na wanafiki watupu, akawakumbatia huku akiwaangamiza wapinzani.
 
Haya yalikua ni maamuzi ya kijinga bora yamefutiw mbali.
 
Ni maagizo ya kipumbavu.

Lazima yatupiliwe mbali.
Ila Profesa Ndalichako aliyapokea maagizo kwa heshima na unyenyekevu mkubwa! Ilikuwaje alishindwa kumshawishi Bosi wake kuhusu huo upuuzi!

Na kama Bosi angemkatalia, si angejiuzulu! Au kukubali kufukuzwa Uwaziri na ikibidi hata Ubunge wake wa kuteuliwa kwa heshima! Ila kwa sababu ya njaa, akaamua kuweka taaluma yake pembeni na kuamua kupokea kila aina ya maagizo! Yakiwemo haya ya hovyo!

Njaa na unafiki ni vitu vibaya sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…