Songwe: Basi la Kampuni ya Kilimanjaro Express lapata ajali, watu wanne wafariki dunia

Songwe: Basi la Kampuni ya Kilimanjaro Express lapata ajali, watu wanne wafariki dunia

SAULI nae kapepesa kidogo usiku huu huu hapo hapo Senjele sijui shida nini hapo
Screenshot_20220315-001328_1.jpg


Sent from my TECNO CD6j using JamiiForums mobile app
 
Sio luxury bus wewe, kuitwa luxury ni tofauti na luxury
Njia ya Dar-mbeya-tunduma - swax hakuna luxury bus hata moja
Sio sauli, New force/Golden deer, Imani plus, tanzanite wala Hao kilimanjaro
Wote ni ordinary bus to semi luxury
Mara Ordinary mara Semi Luxury mbona hueleweki bwashee?
 
Survivors in this accident inabidi mtoe Shukrani ya Pekee kwenye makanisa yenu. It's hard to believe there are survivors.
Huyu dreva inabidi asipewe tena driving licence, he is mad
 
Mtu umezoea kuendesha gari dsm unakuja kumpa lawama dereva wa mkoa mnajua wanakutana na mangp jaribu hata ww kuendesha gari dar to moro utaona kama ni simple ivyo
 
Bus la kampuni ya Kilimanjaro limepinduka asububuhi hii mkoani Songwe likitokea Tunduma kuelekea Jijini Dar es salaam ambapo taarifa za awali zinaeleza ajali hiyo imesababisha watu kadhaa kufariki na uwepo wa majeruhi, taarifa kamili zitakujia hivi punde.

===================

Basi la Kampuni ya Kilimanjaro Express limepata ajali kwa kupinduka asubuhi ya leo Machi 14, 2022 Mkoani Songwe wakati likitokea Tunduma kuelekea Jijini Dar es Salaam.

Taarifa za awali za mashuhuda waliopo eneo la tukio zinaeleza ajali hiyo imesababisha watu kadhaa kufariki na uwepo wa majeruhi.

Ofisa Mmoja wa Kilimanjaro Express amekiri kutokea kwa ajali hiyo lakini hakuwa tayari kuelezea kiundani kwa madai siyo msemaji wa kampuni. Juhudi za kumpata RPC wa Songwe, Janeth Mgomi zinaendelea ili kupata ripoti kamili.

UPDATES;

Watu wanne wamefariki papo hapo huku wengine 35 wakijeruhiwa katika ajali ya basi la Kilimanjaro Express lililopindukia korongoni eneo la Senjele wilayani Mbozi Mkoa wa Songwe.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe, Rashid Ngonyani amesema ajali hiyo imetokea saa moja asubuhi baada ya dereva wa basi la Kilimanjaro Express kuwa kwenye mwendokasi na kutaka kuyapita magari mengine yaliyokuwa mbele yake.

Hata hivyo, Mkuu wa Mkoa wa Songwe Omary Mgumba amesema majeruhi wote 35 wanaendelea vizuri ambapo kati yao saba wamelazwa Hospitali ya Wilaya ya Mbeya na wengine 28 wakitibiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Songwe

View attachment 2149697
View attachment 2149696
View attachment 2149698

View attachment 2149968
Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Omary Maumba alimjulia hali miongoni kwa majeruhi wa ajali ya basi kampuni ya Kilimanjaro, Yusuph Ramadhan ambaye yeye na wenzake sita walikimbizwa katika Hospitali Teule ya Ifisi iliyoko mkoani Mbeya. PICHA: Grace Mwakalinga, SONGWE

View attachment 2149979
Hiyo picha ya naona kama Kuna wahuni wameingilia hili tukio Kwa manufaa Yao binafsi, RIP marehemu wote
 
Halafu dereva kama huyo kaua watu kizembe
Halafu anaachiwa mtaani aendelee kuja kuua wengine!

Hivi Kwanini hatuwi seriously kwenye mambo ya msingi yanayohusu Uzima na maisha ya binadamu?
 
Kusema dereva afutiwe leseni haitoshi kuwa adhabu kali hiyo.

Mtu ameua na kusababishia ulemavu wa kudumu wenzie halafu adhabu iwe kufutiwa leseni tu ?

Hapana, haitoshi.
 
Halafu madereva wengine wataendelea
Kuendesha magari kizembe barabarani wakijua hata likitokea la ajali hawatachukuliwa
Adhabu kali.

Eti kufutiwa leseni [emoji848][emoji848]

Futa maisha yataendelea vizuri tu pengine zaidi ya alivyokuwa dereva.

Kwani kazi ni udereva tu? Lakini anakuwa ameshaharibu maisha ya wengine halafu yeye aendelee kula maisha mema mtaani?! Hapana
 
Halafu madereva wengine wataendelea
Kuendesha magari kizembe barabarani wakijua hata likitokea la ajali hawatachukuliwa
Adhabu kali.

Eti kufutiwa leseni [emoji848][emoji848]

Futa maisha yataendelea vizuri tu pengine zaidi ya alivyokuwa dereva.

Kwani kazi ni udereva tu? Lakini anakuwa ameshaharibu maisha ya wengine halafu yeye aendelee kula maisha mema mtaani?! Hapana
Ndugu sibado mahakama Jpo sheria za usalama barabaran adhabu yake si kubwa hTa ukiiuwa mamia
 
Nyanda za juu kusini aina zao za usafiri zinashangaza sana.
Ruti ndefu nyingi hapa Tz hazina gari luxury kama ilivyo ruti fupi fupi za dar - Dom au Dar - Arusha Dar - Tanga.
 
Back
Top Bottom