Soon nakuwa mama wa kambo. Nahitaji maombi yenu na ushauri wa maisha haya mapya

Soon nakuwa mama wa kambo. Nahitaji maombi yenu na ushauri wa maisha haya mapya

Bond, upendo utajengeka tu automatically kutegemea na ninyi wenyewe. Ila cha msingi ni mpokee na mtreat kama ambavyo unawatret watoto wako. Kila mzazi ana parenting style, so mlee kama unavyowalea watoto wako wengine. Kwa kuwa alikuwa analelewa na mama yake, inawezekana yakawa ni malezi ya aina tofauti na ya kwako; so kama kuna vya kubadilisha vibadilishe taratibu na kwa upendo na yeye anaweza akaadapt taratibu kadri anavyokaa na wadogo zake: kuna mengine hutoweza kuyabadili na as long as hayana tatizo basi unayaacha tu. Isijeonekana kana kwamba unajifamya wewe malezi yako ndiyo perfect kuliko ya mama yake; mkaanza mtimbwili.

Yes kuanza kumlea mtoto ambaye tayari ana ufahamu wake sio rahisi sana tofauti na ukianza kumlea mtoto tangu akiwa mdogo. Kuna watoto ni wema tu naturally, labda na mama yake ndiyo wale wenye hekima kashamwambia aje aishi na wewe vizuri so mtajikuta tu taratibu mambo yanakaa sawa.

Au anaweza akaja ashaambiwa kuwa mama wa kambo ni watesaji, au kashajazwa sumu kuwa huyu ndiyo kasababisha baba yako na mama yako wasiwe pamoja, so anakuja ameshajipanga. Don't fight with the kid, prove him/her wrong kwa moyo wako mweupe kwake. Ifike hatua mtoto mwenyewe aanze kujiuliza mbona niliyokuwa naambiwa sio nayoyaona. Akizidi kukuletea majaribu, mkabidhi baba yake.

Kama umeolewa kwenye familia yenye mawifi wanaojirambua basi kheri. Ila kama ndiyo umeolewa kwenye hizi familia zenye mawifi wasiostaarabika, jiandae kisaikolojia kuziba masikio na kujifanya bubu. Maana mawifi wanawatumiaga sana watoto wa kambo kujiingiza kwenye ndoa za kaka zao na kuleta mitafaruku, unless ukute mtoto ana akili akagoma kutumika au baba ni mkali akawanyamazisha dada zake. But all in all, mtreat vizuri huyo mtoto, akija kukushukuru baadaye sawa, asipokushukuru sawa pia; ila as long as ulimtendea mema wakati unatimiza wajibu wako, basi utakuwa na amani. Hata watoto wetu wa kuwazaa wengine hawana shukrani pia

Tatu usiwe defensive na epuka maneno yoyote ya kumkumbusha huyo mtoto kuwa si mtoto wako. Akikosea muadhibu kama mtoto aliyekosea sio ndiyo unaanza "aah umetumwa na mama ako eeh, ntakukomesha", sijui umenishinda tabia nenda tu kwa mama ako; mtoto wako akikushinda unampelekea nani? Kama ambavyo watoto wako wa kuwazaa wanaweza kuwa na tabia za ajabu, hata mtoto wa kambo anaweza kuwa na tabia za ajabu vilevile; so deal naye kama ambavyo ungedeal na mwanao wa kumzaa

Usiache kujiombea na kumuombea kama unavyowaombea watoto wako, akiwa mtoto mwema ni faida kwenu wote, na akiwa jaribu basi amini ni mzigo wenu nyote pia. Panda mbegu njema kwa huyo mtoto, regardlessly. Ombea amani ya nyumba yako na watoto wako wote.

Hayo mambo ya baba yake kusema sijui atapima DNA sijui hawajafanana, muachie baba mtoto. As long as kamleta nyumbani kwenu na kukwambia huyo ni mtoto wake, basi mpokee na kumlea vizuri.

Wewe dada nimekupenda bure, ni km ulikua unaandika nnachowaza.... asipouona ushaur huu bas hakuna ushauri mwingine utaomfaa
 
Bibie kwani mumeo ulizaliwa nae hadi mkatengeneza bond? Kama mlikutana ukubwani na mkatengeneza bond basi amini kuwa bond inatengenezwa wakati wowote ule.

It seems hauko tayari kuwa mama wa huyu mtoto, ndio maana unajiuliza sana. Hata kuanzisha uzi pia ni dalili ya hilo.

Ulifahamu uwepo wake hata kabla ya ndoa yenu, je hamkujadiliana mstakabali wake? Kumfanyia shoping haimaanishi unamkubali, maana kama baba katoa pesa mwanae afanyiwe shoping nawe ndoa waitaka unadhani utafanya nini? Ungemuhitaji ungesisitiza aje angalau kipindi cha likizo ili mtengeneze hiyo bond ulokazana nayo.

Kama ndani ya nafsi yako unahisi kusita, unahisi hautokuwa mama bora kwa huyo mtoto its better ukamuacha kwa mama yake ila mkahakikisha mahitaji yake anayapata ipasavyo.
 
Relax beautiful, take everything easy, don't complicate anything before it becomes complicated!Anavyoanguka ng'ombe ndivyo anavyochinjwa sio lazima umburuze kibla,Wewe ni mama wa huyo mtoto upende usipende,hata mtoto anawaza hivyo na hayo maisha kwake yatakuwaje,msaidie kuyafanya rahisi nawe upande wako yatakuwa rahisi
 
imagine kupiga simu kila wakati kuulizia mtoto anaendeleaje, mara mpe simu mwanangu niongee naye, mara utume pesa unakuwa kama unahudumia familia mbili, kwa watu ambao mlishawahi kukutanisha vikojoleo mkipigiana simu mara moja mbili au ukienda kumtembelea mtoto kwa mamake, ni mara chache sana utakosa kukumbushia kama binadamu mwenye madhaifu. kukata mzizi wa fitna ni kuweka mazingira ya kutokuwa na sababu ya kuwasiliana. hata hivyo , kama yeye anaona hiyo ni issue mwache, kuna siku atakuta mtoto wa pili kwa mchepuko. na hilo litakuwa fundisho kwake, manake kama yeye ana watoto na yule ana watoto hapo kipimo kitakuwa nani bora kwasababu kote kuna watoto wa kutosha. nitaawaacha wapambane mbabe niendelee naye.ndivyo akili za wanaume zilivyo.

unasema nisubiri agundue tunapasha kiporo...simwogopi hata nusu, na wala siwezi kukataa akiuliza, yeye mwenyewe nafikiri kama mtu mzima anajua kinachoendelea kama watu mnawasiliana mara kwa mara namna ya kulea mtoto wenu, kuna mengi mnaweza kujadili na kujadili na kukumbushana story n.k
Bwana we hata usitafute justifications za madhambi yako. Wewe kama ni mzinzi ni mzinzi tu. Huyo mama mmeshatengeneza muunganiko wa milele haijalishi mtoto yuko wapi. Je ukimchukua unafikiri mama yake hatopiga simu kutaka kumjulia hali mwanae? Bado utatafuta tu kisingizio cha kufanya madhambi yako. Akili ulipewa, itumie.
 
Senkyu vere machi. Anatafuta tu justification hapa
Bwana we hata usitafute justifications za madhambi yako. Wewe kama ni mzinzi ni mzinzi tu. Huyo mama mmeshatengeneza muunganiko wa milele haijalishi mtoto yuko wapi. Je ukimchukua unafikiri mama yake hatopiga simu kutaka kumjulia hali mwanae? Bado utatafuta tu kisingizio cha kufanya madhambi yako. Akili ulipewa, itumie.
 
Mkeo anakosea sana; ila wewe usitafute justification ya kulala na mzazi mwenzio kisa mawasiliano ya mtoto. Kama bado mnatakana, hata huyo mtoto akija kuishi na mkeo bado mtaendelea kupasha kiporo na huyo baby momma wako. Na kwa nini mliachana kama bado mnatakana? Kwa nini mkeo anamkataa mtoto, subiri agundue mnapasha kiporo, utaenjoy show
Tukisema ya polygamy mtaanza kelele
 
Hapana anakosea: alijua kama kuna mtoto, hajafanyiwa surprise ndoani. Kama alijua hana wito wa kulea mtoto wa kambo, angesema mapema asiolewe au waoane lakini wakiwa wamekubaliana kuwa mtoto atakaa kwa mama yake.
Walaa huyo mke hakosei, kulea mtoto yeyote asie wako ni kipaji. Kama amejigundua hana hicho kipaji its better alivyokataa kuliko akubali kumpokea kishingo upqnde halafu aje asimangwe kwa kumnyanyasa mtoto.
 
Sio kelele, bali fact. Usipoamua kuridhika hata upewe wanawake mia 3 hutoridhika bado. Na huyu ni issue tofauti, kwani polygamy inaruhusu kulala na mzazi mwenzio?
Angeifanya mwanzo kila mke angekaa na mwanawe. Jamaa anaonekana bado anampenda mwanamke wake wa kwanza
 
Angeoana sasa na baby momma. Sio mtu mmeachana, kaenda kuoa kwingine afu wewe unabaki mchepuko. Yaani unatoka kuwa main chick unahamia kuwa side ostrich pyeeee
Angeifanya mwanzo kila mke angekaa na mwanawe. Jamaa anaonekana bado anampenda mwanamke wake wa kwanza
 
Bwana we hatSan

sitafute justifications za madhambi yako. Wewe kama ni mzinzi ni mzinzi tu. Huyo mama mmeshatengeneza muunganiko wa milele haijalishi mtoto yuko wapi. Je ukimchukua unafikiri mama yake hatopiga simu kutaka kumjulia hali mwanae? Bado utatafuta tu kisingizio cha kufanya madhambi yako. Akili ulipewa, itumie.
Nasoma comments zako na Heaven Sent natabasamu huku mnaandika Fact mbarikiwe
 
Mi pia namfeel sana shangazi yangu kuliko hata mama yangu yaani alinichukua nikiwa mdogo lakini alinilea kama binti yake yaani mpaka kuna vitu nkikumbuka nabaki kujiuliza ntamlipa nini shangazi yangu alafu pia nilijifunza kwamba anaroho nzuri ya kuzaliwa nayo maana kuna watoto wa marehemu shemeji yake tulikuwa tukiishi nao lakini nao walikuwa kama watoto wake
Zawad ni kumjali tu na kumtunza kwa kadir ya uwezo ila cha kulipa hakuna
 
Acha ubinafsi wewe ndezi,akija si ndo utabond naye,wasiwasi wako ni hivo vihela vya jamaa ambavyo mama wa huyo dogo kachangia kwa asilimia nyingi,huijui kesho,so mpokee mtoto,mlee Kama mwanao , mengine yatajiset,kausha huyo ndo lango la hela la baba yake,yangu ni hayo tu,btw hawez kula kila ya mchele kwa siku Mamie🤣🤣
Ubinafsi sina kwa kweli. Ningekuwa nao nisingekubali hata aje. Mama wa mtoto wala hayuko kwenye picha na hata malezi mtoto kalelewa na grandparents kuanzia mapema kabisa less than 3 years old.
 
Wanawake wengi we luck emotional intelligence.Huyo ni mtoto wa Mume wako na ameamua kumleta ndani .Card zote umeshikilia mkononi unataka kuwa mama wq kambo au no ?,unaitaka ndoa au no,unampenda Mume wako au no ,unataka mumewe awe happy or no .Kama majibu yote no Vunja ndoa kama yes kaa kwenye ndoa .Na kwa wewe kuwa happy kwenye ndoa lazima Mume wako awe happy pia .Marriage ni institut
Dalili mbaya nilizoona kwenye maandishi yako

1.Ukijiona unaanza kujisemesha "ninge" "ange" "tunge"
2.Hapo ulipoandika ulifahamishwa kwamba kuna kakid ka nje dakika chache kabla ya ndoa
3.Kuongelea suala la DNA wakati hujui alipopita/anapopita huyo mume wako...hiyo ni mbinu tu kaitumia mume wako kukuchota akili ,huyo ni mwanae 100%
4.Bond,bond na mtu huwa inatengenezwa haijalishi mmekutana akiwa na umri upi

Kimsingi kama mwanaume kaamua kumleta mwanae hiyo ni dalili nzuri kwako,kakuamini...usivunje uaminifu na upendo uliopo kati yako na mume sababu ya mtoto

Kama una roho mbaya jitahidi upunguze ama kama utaweza uiache

Comment ya chapwa24 pia imenifunza jambo huko mbeleni nikukutana na jambo kama lako

Hahahah nimecheka! dalili mbaya tena jamani! Well nimekupata. Ukweli roho mbaya sina. Sina mpango wa kutesa mtoto wa mtu wala nini.
 
Unataka kujiandaa kisaikolojia kwani unaletewa fisi ufuge? We jilazimishe hakikisha anapata chakula, mavazi, malazi na elimu kama wanao. JILAZIMISHE maana kumpenda mtu si uamuzi. Hatuchagui kupenda. Si lazima umpende, ila mahitaji yake ni lazima.
Kama unaishi na mtu na humpendi si itakuwa unafiki jamani! mimi sijawahi mchukia coz hamna mtu ana apply azaliwe. Nimeshea tu kupata ushari na iwapo kuna maandalizi yoyote ambayo natakiwa niwe nayo haswa ya kisaikolojia basi nisaidiwe kuyajua. Lakini suala sijui la chakula, mavazi, malazi, elimu hakuna shida. Anapata na ataendelea kupata
 
Back
Top Bottom