Special Thread: Video na picha kutoka Vikosi vya Jeshi la Ukraine walio Frontline dhidi ya Urusi

Ni kweli ngoja tuone muda utaongea. Labda waamue kumuacha peke yake.

Lakini kwa ukiangalia kwa jicho la tofauti unaweza kuona hawa jamaa wanataka kumchosha Mrusi target yao uchumi wake uyumbe.

Sasa hivi wanaweka wazi kwamba wanajeshi wa Marekani wapo Ukraine na wanawasaidia Waukraine.

Wanajiamini nini hawa watu.? Wameshausoma mchezo wote.
 
Wanajeshi ni Ukraine, Vifaa NATO. Nakuhakikishia Mrusi hachomoi. Ile Meli ya Marekani ilokuja jana tusaidiana kutafuta imetia nanga wapi. Au imeenda Uturuki. Imekuja na Navy Seal wa Marekani wale walomuua Osama
 
Ok,muda utaongea

Ila siko upande wowote

Ova
Nilikuelewa, hapo niliongelea in general kwa mtazamo wangu kwamba anayepiga na kupigwa katika mazingira halisi yanakupa taswira fulani au kuwaza nje ya box.

Upande mmoja unaweza kuonyesha mmoja anapigwa sana katika eneo dogo lakini anayepigwa kwa kurudishwa nyuma na kuondolewa sehemu aliyokuwa ameikalia na kusema ni yake, huyo ndiye amepigwa haijalishi alikuwa amempiga kwa kiasi gani aliyemvamia.

Pia Russia anapiga kwa kuharibu miundombinu, mali na watu kwasababu hana cha kupoteza maana nchi Siyo yake na hana hasara kwa wakati huu.

Ukraine kwa kuwa ni nchi yake anapiga kwa target ili asisababishe hasara nakuzidi kuharibu nchi yake.Kwahiyo hata wakionyesha kuadvance zaidi haitaonyesha uharibifu sana kama Russia anavyofanya.

Nchi nyingi hapa duniani huwa zinaogopa na kuepusha vita isipiganwe katika nchi zao, mojawapo ya nchi hiyo ni USA,umewahi kujiuliza ni kwanini?

Sababu ni kuharibu,miundombinu,mali ,raia na uchumi kwa kiasi kikubwa,rejea kisa chake na huyu huyu Ruassia walivyoweka missiles Cuba, huku yeye akiwa ameziweka Turkey.

Vita ya kupigiwa nyumbani kwako ni mbaya sana, hayo niliyoyaeleza hapo juu hayaepukiki. Serikali iwe na mitaala ya historia na madhara ya vita. Somo la uzalendo ni muhimu sana kwa vijana wetu.

Tanzania hatujui shida, hatujawahi kukimbia wala kuishi katika dhiki na mateso yanayotokana na vita. Tusiombee hii hiki kitokee hapa nchini mwetu ni kibaya mno.
 
Wanajeshi ni Ukraine, Vifaa NATO. Nakuhakikishia Mrusi hachomoi. Ile Meli ya Marekani ilokuja jana tusaidiana kutafuta imetia nanga wapi. Au imeenda Uturuki. Imekuja na Navy Seal wa Marekani wale walomuua Osama
Hapo ndipo kuna kazi hawa jamaa ni muziki mnene, kwanza hiyo training watakayoitoa kwa Waukraine itawapa motisha wa nguvu.

Usikute wametia nanga Uturuki au Odessa na Mrusi hajajua.
 
Hivi Black Sea ndo Bahari nyeusi? Basi kuna Meli ya Marekani imeletwa kulinda ili yasiyokee mashambulizi ya Urusi kutoea black sea. Imetengenezewa Automatic anti-ballistic missile system. Meli moja bahari yote. Si mchezo. Kumbe Mrusi mdogo tu. Anashindwa kuilipua?! Bado nafuatilia jinala meli ili tujue details zake
 
Aisee! Kwahiyo hapa wanamuonyesha kwamba zile meli zake hazina lolote kwa meli moja. Bahari nzima meli moja? Ni maajabu haya aisee.
 
Sasa kwasababu kama hii ya msingi, iweje Russia aonekane ni mzuri, ameifanya dunia iwe na mfumuko mkubwa wa bidhaa kwa vita aliyoianzisha na bado akafunga bandari, kama adui yake ni Ukraine kwanini ataabishe wengine? Bado hapo hapo anaombwa kuungwa mkono, mhhh!

Russia hana huruma na watu wake, Waukraine wala wanadamu wa mataifa mengine.

Kwasababu hii namuona US ana haki ya kuikomboa dunia kama alivyowahi kufanya huko nyuma japo kuna haters wake hawataki kuukubali huu ukweli.

Siku anayesimamia haki ndiye hushinda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…