Special Thread: Video na picha kutoka Vikosi vya Jeshi la Ukraine walio Frontline dhidi ya Urusi

Naona putin ashachukua majimbo Ukraine na kuyafanya yawe chini ya urusi....

Ova
Maneno tu. Hata umoja wa Mataifa hauruhusu kuingilia mipaka ya nchi kimabavu. Mfano Uganda ije iteke Kagera, ifanye igizo la kupiga kura ishinde iseme Kagera ipo Uganda? Akili matope. Alikosea, Mrusi alitakakiwa awaachie Waukraine wenyewe wapiga kura na wahesabu wenyewe. Sasa kura zimepigwa Urusi, muangalizi Urusi, Msimamizi urusi, mhesabu kura Urusi, mtangaza matokeo Urusi, Mshindi Urusi. Dunia haiwezi kubali. Hata taahira atagundua kama ni uongo huu.


Mbele ya mtutu wa bunduki utakataa kupiga kura. Kumbuka kura zilikuwa za wazi.

Kumbuka wananchi wa hayo maeneo ni mateka wa Urusi. Ukiwa mateka unakuwa na sauti?
 
Unajitekenya na kucheka mwenyewe. Ubeberu una vituko sana.
 
Wanajeshi wa Urusi waliopo Lyman wametangaziwa kwa Spika kubwa Wajisalimishe kwani wameshazungukwa na nchi yao imewatelekeza. Wamepewa muda wajisalimishe kabla ya kuteketezwa. Akili kichwani mwao sasa.
Your browser is not able to display this video.
 
Kikosi Maalum cha Ukraine kimevamia leo Usiku Kreminna karibu na Luhansk. Hiyo miliyo ya risasi ni Kikosi cha Ukraine, huyu anayeongea ni mrusi wakiwa wanaretreat. Hapo wanakimbia ni vufaa wameviacha. Walikuwa wanakuja kuwasaidia Wenzao waliozungukwa Lyman.
Your browser is not able to display this video.
 
Majeshi wa Urusi yanaonekana yakiretreat Lyman. Lakini huko wanapoenda hakuna njia. Leo asibuhi taarifa za kiintelejinsia zinadai wanajeshi Elfu 5 na mia 5 wamekwamba Lyman. Tofauti na jana ambapo ikikadiliwa ni wanajeshi 3000.
 
Ukraine wakiikomboa Kreminna na Rubizhne watakuwa wamekata supply route ya kupeleka silaha Severodonetsk na Lysychans'k.

Wakifanikiwa hilo Severodonetsk na Lysychans'k wanazikomboa kiulaini.

Mbinu wanayotumia sasa hivi Ukraine ni kutohangaika na Warusi waliong'ang"ania kwenye miji mikubwa. Wanapambana kuzifikia main supply route zinazozunguka miji hiyo wazizibe kwanza ndo wanawashughulikia vizuri.

Hongera ukraine troops
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…