Mh. Zelenskyy ni kijana shupavu sana, ana ushawishi na mtu mwenye msimamo usioyumba.Safi sana mheshimiwa zelensky
1. Jeshi la Ukraine linamtii na kumpenda sana.
2. Raia wa Ukraine wanampenda sana
3. Yuko vizuri kwenye Diplomasia na nchi yake ina mahusiano mazuri na nchi nyingi za EU na USA. Eneo hili kalifanya vizuri sana. Bila kuwa na ushawishi EU, NATO, USA wangemwangalia tu na wasingemsaidia.
4. Putin alimdharau Mh. Zelenskyy, hakujua karama aliyonayo na ushawishi wake kwa nchi tajiri.
5. Putin kuanza kuibembeleza na kuomba Uturuki na USA ili imshawishi Mh. Zelenskyy akubali mazungumzo wayamalize ni ishara kuwa sasa kiburi na dharau za Putin zimeanza kutoka. Vijana wanasema Putin katolewa wenge, sasa akili imekaa sawa.
6. Ni ukweli usiopingika kuwa Putin hajataka mazungumzo ili wamalize vita la hasha, anajaribu kutafuta uchochoro wa kuepuka aibu.
(a) Vikwazo vya kiuchumi vimembana mbavu. Uchumi wake umesinyaa sana, hataweza kuhimili vita ikiendelea.
(b) Vikwazo vya kuzuia suppliers wasimuuzie Russia materials kwa ajili ya kutengeneza silaha, kumemfanya production capacity ya military equipment & supplies iwe chini sana.
(c) Kashajua kuwa vita kashindwa na kwamba hata Crimea sasa inarudi Ukraine.
(d) Manpower (Skilled & Experienced Soldiers) yenye uzoefu kwenye vita imepungua na vita ikiendelea hali itakuwa mbaya.
(e) Upungufu wa silaha ni sababu mojawapo inayomsukuma kuomba mazungumzo ya kusitisha vita.
(f) Pressure ya ndani inazidi kuwa kubwa, hata waliokuwa wanamuunga mkono kuivamia Ukraine wameanza kumgeuka. Wanasema amepeleka wanajeshi kwenda kuuawa. Kiongozi wa Chechen na Wagner group nao wanasema kuwa jeshi la Urusi ni dhaifu na hawa silaha Bora. Hii si ishara nzuri kwa Putin.
Mh. Zelenskyy anatakiwa akanyagie mafuta pale pale na aongeze nguvu zaidi, mpaka Putin adondoshe taulo na kuchutama.