I agree with you humu kuna baadhi ya amateurs wanafanya mtazamo kwa kushabikia nchi fulani. Urusi kaonesha performance mbaya sana ukizingatia anapigana na competitor mdogo. Zile columns za magari ya jeshi zinazoenda bila air cover, kukosa supplies, kupigana bila kwanza kuharibu airforce ya adui na viwanja vyake, etc.
Urusi hajanishawishi kama anaweza wage an all out war with NATO. Hata asipowekewa vikwazo akawa na uchumi uleule na support kubwa kwake ila uwezo wake kwenye field ni hauridhishi. Unapigana na jirani, alafu some of your troops wanakosa mafuta wanatelekeza silaha. Ukisafiri 10,000 km itakuaje si majeshi yanakuwa isolated.
Tatizo la Urusi ni logistics. Vita na Japan napo Urusi ilifeli kufanya mobilization ya wanajeshi na silaha kutoka central na Western kwenda far East. Vita ya kwanza walikuwa poor hivihivi walipigwa na Ujerumani karibia battle zote, ila Ujerumani ya WW1 ilikuwa inapiga hakuna mfano. Vita ya pili ndio walifanya mass production pale Stalin alipodai "Quantity has a quality all its own" wakatoa units nyingi za silaha ila ubora wa kawaida na walishinda kwa hili.
Wanajeshi wa Urusi kufa sana haiwatishi kivile. Vita zao zote huwa wanakufakufa. Nchi inayoogopa zaidi wanajeshi kufa ni Israel
Kwa kawaida kwanza tukubali Russia wanajua nini wanafanya kuliko sisi, zile misafara ya gari zao jana kutembea umbali ule unafikiri hawakufanya assessment ya kwamba nini kinaweza kutokea? Mbona misafara imefika salama? tujue kwamba kuna wataalamu zaidi wa mambo ya kivita huko Russia kuliko sisi tunavyosoma taarifa mitandaoni.
Nadhani utakubali kwamba Russia haikutumia nguvu kubwa sana wakati wa uvamizi kwa Ukraine ilitumia nguvu kidogo na silaha ambazo sio nzito sana, ila baada ya mazungumzo kufeli na kuzagaa propanganda mitandaoni kwamba wanajeshi wao wanakufa sana hapo ndio wakawa serious, mara taarifa kwamba Russia imeshindwa kuingia Kyiv, sasa nini kimewezekana mbona wako Kyiv na jeshi la Ukraine halionekani lilipo.
Kwa mtazamo wangu ni kwamba Russia LABDA walitaka wafanye uvamizi mdogo ili kuwavuta Ukraine kwenye mazungumzo ila walipoona mazungumzo yamefeli na Rais wa Ukraine kasaini kujiunga EU hapo ndio kaamua kuwa serious.
wewe ni shahidi nini kimetokea, Ukraine leo hamna habari ya kuandikwa kuhusu jeshi la Ukraine kila unapoangalia wanaongelea heavy missiles without resistance yyte kutoka jeshi la Ukraine na Russia wameanza kutumia heavy missiles zenye high accuracy kitu ambacho mwanzo hawakufanya.
Kama ulifuatilia ule mgogoro wa juzi juzi wa Israel na Hamas, Israel toka inaanza ilikua inatumia silaha nzito zenye high accuracy toka mwanzo na walikua wanafanya vitu ambavyo Russia anafanya sasa kama kutoa taarifa kwamba atapiga sehemu flan mda flan hivyo wananchi waondoke.
Kwa kuangalia kama Russia wangetumia nguvu hii toka mwanzo wa Uvamizi unadhani Ukraine ingeweza kuwithstand vita mda wote huu?
Mda huo huo NATO wameshamaliza vikwazo vyao kuweka na wamesema hawapeleki jeshi Ukraine na hawaweki No fly zone kwa sababu italeta mtafaruku direct na Russia.
Hao wote wanajuana uwezo wa kivita acha sisi tunaosoma taarifa wanazoamua kurelease wao, leo hii unaskia Russia au US kila mmoja ana nuclear warhead 5000+ hizo ni taarifa wanazoamua kuachia hadharani ila deep inside si ajabu kila mtu ana zaidi ya 10,000+.
Leo hii utakuta watu wanasema Russia hakutegemea vikwazo vikubwa namna hiyo anafikiri washauri wa Putin hawawezi kufanya analysis za nini NATO zitafanya mara wakishaanza kuivamia Ukraine na watatokaje.
Kikubwa ninachounga mkono ni kwamba kila mtu ana mtazamo tofauti kuhusu hii vita na kila mtu ana upande anaotaka ushinde kwa sababu zake binafsi either mapenzi juu ya nchi/uhasama/chuki/ au vyovyote lakini hiyo isipelekee watu wabishane kwa matusi, hoja/mitazamo ndio mpango.