Hii chai ulisahahu kuweka sukari,imekuwa chungu mno Mkuu.kwa hadi sasa vita ya ukraine na urusi , marekani na member wa nato washasurrender ina maana ukraine inamalizwa soon,kinachosubiliwa endapo akimaliza kwa ukraine je atashambulia member kamili wa nato walioko karibu na urusi,na hapo ndo nadhani vita kamili itaibuka kwa sababu mkataba wa NATO unasema mmoja akivamiwa lazima wengine wampe sapoti ya kijeshi
Mkuu nani alisema itakuwa operation ya masaa 24?? Weka hapa hiyo statement. Nilivyomsikia Putin alisema wataenda kulinda watu pale DONBAS Region, hiyo ndio operation yao maalum.So ile operation ya masaa 24 sasa hivi itakuwa ya mwezi mzima kwakuwa Kyv ina watu wengi si ndiyo Mkuu.
Kuna China na N.Korea mkuu , wazungu ni watu timamu sana[emoji769]NATO wangemuwai wakamgonya nyuklia bihashara ikaisha. Kwa nn? Putin asumbue watu
Kama ni hivyo kilichokuwa kinawafanya mseme Russia anakwenda kufanya operation maalum tu ndani ya masaa 24 anamaliza mchezo Ukraine ni kipi sasa (japokuwa unaweza kuwa si wewe but Pro Russia wengi humu ndiyo walikuwa wanatupigia makelele hayo ) kama mnalijua hilo la uwezo wa Ukraine kijeshi pia.Tunajua ni aibu the so called Super Power kijeshi kupewa upinzani mkali na Underdog Ukraine,tunawaelewa mnavyojaribu kumsitiri mtu mzima aliyevuliwa nguo na mtoto
Sasa mkuu unaamini ulikuwa unatoa hoja nzito nzito za kueleweka bado wakapiga kofuli?Eti ujinga wako.... [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Hiyo Dunia iliamuaje wakati LIBYA inavamiwa?
Kwa hiyo huyo jamaa yuko na Putin Ofisini?Kuna jamaa nipo naye hapa kijiweni ametujulisha habari za ndani ndani kabisa , Putin anafunga mahesabu Ukraine wiki hii anaendelea mbele kuichukua na Finland[emoji205]
IKo hiviii, Urusi kwenye vita hii haiko peke yake. Nchi zote zenye ugomvi na mataifa ya magharibu ni wadau muhimu kwenye vita hii. Nchi zote ambazo zinanyonywa na nchi za magharibi ni wadau kwenye vita hii, nchi zote zilizowahi kutawaliwa na mataifa yanayounda NATO ni wadau kwenye vita hii.Hapa ndugu zetu warusi itagharimu maisha vijana wao ambao wako front, humu ndani wachangiaji wengi hawaijui principles za medani zaidi yakuwa na mahaba kwa Putin na jeshi lake. Military supply kwenye uwanja wa medani ni kitu muhimu sana ambapo mara nyingi unafanikiwa kama ukipata air superiority yaana kuharibu air defence system ya adui yako, urusi ilijua itamaliza vita mapema kumbe Ukraine sio wezembe wamekata supplies kwa kuharibu barabara kwenye baadhi ya maeneo, Kuna baadhi ya convoys zimeshambuliwa na kuharibiwa vibaya, vijana wa Ukraine wengina wanatumia guerrilla warfare strategy kuharibu military hardware za urusi ndio maana urusi wameanza kurusha makombora kutokea black sea kama fire support
Ikiwezekana wakupe permanent ban kabisa 🙂. Nenda kwa Putin mkaanzishe Twitter yenu huko mcomment kwa uhuru,au mambo ya maendeleo hamna habari nayo mko busy na masilaha ya Nyuklia peke yake,halafu mnataka kuja kutumia uvumbuzi wa wenzenu kuwatole povu.Duh, nimekula ban huko twitter. Yaan ukicomment vibaya kuhusu UKRAINE unakula mua.
Akiwa neutral ndo anavamiwa pale Mrusi akijisikia kuivamia UkraineHawezi!
Kwa sababu kila mtu anajua consequences zitakazotokea. Njia pekee ambayo ni salama ni Ukraine akubaliane na masharti ya Mrusi, awe neutral.
Options wanazo, Waliyajua hayo.Watumie huawei za rafiki yao China zisizo na Android,hawana jinsi kama ndiyo hivi.
Warussi wa kwa mtogole hao wanashangilia 😂
[emoji3][emoji3][emoji3]Mimi ndio maana kwenye mashindano ya Mbio huwa simuamini mkimbiaji anayechomoka mwanzo kwa mbwembwe
Wakati mdogo nilkuwa naamini kabisa Iddi Amin ana kichwa cha nyoka usiku na pia anachinja watoto zake anaweka kwenye fridge na hata mkewe akimtamani anamchinja na kumla. Joka. kuja kuwa mkubwa na kujuwa ukweli kumbe jamaa alikuwa na watu wengi tu wanampenda.Propaganda zimewaathiri sana watu humu. Utumwa wa kifikra utumwa mbaya mno!
Ndio, unajua ukichangia mada kwa kiingereza inakuwa rahisi kuwa detected. Mi nilikuwa nadeal na CNN, BBC, REUTERS nk wakipost kitu na kama nimeona wazi hii ni propaganda huwa nashindilia comment huku nikimaalizia kuunga mkono URUSI wazidi kuifumua UKRAINE.Sasa mkuu unaamini ulikuwa unatoa hoja nzito nzito za kueleweka bado wakapiga kofuli?
Muongezee Birika la kahawa mkuu,mpatie na kashata sinia zima awe anashushia,Bill yote kwangu 😂Kuna jamaa nipo naye hapa kijiweni ametujulisha habari za ndani ndani kabisa , Putin anafunga mahesabu Ukraine wiki hii anaendelea mbele kuichukua na Finland🐒
Kama ni hivyo kilichokuwa kinawafanya mseme Russia anakwenda kufanya operation maalum tu ndani ya masaa 24 anamaliza mchezo Ukraine ni kipi sasa (japokuwa unaweza kuwa si wewe but Pro Russia wengi humu ndiyo walikuwa wanatupigia makelele hayo ) kama mnalijua hilo la uwezo wa Ukraine kijeshi pia.Tunajua ni aibu the so called Super Power kijeshi kupewa upinzani mkali na Underdog Ukraine,tunawaelewa mnavyojaribu kumsitiri mtu mzima aliyevuliwa nguo na mtoto
NATO iwe mara ngap mlangoni mwa Russia , Russia anatumia hiyo iwe sababu ya yy kuizuia Ukraine kujiunga NATO ila in reality ana sababu zake zakiuchumi na sio sababu za kiusalama kama anavyojigamba hadharani , Latvia na Estonia ji majirani wa Russia ila pia ni members wa NATO ila Russia did nothing to stop them from joining NATOSasa haya ni mawazo yako!
Wachambuzi wanasema Russia bado wanawahitaji raia wa Ukraine, ile nchi bado ipo na ni jirani yao na itabakia kuwa hivyo. Hakutakuwa na sababu ya kufanya uvamizi mkubwa kama alivyofanya Syria. Akifanya uvamizi wa namna hiyo atatengeneza adui mwengine mkubwa wa kizazi na kizazi ambaye ni jirani na ni mazingira hatari kwa usalama wa nchi ya Russia.
Kimkakati inambidi adili na wanajeshi tu baada ya amiri jeshi mkuu wa nchi ya Ukraine kukataa makubaliano waliyoyapendekeza. Na ndiyo maana akaanza na kupunguza nguvu ya jeshi la Ukraine kwa kushambulia base za kijeshi na maghala ya kuhifadhia silaha pamoja na viwanda vinavyojihusisha na utengenezaji wa silaha. Lengo no kupunguza nguvu za jeshi la Ukraine.
Operation inayofuata ndiyo hiyo ambayo anayoifanya sasa hivi na ni operation ngumu ambayo ni urban warfare. Ikiwa ni kuiondoa serikali ambayo kwake anaiona ni hatarishi. Kwa kuzuia uharibifu mkubwa wachambuzi wanasema ameingia na silaha za nyuma si za kisasa.
Urban warfare ni ngumu na ugumu wa hapa si kwamba Russia hana uzoefu. Ugumu wa hapa ni mnapambana kwenye makazi ya watu ambao ni raia, ambao sheria za kivita zinawalinda. Shambulio lolote dhidi yao ni uhalifu wa kivita kwa sababu umeshambulia wasiyostahiki. Na huu ni mtego kwa Russia, majeshi ya Ukraine yanajificha kwenye makazi/majengo ya makazi ya raia.
Kuna suala hapa umelisahau. Russia lengo la hii vita ni kulinda usalama wa nchi yake. Sote tunafahamu NATO ikiwa mlangoni kwake ni hatari. Ukraine pia inakuwa kijeshi ikiwa NATO na ikijijengea na uwezo wa kutengeneza mabomu ya nyuklia hatoweza kumdhibiti. NATO wanalijua hili na wanajua kuwa Ukraine ni kete muhimu dhidi ya Russia.
Naam; Ukraine ni nchi huru ina wajibu wa kufanya maamuzi yake lakini ni hatari kufanya maamuzi yatakayo hatarisha usalama wa nchi jirani yako. Russia anachofanya ni kumdhibiti Ukraine mapema. Ikiwa Russia mkakati huu utafeli wachambuzi wanasema itamlazimu alazimishe mazingira. Nayo ni kutunisha msuli wake. Akifanya hivyo maangamivu ya Syria miji kuwa gofu yatahamia Ukraine. Na Ukraine itaumia.
Russia inacheza mahesabu hapa! ni mahesabu yanayohitaji umakini wa hali ya juu. Atakayeumia zaidi ni Ukraine ikiwa akikaza msuli.