LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

Live coverage on JamiiForums
Raia wa Eukraine wanaumia na risasi na mabomu.

Raia wa russia wataathirika na vikwazo.

wa USA na washirika si watu wazuri. Ifike mahala kabla hamjapigana muitane muulizane kwann tunapigana? Hawa wanaoitwa washirika wetu wanapoteza nn mmoja wetu akishindwa?
 
huwa ana uraia pacha russia/israel na tayari ameshaukana uraia wa urusi na hufanya hivi mara nyingi pale panakuwa na tafrani ya urusi na nchi za magharibi ila baadae hurudi kuwa mrusi
Muache uongo....lini ulisikia kaukana uraia wa urusi?
 
Ukifuatilia huu mgogoro ni family matter. "Nilikuambia usiende kula kwa majirani, kwa nini umeemda kula" wamama wa wakati huo.

Hii issue itamalizwa kati ya Putin na rais wa Ukraine passipo hata mediator, becaise its a family matter
 
Kuna madai kwamba Air defense systems za USA&CO zinafanya vizuri na mpaka sasa helicopter na ndege nyingi za Mrusi zimeteketezwa

Ila pia Ukraine ameshapoteza mji wa Kharkhiv kwa maadui
 
Mrusi anafyatua makombora ya Kalibr na aina zake nyinginezo za Cruise missiles kwa kutumia Bomber warplanes anazoziweka mbali na uwanja wa vita
 
Take it from me, hakuna vita hapo!

Kwa watu wa dini wenye mioyo minyoofu, hiyo ni ishara kubwa sana kwamba sasa uovu wa wanadamu umefikia kikomo kama ilivyokuwa wakati wa Gharika na Sodoma na Gomora.

Mungu yule wa Gharika na Sodoma na Gomora ndiye yule yule ambaye tunaye sasa. Hajabadilika.

Amekuwa na subira kwa muda mrefu, sasa:"Enough is enough "
Dah. Unajionaje sasa.
 
Tatizo watz tuna ujuaji wa kinonko sana.

Urusi ikiamua itaivamia Ukraine na Marekani hatofanya chochote zaidi kulialia na kuweka vikwazo.

Marekani na vibaraka wake wangekuwa na nia ya kweli kuisaidia Ukraine wangeisadia kukomboa majimbo mawili yanayo shikiliwa na waasi.

Inashangaza eti jeshi ambalo limeshindwa na kukundi cha waasi chenye wapiganaji wasiozidi 50,000 eti kije kukabiliana na moja wapo ya jeshi kubwa duniani.

Iwapo vita itatokea nakuhakikishia jeshi la Ukraine halitaweza kuhimili nguvu ya jeshi la Urusi hata ndani ya wiki mbili.
Dah. Upo sahihi.. ndani ya saa 12 tu wameona cha moto.
 
Aivamie Ukraine akose mradi wa gas wa Nord Stream 2?..NATO walishamwambia Putin very clear,hawezi pata vyote,achague kimoja,aivamie Ukraine akose Nord Stream 2 au aachane na Ukraine inversion abakize Nord stream 2.

Unafikiri Putin ni mjinga hivyo akose mradi utaofaidisha genereations sababu ya vita Ukraine.

Kila kitu ni leverage boss sio ubabe wa kijinga mnaoupigania huku usio na kichwa wala miguu.

Leo Sergei Lavrov amesema baadhi ya wanajeshi waliokuwa mpakani Ukraine wameanza safari ya kurudi kambini,Hata satellites za Marekani wame confirm movements za wanajeshi ku withdraw.

Vita sio lelemama aisee
Ameamua akose huo mradi
 
Hatari sana, Mungu awafanyie wepesi wahanga wote wa hiyo vita
 
Urusi na Ukraine, ili kuelewa chanzo cha mgogoro wao vizuri ni muhimu kujua kidogo historia ya nyuma kuhusu uhusiano baina yao.

Hapo zamani nchi hizi zote zilikua zinaunda Umoja wa kisovieti (USSR), na muungano huo uliundwa rasmi mwaka 1922 na kuvunjika mwaka 1991.

Umoja huo ulipovunjika Ukraine ilijipatia uhuru wake kwa mara ya pili mwaka huo huo 1991,
hapo awali walipata uhuru wao mwaka 1917 lakini baadae ndio waliunganishwa kwenye umoja wa Kisovieti mwaka 1922 ambao kwa wananchi wengi wa Ukraine waliona hauna manufaa yoyote kwao.

Tangu kuvunjika kwa muungano huo, Urusi na Ukraine zimekua na mvutano wa hapa na pale chanzo kikuu kikitajwa kua maslahi ya kiusalama zaidi, Na Urusi ndio amekua tishio zaidi sababu ndio taifa lenye nguvu zaidi kwa ukanda huo na Dunia kwa ujumla.

CHANZO CHA UGOMVI ni pale Serikali ya Ukraine ilipo badiri mpango wake na kutaka kujiunga na NATO,

Uamuzi huu haukuwafurahisha Urusi ambao waliamua kujibu kwa kupeleka wanajeshi zaidi ya 100,000 kwenye mpaka wa Ukraine.

Kwa mujibu wa picha zilizotolewa na Wizara ya ulinzi ya Urusi zilionesha vikosi vyake vikiendelea na mazoezi ya kijeshi kwenye eneo la mpaka huo.

NATO - Ni jeshi la pamoja linaloundwa na nchi 27 za ulaya, Marekani, Canada na Uturuki. Nchi zinazounda umoja huu kwa kiasi kikubwa zinafuata misingi ya Kibepari na nyingi pia zimekua na uadui na nchi ya Urusi katika masuala mbalimbali kama vile uchumi na siasa

KWANINI UKRAINE WANATAKA KUJIUNGA NA NATO ,Chanzo kikuu ni kujiimarisha kiusalama, Tangu Umoja wa Kisovieti ulivyovunjika, Hofu mara kadhaa imekua ikitokea kwamba Urusi anaweza kuivamia Ukraine, Lakini mara zote Urusi amekua akipinga mpango huo.

Licha ya kupinga,
Mwaka 2014 Urusi walifanikiwa kutwaa Rasi ya Crimea ya kusini mwa Ukraine, Na kuanza kuwaunga mkono waasi wanaoiunga mkono Urusi ambao waliteka sehemu kubwa za Mashariki mwa Ukraine.

Urusi walitwaa Pwani hiyo baada ya kutokea kwa Mapinduzi Ukraine mwaka huo huo 2014

ambayo yalimuondoa madarakani Rais wa wakati huo Viktor Yanukovych ambae anatajwa kua alikua ni kibaraka mkubwa wa Urusi.

Na mpaka sasa sehemu kama Donetsk na Luhansk kutokea Ukraine ni maeneo ambayo yalijitangaza kuwa huru na hata vita iliyokua inaendelea Ukraine kabla ya hii inayotaka kutokea ilikua ni kutokea vikosi vya hizo sehemu ambazo zinataka kuendelea kujiongoza zenyewe.

Inasemekana Urusi amekua akitoa msaada wa kijeshi kwa waasi hao ili kuiondoa kabisa serikali ya Ukraine, Na ndio maana serikali ya Ukraine ikaja na mpango wao wa kujiunga NATO ili kutaka kupata misaada ya usalama sababu kadili siku zilivyo enda ndio serikali hiyo ilizidi kua hatarini kwani Urusi ilifanya mbinu nyingi hatari za chinichini.

Moja ya hatari nyingine inayoendelea pia ndani ya Ukraine, Ni mipasuko ambayo kuna watu wanatamani kuwa chini ya Urusi na wengine wanataka kubaki kama walivyo.

Kwenye mgogoro huo NATO haikuingilia moja kwa moja, Lakini jibu lao lilikua ni kupeleka wanajeshi wa ziada katika nchi za Ulaya Mashariki kwa mara ya kwanza, zikiwemo Estonia, Latvia, Lithuania, Poland na Romania.

Sasa hali hiyo ndio inawafanya Urusi kila siku kupiga kelele kwamba vikosi hivyo viondolewe, Ina maana kama NATO wataendelea kupeleka vikosi zaidi Ukraine ni kuzidi kuongeza tishio zaidi kwa usalama wa Urusi.

HIVYO BASI, Chanzo cha mgogoro wa Urusi na Ukraine ni; Urusi hataki kuona Ukraine akijiunga na NATO kwa hofu ya usalama kwake wakati nao Ukraine wanataka kufanya hivyo kwa hofu ya usalama ndani yake yote ni kwa sababu ya matendo ambayo wanadai yanafanywa na Urusi ndani ya nchi hiyo.

Je hii ni WW3 [emoji848]

Kama vita itazuka inaweza kua Vita ya Tatu Ya Dunia, sababu itahusisha mataifa mengi kwa wakati mmoja na zaidi ni hofu ya matumizi ya silaha za Nyuklia ambazo zinaweza kuathiri karibia dunia nzima, Na ikumbukwe Urusi yeye anaungwa mkono na Korea Ya Kaskazini, Venezuela na China ambazo nazo ni nchi zenye nguvu kijeshi.
.

IMG-20220224-WA0052.jpg
 
Back
Top Bottom