LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

Live coverage on JamiiForums

Zaidi ya special operation in Ukrain kutaka kuiondolea uwezo wa kijeshi na unazi mambo leo. ankai jua wamefika hapa pia

 
ha ha ha umechemka leo ni siku ya mazungumzo na kuokoa raia leo hakukuwa na mapigano ha ha ha mapigano yataanza usiku
 
Hizi ni porojo za kwenye vijiwe vya kahawa, kuna mfumo wa ulipaji pesa ulioanzishwa na Russia lkn una changamoto kubwa kwamba ukijisajili kuitumia basi moja kwa moja unakuwa umejiondoa kwenye SWIFT na ndio maana hata China ameshindwa kujiunga nayo.

Sasa wewe unafikiri China akijiondoa SWIFT nani atakuwa amepoteza. Hakuna nchi hata moja duniani anayoweza kukubali kuacha kufanya biashara na nchi za magharibi ndio eti ifanye biashara na Russia ambaye hana chochote cha maana. Hivyo hizo ni porojo za vijiweni tu.
 
Wanajeshi wa Ukraine Wanajifichaje kwa Raia? Kwani wao sio Raia wa Ukraine? Wao ni Raia usisahau wako huru kuwa popote kwenye nchi yao iwe kwenye nyumba za wa Ukraine wa kawaida au porini ni wako kwao.Huwezi kuwapangia kuwa wawe wapi.Ni nchi yao
Sasa pakipigwa wasianze kulalamika
 
Acheni porojo za kwenye vijiwe vya kahawa bwana. Mipaka gani hiyo ambayo ipo chini ya warusi. Tuonyeshe tuzione.
Daaa wee acha hawa warusi wa samvi la chole wana vituko sana aisee yaani wanajifanya kuwa wao pekee ndo wanzipata habari za vita na wao pekee ndo wana acces ya kupata taarifa za front line wakati sisi tunazo

Nimemuuliza anitajie ni mipaka mingapi ya Ukrain iliyo chini ya majeshi ya warusi kakimbia mita mpaka sasa ivi sijamuona kuja kukilijibu swali langu

Yaani anajiokotea tu vitaarifa uchwara uko porini anakuja kuvibwaga apa akidhani wote ni mambumbu kama yeye
 
Tupo njiani kwenda kuchukua kinu chetu cha 3View attachment 2142333
Hao wavamizi wa Russia wanaambaa ambaa tu pembezoni na mpaka wao ikionyesha walivyo waoga. Hatuna sababu ya kuiogopa tena Russia.

Wamekuwa kumbe ni watu wa propaganda tu kumbe hamna lolote, wanabaki kurusha makombora hovyo kubomoa majengo na kuua tu raia wasio na hatia. Hopeless kabisa.
 
Tuanze kwanza kwenye mipaka ya ukraine na warusi, ipo kwenye imaya ya nani?.ili tujue story za kwenye kahawa zinatoka wapi
Jamaa reasoning capacity yako ni ndogo mno ivi unajua kati ya mrusi na mukrain nani kamvamia mwenzie tuanzie apo kwanza alafu uko mbele utapata jibu lako ukishajua kuwa kati ya hawa wawili ni nani kamvamia mwenzie basi hutokaa uulize tena swali la kijinga na kipumbavu namna hii
 
Hii ishu wanaigiza sahizi eti wanapumzika kupigana ili waendelee baada ya kuwatoa wananchi.... ukraine ilishasema wananchi wachue silaha sahizi inaonekana jeshi linajificha nyuma ya raia.. waondoke waende wapi wapo kwenye nchi yao....
Ili wakianza kuwatwanga kusiwe na yeyote atakaye sema anaua raia
 
Haya ni maneno ya kwenye kanga ila ukija uwanjani warusi wanasonga mbele, wala hakuna hata dalili ya kurudi nyuma.muda sio mrefu tutatangaza umiliki wa kinu cha 3.na kufanya tuwe tuna miliki 75% ya umeme wa ukraine.
Duuh we jamaa ado hujaaamka usingizin emu stuka basi acha kuwa kama umenyweshwa methadon
 
Putin inatakiwa ampeleke mtoto wake kwenye hivi vita, aache kuswaga watoto wa wengine kuwapeleka kwenye hivi vita vya kipumbavu alivyoviasisi ona sasa watoto wa watu wanavyouwawa kinyama. Hovyo kabisa huyu dikteta.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…