LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

Live coverage on JamiiForums
Huu uzi mzuri Kama unanpenda hbr za kimataifa adhari za Vita kwa africa Ni zipi ikiwa afrca Hana maslai na kundi lolote hap.
Majibu plz kwa wataalam. Ahamed rajabu Ni mchambuzi mzuri San embu ajitokeze
 
Pia usisahau raisi wa Ukraine ameamua kutafakari upya suala la kujiunga NATO
 
Donesk gani iyo mkuu ambayo ipo chini ya serikali?
 
Huyo Hitler alipigwa na Warusi na siyo taifa lingine kamaulikuwa hujui sasa ujue
Urusi akitumia taarifa za kiintelijensia za baba mzazi wa computer Allan turring...bila hivyo huenda matokeo ya Vita yangekua tofauti
 
 
Naona walalahoi wa US na Urusi mnatupiana maneno tu bure hapa akati mradi wa umeme wa maji umejengwa chini ya kiwango huko. ( kwamujibu wa mb Msukuma)

Endeleeni kushabikia vita alafu yakwenu yanakwenda hovyo.
 
Russia anavyo vyote uwingi wa mabomu ya nuclear na mabomu hatar zaid duniani ! Na sio mabomu tu na silaha hatar zaid ya kutosumbuliwa duniani.

Kwanini Iran hawataki amiliki mabom ya nuclear ? Biden aliwaambia american citizen waondoke Ukraine kabla uvamizi haujatokea sababu hatopeleka even a single mwanajeshi kuwa evacuate raia wake na akawaambia being there na tukajibizana risasi na mrusi ina maanisha ni world war tayar.

Do you think Russia ni china kwenye umiliki wa silaha ?
 
Russia ame suffer enough kwenye uchum na hawez ku risk zaid ya hapo. Vikwazo vingi alivowekewa vimemfanya asiwe na makali kwenye uchumi lakin kwenye uwanda wa vita mkuu yule jamaa si mchezo.
Marekani anatudanganya na propaganda nying ukion analazimisha kitu ujue anataka afaidike yeye.
 
Hawafuatiliii hizi mambo wako wanasikiliza sana sky news, cnn, wion na nyingine nying lakini hawasikilizi habari pia za upande wa pili.
Ku engage in a war with russia kwa sasa ni kuiweka ulaya yote mashakani kuliko hizo propaganda channel za western bloc zinavyodai. Marekani yuko far huko.
Croatia ashagoma, German mwenyewe mguu ndan mguu nje, hungary ashagoma na nchi kibao zinaona hakuna haja ya kutaka kuingia kwenye vita ambayo waathirika wakubwa ni wao.
 
Huyo Hitler alipigwa na Warusi na siyo taifa lingine kamaulikuwa hujui sasa ujue
unajua back up ya mrusi kumpiga Hitler aliipata wapi?.
acheni ushabiki wa kishamba US ndiye alitia nguvu upande wa Urusi ndiyo maana habari inasomeka hivyo, asingelifanya hivyo habari ingelikuwa kinyume chake.

unajua Japan aliwai Kalia eneo Urusi kimabavu wakati huo anatawala China, ufiripino, Siberia, Taiwan, Hong Kong,Manchuria.

Japan ndiyo mtabe wa huo ukanda, sio hao wazungu njaaa na wauza Vodka.. Japan ikiwa katika ubora wake akakutana jinamizi...
sasa kamuulize Japan nini kilimfanya asiwe interested na vita hadi LEO? na wana siku mahalum ya kusikitika nchi nzima.
sasa hayo yametokea enzi hizo wakati baadhi ya wazungu wa Urusi wanatumia vibatali majumbani mwao unless uniambie toka wakati huo US walisimama kudeal na sayansi ya nyuklia na mabomy yote kwa ujumla ndiyo nitakubaliana na madai yako kua US ni mchumba tu kwa Urusi.
 
Watu wametengeneza silaha nyingi na za hatari lakini kiuhalisia hawatazitumia na badala yake migogoro itasuluhishwa mezani.

Katika dunia ya leo vita ni ghali sana na unapopigana kisha vita vikiisha na uchumi wako unakuwa umesambaratika kabisa na kuujenga tena ni kazi ngumu kushinda vita vyenyewe na haijalishi kama ulishinda hivyo vita au la.

Hiyo scenario ndio kila nchi inajaribu kuepuka bila kujali nchi ni kubwa au ndogo na inapofika hapo ndio maana hata Russia leo hii nimesikia wameanza kuondoa wanajeshi wao kutoka kwenye mpaka wao na Ukraine.

Russia wameona isiwe shida kwani wakiwekewa vikwazo wameona hawana dawa ya vikwazo na wanafahamu athari ya vikwazo vya kiuchumi ni mbaya kuliko kuikalia ardhi ya Ukraine kwa nguvu hivyo naona wanaelekea kukubali yaishe.
 
Taifa la Ukraine ni miongoni mwa nchi zinazomiliki silaha za Nyuklia na makombora ya masafa marefu

Ni taifa kubwa tu la watu milioni 45 kulingana na takwimu za mwaka 2020

Jamaa wana silaha za kila aina lakini wanapigwa biti na mrusi wanaufyata

Kila mtu anaijua nguvu ya Putin na Urusi,lakini nachotaka kusema hapa ni kuwa, kama nchi nyingine tusiwe kama Ukraine

Hata kama ni Russia na manguvu yote ukraine alitakiwa akitishiwa kuvamiwa naye aonyeshe misuli ya umwamba

Taifa la watu milioni 45 sio taifa dogo wakuu ni taifa ambalo linaweza kuwa na uwezo wa kutunisha misuli kwa taifa hata lenye watu milioni 300

Sasa wapo milioni 45 wanakua waoga hivyo na wanaonyesha udhaifu mkubwa,jee wangekua milioni 3 au 4 jee?

Taifa la watu milioni 45 mkiamua kuwekeza kwenye jeshi na uwezo mkubwa mnauwezo wa kulitunishia misuli dola lolote hapa ulimwengu, milioni 45 inakutosha kuwa superpower nawe ukatunisha misuli

Na silaha za nyukilia wanazo lakini wamekua watu waoga hivyo?Vita ikitokea Ukraine wakijipanga wakipigana na Russia hata kama mrusi atashinda lakini wangemuachia russia makovu fulani au kumporomosha kiuchumi,kwamba vita viww virefu vya kufa na kupona.

Ukraine anapitwa hadi na nchi kama Israel ambayo ina idadi ndogo lakini wanatunishia misuli madola makubwa,kila kitu ni kujipanga,Israel sio wengi ni nchi ndogo lakini kijeshi wanajitahidi vipi hao ambao wapo milioni 45 na wamejionyesha dhaifu hivyo

Una makombora ya masafa marefu yanayofika Moscow halafu unatishiwa kuvamiwa?Kwanini usitamke wazi kabisa kwamba ukivamiwa utaishambulia Moscow kwa makombora ya masafa marefu?

Hii nchi ni ya ajabu sana. Mimi kwa hili nasimama na Urusi katika huu mgogoro lakini Ukraine wanafeli sana masilaha yote hayo lakini wameshindwa hata kupiga mkwara tena watavamiwa na hawatafanya kitu,hawa jamaa ni useless kabisa

Ukraine hawafai kuigwa
 
Ukizidisha sana ubabe wapenda amani wanachange mind zao wanaona its time ya kummaliza mbabe so Russia anatumia mfumo wa Hitler ambao ulichokwa mno so Russia inaweza kuwa ndio mwisho wa ubabe wao forever... tena ikija vita basi usimamishwaji wake crimea itakuwa sharti irudishwe Ukraine so ni pata potea kwa Russia
 
Are you kidding me Putin was KBG director .Huyo ana create story Ukraine started watch Putin
 
Are you kidding me Putin was KBG director .Huyo ana create story Ukraine started watch Putin
kuwa KGB hakufanyi Putin asiwe wa kubebeka, hata Gharib bilali kasomea utengenezaji wa mabomu ya nyukilia ila sasa kaanzisha Ufugaji wa kwale.

kutaja taja majina KGB sijui nini nini vile kusiwatiwshe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…