Spika Job Ndugai, amejiuzulu Uspika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Spika Job Ndugai, amejiuzulu Uspika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ndugai kosa la kwanza lilikuwa kuomba msamaha kisha ukajiuzulu, inawezekana ulishinikizwa kufanya hivyo. Lakini hili la kujiuzulu huenda ni somo kwa ulimwengu juu ya mambo ya hovyo yanayo trend Tanzania, kama muhimili unaopaswa kuihoji serikali haujiamini ni nani mwingine anao huo uwezo?


Watanzania tukubali tusikubali ni kwamba Nchi sasa ipo katika sintofahamu kubwa.


Aaarghhh Ndugai bwana mbona umewaacha tena wale Covid-19 mjengoni?😣
 
Kitendo cha kuomba msamaha na kisha kujiuzuru, Naona kama vile Job amekikosea adabu cheo cha uspika. Angekomaa tu na msimamo wake.

Bunge ni muhimili unaojitegemea. Pia Kazi ya Bunge ni kutunga sheria, kukosoa na kuisimamia Serekali. Hivyo Job kuikosoa Serekali ilikuwa haki yake ya Kikatiba.
 
Mode, mimi ni Tomaso, this letter doesn't look real! is this bonafide genuine?. Headed paper gani hii haina address?.
Hiyo barua ya kujiuzulu ikowapi?.
please do the needful.
Update.
Nimethibitisha hii ni kweli, bonafide genuine

Samahani Mkuu Roving Journalist kwa kukudoubt,
Tomaso ndivyo alivyo.
P
We subiri genuine, kimeishanuka. Address ya nini wakati hakuihitajiki reply. Na Bunge huwa ni moja tu.
 
Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai ametangaza kujiuzulu nafasi hiyo leo Januari 06, 2022 ikiwa ni siku chache tangu kusambaa kwa video ambayo alinukuliwa akisema ipo siku Nchi itauzwa kutokana na madeni

Amesema ameandika Barua ya kujiuzulu kwa Katibu Mkuu wa CCM na uamuzi huo ni binafsi na hiari, na ameuchukua kwa kuzingatia maslahi mapana ya Nchi, Serikali na Chama

#JamiiForums

Mbunge wa Kongwa (CCM), Job Ndugai tarehe 10 Novemba 2020, alichaguliwa kuwa Spika wa Bunge la 12 baada ya kupata kura 344 kati ya kura 345 zilizopigwa sawa na asilimia 99.7. Kura moja ilimkataa. Ndugai alikuwa spika katika Bunge la 11 la 2015 - 2020.

Hapo awali akizungumza Desemba 28 katika mkutano mkuu wa pili wa wanakikundi cha Mikalile Ye Wanyusi uliofanyika jijini Dodoma, Ndugai alitetea uamuzi wa Bunge kuanzisha tozo za miamala ya simu, kuliko kuendelea kukopa kwani ipo Siku Nchi itapigwa Mnada

“Juzi mama ameenda kukopa 1.3 trilioni. hivi ipi bora. Sisi Watanzania wa miaka 60 ya uhuru kuzidi kukopa na madeni au tubanane banane hapa hapa, tujenge wenyewe bila madeni haya makubwa makubwa haya yasiyoeleweka. Ni lini sisi tutafanya wenyewe ‘and how’ (na kwa vipi),” alisema Spika Ndugai.

Job Ndugai alihoji wanaofurahia nchi kukopa na kwamba deni limefika Sh70 trilioni.

Kwa mujibu wa taarifa yake kwa umma, Ndugai amesema kuwa amemuandikia barua Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya kujiuuzulu nafasi hiyo ikibainisha kuwa uamuzi huo wa kuachia nafasi hiyo ameufanya kwa hiari.

“Naomba kutoa taarifa kwa uma wa watanzania kuwa leo Tarehe 06 Januari 2022 nimeandika barua kwenda kwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kujiuzulu nafasi ya Spika wa Bunge la Jamhuri wa wa Tanzania” imesema sehemu ya taarifa hiyo nakuongeza

“Pia nakala yangu hiyo ya kujiuzulu nimewasilisha kwa katibu wa Bunge
View attachment 2070821
Habari njema na Nuru mpya Kwa democrasia , uhuru wa kweli na haki katika taifa letu nauona mwanzo mpya Kwa bunge litakalo tekeleza wajibu wake ipasavyo, Sasa tuhamie Kwa wale wa NEC na wanaokwamisha kupatikana katiba mpya .
 
Alitakiwa ajiuzuru bila kuomba ule msamaha na hapo ndipo lengo la anachokiamini kingekuwa hai
Absolutely! Alikosea sana kuomba radhi, hapo nilimshangaa sana. Ila kitendo cha kujiuzulu kwangu ni kitendo cha kishujaa kabisa. Ni watanzania wangapi wakipishana mawazo na watawala wanachukua maamuzi magumu kama haya ya Ndugai na Lowasa?
 
Zama mpya za kuelekea demokrasia halisi
 
Karma!!hii kitu ni mbaya sana, yaani hakuna aliyekuwa anaweza kuwaza kuwa kuna siku hiki kidubwana kitaweza kuanguka kirahisi hivi!!!
Screenshot_20220106_173309_com.android.gallery3d_edit_40288593337081.jpg
 
Mwendazake aliwafanya watu waka sahau uongozi wakadhani vyeo walivyo navyo ni mali yao. Mungu huwa chukia wanao tesa viumbe wake. Sasa na aseme tena kwamba ana uwezo wa kuzuia mtu asiongee hadi bunge liishe. Asante Mungu usie sinzia. Covid jiandaeni.
 
Bado naendelea kumdharau kwa kushindwa kusimamia kile alichokuwa anakiamini,hakutakiwa kuomba msamaha angekaza mwanzo mwisho halafu akiona upepo siyo ajiuzulu kama hivi.

Alichofanya hapo amewawahi ili kuepuka aibu ya kustaafishwa kwa lazima but kisiasa kwa wenye akili haja-gain chochote.
 
Hana ujumbe wowote huyo alimpinga magufuli kabla hata mwili wakke haujaoza mnafiki mkubwa.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Yaani nilishangaa mno kwa vijembe vyake kwa marehemu na kuruhusu mijadala ya kumchafua marehemu. Mnafiki Sana huyu kenge wa Kigogo. Na ubunge astaafu kabisa
 
Duh watu wabaya sana, wameshililiankooni mpaka jamaa kaachia ngazi
 
Back
Top Bottom