Spika Ndugai alikuwa na hoja ya msingi, tatizo sio kukopa bali kukopa wakati kuna tozo za miamala ambazo mlidai zanajenga madarasa na vituo vya afya

Spika Ndugai alikuwa na hoja ya msingi, tatizo sio kukopa bali kukopa wakati kuna tozo za miamala ambazo mlidai zanajenga madarasa na vituo vya afya

Bunge la JMT lilipitisha tozo ambazo ama kwa hakika zilizua tafrani na kuzua kilio kwa wananchi, bila hata aibu Mwigulu Nchemba akainuka na kudai kuwa ambae hataki kulipa tozo basi ahamie Burundi.

Sasa kama mlipitisha tozo na mkadai kuwa zinajenga, shule, madarasa, zahanati na vituo vya afya mkopo wa tril 1.3 ajili ya madarasa wa nini?

Hizi tozo mnazokamua wananchi zinatumika kama kwa nini maana mlisema zitajenga madarasa na vituo vya afya.

Ndugai alimchukia sana Prof Assad alioelezwa kuwa bunge lake ni dhaifu, lakini ukweli ni kuwa ni dhaifu, halima meno kuikabaka serikali kwa makosa inayofanya.

Whether kuna watu wa Ccm wanataka kiti cha urais 2025 au hapana lakini ukweli ni kuwa kuna tozo zinaumiza wananchi ili hali kuna mkopo umejenga madarasa.
Sasa mama Samia mbona hazungumzii kama tozo basi au la?
Kwa mtazamo wangu, speaker Alijua fika jambo alilokuwa anataka kufanya; kuonyesha hadharani kwamba haridhishwi na hatua za kiuchumi za bi mkubwa. Akaamua kubwatuka.

Jambo ambalo hakulitegemea ni public reaction. Alidhani ataungwa mkono na watu wengi, haswa ndani CCM. Yaliyotokea nikinyume. Kimya kimetandaa ndani ya Chama.

Lakini pamoja na hayo, bwana speaker hana washauri waziri wa Public Relations. Hakutakiwa kusubiri mpaka Rais Samia aende jukwaani kuzungumzia hilo suala. Au kurudisha mapigo.

Baada ya kuona mjadala unapoelekea, alitakiwa kwenda kuomba poo kwa bi mkubwa haraka iwezekanavyo. Badala yake, ameenda kuitisha news conference kabla ya kuyamaliza na bosi wake.

Haya ndio matokeo yake. Masikio kutaka kuyapita mabega. Two most powerful people in the country wanatupiana maneno hadharani. Na wote ni CCM. Ni mpasuko ulioje?

Speaker ana mbinu nyingi za kuweza kuwasilisha malalamiko yake kuhusu jambo lolote., tena moja kwa moja kwa Raisi kuliko hii mbinu aliyotumia. Lakini alijua alichokuwa anakifanya. Alikuwa anatingisha kibiriti kama kimejaa. Bi mkubwa kaja in full force.
 
Huko vijijini unakotolea mfano ujue kwamba kulikuwa na harambee za ujenzi wa madarasa na miundo mbinu kama hiyo; zile jitihada za kujenga zingeendelea kwa hamasa zaidi, na tozo zifanye finishing.
Je wananchi waendelee kuamini kuwa serikali inaweza kila kitu, wao wazaliane tu? Kama siyo, je on nini ni mchango wao wa maana kwenye miundombinu?
Kila kijiji kina mambo yake ukiachana na mambo ambayo yapo kitaifa.

Ukienda baadhi ya vijiji vya kaskazini hawataki kuisubiri bajeti ya serikali, wao wanafanya sehemu yao halafu serikali itaendeleza walipoishia.

Ukienda huko kusini vipo vijiji hata vyoo hawajengi na serikali ikijenga inatakiwa iwape elimu wavitumie.

Matumizi na bajeti za serikali haizuii wanakijiji kujifanyia maendeleo kwa kasi yao wanayoihitaji. Ila WASILAZIMISHWE NA KUPEANA ADHABU, WAKUBALIANE NA SERIKALI ITAENDELEZA WANAPOISHIA KUTEGEMEANA NA BAJETI.
 
Kila kijiji kina mambo yake ukiachana na mambo ambayo yapo kitaifa.

Ukienda baadhi ya vijiji vya kaskazini hawataki kuisubiri bajeti ya serikali, wao wanafanya sehemu yao halafu serikali itaendeleza walipoishia.

Ukienda huko kusini vipo vijiji hata vyoo hawajengi na serikali ikijenga inatakiwa iwape elimu wavitumie.

Matumizi na bajeti za serikali haizuii wanakijiji kujifanyia maendeleo kwa kasi yao wanayoihitaji. Ila WASILAZIMISHWE NA KUPEANA ADHABU, WAKUBALIANE NA SERIKALI ITAENDELEZA WANAPOISHIA KUTEGEMEANA NA BAJETI.
Ukiwa mkuu wa familia, una watoto wawili:
1. Anajishughulisha kujiletea maendeleo; na wa
2 anazurura tu na kunywa, kuzaa.
Je utamsisitiza yupi kuendeleza juhudi ili akupunguzie mzigo wa kulea familia?
Je unajua kuwa huko tunakokwenda kupeleka bakuli wanatudharau na kutudhihaki kuwa wazembe?
Je unajua juhudi zinazofanyika vijijini kutoa mwelekeo wa mipango hasa ya miundombinu?
Kwa mtizamo wako, rasilimali za nchi zitawekwa dhamana ya mikopo, kama ilivyoanza kwa majirani zetu - Uganda, Zambia.
 
Hili ndio tatizo la kuongozwa na jinsia hii, jinsia hii mara zote hutaka isifiwe hata kama imetinyanga kazi, hii jinsia huwa haipendi kukosolewa hata kidogo.

Huyu kiongozi mpaka kanifanya nikakumbuke ka ex(kademu) kangu hivi , ilikuwa hata ukikashauli tu cha kufanya juu ya jambo fulani kanabwatuka , mara oooh unafikiri mimi sina akili ya kuwaza nini cha kufanya, mara kasuse tuu.

Sasa msishangae na huyu mvua pweza juu ya haya yanayojitokeza
 
Ukiwa mkuu wa familia, una watoto wawili:
1. Anajishughulisha kujiletea maendeleo; na wa
2 anazurura tu na kunywa, kuzaa.
Je utamsisitiza yupi kuendeleza juhudi ili akupunguzie mzigo wa kulea familia?
Unazungumzia familia yenye watoto M60 na nyumba 31 au tuseme mikoa.... Mfano wako ufanane na uhalisia.

Je unajua kuwa huko tunakokwenda kupeleka bakuli wanatudharau na kutudhihaki kuwa wazembe?
Je unajua juhudi zinazofanyika vijijini kutoa mwelekeo wa mipango hasa ya miundombinu?
Kwa mtizamo wako, rasilimali za nchi zitawekwa dhamana ya mikopo, kama ilivyoanza kwa majirani zetu - Uganda, Zambia.
Unafahamu nn kuhusu taratibu za rasilimali za nchi kuwekwa dhamana ya mikopo?
 
Leta mapendekezo yenye tija yatakayofit ndani ya Jamhuri. Hii sio korea.

Jambo lolote la maendeleo ni mzigo kwa anayetaka hayo maendeleo.
Sawa hii siyo korea, kipindi mnalinganisha deni la taifa letu na mataifa mengine mlitaka tufanane nao kimadeni? Jifunze kuiga kwa waliofanikiwa
 
Kwa matiki hii unakubali kuwa zifutwe na serikali itumie mkopo kuliko kuumiza wananchi. Hakuna anayepinga kukopa bali kwa nini ukope huku unatoza tozo ambazo hazina manufaa?
Aje akujibu hapa hapa.
 
Back
Top Bottom