Lachine
JF-Expert Member
- Nov 10, 2020
- 226
- 307
Kwa mtazamo wangu, speaker Alijua fika jambo alilokuwa anataka kufanya; kuonyesha hadharani kwamba haridhishwi na hatua za kiuchumi za bi mkubwa. Akaamua kubwatuka.Bunge la JMT lilipitisha tozo ambazo ama kwa hakika zilizua tafrani na kuzua kilio kwa wananchi, bila hata aibu Mwigulu Nchemba akainuka na kudai kuwa ambae hataki kulipa tozo basi ahamie Burundi.
Sasa kama mlipitisha tozo na mkadai kuwa zinajenga, shule, madarasa, zahanati na vituo vya afya mkopo wa tril 1.3 ajili ya madarasa wa nini?
Hizi tozo mnazokamua wananchi zinatumika kama kwa nini maana mlisema zitajenga madarasa na vituo vya afya.
Ndugai alimchukia sana Prof Assad alioelezwa kuwa bunge lake ni dhaifu, lakini ukweli ni kuwa ni dhaifu, halima meno kuikabaka serikali kwa makosa inayofanya.
Whether kuna watu wa Ccm wanataka kiti cha urais 2025 au hapana lakini ukweli ni kuwa kuna tozo zinaumiza wananchi ili hali kuna mkopo umejenga madarasa.
Sasa mama Samia mbona hazungumzii kama tozo basi au la?
Zitto: Tozo za miamala ziondolewe kwa sababu kuna hela ya IMF
Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe amesema tozo za miamala ziliwekwa na serikali katika bajeti ya serikali ya mwaka 2021/2022 ili kuwezesha ujenzi wa madarasa nchini. Hivi karibu Serikali imepata fedha kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa(IMF) ambazo zimetangazwa kutumika kujenga vituo na...www.jamiiforums.com
Jambo ambalo hakulitegemea ni public reaction. Alidhani ataungwa mkono na watu wengi, haswa ndani CCM. Yaliyotokea nikinyume. Kimya kimetandaa ndani ya Chama.
Lakini pamoja na hayo, bwana speaker hana washauri waziri wa Public Relations. Hakutakiwa kusubiri mpaka Rais Samia aende jukwaani kuzungumzia hilo suala. Au kurudisha mapigo.
Baada ya kuona mjadala unapoelekea, alitakiwa kwenda kuomba poo kwa bi mkubwa haraka iwezekanavyo. Badala yake, ameenda kuitisha news conference kabla ya kuyamaliza na bosi wake.
Haya ndio matokeo yake. Masikio kutaka kuyapita mabega. Two most powerful people in the country wanatupiana maneno hadharani. Na wote ni CCM. Ni mpasuko ulioje?
Speaker ana mbinu nyingi za kuweza kuwasilisha malalamiko yake kuhusu jambo lolote., tena moja kwa moja kwa Raisi kuliko hii mbinu aliyotumia. Lakini alijua alichokuwa anakifanya. Alikuwa anatingisha kibiriti kama kimejaa. Bi mkubwa kaja in full force.