Spika wa Bunge, Job Ndugai amempa onyo kali Mwanazuoni Jenerali Ulimwengu kutokana na alichokiita tabia yake ya kukashifu Watu mitandaoni.
Akizungumza katikati ya mjadala wa marekebisho ya Sheria mbalimbali uliowasilishwa Bungeni, Spika Ndugai amesema Ulimwengu ambaye ni Mwandishi wa Habari Nguli amekuwa akilikashfu Bunge na Spika apendavyo.
"Jenerali amekuwa akilivunjia heshima Bunge na Spika pia, napenda kumpa onyo kali kuchunga ulimi wake, haipendezi Mtu wa umri wake kuwa anaongea ovyoovyo, akiendelea na sisi tutaacha ukimya itabidi Watu washughulike nae ndani na nje yaani Mahakamani, habari imfikie uvumilivu wetu umefika mwisho, sisi sio kama anavyodhani" ——— Spika Ndugai