Spika Ndugai: Nampa onyo kali Jenerali Ulimwengu kuchunga ulimi wake, haipendezi mtu wa umri wake kuwa anaongea ovyo ovyo

Leo trh 11. 11. 2021 Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai amempa onyo kali kwa Mzee Jenerali Ulimwengu kutokana na tabia yake ya kutoa lugha za kejeli na dharau kwa viongozi mbalimbali na haswa Bunge.

kwa maoni yangu naona,
ni muhimu mzee Jenerali akajitathimini juu ya kauli zake anazo zitoa.
mzee ulimwengu ni mtu maarufu na ana heshimika ktk jamii, hivyo ni bora akaendelea kulinda heshima yake kwa kuwa makini na kauli zake anazo zitoa ambazo hazifai kuwatamkia binaadmu wenzake.

waswahili wanasema, "Heshima ni kitu cha bure"



 
Sahihi kabisa kuna maneno ya kuongea kwa lengo la kutoa maoni yako
Maoni huwa hayabezi watu hayadhalilishi watu hayakebehi watu
Uhuru wa maoni upo lakini si kwa kudhihaki watu
Hata mimi amenikwaza
 
Mzee ulimwengu inapaswa ajitafakari, au kama ana washauri basi awabadilishe au atafute washauri wazuri.
 
Siasa za Tanzania ni za kuheshimiana....hatuko katika nchi za magharibi....

Kwani haiwezekani mtu kukosoa bila ya kumdharau mwingine?!!!!

Inashindikanaje mtu kumkosoa mwingine bila ya kummwagia DHIHAKA ZENYE CHUSHO?!!!

Siempre JMT
 
Sahihi kabisa kuna maneno ya kuongea kwa lengo la kutoa maoni yako
Maoni huwa hayabezi watu hayadhalilishi watu hayakebehi watu
Uhuru wa maoni upo lakini si kwa kudhihaki watu
Hata mimi amenikwaza
Amesemaje mkuu?
 
Taarifa gani kwa mafano, iweke hapa tuichambue bila kujadili mambo kwa juu juu tu.
 
Sahihi kabisa kuna maneno ya kuongea kwa lengo la kutoa maoni yako
Maoni huwa hayabezi watu hayadhalilishi watu hayakebehi watu
Uhuru wa maoni upo lakini si kwa kudhihaki watu
Hata mimi amenikwaza
Naunga mkono hoja.
 
Sahihi kabisa kuna maneno ya kuongea kwa lengo la kutoa maoni yako
Maoni huwa hayabezi watu hayadhalilishi watu hayakebehi watu
Uhuru wa maoni upo lakini si kwa kudhihaki watu
Hata mimi amenikwaza
Mtu akikwita 'mbwa' wakati wewe siyo mbwa, Inakuuma nini?
Ikikuuma, jitathmini. Unakuwa na Tatizo. Sana ningemshauri Spika iwapo sheria za Bunge zinaruhusu, wamwite Jenerali siku ili WAHOJIANE. Awaelimishe, wamwelimishe. Basi. Nakumbuka miaka ya nyuma Serikali na Chama kilikuwa kikimtumia sana mheshimiwa Nape ktk scenario kama hizi. Alikuwa anajitosa kwenye mijadala ya wazi kupangua hoja mbalimbali zilizokuwa zikielekezwa kwa Chama na Serikali yake. Alifanikiwa sana. Hii ya kutisha kwenda mahakamani, Ni uchanga kisiasa.
 
Mpuuuzi huyo, Hana uwezo wa kumtisha ulimwengu
 
Jenerali kumfuatilia ni kumpa kiki. Waachane nae.
 
Ulimwengu ana akiri sana. Tatizo amezaliwa katika nchi ambayo watu wake wengi hawana akiri. Huyo angekuwa nchi za watu wenye kujitambua angekuwa mshauri wa Rais. Huyo baba anajua vitu vingi mno na ni mwansheria mbobezi na ni mwana.habari mguli. Mimi ningependa niwe kama yeye kwakweli
 
Head of the Main Law Making Institution in the Country communicating threats in no uncertain terms and by virtue of his position as a Public Officer to a law abiding Citizen is illegal, scandalous and dangerous.
 
Huyu Spika kazi pekee anayoimudu ni kuhangaika na watu wanaokinzana naye kuliko kulisaidia Taifa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…