Spika Ndugai: Nitawalinda wabunge wa Viti Maalumu CHADEMA kwa nguvu zote, Mnyika akajifunze kwa Dkt. Bashiru kazi za Katibu Mkuu

Spika Ndugai: Nitawalinda wabunge wa Viti Maalumu CHADEMA kwa nguvu zote, Mnyika akajifunze kwa Dkt. Bashiru kazi za Katibu Mkuu

Kwa busara tu, Mnyika ajiuzulu. Kwanza anapwaya sana kweny nafasi, hana elimu. Mwenyekiti elimu ni sifuri, KM hana elimu.. Ndo mana chama imekuwa genge la wahuni tu, hakuna mwenye uelewa ya nini kifanyike wapi na kwa muda gn?? Kila mtu msemaji na mtoaji wa matamko. Cheki hata Lisu anatoa matamko tena bila makubaliano ya vikao, ni uropoaji tu. Ni hatari kwa mustakali wa chama.
 
Kwasababu wameshakula kiapo, hivyo nao ni sehemu ya mhimili wa nchi, ambao ni bunge.
Kuna taratibu za kichama pia ambazo zina kupa uhalali wa kuwa hapo na usipo zifata utaadhibiwa... Hivyo tuelewe hilo pia.

Mwenyekiti na Rais wetu alisema wabunge wa chama chetu naweza kuwadhibiti ni kwa kanuni na taratibu za chama, kama kwa sheria za nchi basi haiwezi kuwa wabunge wa CCM pekee ni wa vyama vyote ana weza Fanya hivyo kwa mamlaka aliyo nayo
 
Spika Ndugai amesema kanuni za bunge zinamtaka kuwalinda wabunge walio wachache na maslahi yao naye atafanya hivyo kwa nguvu zake zote.

Ndugai amesema wabunge 19 wa Chadema wameteuliwa kihalali na kama Chadema wana matatizo nao walipaswa kuwaita kwa heshima na kuwasikiliza badala ya kuwahukumu na kuwafokea kupitia vyombo vya habari.

Spika Ndugai amesisitiza kuwa Mnyika bado hajakomaa kisiasa hivyo amemshauri aende kwa Katibu mkuu wa CCM Dr Bashiru akafundishwe namna Katibu mkuu anavyopaswa kutenda kazi zake kwa ufanisi.

Source TBC Aridhio

Maendeleo hayana vyama!
Namna pekee ya kuthibitisha uhalali wa hawa wabunge ni NEC kuonyesha barua ya uteuzi wao kutoka Chadema. Na kuweka wazi fomu walizojaza kukubali uteuzi huo zikiwa na sahihi za viongozi wenye mamlaka ya kufanya hivyo.

Mnyika kasema hadharani kuwa yeye kama Katibu Mkuu hajaandika barua yeyote na kuwa chombo chenye mamlaka ya kikatiba ya chama chake ya kufanya uteuzi huo hakijafanya hivyo. Hiyo ni dalili ya kiongozi aliyekomaa na anaejua wajibu wake kama Mtendaji Mkuu wa Chama.

Kwa vile Spika sio mwanachama wa Chadema, yeye kama sisi anatakiwa kusubiri matokeo ya kikao cha Kamati Kuu ya Chadema na wanachama wao. Uzuri ni kuwa baadhi ya anaosema atawatetea walikuwa wajumbe wa Kamati Kuu ambayo iliamua kuwatimua wabunge ambao walikaidi agizo la chama chao kutoingia bungeni na kujitenga kutokana na uwepo wa COVID-19. Kama nakumbuka vizuri wao ndio wakali wakiwaambia wakina Lijualikali kuwa wamepewa adhabu waliostahili na wasilie lie. Tunatumaini nao vile vile watapokea uamuzi wowote wa Kamati Kuu yao kwa moyo mkunjufu.

Spika anaweza kuamua la kufanya baada ya maamuzi kufanyika. Sasa hivi anaonekana tu kama mtu anaejaribu kuingilia taratibu ambazo hazimuhusu.

Amandla...
 
Spika Ndugai amesema kanuni za bunge zinamtaka kuwalinda wabunge walio wachache na maslahi yao naye atafanya hivyo kwa nguvu zake zote.

Ndugai amesema wabunge 19 wa CHADEMA wameteuliwa kihalali na kama CHADEMA wana matatizo nao walipaswa kuwaita kwa heshima na kuwasikiliza badala ya kuwahukumu na kuwafokea kupitia vyombo vya habari.

Spika Ndugai amesisitiza kuwa Mnyika bado hajakomaa kisiasa hivyo amemshauri aende kwa Katibu mkuu wa CCM Dr Bashiru akafundishwe namna Katibu mkuu anavyopaswa kutenda kazi zake kwa ufanisi.

Chanzo: TBC Aridhio

Maendeleo hayana vyama!
CD4 ikishuka sana, kisayansi mtu hutambulika kuwa hafai kufanya maamuzi sahihi yenye athari hasi kwa watu wengine.

Sent from my Nokia 2.1 using JamiiForums mobile app
 
Kwa busara tu, Mnyika ajiuzulu. Kwanza anapwaya sana kweny nafasi, hana elimu. Mwenyekiti elimu ni sifuri, KM hana elimu.. Ndo mana chama imekuwa genge la wahuni tu, hakuna mwenye uelewa ya nini kifanyike wapi na kwa muda gn?? Kila mtu msemaji na mtoaji wa matamko. Cheki hata Lisu anatoa matamko tena bila makubaliano ya vikao, ni uropoaji tu. Ni hatari kwa mustakali wa chama.
Hujielewi.
 
Spika Ndugai ametoa ufafanuzi mzuri sana!
Ila sidhani kama Mnyika kamwelewa. Mnyika kupayuka hadharani bila kujuwa msimamo wa wakubwa wake ukoje na maamuzi ya vikao vya juu yatakuwaje ni kupwaya kwenye wadhifa wake wa katibu mkuu. Aliyoyasema yalipaswa kusemwa na katibu mwenezi au mwenyekiti mwenyewe ambao nao ingalikuwa ngumu kusema hayo kabla ya maamuzi ya vikao vya chama.

Kama kamati kuu ya chama itaamua kinyume na alichokisema, Mnyika atapaswa kujiuzuru ukatibu mkuu.
 
Kwa busara tu, Mnyika ajiuzulu. Kwanza anapwaya sana kweny nafasi, hana elimu. Mwenyekiti elimu ni sifuri, KM hana elimu.. Ndo mana chama imekuwa genge la wahuni tu, hakuna mwenye uelewa ya nini kifanyike wapi na kwa muda gn?? Kila mtu msemaji na mtoaji wa matamko. Cheki hata Lisu anatoa matamko tena bila makubaliano ya vikao, ni uropoaji tu. Ni hatari kwa mustakali wa chama.
Unazungumzia elimu ipi bob?
 
Kwa busara tu, Mnyika ajiuzulu. Kwanza anapwaya sana kweny nafasi, hana elimu. Mwenyekiti elimu ni sifuri, KM hana elimu.. Ndo mana chama imekuwa genge la wahuni tu, hakuna mwenye uelewa ya nini kifanyike wapi na kwa muda gn?? Kila mtu msemaji na mtoaji wa matamko. Cheki hata Lisu anatoa matamko tena bila makubaliano ya vikao, ni uropoaji tu. Ni hatari kwa mustakali wa chama.
lipumba mwenye elimu na anayofanya ni upuuzi mtupu elimu na kuelimika ni vitu viwili tofauti ndugu
 
Back
Top Bottom