Leo Spika wa Bunge letu LA JMT Mh Job Ndugai ameongea na vyombo vya habari kuhusu mambo mbalimbali ya kibunge na mengineyo.
Moja kubwa lililowagusa wananchi ni kitendo chake cha kumuomba radhi Mh Rais Samia na watanzania wote kwa ujumla kutokana na sintofahamu iliyojitokeza ya kusambaa taarifa mitandaoni za kumkosoa Mh Rais kwa kile alichokiita "Nchi Kuuzwa kwa madeni"
Mm binafsi Nampongeza Mh Spika Ndugai kwa ukomavu wake wa kukiri makosa na kuomba msamaha kwa hilo.
Kuomba msamaha ni jambo dogo sana ila sio wote wanaoweza kufanya hivyo.kuomba msamaha ni kitendo cha kiungwana miongoni mwa waungwana iwe umekosea kweli or hujakosea.
Spika umeonyesha Utanzania wetu ulivyo kwa vitendo.Hongera sana.huu ndio Utanzania tuliorithishwa na wakubwa zetu waliotangulia.
Hapa katikati tulipitia maisha tamaduni na mazoea ya nchi zingine ambazo kimsingi tuliozoea Utanzania wetu tulikuwa tukipata tabu kuenenda na utamaduni Mpya ambao hatukuuzoea.
Watanzania utamaduni wetu ni Kukaa mezani kumaliza tofauti zetu na siku zote anaekubali kushindwa ndie mshindi.kuomba radhi na kukubali kubeba lawama iwe umehusika na kosa unalotuhumiwa nalo or hapana hii ndio sifa ya kiongozi mwenye busara.
Kuna wajinga wengi tu wanakukebehi na kukukejeli kwa kitendo chako cha kuomba radhi,naomba nikutie moyo kwamba tupo sisi ambao tunafikiri nje ya hizo dhihaka na kuona mantiki ya ulichokifanya kwa mustakali mwema wa nchi yetu.
Umeonyesha unazo sifa za kuwa kiongozi mwema,mzuri na unaeweza kubeba mizigo ya watu wengine kwa maslahi mapana ya watu wako.Hongera sana Mh Spika Ndugai.
Miaka ya Nyuma kidogo kwenye miaka ya 1980 Rais mstaafu wa awamu ya Pili Mzee wetu Ali Hassan Mwinyi,aliwajibika kubeba mzigo wa watu wengine alipokuwa Waziri wa mambo ya ndani kwa kujiuzulu nafasi yake kwa makosa yaliyofanywa na watu wa chini yake.
Inahitaji ukomavu wa hali juu,Uwajibikaji,Busara na hekima kuweza kubeba na kuzikubali "dhambi" hadharani na kuomba msamaha hadharani.kwangu mm hili ni jambo LA kishujaa kwa kiongozi mkubwa kaliba ya Spika wetu.
Huu ni mfano wa kuigwa kwa viongozi wengine, kiongozi sio malaika nae ni binadamu kama binadamu wengine hivyo kukosea ni jambo LA kawaida iwe kwa kujua or kutojua.So kitendo cha kuomba msamaha kinaonyesha na kuthibitisha ubinadamu alionao kiongozi.
Nina mengi ya kuzungumzia Ushujaa huu ila naomba niishie hapa, Hongera Mh Spika Ndugai.
Sent from my TECNO L8 Lite using
JamiiForums mobile app