Spika Tulia Ackson: Mdee na wenzake 18 wako bungeni kihalali, aeleza kuhusu kurejea kwa Bunge LIVE!

Spika Tulia Ackson: Mdee na wenzake 18 wako bungeni kihalali, aeleza kuhusu kurejea kwa Bunge LIVE!

Spika Dkt. Tulia Ackson amesema kuwa Wabunge 19 wa Viti Maalum wa CHADEMA ni halali, kwani wangekuwa haramu wasingekuwepo bungeni. Amesema bunge likipewa taarifa rasmi kuwa wamefukuzwa uanachama, watakoma kuwa wabunge, kwani mbunge sharti awe mwanachama wa chama cha siasa.
Si ndio maana nimesema wasiwasi unautoa wapi? Si hata Ndugai alisema hivyo? Kama wanajua kuwa wao ni watenda haki kwa nini walijipa kinga haraka haraka?

Hilo suala la ubunge halina nafasi hapa. Hata wakisamehewa na Chadema wataendelea kuwa wabunge haramu kwa sababu waliingia bungeni kinyume na taratibu.

Lakini hamna anaewashangaa. Kwenu haramu ni uamuzi wa Spika na sio kutokana na taratibu na sheria.

Amandla...
 
Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson akizungumza na Wahariri wa Vyombo vya Habari. leo Februari 14, 2022 ameeleza kuwa Mdee na wenzake 18 wako bungeni kihalali...
Huyu dada naona arrogance itaongezeka kadri ya siku .... atakuwa kama mtanguliziwake. Wenyewe wanasema madaraka hulevya ...!!
 
Wanataka warudishe liwe live baada ya kuona halina mvuto.

Ni mtu asiye na kazi za kufanya ndio ataangalia ujinga huo wa vikao vya CCM.
 
Kitu ambacho kinatafakarisha wenda chadema wamebariki hilo. Maana sarakasi zimekua nyingi
Sasa kama Covid19 walikata rufaa na rufaa hazijajibiwa mpaka leo that means kuna jambo lilikuwa linasukwa.

Alafu mle ndani kuna mapandikizi ya ccm kina Bulaya, Bananga, n.k.

Na bila shaka JPM na Ndugai walitegesha bomu la Covid19 kwa lengo la kuhalalisha mgogoro wa kukisambaratisha CDM.
 
Huyu dada anafikiri sisi wote wajinga kama alivyo yeye? Halafu eti anajiita Ameokoka, eti na mbinguni anakwenda?
 
Leo tumesikia spika wa bunge akisemakina Covid 19 wako bungeni kihalali. Nyie mna wahadaa Watanzania kwamba hamja wapeleka bungeni. Kwa kauli ya spika, tuna hitaji taarifa toka Chadema
Mode naomba msiunganishe huu uzi
 
Ni jambo jema!

Alichosema Spika Tulia ni kwamba bunge hupokea majina kutoka Tume ya uchaguzi na wao kazi yao ni kuwaapisha tu.

Je, NEC waliyapata wapi hayo majina?
 
Sasa unategemea kauli gani mpya zaidi ya kurudia kusema hawajawatuma?.
 
Total rubbish, wewe ukihukumia kifungo miaka 4 jela ukakata rufaa hutatumikia kifungo chako mpaka rufaa yako isikilizwe?
Mkuu, utawala uliopita, na ukichanganya na mambo ya Ndugai, ilikuwa hakuna kufuata sheria. Ukumbuke kuwa, huyo Ndugai aliikataa barua halali ya Chama kwa kudai haitambui. Kwa sasa, sina shaka mambo yamebadilika!
 
Leo tumesikia spika wa bunge akisemakina Covid 19 wako bungeni kihalali. Nyie mna wahadaa Watanzania kwamba hamja wapeleka bungeni. Kwa kauli ya spika, tuna hitaji taarifa toka Chadema
Mode naomba msiunganishe huu uzi

..Mnyika alishaandika barua kwa Spika kwamba Chadema imewafuta uanachama Halima na wenzake.

..Sheria inaelekeza kwamba mbunge aliyetokana na chama akifukuzwa ktk chama chake anapoteza sifa ya ubunge.

..Kwa hiyo anayetakiwa kutoa maelezo ya uhalali wa ubunge wa kina Halima ni Spika, na sio Mnyika.

..Spika anatakiwa aeleze sheria inayompa mamlaka ya kuendelea kuwakubali watu wasio na chama bungeni.

..Zaidi, vyombo vya DOLA vilitakiwa kuchunguza Halima na wenzake wamefika vipi bungeni kwani Chadema wanadai hawajawahi kufanya kikao cha kuteua wabunge wa viti maalum.
 
Chadema kisipobadilika kimtizamo na kiharakati basi itakua ni hatari sana kuwa na Chama Tawala chenye hulka hiyo. Ni nafuu kidogo Kwa CCM mana ni vyama vingi ndani ya Chama kimoja Cha Kijamaa feki .

CCM ina upinzani wa ndani Kwa ndani Tangu kilipoundwa,na kinafanya mabadiliko ya kiini macho mara Kwa mara. CCM inatawala na itaendelea kutawala mana inajua kucheza na akili ndogo za watanzania wengi na pia akili kubwa za wachache Kwa kuwapa fursa za kula nchi mpaka kuvimbiwa.

CCM inacheza na ukabila,CCM inacheza na Udini ,CCM inacheza na ujana ,CCM inacheza na jinsia ,CCM inacheza na Matajiri ,CCM inacheza na maskini. Ni ngumu sana Kwa siasa za upinzani kuiangusha CCM.

Kwa mfano suala la Kina Mdee lilikua ni suala dogo sana. Walipaswa kulishughulikia Kwa misingi yote ya Utawala Bora na Demokrasia.
Chadema ni Chama chenye udikteta mbaya kuliko ule wa Magufuli.

Wale akina mama walitoa udhuru kuwa Wapewe muda wa kujitetea na kusikilizwa . Kwani palikua na tatizo Gani kuwasikiliza ?
Mpaka Sasa wale ni washindi kwenye Misheni yao. Wamefanikiwa kuihadaa Serikali na wanapata mapesa Mengi kuliko hiyo misaada waliyotegemea kuipata Kutoka na bunge la vyama vingi.

Hili ni tatizo kubwa Kwa Watawala kufanya matumizi makubwa kuliko pato halisi la nchi. Chadema mpaka Sasa wameshindwa kusikiliza rufaa yao na kuitolea majibu na kupeleka Taarifa rasmi bungeni Tena mbele ya vyombo vya habari na kuonyesha barua hiyo Kwa wazi.

Chadema ni Chama kibaya kinachopendwa kama ilivyo CCM. Ni hulka ya Watanzania wanapenda kitu kishabiki. Chadema hakijajua kuwa kinafanya makosa Mengi sana ya kiufundi wakitegemea kutumia timua timua kuendesha Chama.

Waarabu walifanikiwa kuingia Afrika ya Kaskazini na kuifanya kuwa kama sehemu yao Kwa kuoa Wanawake wa Kiafrika na kubadili kizazi Cha waafrika na mwishowe waarabu kuwa wengi.

Kuna wakati unaweza kupambana na adui yake Kwa akili TU na ukamshinda bila kutumia nguvu. Chadema muda wote wanatumia ubabe kupambana na wababe wenye Dola , CCM.

Fungueni Kesi ya Kikatiba kupinga Hao Wabunge feki kukaa bungeni! Hukumu ikitoka hata 2030 ipo siku waliohusika watafikishwa mahakamani Kwa uhujumu uchumi mana wametumia mabilioni ya walipa tozo huku mafuta,sukari, Kodi , vifaa vya ujenzi n.k. Vikizidi kupanda bei. Watu wameoneana Muhali na kuruhusu mabilioni ya fedha za umma kupotea bila sababu wakati ambapo Vijana wengi wapo mitaani bila ajira.

Hukumu ikitoka kwamba katiba ilikiukwa Iko siku watu watakimbia kimbia na kujificha. Vinginevyo Chadema hawana uhakika Wala matumaini ya kushika Dola siku Moja.

Vinginevyo Chama kiwasamehe ili wafanye siasa kama kawaida na Sauti ya upinzani isikike bungeni Kwa uchache wake na vurugu zao zianze upya. 2025 wawapige cheni kwenye kura za maoni ndani ya Chama. Wawaache waendelee na Ubunge wao kihalali lakini wawavue uongozi ndani ya Chama.

CCM hua hakipotezagi muda mrefu kushambulia mtu lakini chadema miaka nenda Rudi kinaweza kuendeleza malumbano tu hata kama hayana tija yoyote. Kuna watu walikimbilia CCM Kwa tamaa ya madaraka na uteuzi kutokana na ugumu wa maisha. Mbowe alitakiwa awaambie Vijana wake wasipoteze muda kuwatukana na kuwadhalilisha kwenye mitandao.

Hao hao Huko ndani ya CCM ndio wangetumika kuibamoa CCM na kutoa Siri za ndani lakini badala yake ni matusi na kejeli mpaka wanageuka na kuwa wabaya zaidi.

Bunge linataka kujua kuwa utaratibu wa kufukuzwa kwao umefuatwa Kwa misingi ya Katiba ya Chama kinachojiita Cha kidemokrasia.

Hivi vyama vyote vya Kiafrika ni vya ajabu sana kwenye Demokrasia ya ndani matokeo yake vikiingia madarakani vinakuwa vya hovyo kabisa. Demokrasia hua haidanganyi ,mtu anayefaa hata iweje atashinda TU hata Kwa kura Moja. Uongozi ni karama. mfano hata kama pangekua na kampeni na uwazi kiasi Gani Sumaye asingemshinda Mbowe. Lakini figisu figisu na hofu vikasababisha uchaguzi kuwa wa kisanii usio na uhuru Wala usawa na haki.
 
Siasa ilivyo unaweza kukuta Kina Mbowe na hao Kina Mdee WALIYAJENGA VIZURI TU halafu wanawazuga tu watu .

..kwenye nchi za wenzetu Director of Criminal Investigation angechunguza kilichotokea na kama kuna uhuni / ufisadi umefanyika ingejulikana.
 
Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson akizungumza na Wahariri wa Vyombo vya Habari. leo Februari 14, 2022 ameeleza kuwa Mdee na wenzake 18 wako bungeni kihalali...
niliona na kusoma cv yake uyu mdada ilikuwa inaonesha kama ni mdada fulan ambaye ameitendea sana haki shule yake....lakini kauli yake kuhusu akina mdee inanitia shaka kidogo juu ya iyo cv yake nilivyoiongelea, ina maana huyu mh ameshindwa kabisa kutafsir sheria?

ametuambia kwamba akina mdee ni wabunge halali kabisa na wakati huo huo anatuaminisha kwamba ili uwe mbunge halali ni lazima uwe na chama , akaendelea kwa kusema kuna taratibu flan za kichama ambazo akina mdee hawajazikamilisha , sasa kama kuna taratibu hawajazikamilisha watakuwaje wabunge halali?

kuna majina fulan ambayo huwa tunapenda kuyatumia endapo mtu anakuwa hajakidhi vigezo, mfano : bw & bi harushi mtarajiwa maana yake hapo kuna kitu kinaendelea kuelekea kwenye tukio la harus

- prof mfawidhi - kuna kitu hapo kinaendelea kuelekea u prof
sasa jeh! ni vipi kuhusu hao wabunge ambao hawajakidhi vigezo halafu tuseme ni wabunge halali?
 
Mpaka wanakata rufaa maanake siyo wanachama wa CHADEMA
Bunge linaendeshwa kiutashi zaidi kuliko sheria na kanuni.Msekwa alisema kwa kipindi hicho yeye akiwa Spika Covid hawana uhalala,Ila kwasasa kama katiba imebadilishwa basis wanawezakuwa halali
 
Back
Top Bottom