sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,407
- 19,264
yule ni mnyakyusa, ila kana tamaa kale kadada.Huenda sio mnyakyusa pure bali ni mnyasa kutoka Malawi
ni sahihi kabisa, bunge limekua uchochoro wa kupitishia haramu katika nchiBunge sio muhimili unao jitegemea tena, ni kichaka cha maharamia
tulia katuaibisha wanyakyusa kwa kupitisha ule mkataba wa kuuza nchiPasi na Shaka unapozungumzia wanyakyusa ni kabila ambalo limeweza kutoa wanasiasa Nguli kutoka mikoa ya kusini.
Spika kutoa assist kubwa kuanzia zoezi la kuwaondoa wamasai mbugani hadi hapa tulipo sasa bandari kukodishwa milele kwa waarabu, imeleta maswali mengi sana,''
wataiba kura kama magufuli alivyofanyaFikilia wewe ni Spika na Mbunge wa mbeya Mjini.
Umepitisha Mkataba Bungeni na Kujikuta wakati Mugumu hata kuutetea kwa wananchi. Na hata ukijaribu kuutetea wananchi hawakuelewi.
Hapo hapo Jimboni kwako kunafunguliwa kesi ya huo mkataba na wananchi wanafurika mahakamani kusikiliza hiyo kesi.
Mda huo huo wazee wajimboni kwako na kwa wingi wanajitokeza kuupinga mkataba.
Hapo ndo utajua namna gani spika hali vikakaa tumboni.
Shujaa Magufuli hayupo Pambaneni na hali zenu πππ₯wataiba kura kama magufuli alivyofanya
Kanisa Moja Takatifu la Mitume πWanambeya hata bandari hawajui ni kitu gani. TULIA TRUST FUND ndio mkombozi wao
Yeye hata haimsumbui.
Anajua kuna wajinga bado watampigia kura.
Ametoa wapi helaTulia amewapelekea TULIA TRUST FUND inayowakomboa kiuchumi, iyo bandari haijawahi kuwasaidia
kutoka kwa wafadhiliAmetoa wapi hela
Apimwe dna huyuSpika wa Bunge Dr Tulia Mwansasu umetuaibisha na kutushushia heshima wanyakyusa wenzako kwa kitendo chako cha kukubali kutumika na kupitisha mkataba wa kitapeli wa bandari.
Unatufahamu wanyakyusa hatutaki ujinga kwenye mambo ya msingi, umepewa dhamana kubwa ya kuendesha chombo kikubwa katika nchi (Bunge) ila nasikitika kusema kwamba umetusaliti wanyakyusa kwa kukubali na kuutetea huo mkataba wa kitapeli wa bandari.
Utafanya wananchi watushushe heshima wanyakyusa kwa kutotupa nafasi nyingine kubwa ya kiuongozi katika nchi kwa sababu yako.
Tulia nakukumbusha kuna mambo ya kufanya siasa na utani lakini sio kufanya siasa na utani kwa jambo muhimu kama bandari, katika hili usipojisahihisha haraka hatutokuacha salama.
Umeshusha heshima kubwa waliyoiweka wazee wetu kina Mwandosya, Mwamunyange, Mwang'onda, Mwakibolwa n.k n.k kwenye utumishi wao wenye uadilifu katika nchi na uzalendo wao.
Kumbuka 2025 utakuja Mbeya kuomba kura kutetea ubunge wako, ila usipokataa au kurekebisha huo mkataba wa kitapeli wa bandari na sisi tutakukataa mapema.
Tumekutumia ujumbe kupitia wakili Boniface Mwabukusi ili akuoneshe taratibu na tamaduni zetu wanyakyusa, najua umemuona akikupa ujumbe kwenye hiyo video katika mtandao wa youtube, kama haujiona hiyo video nakusihi nenda kaangalie.
Unaomda wa kujisahihisha, wewe ni binti yetu tunakupenda na ndio maana tunakupa huu ujumbe wako kwa heshima yako na pia kutunza heshima ya wanyakyusa na nchi kwa ujumla.
Achana na huo mkataba wa kutaka kuuza nchi kwa kigezo cha uwekezaji, kumbuka Rungwe (Tukuyu) ni ardhi takatifu ukiendelea na huo mkataba wa bandari hautotakiwa kukanyaga Tukuyu milele.
Bado haimpi authority ya kuwadanganya.Tulia amewapelekea TULIA TRUST FUND inayowakomboa kiuchumi, iyo bandari haijawahi kuwasaidia