Spika wa Bunge Tulia Ackson anashangaa kwanini hadi leo polisi bado inamshikilia Kada wa CHADEMA Kombo Mbwana

Spika wa Bunge Tulia Ackson anashangaa kwanini hadi leo polisi bado inamshikilia Kada wa CHADEMA Kombo Mbwana

Hangaya alisema anasomaga
hii habari ingeandikwa kiudaku udaku angeisoma na kutolea maamuzi.
 
Akiongea na Wasafi FM leo Spika wa bunge Mh. Tulia Ackson amesema anashangaa kwanini hadi leo hii polisi bado inamshikilia Kombo Mbwana kada wa CHADEMA.

Mbwana alipotea tangu June 15 baada ya kutekwa nyumbani kwake na watu wasiojulikana huko Tanga, awali polisi ilikana kuwa naye baadae ikakiri kumshikilia.

Tulia amesema "siyo sahihi kwa polisi kumshikilia mtu bila kutoa taarifa kwa jamii kwa sababu inaweza kuzua taharuki".

Alikuwa akijibu swali aliloulizwa na Waandishi wa habari kina Kitenge, 'ni kwa nini Polisi inakamata watu na kuwaficha bila kutoa taarifa hii inapelekea jamii kuhisi kuwa polisi inahusika na utekaji'.

Tulia aliongeza kusema, hili ni changamoto na linahitaji marekebisho ya sheria.
Kwa hili bunge la kijinga hakuna kitu kitafanyika
 
Yale yalee ya magu kuja kutulalamikia wananchi na kutamani angekuwa IGP! Nchi ina mazingaombwe hii🙆‍♀️🙆‍♀️🙆‍♀️
Ya Magu yanazungumzika.

Point yake alikuwa akiwashangaa Polisi kukosa meno, ulimaanisha uwajibikaji dhaifu wa Polisi.

Hali ilivyokuwa wakati ule, ndivyo imejirudia sasa.

Hapo katikati Polisi waliituliza nchi, majambazi wale wa kutumia silaha za moto na za ncha kali walianza 'kukamatwa harakaharaka' na bahati mbaya majambazi wote walifia njiani wakikimbizwa hospitali, hadi nchi ikapoa.
 
Hajaminywa vizuri nini? Kwanini hajatoka?

Mpaka kieleweke.
 
Kama mkuu wa mhimili asingepaswa kushangaa anatakiwa achukue hatua ya kuruhusu bunge litoe muongozo nini kinakwamisha maendeleo hayo kwenye mfumo wa haki jinai.

Tena kama mbobezi wa sheria inasikitisha zaidi.
 
Pale Mafwele atakapokutana na mzee Kibao mbinguni
Mbinguni hakuna kilichokinyonge kitakachoingia!Tutamalizana hapa hapa na Muumba siku ya kiama :Hapo ndipo watakapomwona mwana wa Adamu akija mawinguni kwa nguvu nyingi na Utukufu.Ndipo atakapowatuma Malaika na kuwakusanya wateule wake Toka Pepo nne,Toka upande wa mwisho wa nchi hata upande wa wa mwisho wa mbingu''(Marko13:26,27) .
 
Back
Top Bottom