Startimes Tanzania: Support thread (maswali, maoni na ushauri)

Startimes Tanzania: Support thread (maswali, maoni na ushauri)

nimelipia lakini sioni channel na nyingine zina scratch tarehe ya kulipia 01/08/2015 kiasi 27,000/- kifurushi sibuka+uhuru namba ya uthibitisho ya huduma BP 15081.1810.B04071 Tigo pesa
sehemu ninayoishi ni Kisota kigamboni cha ajabu balance yangu inasoma 3,700
nambari ya king'amuzi ni 02035358589 simu yenu 0764 700 800 haipatikani nifanyenini
 
naishi Mbezi beach makonde nina kingamuzi cha startimes nataka kuweka hudume ambayo nitaona channel zote especially za cnn BBC ALJAZEERA NA NYINGINEZO naitaji pia fundi aje kuangalia dish langu cmu yangu 0784 640376
 
mi nataka kujua jinsi ya kulipia nione Chanel ya sibuka kwa mwezi
 
Kwa kweli nashukuru kwa uzi huu, Mimi ninaishi majohe Kwangozoma nina king'amuzi cha Star Time vile vya kwanza kabisa yaani hata mfumo wa kuwa kutakuwa na ving'amuzi ilikuwa hakuna.Hivyo kwa sasa Channel karibia zote zinascrach na kuandika No signals. Nimejaribu kununua aternal jingine lakini bado tatizo linaendelea natumia aternal ile ya magnetor. Naomba majibu tafadhali kama ni old one au vipi nijue ili nijipange.Maana nina ugomvi sana na watoto wangu juu ya king'amuzi hiki.
 
Mimi Naitwa MILANZI naishi MBEZI nimenunua vocha ya sh. 10,000 juzi nimeweka katika decoder 02035160274 nimepata baadhi tu ya channels kunfu inaganda na baadhi. Na ile offer mliosema siioni hapa tatizo mini? Startimes?.
 
Jibu Pia Kwenye Thread Husika Ili Tusio Tumia Huduma Zenu Tuone Ikiwa Mmerekebisha Matatizo Ya Wateja Wenu Ama Porojo
Kuna Makampuni
Mengi Yameanzisha Thread Halafu Hajibu Hoja
 
mi nataka kujua jinsi ya kulipia nione Chanel ya sibuka kwa mwezi

Mkuu waweza kulipia kwa tigopesa kwenye cm yako kwa namba *150*63# kisha fuata maelekezo. Hakikisha unakuwa na namba ya smrt card yako karibu maana utaulizwa kuingiza.
Star Times nilitarajia mtakuwa mkitujibu shida zetu kwa wakati ljn naona mko kimya sana sijui huu uzi mliuweka wa nn kama hamtaki kutoa ushirikiano kwa wateja wenu.
 
Mimi nimenunua king'amuzi jana jioni kufika home kinanipa meseji hii ..NO ACCESS.. NOT SUBSCRIBED.. tatizo nini? Halafu namba yenu ya huduma kwa wateja haipokelewi inaishia kunilia salio langu tu.
Mwenye ujuzi mnipe msaada sababu naona hata maswali ya watu huku hayajibiwi!
 
Nimelipia kifurushi lakini naona local channels tuu (star tv, tbc1, ch10 na itv) huu ni ubabaishaji
 
Nipo ubungo king'amuzi cha Star time kimekata sjui kwa nn? Kinasumbua sana iki king'amuzi
 
Nipo Sengerema king'amuzi ni shida.kina katakata ile mbya.channel zilizo strong ni Tv1na Tbc ninampango wa kuachana nanyi
 
Nimenunua king'amuzi dar cha 34000 nikaja nacho zenji hakioneshi channel ata moja,hakina ata mwezi mmoja na nusu na kina ofa yangu ya miezi 7.5,nilipowapigia huduma kwa wateja wakanielekeza niende kweny ofisi zao zilizopo apa zanzibar/mlandege,nilipofika wakanambia ni kweli kwa aina ya kingamuzi nlichopewa hakiwezi kuonesha zanzibar kwasababu minara yake haipo ambayo ni T2 km ckosei,nkawaomba wanibadulishie basi maana ndo utaratibu ulivo,lakini nliwashangaa walipotaka niwape na pesa ambayo ni sawa na ile ya kingamuzi kipya uku wakijidai ndo wananibadilishia.

Nilipowauliza iyo pesa yote ya nini na wakati nna warranty ya mwaka mzima wakadai eti ni ya vocha,nkawaambia mimi ctaki iyo vocha yenu ya 30000 coz icho kinhamuzi changu bafo kina ofa ya kutosha tu,kutoa elfu 30 tn ni sawa unaniuzia kingamuz kingine na sio kunibadilishia uko,mtoa huduma akanambia ndio utaratibu ulivo,nkaona huu ni utapeli tu na hii kampuni haiko makini katika kuwasaidia wateja bali kuwaibia tu,ilibidi nidai kingamuzi changu niondoke maana siku ya kwanza naenda ofisini kwao waliniomba nikiache ili waniombee cha kureplace tn waliniambia kwa tatizo langu ctotakiwa kulipia tena,but nlishangaa nliporudi tena wale vijana wamenigeukia,nusu nimrambe mtu makofi.

Wadau ebu mnaoijua hii kampuni kinagaubaga,hili langu limekaaje,mi ctaki icho kifurushi chao cha 30 elfu coz cha kwanza ni 34 elfu sas apo c bora kununua kipya tu hlf ukawa na viwili kuliko kutoa 30 elfu hlf na kile kingine unawaachia eti wamekubadilishia,apa wamebadilisha au wamekuuzia kingine?NAWASILISHA na kama wahusika mmo humu naomba muongozo.
 
Star Times Tanzania
ilikuwa ukishindwa lipia king'amuzi unaona local channels bure, but juzi nlishangaa mlikata zote ikabakia TV1 tu hadi nkalipia elfu 10 ina maana mmebasilisha utaratibu au???
 
Last edited by a moderator:
Star Times Tanzania
ilikuwa ukishindwa lipia king'amuzi unaona local channels bure, but juzi nlishangaa mlikata zote ikabakia TV1 tu hadi nkalipia elfu 10 ina maana mmebasilisha utaratibu au???

Hawaeleweki kabisa hawa ndugu, they are hopeless kabisa. wanaudhi kwelikweli.
 
Nimenunua kifurushi cha 20000 maana yake ni Uhuru, lakini mbona nikienda kwenye baadhi ya Chanel zinagoma zinasema, this channel belong to Uhuru plz recharge, mini naana yake
 
Back
Top Bottom