Startimes Tanzania: Support thread (maswali, maoni na ushauri)

hakikisha umekiweka inavotakiwa kisha zima king'amuzi uwashe tena,(zima kwa kutumia ile power buttom)
 
Wakuu msaada king’amuzi changu cha star time dish kinanletea sms ifuatayo card problem check card please insert your smart card again & make sure the direction is correct nafata hayo maelekezo lakin ngoma imegoma any solution pls
chomeka kadi hadi mwisho, Jaribu kuivuta nje kidogo kama milimita 2 usivute sana.
Zima na kuwasha king'amuzi

From JF App
 
Chip Isafishe Kwa Baadhi Ya Watu Walivyoshauri
Hata Yangu Ilikuwa Hivyo Hivyo Nasafisha Inapiga Kazi. Jitahidi Ikikaa Sawa Sawa Usipende Kuichomoa Na Kuingiza Mara Nyingi Sana Inalika Chip. Tatizo Kubwa Sana Vumbi Kwenye Chip
 


Binafsi nawashukuru kwa kuwa na njia hii ya mawasiliano. Kwa leo naomba kujua tu kwa mfano kuna channel siitaki iangaliwe nyumbani kwangu kama TBC nifanyeje kuiondoa kwenye orodha ya channel zilizopo?
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Binafsi nawashukuru kwa kuwa na njia hii ya mawasiliano. Kwa leo naomba kujua tu kwa mfano kuna channel siitaki iangaliwe nyumbani kwangu kama TBC nifanyeje kuiondoa kwenye orodha ya channel zilizopo?
 
Mimi ni mwangaliaji mkubwa wa channel zenu hasa swahili channel na mambo channel sasa hili tangazo Lenula mambo ya Solar refu mpaka linaboa yani kwanza kelele nyingi Kwa kifupi linaboa tangazeni vipande vifupi yani mkiweka TV Shopping watu wanahama chanel
 
Binafsi nawashukuru kwa kuwa na njia hii ya mawasiliano. Kwa leo naomba kujua tu kwa mfano kuna channel siitaki iangaliwe nyumbani kwangu kama TBC nifanyeje kuiondoa kwenye orodha ya channel zilizopo?
Very simple nenda channel setting kisha shusha kivuli kwenye chanel usiyoipenda bonyeza button ya blue then ok
 
Waga nalipia kifurushi Cha tzs 9K Sasa nataka nikalipie Cha 18k napataje hiyo huduma?
 
STARTIMES Mungu anawaona,niliwapigia simu kuwaomba mfungue FTA CHANNELS kwenye kisimbuzi changu na nyinyi mkanielekeza niende ofisi yenu iliyo jiran,nmefka pale mnaniambia niwape elfu 44 ndo mnifungulie FTA channels!!!basi nmekata shauri bora nikiweke stoo,local channels zishakuwa anasa!!!
ofisi niloenda
mbeya mjini,uhindini opposite posta
 
Umenena ukweli. Hata Mimi nimeona jinsi hili tangazo linavyoboa. Ni refu kama vile kipindi.
 
Habari zenu wakuu. Mimi namiliki king'amuzi cha Star times, lakini nimezoea kubadilishabadilisha malipo kutegemea na chaneli ninazozitaka kwa wakati huo. Naomba mturahisishie kwa kuweka options za kuchagua kifurushi anachokitaka mlipiaji badala ya kulazimika kuwapigia simu ili tuwaambie kifurushi tunachokitaka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…