KERO Stendi kuu ya mabasi ya Moshi (Kilimanjaro) imejaa ujinga, upuuzi, uchafu na ushamba uliopitiliza

KERO Stendi kuu ya mabasi ya Moshi (Kilimanjaro) imejaa ujinga, upuuzi, uchafu na ushamba uliopitiliza

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Kwa wiki nzima nikiwa na miche miche Moshi mjini, nikisafiri, kusafirisha watu na kupokea watu fulani fulani ikiwemo watalii kadhaa.
wewe fly kecha unatakiwa ujue hii nchi ni masikini africa ni masikini pia kwaiyoo hiyoo stand ungefunge macho upite hivi. ila tupa uchafu ndo utajua hujui. happy new year
 
Hakuna stendi hapo, ni pango la walanguzi, madalali, matapeli na wazururaji tu.
 
Uliyosema 90% ni kweli! Yaan pale stand sjawahi kupelewa!

Sijuwagi tofauti ya ile stand kubwa na ile stand ndogo! Maana kwenye stand kubwa had vi hiace vya kwenda uru vimejazana huko
 
Ukishangaa ya Moshi utayaona ya Arusha, sipendi kushukia wala kupandia kwenye hizo stendi, zimejaa wahuni sjapata kuona,
 
Nikiwa katika pitapita zangu za kusafiri mwishoni mwa mwaka huu wa 2023 nikajikuta mikoa ya kaskazini, nikatua Stendi kuu ya mabasi ya mikoani pale Moshi mjini na hapo nikakutana na mambo ya ajabu, yaani uchafu, ushamba na ujinga wa kiwango cha juu kupitiliza tena mamlaka za serikali zikisimamia.

Hivi inakuwaje mji wenye sifa ya usafi kuliko miji yote hapa Tanzania na pilikapilika za kitalii kuwa katika hali ile. Kwa sifa za mkoa wa Kilimanjaro na asili ya kipekee ya wenyeji wake (maendeleo na ustaarabu) nisingetegemea kuyakuta haya.

Sote tunajua, kwa mgeni mji huanzia stendi na huishia stendi, na kwa kuwa watu wengi hupenda kujifunza au kutaka kuiga ya Kilimanjaro basi nimeyaweka wazi haya ili kuwananga wahusika yamkini labda watajirekebisha.

Na hapa JF nitachambua kwa kina kila kitu cha kijinga, ushamba, upumbavu na uchafu uliopitiliza nilichokutana nacho pale stendi kuu ya mabasi Moshi mjini(Kilimanjaro).

Kwanza nikiri wazi, japokuwa hii stendi ilijengwa zamani kidogo (zaidi ya miaka 20 iliyopita) tena katikati ya mji wa Moshi lakini ubunifu wake bado unaonekana uko kisasa sana (standard bus stand design) japokuwa matumizi yake bado yako kizamani mnoo kwa Moshi. Na haya ndio kwa haraka haraka niliyoyaona;

1. Hakuna eneo rasmi la abiria kusubiria (Passenger waiting area). Yaani eneo rasmi lililojengwa kusubiria abiria limejazwa meza za ovyo za walanguzi na mawakala wa kukatia tiketi za mabasi, biashara ndogo ndogo, milingoti ya bendera za CCM nk. Yaani pamekaa kitapeli kwa 100%.

2. Hakuna ofisi rasmi hata moja ya makampuni ya mabasi ndani ya stendi. Vyumba vyote vimepangishwa biashara zingine zisizohusiana na usafirishaji. (Baada ya kudodosa sana nikaelezwa fremu karibu zote za chini ndani ya hiyo stendi ni miradi rasmi binafsi ya wakubwa ndani ya Manispaa ya Moshi na baadhi ya vigogo wa CCM mkoa, wamejimilikisha hizo fremu kifisadi na kuwapangisha watu vile wanavyojisikia na ndio kikwazo cha kuzuia kukamilika ujenzi wa stendi mpya maeneo ya Majengo)

3. Stendi imegeuzwa kuwa ni soko rasmi la wamachinga. Kila biashara ya uchuuzi, ulanguzi mdogo mdogo, mama lishe, shoe shine, kupaka rangi kucha, utapeli, udangaji nk unaikuta ndani ya stendi. Yaani ile sio stendi bali ni soko holela.

4. Hakuna sehemu rasmi za kutupia takataka ndogo ndogo za mikononi, ni kama hakuna dustbin kabisa. Takataka unaweza kutupa popote na hakuna yoyote wa kukukataza.

5. Hakuna taa zinazowaka usiku eneo la parking za mabasi, kumebakia magofu ya milingoti ya chuma na mabaki ya taa chakavu zilizokufa.

6. Miundo mbinu ya kudumu imechakaa kupitiliza. Kingo za kuta kuzunguka stendi zimebomoka na kupauka, barabara za ndani zimejaa mashimo balaa. Ni kama mahandaki ya kule Gaza.

7. Eneo lote la stendi limezungukwa na utitiri wa vibanda holela, vya ovyo ovyo ambavyo kila mtu anajiwekea atakavyo.

8. Kwa zaidi ya asilimia 80 ya eneo la stendi kumejaa magari ya Noah, Hiace na Coaster za kwenda maeneo ya karibu karibu ndani ya Kilimanjaro na machache ya Arusha badala ya mabasi ya masafa marefu ndani na nje ya nchi.

9. Stendi imepakana na kuunganika na na dampo dogo la takataka. Yaani kunanuna na taka taka kuzagaa mara kwa mara huku baadhi ya watu wakienda haja ndogo za papo kwa papo.

10. Kuna vyoo vya kulipia vinavyotoa harufu kali kuelekea nje huku utitiri wa biashara zingine (zikiwemo za vyakula) zikizunguka maeneo hayo hayo. Huhitaji kuuliza vyoo viko wapi, harufu ya vyoo inakuelekeza vilipo.

11. Hakuna alama zozote au vibao vyenye kueleza na kuelekeza maeneo mbalimbali (ukiondoa vyooni). Yaani pamekaa kienyeji mnoo, utadhani watu wote ni wenyeji wanaoishi ndani ya stendi hiyo siku zote.

12. Hakuna eneo/ofisi ya maulizo (Customer enquiry). Ukipata shida au changamoto hujui uanzia wapi, uulize wapi, ulalamike wapi au umuulize nani.

13. Mazingira ya kiusalama ni sifuri. Emergency Assemble point hakuna, hakuna ofisi rasmi za polisi (kuna trafiki wanaokaa kaa njia ya kutokea mabasi muda fulani) nk.

14. Hakuna wabeba mizigo rasmi wala toroli rasmi za kubeba mizigo ya wasafiri. Kumejaa mateja na wapiga debe wanaomvamia msafiri yoyote mwenye mizigo na kumbabaisha.

15. Nyakati za usiku mara nyingi stendi hufungwa kabisa. Hivyo mabasi kulazimika kushushia abiria nje ya stendi.

16. Kumejaa kelele za muziki kutoka kwenye maduka, vibanda, baa uchwara na vispika vya matangazo ya biashara. Yaani pako vururu vururu.

17. Sehemu kubwa ya juu ghorofani ni kama haitumiki kabisa, sijui bado inajengwa! Ama imekosa wapangaji? Pamekaa kama gofu la kale.

18. Ndani ya jengo la stendi kuna vibanda umiza kwa ajili ya kuonyesha video, mpira, kuchoma CD, kudanga na kucheza kamari (betting).

19. Kumejaa takataka zilizozagaa balaa. Haijarishi ni muda gani, iwe asubuhi, mchana au usiku, ni machupa ya maji, vifungashio vya plastiki mpaka maganda ya matunda.

20. Parking ya magari binafsi na tax haileweki, kila mara huzaa migongano na mizozo. Hakuna tofauti kati ya tax rasmi, tax bubu na gari binafsi. Eneo la parking za magari lipo lakini utaratibu hauleweki na usalama ni duni. (Japokuwa kuwa kuna eneo rasmi, safi na bora la parking/stendi ya pikipiki).

21. Miundo mbinu ya kunawa mikono imebakia magofu ndani ya stendi, haifanyi kazi na bado ipo ndani ya stendi kama kumbukumbu ya kudumu!. Yaani usafi wa kunawa mikono uliletwa Moshi na Covid na ukafa baada ya covid kufifia.

Kwa leo niishie hapo, ni mengi nimejionea lakini kwa uhakika hayo ndio nimeweza kuandika, kama huamini siku moja pita pale na kushuhudia mwenyewe.
Moshi unaionea TU kaka, njoo Huku dar Kwa Chalamila, njia zote, namaanisha zote zimewekwa kuwa masoko
 
ULICHOSEMA KWA MOSHI NI KWELI

Mimi nimetokea maeneo hayo, Moshi kuna Ujinga na Ushamba katika Manispaa ya Mji, hawajali chochote cha maana zaidi ya Rushwa/ Pesa

Kingine kwa pale Moshi, kuna yale majengo ya frame pale stendi yalijengwa na baadhi ya Wananchi wenye uwezo kwa mkataba wa kupewa fremu

Sasa hao wanachojali ni kupata pesa tu na kujenga huko vijijini na maeneo mengine

Kwa Mfano kuna Mtu anaitwa NOVATUS KIMARIO, huyu pale ana maduka nane (8) ya Cosmetics matatu, ya vyakula vya kawaida kama Mini supermarket n.k. Sasa huyu Jamaa ama maduka yanayoangalia stendi kbs na pale nyuma katikati ya jengo...huyu hata Halmashauri ya Mji haimwambii chochote japo Wananchi wa chini wanamlalamikia kwa mengi

Pia wapo wengine kadhaa...yaani mji unamilikiwa na watu wachache wanaoonga viongozi wa Halmashauri

Ndio maana mpango wa stendi mpya imekwama na sio kwamba Halmashauri haiingizi pesa

UJINGA MTUPU
 
Hayo mambo uliyoyataja yanapatikana kila sehemu sio moshi tu anyway mm kinachonikwaza pale stand ni mtu unajua unapoenda lakini madalali wanavyokuganda kukufuata kama vile umepotea
Hao madalali kwani kuna sehemu nchi wanapokesekana?
 
Nikiwa katika pitapita zangu za kusafiri mwishoni mwa mwaka huu wa 2023 nikajikuta mikoa ya kaskazini, nikatua Stendi kuu ya mabasi ya mikoani pale Moshi mjini na hapo nikakutana na mambo ya ajabu, yaani uchafu, ushamba na ujinga wa kiwango cha juu kupitiliza tena mamlaka za serikali zikisimamia.

Hivi inakuwaje mji wenye sifa ya usafi kuliko miji yote hapa Tanzania na pilikapilika za kitalii kuwa katika hali ile. Kwa sifa za mkoa wa Kilimanjaro na asili ya kipekee ya wenyeji wake (maendeleo na ustaarabu) nisingetegemea kuyakuta haya.

Sote tunajua, kwa mgeni mji huanzia stendi na huishia stendi, na kwa kuwa watu wengi hupenda kujifunza au kutaka kuiga ya Kilimanjaro basi nimeyaweka wazi haya ili kuwananga wahusika yamkini labda watajirekebisha.

Na hapa JF nitachambua kwa kina kila kitu cha kijinga, ushamba, upumbavu na uchafu uliopitiliza nilichokutana nacho pale stendi kuu ya mabasi Moshi mjini(Kilimanjaro).

Kwanza nikiri wazi, japokuwa hii stendi ilijengwa zamani kidogo (zaidi ya miaka 20 iliyopita) tena katikati ya mji wa Moshi lakini ubunifu wake bado unaonekana uko kisasa sana (standard bus stand design) japokuwa matumizi yake bado yako kizamani mnoo kwa Moshi. Na haya ndio kwa haraka haraka niliyoyaona;

1. Hakuna eneo rasmi la abiria kusubiria (Passenger waiting area). Yaani eneo rasmi lililojengwa kusubiria abiria limejazwa meza za ovyo za walanguzi na mawakala wa kukatia tiketi za mabasi, biashara ndogo ndogo, milingoti ya bendera za CCM nk. Yaani pamekaa kitapeli kwa 100%.

2. Hakuna ofisi rasmi hata moja ya makampuni ya mabasi ndani ya stendi. Vyumba vyote vimepangishwa biashara zingine zisizohusiana na usafirishaji. (Baada ya kudodosa sana nikaelezwa fremu karibu zote za chini ndani ya hiyo stendi ni miradi rasmi binafsi ya wakubwa ndani ya Manispaa ya Moshi na baadhi ya vigogo wa CCM mkoa, wamejimilikisha hizo fremu kifisadi na kuwapangisha watu vile wanavyojisikia na ndio kikwazo cha kuzuia kukamilika ujenzi wa stendi mpya maeneo ya Majengo)

3. Stendi imegeuzwa kuwa ni soko rasmi la wamachinga. Kila biashara ya uchuuzi, ulanguzi mdogo mdogo, mama lishe, shoe shine, kupaka rangi kucha, utapeli, udangaji nk unaikuta ndani ya stendi. Yaani ile sio stendi bali ni soko holela.

4. Hakuna sehemu rasmi za kutupia takataka ndogo ndogo za mikononi, ni kama hakuna dustbin kabisa. Takataka unaweza kutupa popote na hakuna yoyote wa kukukataza.

5. Hakuna taa zinazowaka usiku eneo la parking za mabasi, kumebakia magofu ya milingoti ya chuma na mabaki ya taa chakavu zilizokufa.

6. Miundo mbinu ya kudumu imechakaa kupitiliza. Kingo za kuta kuzunguka stendi zimebomoka na kupauka, barabara za ndani zimejaa mashimo balaa. Ni kama mahandaki ya kule Gaza.

7. Eneo lote la stendi limezungukwa na utitiri wa vibanda holela, vya ovyo ovyo ambavyo kila mtu anajiwekea atakavyo.

8. Kwa zaidi ya asilimia 80 ya eneo la stendi kumejaa magari ya Noah, Hiace na Coaster za kwenda maeneo ya karibu karibu ndani ya Kilimanjaro na machache ya Arusha badala ya mabasi ya masafa marefu ndani na nje ya nchi.

9. Stendi imepakana na kuunganika na na dampo dogo la takataka. Yaani kunanuna na taka taka kuzagaa mara kwa mara huku baadhi ya watu wakienda haja ndogo za papo kwa papo.

10. Kuna vyoo vya kulipia vinavyotoa harufu kali kuelekea nje huku utitiri wa biashara zingine (zikiwemo za vyakula) zikizunguka maeneo hayo hayo. Huhitaji kuuliza vyoo viko wapi, harufu ya vyoo inakuelekeza vilipo.

11. Hakuna alama zozote au vibao vyenye kueleza na kuelekeza maeneo mbalimbali (ukiondoa vyooni). Yaani pamekaa kienyeji mnoo, utadhani watu wote ni wenyeji wanaoishi ndani ya stendi hiyo siku zote.

12. Hakuna eneo/ofisi ya maulizo (Customer enquiry). Ukipata shida au changamoto hujui uanzia wapi, uulize wapi, ulalamike wapi au umuulize nani.

13. Mazingira ya kiusalama ni sifuri. Emergency Assemble point hakuna, hakuna ofisi rasmi za polisi (kuna trafiki wanaokaa kaa njia ya kutokea mabasi muda fulani) nk.

14. Hakuna wabeba mizigo rasmi wala toroli rasmi za kubeba mizigo ya wasafiri. Kumejaa mateja na wapiga debe wanaomvamia msafiri yoyote mwenye mizigo na kumbabaisha.

15. Nyakati za usiku mara nyingi stendi hufungwa kabisa. Hivyo mabasi kulazimika kushushia abiria nje ya stendi.

16. Kumejaa kelele za muziki kutoka kwenye maduka, vibanda, baa uchwara na vispika vya matangazo ya biashara. Yaani pako vururu vururu.

17. Sehemu kubwa ya juu ghorofani ni kama haitumiki kabisa, sijui bado inajengwa! Ama imekosa wapangaji? Pamekaa kama gofu la kale.

18. Ndani ya jengo la stendi kuna vibanda umiza kwa ajili ya kuonyesha video, mpira, kuchoma CD, kudanga na kucheza kamari (betting).

19. Kumejaa takataka zilizozagaa balaa. Haijarishi ni muda gani, iwe asubuhi, mchana au usiku, ni machupa ya maji, vifungashio vya plastiki mpaka maganda ya matunda.

20. Parking ya magari binafsi na tax haileweki, kila mara huzaa migongano na mizozo. Hakuna tofauti kati ya tax rasmi, tax bubu na gari binafsi. Eneo la parking za magari lipo lakini utaratibu hauleweki na usalama ni duni. (Japokuwa kuwa kuna eneo rasmi, safi na bora la parking/stendi ya pikipiki).

21. Miundo mbinu ya kunawa mikono imebakia magofu ndani ya stendi, haifanyi kazi na bado ipo ndani ya stendi kama kumbukumbu ya kudumu!. Yaani usafi wa kunawa mikono uliletwa Moshi na Covid na ukafa baada ya covid kufifia.

Kwa leo niishie hapo, ni mengi nimejionea lakini kwa uhakika hayo ndio nimeweza kuandika, kama huamini siku moja pita pale na kushuhudia mwenyewe.
Asante sana tutayafanyia kazi mambo haya yote.
 
Nikiwa katika pitapita zangu za kusafiri mwishoni mwa mwaka huu wa 2023 nikajikuta mikoa ya kaskazini, nikatua Stendi kuu ya mabasi ya mikoani pale Moshi mjini na hapo nikakutana na mambo ya ajabu, yaani uchafu, ushamba na ujinga wa kiwango cha juu kupitiliza tena mamlaka za serikali zikisimamia.

Hivi inakuwaje mji wenye sifa ya usafi kuliko miji yote hapa Tanzania na pilikapilika za kitalii kuwa katika hali ile. Kwa sifa za mkoa wa Kilimanjaro na asili ya kipekee ya wenyeji wake (maendeleo na ustaarabu) nisingetegemea kuyakuta haya.

Sote tunajua, kwa mgeni mji huanzia stendi na huishia stendi, na kwa kuwa watu wengi hupenda kujifunza au kutaka kuiga ya Kilimanjaro basi nimeyaweka wazi haya ili kuwananga wahusika yamkini labda watajirekebisha.

Na hapa JF nitachambua kwa kina kila kitu cha kijinga, ushamba, upumbavu na uchafu uliopitiliza nilichokutana nacho pale stendi kuu ya mabasi Moshi mjini(Kilimanjaro).

Kwanza nikiri wazi, japokuwa hii stendi ilijengwa zamani kidogo (zaidi ya miaka 20 iliyopita) tena katikati ya mji wa Moshi lakini ubunifu wake bado unaonekana uko kisasa sana (standard bus stand design) japokuwa matumizi yake bado yako kizamani mnoo kwa Moshi. Na haya ndio kwa haraka haraka niliyoyaona;

1. Hakuna eneo rasmi la abiria kusubiria (Passenger waiting area). Yaani eneo rasmi lililojengwa kusubiria abiria limejazwa meza za ovyo za walanguzi na mawakala wa kukatia tiketi za mabasi, biashara ndogo ndogo, milingoti ya bendera za CCM nk. Yaani pamekaa kitapeli kwa 100%.

2. Hakuna ofisi rasmi hata moja ya makampuni ya mabasi ndani ya stendi. Vyumba vyote vimepangishwa biashara zingine zisizohusiana na usafirishaji. (Baada ya kudodosa sana nikaelezwa fremu karibu zote za chini ndani ya hiyo stendi ni miradi rasmi binafsi ya wakubwa ndani ya Manispaa ya Moshi na baadhi ya vigogo wa CCM mkoa, wamejimilikisha hizo fremu kifisadi na kuwapangisha watu vile wanavyojisikia na ndio kikwazo cha kuzuia kukamilika ujenzi wa stendi mpya maeneo ya Majengo)

3. Stendi imegeuzwa kuwa ni soko rasmi la wamachinga. Kila biashara ya uchuuzi, ulanguzi mdogo mdogo, mama lishe, shoe shine, kupaka rangi kucha, utapeli, udangaji nk unaikuta ndani ya stendi. Yaani ile sio stendi bali ni soko holela.

4. Hakuna sehemu rasmi za kutupia takataka ndogo ndogo za mikononi, ni kama hakuna dustbin kabisa. Takataka unaweza kutupa popote na hakuna yoyote wa kukukataza.

5. Hakuna taa zinazowaka usiku eneo la parking za mabasi, kumebakia magofu ya milingoti ya chuma na mabaki ya taa chakavu zilizokufa.

6. Miundo mbinu ya kudumu imechakaa kupitiliza. Kingo za kuta kuzunguka stendi zimebomoka na kupauka, barabara za ndani zimejaa mashimo balaa. Ni kama mahandaki ya kule Gaza.

7. Eneo lote la stendi limezungukwa na utitiri wa vibanda holela, vya ovyo ovyo ambavyo kila mtu anajiwekea atakavyo.

8. Kwa zaidi ya asilimia 80 ya eneo la stendi kumejaa magari ya Noah, Hiace na Coaster za kwenda maeneo ya karibu karibu ndani ya Kilimanjaro na machache ya Arusha badala ya mabasi ya masafa marefu ndani na nje ya nchi.

9. Stendi imepakana na kuunganika na na dampo dogo la takataka. Yaani kunanuna na taka taka kuzagaa mara kwa mara huku baadhi ya watu wakienda haja ndogo za papo kwa papo.

10. Kuna vyoo vya kulipia vinavyotoa harufu kali kuelekea nje huku utitiri wa biashara zingine (zikiwemo za vyakula) zikizunguka maeneo hayo hayo. Huhitaji kuuliza vyoo viko wapi, harufu ya vyoo inakuelekeza vilipo.

11. Hakuna alama zozote au vibao vyenye kueleza na kuelekeza maeneo mbalimbali (ukiondoa vyooni). Yaani pamekaa kienyeji mnoo, utadhani watu wote ni wenyeji wanaoishi ndani ya stendi hiyo siku zote.

12. Hakuna eneo/ofisi ya maulizo (Customer enquiry). Ukipata shida au changamoto hujui uanzia wapi, uulize wapi, ulalamike wapi au umuulize nani.

13. Mazingira ya kiusalama ni sifuri. Emergency Assemble point hakuna, hakuna ofisi rasmi za polisi (kuna trafiki wanaokaa kaa njia ya kutokea mabasi muda fulani) nk.

14. Hakuna wabeba mizigo rasmi wala toroli rasmi za kubeba mizigo ya wasafiri. Kumejaa mateja na wapiga debe wanaomvamia msafiri yoyote mwenye mizigo na kumbabaisha.

15. Nyakati za usiku mara nyingi stendi hufungwa kabisa. Hivyo mabasi kulazimika kushushia abiria nje ya stendi.

16. Kumejaa kelele za muziki kutoka kwenye maduka, vibanda, baa uchwara na vispika vya matangazo ya biashara. Yaani pako vururu vururu.

17. Sehemu kubwa ya juu ghorofani ni kama haitumiki kabisa, sijui bado inajengwa! Ama imekosa wapangaji? Pamekaa kama gofu la kale.

18. Ndani ya jengo la stendi kuna vibanda umiza kwa ajili ya kuonyesha video, mpira, kuchoma CD, kudanga na kucheza kamari (betting).

19. Kumejaa takataka zilizozagaa balaa. Haijarishi ni muda gani, iwe asubuhi, mchana au usiku, ni machupa ya maji, vifungashio vya plastiki mpaka maganda ya matunda.

20. Parking ya magari binafsi na tax haileweki, kila mara huzaa migongano na mizozo. Hakuna tofauti kati ya tax rasmi, tax bubu na gari binafsi. Eneo la parking za magari lipo lakini utaratibu hauleweki na usalama ni duni. (Japokuwa kuwa kuna eneo rasmi, safi na bora la parking/stendi ya pikipiki).

21. Miundo mbinu ya kunawa mikono imebakia magofu ndani ya stendi, haifanyi kazi na bado ipo ndani ya stendi kama kumbukumbu ya kudumu!. Yaani usafi wa kunawa mikono uliletwa Moshi na Covid na ukafa baada ya covid kufifia.

Kwa leo niishie hapo, ni mengi nimejionea lakini kwa uhakika hayo ndio nimeweza kuandika, kama huamini siku moja pita pale na kushuhudia mwenyewe.
Stendi ni ya kishenzi sana ile, nilishawahi kuona katoto ka kichagga kamechuchumaa kanakunya huku raia wakimwangalia tu, naulizia watu mama wa yule mtoto yuko wapi wakasema mama yake anafanya kazi kwenye banda lile lile alilokuwa anakunya mwanawe na hashituki ukimwambia analeta ugomvi na kuuliza unataka mwanangu akanye wapi sasa.
 
Nikiwa katika pitapita zangu za kusafiri mwishoni mwa mwaka huu wa 2023 nikajikuta mikoa ya kaskazini, nikatua Stendi kuu ya mabasi ya mikoani pale Moshi mjini na hapo nikakutana na mambo ya ajabu, yaani uchafu, ushamba na ujinga wa kiwango cha juu kupitiliza tena mamlaka za serikali zikisimamia.

Hivi inakuwaje mji wenye sifa ya usafi kuliko miji yote hapa Tanzania na pilikapilika za kitalii kuwa katika hali ile. Kwa sifa za mkoa wa Kilimanjaro na asili ya kipekee ya wenyeji wake (maendeleo na ustaarabu) nisingetegemea kuyakuta haya.

Sote tunajua, kwa mgeni mji huanzia stendi na huishia stendi, na kwa kuwa watu wengi hupenda kujifunza au kutaka kuiga ya Kilimanjaro basi nimeyaweka wazi haya ili kuwananga wahusika yamkini labda watajirekebisha.

Na hapa JF nitachambua kwa kina kila kitu cha kijinga, ushamba, upumbavu na uchafu uliopitiliza nilichokutana nacho pale stendi kuu ya mabasi Moshi mjini(Kilimanjaro).

Kwanza nikiri wazi, japokuwa hii stendi ilijengwa zamani kidogo (zaidi ya miaka 20 iliyopita) tena katikati ya mji wa Moshi lakini ubunifu wake bado unaonekana uko kisasa sana (standard bus stand design) japokuwa matumizi yake bado yako kizamani mnoo kwa Moshi. Na haya ndio kwa haraka haraka niliyoyaona;

1. Hakuna eneo rasmi la abiria kusubiria (Passenger waiting area). Yaani eneo rasmi lililojengwa kusubiria abiria limejazwa meza za ovyo za walanguzi na mawakala wa kukatia tiketi za mabasi, biashara ndogo ndogo, milingoti ya bendera za CCM nk. Yaani pamekaa kitapeli kwa 100%.

2. Hakuna ofisi rasmi hata moja ya makampuni ya mabasi ndani ya stendi. Vyumba vyote vimepangishwa biashara zingine zisizohusiana na usafirishaji. (Baada ya kudodosa sana nikaelezwa fremu karibu zote za chini ndani ya hiyo stendi ni miradi rasmi binafsi ya wakubwa ndani ya Manispaa ya Moshi na baadhi ya vigogo wa CCM mkoa, wamejimilikisha hizo fremu kifisadi na kuwapangisha watu vile wanavyojisikia na ndio kikwazo cha kuzuia kukamilika ujenzi wa stendi mpya maeneo ya Majengo)

3. Stendi imegeuzwa kuwa ni soko rasmi la wamachinga. Kila biashara ya uchuuzi, ulanguzi mdogo mdogo, mama lishe, shoe shine, kupaka rangi kucha, utapeli, udangaji nk unaikuta ndani ya stendi. Yaani ile sio stendi bali ni soko holela.

4. Hakuna sehemu rasmi za kutupia takataka ndogo ndogo za mikononi, ni kama hakuna dustbin kabisa. Takataka unaweza kutupa popote na hakuna yoyote wa kukukataza.

5. Hakuna taa zinazowaka usiku eneo la parking za mabasi, kumebakia magofu ya milingoti ya chuma na mabaki ya taa chakavu zilizokufa.

6. Miundo mbinu ya kudumu imechakaa kupitiliza. Kingo za kuta kuzunguka stendi zimebomoka na kupauka, barabara za ndani zimejaa mashimo balaa. Ni kama mahandaki ya kule Gaza.

7. Eneo lote la stendi limezungukwa na utitiri wa vibanda holela, vya ovyo ovyo ambavyo kila mtu anajiwekea atakavyo.

8. Kwa zaidi ya asilimia 80 ya eneo la stendi kumejaa magari ya Noah, Hiace na Coaster za kwenda maeneo ya karibu karibu ndani ya Kilimanjaro na machache ya Arusha badala ya mabasi ya masafa marefu ndani na nje ya nchi.

9. Stendi imepakana na kuunganika na na dampo dogo la takataka. Yaani kunanuna na taka taka kuzagaa mara kwa mara huku baadhi ya watu wakienda haja ndogo za papo kwa papo.

10. Kuna vyoo vya kulipia vinavyotoa harufu kali kuelekea nje huku utitiri wa biashara zingine (zikiwemo za vyakula) zikizunguka maeneo hayo hayo. Huhitaji kuuliza vyoo viko wapi, harufu ya vyoo inakuelekeza vilipo.

11. Hakuna alama zozote au vibao vyenye kueleza na kuelekeza maeneo mbalimbali (ukiondoa vyooni). Yaani pamekaa kienyeji mnoo, utadhani watu wote ni wenyeji wanaoishi ndani ya stendi hiyo siku zote.

12. Hakuna eneo/ofisi ya maulizo (Customer enquiry). Ukipata shida au changamoto hujui uanzia wapi, uulize wapi, ulalamike wapi au umuulize nani.

13. Mazingira ya kiusalama ni sifuri. Emergency Assemble point hakuna, hakuna ofisi rasmi za polisi (kuna trafiki wanaokaa kaa njia ya kutokea mabasi muda fulani) nk.

14. Hakuna wabeba mizigo rasmi wala toroli rasmi za kubeba mizigo ya wasafiri. Kumejaa mateja na wapiga debe wanaomvamia msafiri yoyote mwenye mizigo na kumbabaisha.

15. Nyakati za usiku mara nyingi stendi hufungwa kabisa. Hivyo mabasi kulazimika kushushia abiria nje ya stendi.

16. Kumejaa kelele za muziki kutoka kwenye maduka, vibanda, baa uchwara na vispika vya matangazo ya biashara. Yaani pako vururu vururu.

17. Sehemu kubwa ya juu ghorofani ni kama haitumiki kabisa, sijui bado inajengwa! Ama imekosa wapangaji? Pamekaa kama gofu la kale.

18. Ndani ya jengo la stendi kuna vibanda umiza kwa ajili ya kuonyesha video, mpira, kuchoma CD, kudanga na kucheza kamari (betting).

19. Kumejaa takataka zilizozagaa balaa. Haijarishi ni muda gani, iwe asubuhi, mchana au usiku, ni machupa ya maji, vifungashio vya plastiki mpaka maganda ya matunda.

20. Parking ya magari binafsi na tax haileweki, kila mara huzaa migongano na mizozo. Hakuna tofauti kati ya tax rasmi, tax bubu na gari binafsi. Eneo la parking za magari lipo lakini utaratibu hauleweki na usalama ni duni. (Japokuwa kuwa kuna eneo rasmi, safi na bora la parking/stendi ya pikipiki).

21. Miundo mbinu ya kunawa mikono imebakia magofu ndani ya stendi, haifanyi kazi na bado ipo ndani ya stendi kama kumbukumbu ya kudumu!. Yaani usafi wa kunawa mikono uliletwa Moshi na Covid na ukafa baada ya covid kufifia.

Kwa leo niishie hapo, ni mengi nimejionea lakini kwa uhakika hayo ndio nimeweza kuandika, kama huamini siku moja pita pale na kushuhudia mwenyewe.
True, hii stendi ni chafu mno haswa wakati wa mvua utakuta vinyesi kila uchochoro tena vikiwa fresh kabisa.
 
Mateja wa Moshi wana vile vikofia vyao vimejikunja kwa mbele hivi.
[emoji16]
Sema stand ya Moshi imetulea sana. 2000s tukitoroka shule tunaenda hapo stand kula, kunyoa, na kuburn CDs pale ghorofani huku tukitafuta videmu toka shule za girls.
[emoji1]
Walevi nao walikuwa wanajinywea banana ghorofani kwenye kona.

Hopefully, stand mpya itakamilika, mambo yatakuwa poa.
 
Hakuna Stendi Pale Ni Eneo La Ajabu Sana Labda Watakapohamia Stendi Mpya Chini Ya Moshi Pazuri
 
I wish mamlaka zingesoma hili bandiko na kuanzia hapa, yaani hii ni starting point nzuri sana. Hongera kwa kuibua changamoto.
 
Nikiwa katika pitapita zangu za kusafiri mwishoni mwa mwaka huu wa 2023 nikajikuta mikoa ya kaskazini, nikatua Stendi kuu ya mabasi ya mikoani pale Moshi mjini na hapo nikakutana na mambo ya ajabu, yaani uchafu, ushamba na ujinga wa kiwango cha juu kupitiliza tena mamlaka za serikali zikisimamia.

Hivi inakuwaje mji wenye sifa ya usafi kuliko miji yote hapa Tanzania na pilikapilika za kitalii kuwa katika hali ile. Kwa sifa za mkoa wa Kilimanjaro na asili ya kipekee ya wenyeji wake (maendeleo na ustaarabu) nisingetegemea kuyakuta haya.

Sote tunajua, kwa mgeni mji huanzia stendi na huishia stendi, na kwa kuwa watu wengi hupenda kujifunza au kutaka kuiga ya Kilimanjaro basi nimeyaweka wazi haya ili kuwananga wahusika yamkini labda watajirekebisha.

Na hapa JF nitachambua kwa kina kila kitu cha kijinga, ushamba, upumbavu na uchafu uliopitiliza nilichokutana nacho pale stendi kuu ya mabasi Moshi mjini(Kilimanjaro).

Kwanza nikiri wazi, japokuwa hii stendi ilijengwa zamani kidogo (zaidi ya miaka 20 iliyopita) tena katikati ya mji wa Moshi lakini ubunifu wake bado unaonekana uko kisasa sana (standard bus stand design) japokuwa matumizi yake bado yako kizamani mnoo kwa Moshi. Na haya ndio kwa haraka haraka niliyoyaona;

1. Hakuna eneo rasmi la abiria kusubiria (Passenger waiting area). Yaani eneo rasmi lililojengwa kusubiria abiria limejazwa meza za ovyo za walanguzi na mawakala wa kukatia tiketi za mabasi, biashara ndogo ndogo, milingoti ya bendera za CCM nk. Yaani pamekaa kitapeli kwa 100%.

2. Hakuna ofisi rasmi hata moja ya makampuni ya mabasi ndani ya stendi. Vyumba vyote vimepangishwa biashara zingine zisizohusiana na usafirishaji. (Baada ya kudodosa sana nikaelezwa fremu karibu zote za chini ndani ya hiyo stendi ni miradi rasmi binafsi ya wakubwa ndani ya Manispaa ya Moshi na baadhi ya vigogo wa CCM mkoa, wamejimilikisha hizo fremu kifisadi na kuwapangisha watu vile wanavyojisikia na ndio kikwazo cha kuzuia kukamilika ujenzi wa stendi mpya maeneo ya Majengo)

3. Stendi imegeuzwa kuwa ni soko rasmi la wamachinga. Kila biashara ya uchuuzi, ulanguzi mdogo mdogo, mama lishe, shoe shine, kupaka rangi kucha, utapeli, udangaji nk unaikuta ndani ya stendi. Yaani ile sio stendi bali ni soko holela.

4. Hakuna sehemu rasmi za kutupia takataka ndogo ndogo za mikononi, ni kama hakuna dustbin kabisa. Takataka unaweza kutupa popote na hakuna yoyote wa kukukataza.

5. Hakuna taa zinazowaka usiku eneo la parking za mabasi, kumebakia magofu ya milingoti ya chuma na mabaki ya taa chakavu zilizokufa.

6. Miundo mbinu ya kudumu imechakaa kupitiliza. Kingo za kuta kuzunguka stendi zimebomoka na kupauka, barabara za ndani zimejaa mashimo balaa. Ni kama mahandaki ya kule Gaza.

7. Eneo lote la stendi limezungukwa na utitiri wa vibanda holela, vya ovyo ovyo ambavyo kila mtu anajiwekea atakavyo.

8. Kwa zaidi ya asilimia 80 ya eneo la stendi kumejaa magari ya Noah, Hiace na Coaster za kwenda maeneo ya karibu karibu ndani ya Kilimanjaro na machache ya Arusha badala ya mabasi ya masafa marefu ndani na nje ya nchi.

9. Stendi imepakana na kuunganika na na dampo dogo la takataka. Yaani kunanuna na taka taka kuzagaa mara kwa mara huku baadhi ya watu wakienda haja ndogo za papo kwa papo.

10. Kuna vyoo vya kulipia vinavyotoa harufu kali kuelekea nje huku utitiri wa biashara zingine (zikiwemo za vyakula) zikizunguka maeneo hayo hayo. Huhitaji kuuliza vyoo viko wapi, harufu ya vyoo inakuelekeza vilipo.

11. Hakuna alama zozote au vibao vyenye kueleza na kuelekeza maeneo mbalimbali (ukiondoa vyooni). Yaani pamekaa kienyeji mnoo, utadhani watu wote ni wenyeji wanaoishi ndani ya stendi hiyo siku zote.

12. Hakuna eneo/ofisi ya maulizo (Customer enquiry). Ukipata shida au changamoto hujui uanzia wapi, uulize wapi, ulalamike wapi au umuulize nani.

13. Mazingira ya kiusalama ni sifuri. Emergency Assemble point hakuna, hakuna ofisi rasmi za polisi (kuna trafiki wanaokaa kaa njia ya kutokea mabasi muda fulani) nk.

14. Hakuna wabeba mizigo rasmi wala toroli rasmi za kubeba mizigo ya wasafiri. Kumejaa mateja na wapiga debe wanaomvamia msafiri yoyote mwenye mizigo na kumbabaisha.

15. Nyakati za usiku mara nyingi stendi hufungwa kabisa. Hivyo mabasi kulazimika kushushia abiria nje ya stendi.

16. Kumejaa kelele za muziki kutoka kwenye maduka, vibanda, baa uchwara na vispika vya matangazo ya biashara. Yaani pako vururu vururu.

17. Sehemu kubwa ya juu ghorofani ni kama haitumiki kabisa, sijui bado inajengwa! Ama imekosa wapangaji? Pamekaa kama gofu la kale.

18. Ndani ya jengo la stendi kuna vibanda umiza kwa ajili ya kuonyesha video, mpira, kuchoma CD, kudanga na kucheza kamari (betting).

19. Kumejaa takataka zilizozagaa balaa. Haijarishi ni muda gani, iwe asubuhi, mchana au usiku, ni machupa ya maji, vifungashio vya plastiki mpaka maganda ya matunda.

20. Parking ya magari binafsi na tax haileweki, kila mara huzaa migongano na mizozo. Hakuna tofauti kati ya tax rasmi, tax bubu na gari binafsi. Eneo la parking za magari lipo lakini utaratibu hauleweki na usalama ni duni. (Japokuwa kuwa kuna eneo rasmi, safi na bora la parking/stendi ya pikipiki).

21. Miundo mbinu ya kunawa mikono imebakia magofu ndani ya stendi, haifanyi kazi na bado ipo ndani ya stendi kama kumbukumbu ya kudumu!. Yaani usafi wa kunawa mikono uliletwa Moshi na Covid na ukafa baada ya covid kufifia.

Kwa leo niishie hapo, ni mengi nimejionea lakini kwa uhakika hayo ndio nimeweza kuandika, kama huamini siku moja pita pale na kushuhudia mwenyewe.
Binafsi nikusifu na nikushukuru kwa maono na hasa kwa kufikiri kiasi cha kuona na kujua mahali pa kuiandika hii kero,

haya yoote uliyaandika yana ukweli kwa 100% .

hivyo ni bora umejitokeza ukaliandika hili ambalo umeliona ili wahusika walifanyie kazi

mimi ninavyoona shida inaanzia pale nia za wahusika ama mamlaka ambao ndiyo wenye kupaswa kusimamia majukumu wanaposhindwa kuutambua wajibu wao na wapi wanapaswa kusimamia yapi

Kwa kuanzia tu ni kwamba mji kama moshi ina ofisi ya manispaa na ama halmashauri ama jiji kuna ofisi za mkurugenzi,meya maafisa mipango miji,afisa biashara kunao madiwani hawa woote hawafahamu ama hawajitambui wajibu wao

Nasema hivyo kwa sababu jengo la stand ya moshi wakati linajengwa hata kama ni miaka mingi huko nyuma lakini ramani na ujenzi wake ulipangwa vizuri sana hivyo ilipaswa tu kufanyiwa matumizi sahihi kama ilivyojengwa yaani sehemu ya kuweka ofisi za mabasi ibakie itumike katika uhalisia wa ramani ya ujenzi I kuwepo eneo la kupumzika wasafiri na sehemu chache za maduka ya huduma ambazo ni muhimu na za msingi kwa ajili ya mahitaji ya wasafiri ikiwepo kama biashara yenye kuhusiana na ubadilishaji wa fedha na maswala mengine yenye kuhusiana na fedha,air line ofisi,snacks shop,pharmas,ofisa usalama kwa rais(polisi),ofisi inayohusika na usimamizi wa kituo kwa ujumla,ofisi ya maulizo na maelekezo kwa wageni na mambo kama hayo hizi ni kwa uchache ila ni baadhi ya huduma ambazo ni muhimu kuwepo na siyo lazima kuwepo na maduka mia moja ama elfu kwa sababu hii siyo shopping mall bazaar bali hii ni stand ama bus terminal hivyo ni makosa kufikiria kwamba wakiondolewa wale wanaofanya biashara pale wataenda wapi na kama tunahitaji kuwa na standards lazima sasa tusiwaangalie wanaofanya biashara pale ila tukishakamilisha ofisi ambazo ni muhimu kuwepo basi kama kuna maeneo ya ziada yaliyobakia na ambayo yapo kwenye utaratibu wa ramani ya mjenzi yatolewe kwa maelekezo ya biashara gani zinahitajika kuwepo na siyo mpangaji kujiamlia kuweka biashara anayohitaji yeye bali tangu mwanzo ofisi ya afisa biashara ianishe biashara zinazohitajika na na zipi za kupewa kipaumbele

na kuwepo na ubao wenye kuelekeza huduma zinazopatikana ndani ya kituo
isiruhusiwe kuweka meza maeneo ambayo ramani haioneshi kama ilipaswa kupangwa meza na wala kusiwepo na kuweka miamvuli inayoonekana kama uchafu ama vichaka wapiga debe wapigwe marufuku kwa maana kutakuwepo na information desks moja ama zaidi kama kutahitajika
kuhusiana matoroli inawezekana kuweka ama kuruhusu kampuni yenye kueleweka ikafanya hiyo kazi kwa kuwekewa utaratibu wa kuvaa sare na vitambulisho na hapa utaona maana na uzuri wa stand ya mabasi

Hivyo haya yote yanawezekana iwapo tu watendaji wa mamlaka zenye kuhusika watajiondoa na kuacha kushiriki katika shughuli za kupangisha ama kujimilikisha biashara kwenye eneo la stand na ikiwa pia mipango ya stand itaachwa ipangwe na mamlaka bila kuingiza siasa ndani yake
zitangazwe tenda pale penye kuhitajika ili kusiwepo na upendeleo kwa afisa biashara ama kiongozi kutoka ofisi ya serkali ama chama cha siasa.
 
Back
Top Bottom