Stendi ya Daladala Mbezi Mwisho ni chafu sana, Mbunge wetu hawezi kujua hilo ana mambo mengi

Stendi ya Daladala Mbezi Mwisho ni chafu sana, Mbunge wetu hawezi kujua hilo ana mambo mengi

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Jana nilifuatilia mjadala ulioanzishwa na JF kuhusu maoni ya sisi Wananchi wa kawaida kwenda kwa viongozi wetu hasa Wabunge, kwanza niwapaongeze sana kwa hicho walichokifanya na ninawashauri wakiendeleza kwa kuwa kero zipo nyingi.

Binafsi naamini wanasiasa ni watu wanaofuata upepo, kuna muda wanaweza kuliona jambo fulani la muhimu na wao watakiwa kulifanyia kazi, lakini kama halina mafufaa kwao au kama haliigiwi kelele wanaweza kuliacha kama lilivyo.

So, nilipoona JF wameanzisha kitu kama hiki inamaanisha kuwa ni kama tutakuwa tunawapigia kelele wakumbuke wajibu wao.

Povu langu mimi pia limfikie Mbunge wetu anayesimamia Jimbo la Ubungo ikiwezekana na viongozi wote ambao watakuwa wanahusika.

Suala la uchafu kwenye kituo cha Daladala cha Mbezi Mwisho kwa kweli ni kero na inatia kinyaa, hivi wao kwa kuwa wanatumia magari ya Serikali na hawaingii pale kituoni ndio maana wanatuchukulia poa ehh?

Kuna siku nimekuta mwanaume kasimama anakojoa katikati ya magari, na hakuna anayejali, harufu za mikojo zimesambaa, kibaya zaidi maeneo hayo ndipo ambapo kuna Watanzania wenzetu wanapanga bidhaa zao kuuza.

Hii ni hatari kwa afya, niwaambie wakati wanapambana kuwaondoa Wamachinga wajue na kufanya usafi au walizingatie hilo, kadiri siku zinavyoenda ndivyo uchafu unavyozidi kuongezeka.


Mbezii.jpg

Mbezi uchafu.jpg
FjhitiDX0AAFjWD.jpg

 
UBUNGO hakuna MBUNGE kuna Mjumbe wa Ccm jimbo la Ubungo Stendi imegeuka ya kawaida sana Vibanda vya Machinga vimezaliwa ndani ya stendi kwenye Corridor za Abiria kusubiria Safari
 
Ile stendi ya mbezi mwisho tatizo sio uchafu ila imezidiwa, daladala bajaji na boda boda zimekuwa nyingi sana kaeneo kenyewe kadogo.
 
Ile stendi ya mbezi mwisho tatizo sio uchafu ila imezidiwa, daladala bajaji na boda boda zimekuwa nyingi sana kaeneo kenyewe kadogo.
Hilo nalo neno, pamekuwa padogo, pamezidiwa.
 
Kero iende kwa mamlaka nzima ya dar es salaam. Kuna kipindi walichoma kodi kwenda kujifunza Rwanda nahsi usafi walioukuta Rwanda uliwakatisha tamaa wakabwaga manyanga. Mitanzania ni michafu balaa watu bado wanatupa takataka barabarani karne hii
 
Stand ya Mbezi mwisho kweli ni chafu sana sana, wale wapiga debe wa stand ya Magufuli wanakojoa ovyo pale stand ya daladala

Machinga wanasababisha uchafu kwa bidhaa zao zilizoharibika wanatupa kwenye mitaro na kusababisha harufu mbaya ya uozo.

Hakuna utaratibu wa kupaga daladala, bajaji wala bajaji wanakaa ovyo ovyo tu.

Machinga nao ndio wanakaa kila kona ya stand wanajaa wao hata hakuna njia ya kupita watu mnapita kwa kubananaaana njia zote wameziba.

Kifupi Stand ya Mbezi inahitaji kuangaliwa upya ni kero kubwa sana.
 
Ile stendi ikifika saa 12 inageuka soko na dala dala umo umo. Sasa sijui nani ana control wale wafanyabiashara kuhakikisha wanafanya usafi
 
Hapa ndipo ninapochoka nikiwafikiria watendaji wa wilaya. Amini usiamini itokee Mhe Rais ahoji kuhusu Suala la Uchafu wa Stand ya Mbezi au aseme Stand ya daladala mbezi imeshazidiwa uwezo, kwa kauli hiyo tu utaona jinsi viongozi na watendaji wa wilaya watakavyoanza kukimbizana na suala litapatiwa ufumbuzi faster tu.

Hii inamaanisha kwamba viongozi wengi na watendaji ngazi za kati na chini Serikalini hasa Mikoa na Wilaya sio wawajibikaji kabisa, Kiongozi mzuri ni yule anayewajibika pasipo kutishiwa au kusukumwa au kuhojiwa na Mkubwa wake.

Binafisi natamani sana Mheshimiwa Rais awaondoe hawa watu. Hivi kweli suala la uchafu wa Stand ni mpaka Mheshimiwa Rais au Waziri Mkuu alitolee tamko!!

hivi kweli suala la Machinga kurudi Stand nyakati za jioni na usiku ni hadi wakuu wa Kitaifa watoe maelekezo kwa viongozi wa Wilaya.

Hivi Kweli Kuzidiwa kwa Stand ya daladala mbezi mwisho ni hadi viongozi wa Kitaifa waumize vichwa wakati kuna viongozi na watendaji wa Wilaya na Mkoa.

Unapokuwa kiongozi wa ofisini ni dhahiri kuna mengi hutayapata. Viongozi wilayani na mkoa wakiwa ni watu wakutoka wangekuwa wanapata mengi sana . Pia wangepata maoni ya wadau/wananchi namna ya kutatua au kupunguza baadhi ya changamoto.

Mfano, iwapo kungejengwa Stand ndogo upande wa juu yaani pale njia ya Goba kungepunguza msongamano kwenye Stand ya Sasa ya daladala kwani abiria wa msakuzi, msumi na wale wanaopanda gari za kwenda Mwenge na Tegeta kupitia Goba wangepandia hapo.

Mhe. Rais wangu Mpendwa na Mhe. Waziri Mkuu tunaomba kukiwa na mabadiliko ya wakurugenzi , watendaji na wakuu wa wilaya muikumbuke na wilaya ya Ubungo.
 
Hapa ndipo ninapochoka nikiwafikiria watendaji wa wilaya. Amini usiamini itokee Mhe Rais ahoji kuhusu Suala la Uchafu wa Stand ya Mbezi au aseme Stand ya daladala mbezi imeshazidiwa uwezo, kwa kauli hiyo tu utaona jinsi viongozi na watendaji wa wilaya watakavyoanza kukimbizana na suala litapatiwa ufumbuzi faster tu.
Hii inamaanisha kwamba viongozi wengi na watendaji ngazi za kati na chini Serikalini hasa Mikoa na Wilaya sio wawajibikaji kabisa, Kiongozi mzuri ni yule anayewajibika pasipo kutishiwa au kusukumwa au kuhojiwa na Mkubwa wake.

Binafisi natamani sana Mheshimiwa Rais awaondoe hawa watu. Hivi kweli suala la uchafu wa Stand ni mpaka Mheshimiwa Rais au Waziri Mkuu alitolee tamko!!!,
hivi kweli suala la Machinga kurudi Stand nyakati za jioni na usiku ni hadi wakuu wa Kitaifa watoe maelekezo kwa viongozi wa Wilaya!!!
Hivi Kweli Kuzidiwa kwa Stand ya daladala mbezi mwisho ni hadi viongozi wa Kitaifa waumize vichwa wakati kuna viongozi na watendaji wa Wilaya na Mkoa.

Unapokuwa kiongozi wa ofisini ni dhahiri kuna mengi hutayapata. Viongozi wilayani na mkoa wakiwa ni watu wakutoka wangekuwa wanapata mengi sana . Pia wangepata maoni ya wadau/wananchi namna ya kutatua au kupunguza baadhi ya changamoto.

Mfano, iwapo kungejengwa Stand ndogo upande wa juu yaani pale njia ya Goba kungepunguza msongamano kwenye Stand ya Sasa ya daladala kwani abiria wa msakuzi, msumi na wale wanaopanda gari za kwenda Mwenge na Tegeta kupitia Goba wangepandia hapo

Mhe. Rais wangu Mpendwa na Mhe. Waziri Mkuu tunaomba kukiwa na mabadiliko ya wakurugenzi , watendaji na wakuu wa wilaya muikumbuke na wilaya ya Ubungo
Tutalaumiana hapa ila usafi+ustaarabu unaanza na
Wewe/mimi
Mtanzania bila bakora haendi

Ova
 
Yaani hii stand ni chafu hadi inanuka! DED wa Ubungo ni aibu kwako!
Mikel Lesta Koma! Stendi ya Daladala Mbezi Mwisho ni mali ya TANROADS na hao TANROADS ndiyo wanaokusanya ushuru, kusimamia usafi na pia kile choo ni cha kwao. Na pia ndiyo wameruhusu biashara pale.

Ubungo Manispaa haihusiki na hiyo stendi.

Halafu Manispaa ya Ubungo haina DED bali ina MD, Municipal Director
 
Hapa ndipo ninapochoka nikiwafikiria watendaji wa wilaya. Amini usiamini itokee Mhe Rais ahoji kuhusu Suala la Uchafu wa Stand ya Mbezi au aseme Stand ya daladala mbezi imeshazidiwa uwezo, kwa kauli hiyo tu utaona jinsi viongozi na watendaji wa wilaya watakavyoanza kukimbizana na suala litapatiwa ufumbuzi faster tu.

Hii inamaanisha kwamba viongozi wengi na watendaji ngazi za kati na chini Serikalini hasa Mikoa na Wilaya sio wawajibikaji kabisa, Kiongozi mzuri ni yule anayewajibika pasipo kutishiwa au kusukumwa au kuhojiwa na Mkubwa wake.

Binafisi natamani sana Mheshimiwa Rais awaondoe hawa watu. Hivi kweli suala la uchafu wa Stand ni mpaka Mheshimiwa Rais au Waziri Mkuu alitolee tamko!!

hivi kweli suala la Machinga kurudi Stand nyakati za jioni na usiku ni hadi wakuu wa Kitaifa watoe maelekezo kwa viongozi wa Wilaya.

Hivi Kweli Kuzidiwa kwa Stand ya daladala mbezi mwisho ni hadi viongozi wa Kitaifa waumize vichwa wakati kuna viongozi na watendaji wa Wilaya na Mkoa.

Unapokuwa kiongozi wa ofisini ni dhahiri kuna mengi hutayapata. Viongozi wilayani na mkoa wakiwa ni watu wakutoka wangekuwa wanapata mengi sana . Pia wangepata maoni ya wadau/wananchi namna ya kutatua au kupunguza baadhi ya changamoto.

Mfano, iwapo kungejengwa Stand ndogo upande wa juu yaani pale njia ya Goba kungepunguza msongamano kwenye Stand ya Sasa ya daladala kwani abiria wa msakuzi, msumi na wale wanaopanda gari za kwenda Mwenge na Tegeta kupitia Goba wangepandia hapo.

Mhe. Rais wangu Mpendwa na Mhe. Waziri Mkuu tunaomba kukiwa na mabadiliko ya wakurugenzi , watendaji na wakuu wa wilaya muikumbuke na wilaya ya Ubungo.

Stendi ya Daladala Mbezi Mwisho ni mali ya TANROADS na hao TANROADS ndiyo wanaokusanya ushuru, kusimamia usafi na pia kile choo ni cha kwao. Na pia ndiyo wameruhusu biashara pale.

Ubungo Manispaa haihusiki na hiyo stendi
 
Jana nilifuatilia mjadala ulioanzishwa na JF kuhusu maoni ya sisi Wananchi wa kawaida kwenda kwa viongozi wetu hasa Wabunge, kwanza niwapaongeze sana kwa hicho walichokifanya na ninawashauri wakiendeleza kwa kuwa kero zipo nyingi.

Binafsi naamini wanasiasa ni watu wanaofuata upepo, kuna muda wanaweza kuliona jambo fulani la muhimu na wao watakiwa kulifanyia kazi, lakini kama halina mafufaa kwao au kama haliigiwi kelele wanaweza kuliacha kama lilivyo.

So, nilipoona JF wameanzisha kitu kama hiki inamaanisha kuwa ni kama tutakuwa tunawapigia kelele wakumbuke wajibu wao.

Povu langu mimi pia limfikie Mbunge wetu anayesimamia Jimbo la Ubungo ikiwezekana na viongozi wote ambao watakuwa wanahusika.

Suala la uchafu kwenye kituo cha Daladala cha Mbezi Mwisho kwa kweli ni kero na inatia kinyaa, hivi wao kwa kuwa wanatumia magari ya Serikali na hawaingii pale kituoni ndio maana wanatuchukulia poa ehh?

Kuna siku nimekuta mwanaume kasimama anakojoa katikati ya magari, na hakuna anayejali, harufu za mikojo zimesambaa, kibaya zaidi maeneo hayo ndipo ambapo kuna Watanzania wenzetu wanapanga bidhaa zao kuuza.

Hii ni hatari kwa afya, niwaambie wakati wanapambana kuwaondoa Wamachinga wajue na kufanya usafi au walizingatie hilo, kadiri siku zinavyoenda ndivyo uchafu unavyozidi kuongezeka.


Unataka Mbunge ashike Fagioa akafagie? Nchi imejaa waswahili, unategemea nini? Yaani watu Istarabu ni zero then utake Mbunge akafagie
 
UBUNGO hakuna MBUNGE kuna Mjumbe wa Ccm jimbo la Ubungo Stendi imegeuka ya kawaida sana Vibanda vya Machinga vimezaliwa ndani ya stendi kwenye Corridor za Abiria kusubiria Safari
Muulize Mkuu wa nchi ndio anaruhusu hayo, na pia je Watanzania wana ustarabu linapo kuja swala la usafi?
 
Back
Top Bottom