Stendi ya mabasi ya mikoani Ubungo kuhamishwa kupisha kituo cha mabasi ya Mwendo Kasi

Stendi ya mabasi ya mikoani Ubungo kuhamishwa kupisha kituo cha mabasi ya Mwendo Kasi

Hivi wakati wanajenga ile ofisi pale jangwani kipindi chote cha ujenzi haijawahi kunyesha mvua wakaona mafuriko au ndio akili za wasomi ziliganda kama uji wa cement [emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]

Maana unaweza kufikiri wakati wooote wa ujenzi wa zile ofisi na yard basi hapakuwahi kunyesha mvua zikafurisha eneo.

Watanzania ni viumbe wazito sana sijui tu. Hata na UDART wenyewe wamerudi kwenye ticket za vishina .

Saa nyingine unaamua kusahau kila kitu ila kuna kodi nilikatwa kwenye pato langu imechezewa pale ndio maana akili yangu haikubali kusahau kabisa. [emoji25][emoji25][emoji25][emoji25][emoji25][emoji25][emoji25][emoji25]
Kiburi tu
 
Nafikiri magari ya kwenda Kaskazini kituo kipelekwe kule Tegeta dawasco na mikoa ya kanda ya ziwa na magharibi kipelekwe Kibaha. Then magari ya kusini yabakie Temeke
Tegeta dawasco bado ni mjini pale, yapelekwe huko Bunju kabisa ikiwezekana. Dar inakua kwa kasi, juzi juzi tu ubungo ilikuwaga nje ya mji leo hapatoshi hata kusogeza mguu.
 
Dar ni kubwa sana stand kuhamia Mbezi Louis ni mbali mno.
Mbezi louis ni karibu sana, labda unakaa Mbande au Kimbiji wewe. Kutoka city center, mbezi bado mi karibu sana. Mji wa Dar umekua sana.
 
Kama picha za uwanja wa timu ile ya jangwani tulivyoonyeshwa kipindi kile.
UWANJA WA SIMBA.jpg


huu wa Boko sio
 
Mbezi louis ni karibu sana, labda unakaa Mbande au Kimbiji wewe. Kutoka city center, mbezi bado mi karibu sana. Mji wa Dar umekua sana.
Unatumia mfano wa City center ndio unasema karibu.
Mbona huzungumzii mtu wa Gongo la mboto, Temeke, Chanika.

Hili jambo liangaliwe tena tusije kujilaumu tena baadae.

Hii stand bora waigawe, nyingine iwe kule Temeke(nadhani hii ipo tayari) kwa magari yaendayo mikoa ya Mtwara na Lindi.

Nyingine iwe Tegeta kwa magari yaendayo Tanga, KLM, Arusha, Manyara via Moshi.

Halafu hii ndio wailete Mbezi Louis.

Lakini bado kutakuwa na adha pia ya mtu anayeishi mbezi(Goba) akitaka kusafiri kwenda Mtwara na pia anayeishi Chanika akitaka kusafiri kuelekea mikoa mingine ambapo inabidi akapande gari Mbezi Louis.
 
Wizara ya maji (wakati wa bajeti yake mwaka huu) wametenga fedha, nafikiri kwa msaada wa Korea Kusini, kujenga mtambo wa kusafisha maji hapo Jangwani. Nini uhusiano wa haya yanayosemwa sasa na hayo ya Wizara ya maji. Ikiwa hayahusiani je hatuoni kama wizara ya maji inaenda tena kupoteza fedha zetu kwa kuwekeza sehemu ambayo haifai?
 
Hivi wakati wanajenga ile ofisi pale jangwani kipindi chote cha ujenzi haijawahi kunyesha mvua wakaona mafuriko au ndio akili za wasomi ziliganda kama uji wa cement [emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]

Maana unaweza kufikiri wakati wooote wa ujenzi wa zile ofisi na yard basi hapakuwahi kunyesha mvua zikafurisha eneo.

Watanzania ni viumbe wazito sana sijui tu. Hata na UDART wenyewe wamerudi kwenye ticket za vishina .

Saa nyingine unaamua kusahau kila kitu ila kuna kodi nilikatwa kwenye pato langu imechezewa pale ndio maana akili yangu haikubali kusahau kabisa. [emoji25][emoji25][emoji25][emoji25][emoji25][emoji25][emoji25][emoji25]
Hawa wasomi wetu ndio chanzo cha matatizo kwa asilimia kubwa.
 
Unatumia mfano wa City center ndio unasema karibu.
Mbona huzungumzii mtu wa Gongo la mboto, Temeke, Chanika.

Hili jambo liangaliwe tena tusije kujilaumu tena baadae.

Hii stand bora waigawe, nyingine iwe kule Temeke(nadhani hii ipo tayari) kwa magari yaendayo mikoa ya Mtwara na Lindi.

Nyingine iwe Tegeta kwa magari yaendayo Tanga, KLM, Arusha, Manyara via Moshi.

Halafu hii ndio wailete Mbezi Louis.

Lakini bado kutakuwa na adha pia ya mtu anayeishi mbezi(Goba) akitaka kusafiri kwenda Mtwara na pia anayeishi Chanika akitaka kusafiri kuelekea mikoa mingine ambapo inabidi akapande gari Mbezi Louis.
Wazo zuri,
Ila hamna namna, tutaifuata tu. Hata ilipotoka Kisutu kwenda ubungo tulisema ni mbali.
 
Kusema ukweli mbezi luis ni mbali sana... labda me ningeshauri tu kwamba kila kampuni ya basi ijenge kituo chake kama walivofanya Dar lux au kilimanjaro express. Hii pia itaondoa wapiga debe.
 
Hata kushuhudia wenyewe walishuhudia nini kuambiwa Mkuu. Ni makusudi yao tu ili kutengeneza mrija wakupiga pesa tu
Hili linadhihirisha kuwa waliopewa nguvu ya kufanya maamuzi kwa ajili ya wengine hawafai na hawana weledi na kazi. Haiwezekani mtu msomi kabisa, anajiita mhandisi, amekaa kwenye jopo la washauri anasema jangwani ijengwe karakana ya magari. He must've been very insane.

Natamani sana kufahamu nani hasa alitoa hiyo proposal, nitamdharau kuanzia siku hiyo.
 
Tegeta dawasco bado ni mjini pale, yapelekwe huko Bunju kabisa ikiwezekana. Dar inakua kwa kasi, juzi juzi tu ubungo ilikuwaga nje ya mji leo hapatoshi hata kusogeza mguu.
Hivi, what's the point kupeleka stand nje ya mji? Hata hatuwezi kujifunza kwa walioendelea?

Tunadhani solutions ni kutoa stand Ubungo kupeleka nje ya mji but that's not, solution ni kutengeneza miundombinu inayokidhi, hata stand ingekuwa Kisutu, kama miundombinu ya barabara ipo vizuri hizo foleni tutazisikia tu.

Tuendelee tu kuhamisha stand, mwisho zitakuwa Chalinze.
 
Kwa nini hao mwendo kasi wasipelekwe huko Mbezi! Wabongo bwana ni shida, yote hii ni kumuongezea shida mlalahoi, nitoke Kigoma, nilale Morogoro, nifike Mbezi nianze safari nyingine ya kwenda Mbagala viongozi hamlioni hili?
 
Walitumia akili gani kuhamisha watu jangwani ?

Baada ya watu kuhama nao wakajenga hapo hapo walipohimsha wananchi
 
Wanataka kuongeza foleni tu ya wasafiri kwenda Mbezi na kutoka Mbezi kwenda mjini. Kwenda Ubungo tunatumia njia 2 lkn huo msongamano wa alfajiri ni hatari, unaweza kuchelewa basi ukiwa kwenye mataa ya Morogoro
/Sam Nujoma Rd maana unaweza kuchukua nusu saa nzima kuingia terminal. Sasa huko Mbezi ambapo tunatumia barabara moja ndio itakuwa balaa !

Vv
 
CCM ilikuwaje mkaruhusu Mwendokasi wajenge kwenye mkondo wa maji? je ni kwamba hamkufanya uchambuzi yakinifu kabla ya kuanza kwa ujenzi?
Bàadae pale Jangwani mtapatumia kufanya nini? au mnapageuza kuwa danguro ?
 
Back
Top Bottom