Stendi ya mabasi ya mikoani Ubungo kuhamishwa kupisha kituo cha mabasi ya Mwendo Kasi

Stendi ya mabasi ya mikoani Ubungo kuhamishwa kupisha kituo cha mabasi ya Mwendo Kasi

stand ya ubungo ina ekari ngapi hadi hiyo ya mbezi kuwa ekari 24?? kwa Tz ya sasa ekari 24 hazitoshi maana kila. cku hali inabadilika na watu wanaongezeka wangetenga hata ekari 100 baadae zingepata matumizi maana sio. kila cku kulipa fidia tuu
 
Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ipo kwenye majadiliano ya kuhamisha kituo cha Mabasi Yaendayo Haraka (UDART), kilichopo Jangwani na kukipeleka kwenye kituo cha Mabasi yaendayo Mikoani Ubungo (UBT).

Hatua hiyo inatokana na eneo hilo la Jangwani kukumbwa na mafuriko ya mara kwa mara hali inayosababisha kuharibika kwa magari hayo.

Akizungumza kwenye kikao cha kawaida cha madiwani jana, Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita, alisema uamuzi huo umefikiwa ili kunusuru magari hayo yasiendelee kuharibika.

Alisema Menejimenti ya Kampuni ya UDART na viongozi wa jiji wapo kwenye majadiliano kuhusu suala hilo ili waweze kufikia mwafaka.

“Kwa sasa tupo kwenye majadiliano kwa ajili ya kuhamisha kituo cha mabasi yaendayo kasi(UDART) cha Jangwani tuweze kukipeleka Ubungo kwa sababu eneo la Jangwani limekuwa likikumbwa na mafuriko ya mara kwa mara mvua inaponyesha,”alisema Mwita.

Alisema suala hilo linaendelea kufanyiwa kazi na Halmashauri ya Jiji hilo ipo kwenye mchakato wa kupanua Mto Msimbazi uweze kuwa na nafasi kubwa ya kusafirisha maji hadi baharini.

Meya alisema jambo hilo linaweza kupunguza mafuriko katika eneo la Jangwani na maeneo karibu na mto huo.

Alisema fedha za upanuzi huo zimekwisha kutolewa, kilichobaki ni utekelezaji wa mradi kuanzia daraja la Salendar hadi Pugu.

“Awamu ya kwanza ya mradi itaanzia Salendar hadi Kigogo, jambo ambalo linaweza kupunguza ukubwa wa tatizo la mafuriko kwa wakazi wa Jangwani na maeneo jirani ya mto Msimbazi,” alisema.

Vilevile, Meya Mwita alisema Serikali Kuu imetoa shilingi bilioni 50 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha kisasa çha mabasi yaendayo mikoani, kitakachojengwa Mbezi Mwisho.

Alisema licha ya kutolewa kiasi hicho cha fedha, jiji limetoa shilingi bilioni nane kwa ajili ya kuwalipa fidia wananchi ambao maeneo yao yatachukuliwa kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo.

“Tunatarajia kupata ekari 24 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha kisasa cha Mbezi Mwisho, ujenzi ambao utaanza wakati wowote kuanzia sasa. Mkakati uliopo ni kuwalipa fidia wananchi wa eneo lile tuweze kuendeleza mradi,” alisema.

Alisema mradi huo utachukua miaka miwili kukamilika na ndani yake kutakua na maduka na nyumba za kulala wageni, jambo ambalo linaweza kuwasaidia kuongeza mapato.

Alisema mwaka huu katika makusanyo yake ya kila mwaka, halmashauri imeingiza shilingi bilioni 22 ambazo zitatumika kwa mambo mbalimbali yakiwamo uendelezaji wa miradi.

Chanzo: Swahili Times
========

Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam ipo kwenye majadiliano ya kuhamisha kituo cha mabasi yaendayo haraka (UDART), kilichopo Jangwani na kupeleka kwenye kituo cha mabasi ya mikoani Ubungo UBT, kutokana na eneo hilo la Jangwani kujaa maji kila mara wakati mvua zinaponyesha.

Picha ya chini ni mchoro wa kituo kipya cha mabasi ya mikoani kitakachojengwa Mbezi Luois jijini Dar es salaam.View attachment 771061View attachment 771062
 
Hakuna mahali nilipotetea ila nimeunga mkono stend kutolewa pale magar yangeendelea kuharibika hata tukipiga kelele sioni serikali ya ccm ikichukua hatua
Kusema ni "mipango ya Mungu" ni utetezi
 
Kufuatia ujenzi wa kituao hicho cha kisasa ktk eneo la mbezi mwisho ni

fursa kwa maeneo ya mbezi, kibamba, kiluvya nk, hoteli za kisasa zitahitajika, mall, Viwanja vya burudani n.k .
Wawekezaji changamkieni fursa hiyo,kwani stendi hiyo sio tu itahudumia mabasi ya mikoani bali pia mataifa mbalimbali.
Pongezi serikali ya mkoa
 
Hivi wakati wanajenga ile ofisi pale jangwani kipindi chote cha ujenzi haijawahi kunyesha mvua wakaona mafuriko au ndio akili za wasomi ziliganda kama uji wa cement [emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]

Maana unaweza kufikiri wakati wooote wa ujenzi wa zile ofisi na yard basi hapakuwahi kunyesha mvua zikafurisha eneo.

Watanzania ni viumbe wazito sana sijui tu. Hata na UDART wenyewe wamerudi kwenye ticket za vishina .

Saa nyingine unaamua kusahau kila kitu ila kuna kodi nilikatwa kwenye pato langu imechezewa pale ndio maana akili yangu haikubali kusahau kabisa. [emoji25][emoji25][emoji25][emoji25][emoji25][emoji25][emoji25][emoji25]
Wazo la kuhamisha Stand y'a mabasi toka Ubungo kwenda Mbezi Luis ni jema n'a kina faida nyingi, ikiwemo kupunguza msongamano/foleni kubwa hasa saa za asubuhi n'a jioni. Ushauri wangu Eneo la ujenzi wa kituo jipya mbezi Luis uzingatie mradi wa upanuzi wa barabara y'a Morogoro rd kwenda njia sita.
 
Mwanadamu sio Mungu ni jambo jema kuhamishia kituo cha mwendokasi ubungo ili stendi ya ubungo iende mbezi luis
WEWE WACHA KUTETEA UFUJAJI WA PESA. MIJI MIKONGWE KAMA LONDON KUNA VICTORIA STATION IMESIMULIWA KTK MAVITABU NA MAIGIZO HAIJAWAHI KUHAMISHWA SABABU YA KUWA KATIKATI YA JIJI HILO. IKO ZAIDI YA MIAKA 100. MWANZO ILIPOKUWA KISUTU ENEO LIKAWA DOGO NA KUHAMISHIA UBUNGO NDIO SAWA. sasa kuhamisha kwa sababu imekuwa katikakati ya jiji si sawa kwa vile baada ya jiji kufika kibaha hapi mbezi itakUWA KATIKATI YA JIJI TENA. TUFIKIRIE ZAIDI. MNAONA RAHISI KUCHUKUA PESA NA KUZITUMIA BILA UCHUNGU. WAULIZE WA LONDONI WAMEFANYAJE NA MJICWAO UNA WAKAZI MILLIONI 20. ENEO LA UBUNGO LINATOSHA KWA MAGARI YOTE YA UDART NA MIKOANI KWA MIAKA ZAIDI YA 100 IJAYO. NI AFADHALI KUNUNUA ENEO LINALOZUNGUKA STENDI MAANA HAKUNA HATA MGOROFA MENGI MUONGEZEE ENEO. HIYO FLYOVER ITASAIDIA MAGARI KUINGIA NA KUTOKA NA STENDI TAYARI IPI KUBWA YA UDART
 
Wataalam round ya kwanza hawakuliona hili!?.. Mbona tunachezea sana hela.
Wote wale waliofanya upembuzi yakinifu kuhusu huo mradi wajibu hizi tuhuma za uzembe uliokithiri na wafunguliwe jarada huko TAKUKURU kwa matumizi mabaya ya fedha za Umma.
 
Umeniacha hoiii!!!!

London haina watu milioni 20 mkuu!!! Yaani wasema theluthi wa idadi ya watu UK wanaishi London?

Hayo mengine nakubaliana nayo!


WEWE WACHA KUTETEA UFUJAJI WA PESA. MIJI MIKONGWE KAMA LONDON KUNA VICTORIA STATION IMESIMULIWA KTK MAVITABU NA MAIGIZO HAIJAWAHI KUHAMISHWA SABABU YA KUWA KATIKATI YA JIJI HILO. IKO ZAIDI YA MIAKA 100. MWANZO ILIPOKUWA KISUTU ENEO LIKAWA DOGO NA KUHAMISHIA UBUNGO NDIO SAWA. sasa kuhamisha kwa sababu imekuwa katikakati ya jiji si sawa kwa vile baada ya jiji kufika kibaha hapi mbezi itakUWA KATIKATI YA JIJI TENA. TUFIKIRIE ZAIDI. MNAONA RAHISI KUCHUKUA PESA NA KUZITUMIA BILA UCHUNGU. WAULIZE WA LONDONI WAMEFANYAJE NA MJICWAO UNA WAKAZI MILLIONI 20. ENEO LA UBUNGO LINATOSHA KWA MAGARI YOTE YA UDART NA MIKOANI KWA MIAKA ZAIDI YA 100 IJAYO. NI AFADHALI KUNUNUA ENEO LINALOZUNGUKA STENDI MAANA HAKUNA HATA MGOROFA MENGI MUONGEZEE ENEO. HIYO FLYOVER ITASAIDIA MAGARI KUINGIA NA KUTOKA NA STENDI TAYARI IPI KUBWA YA UDART
 
Serikali imewavunjia nyumba waliojenga mabondeni na kila siku wanawa lalamikia waliojenga mabondeni.
Halafu serikali hiyohiyo imeruhusu ujenzi wa karakana kuu ya mradi wake wa mabasi ya mwendo kasi hapohapo bondeni na kusababisha hasara ya mabilioni na imeamua kuicha hiyo karakana kuu iliyojengwa kwa mabilioni na kuhamia ubungo naitatumia mabilioni mengine kuirakabati iwe ya kisasa kukidhi vigezo
 
Siku ya uzinduzi wa ujenzi wa Kituo hicho cha Jangwani yeye JPM akiwa waziri mwenye dhamana na JK walikuwepo pale wote.Badala ya kushughulika na mandari ya mkondo wa maji kilikokuwa kinajengwa kituo, Wao walihangaika kumtumbua aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa DART wakati ule Bwana Cosmas Peter Takule.Kumbe hakuna mapana yasiyokuwa na ncha,Leo tunajionea madhara yenyewe.
Hata hivyo lini ulimsikia JPM akiongelea swala la Mwendokasi ?Mwenye nayo UDART mwamjua?Si yule aliyenunua UDA ?Tena ana kashfa za kuuza majineri huko Mwanza na Geita ? Na mwekezaji mwenza si yule alimkingia kifua kwa dhamana za serikali(Treasury Bills) kupata mkopo NMB kununulia mabasi ?Kama vile hamuoni kuna ukimya fulani umetawala mahali fulani....Fungukeni mpaze sauti huduma hii ni mkanganyiko wa kufa mtu mwanzo mwisho,Nasema tena haiwezi kutengemaa hadi Yesu arudi....
 
Tokea mwanzo humu humu Jf watu walisema jangwani hapafai
Ki ukweli wataalamu watanzania akili za zinawatosha wenyewe na familia zao......harafu VODA wakileta CEO kutoka nje mnapiga keleleleee!!!!!
 
Enviromental Impact Assessment vs Political WILL
 
Hawa watu siku zote hawafikiri vizuri na hawajawahi kujali maslahi ya watu. Hivi Ubungo terminal inatakiwa kubaki hapo ilipo ili kunusuru biashara na uwekezaji waliofanya watu au kama itawalipa fidia wenye hotel, guest na biashara.
Mwendo kasi ndio uende mbezi huko ndio watu wanauhitaji zaidi kuliko jangwani.
Mbezi mshavunjia watu hizo fidia watamlipa nani sasa
 
Tanzania haiwezi kubadilika hata siku moja. Hatufanyi kitu kuangalia mbele, kila mtu anafanya kitu kwa kuangalia muda akiwa ofisini, pale jangwani watu waliondolewa kupisha mkondo wa bahari, iweje tena serikali nao wakajenga? Leo tena wahamie Ubungo kwahiyo ile gharama iliyotumika Jangwani itatumika tena Ubungo. Teh teh sijawahi kuona hawa wasomi wetu
 
Unaweza kujenga kitu sehemu sahihi lakin natural calamities huwez kuzikwepa kama ikitokea zikaja tofaut hata huko ma mbele wanahangaika na haya majanga
Pale waliubana mto what will be happen
 
WEWE WACHA KUTETEA UFUJAJI WA PESA. MIJI MIKONGWE KAMA LONDON KUNA VICTORIA STATION IMESIMULIWA KTK MAVITABU NA MAIGIZO HAIJAWAHI KUHAMISHWA SABABU YA KUWA KATIKATI YA JIJI HILO. IKO ZAIDI YA MIAKA 100. MWANZO ILIPOKUWA KISUTU ENEO LIKAWA DOGO NA KUHAMISHIA UBUNGO NDIO SAWA. sasa kuhamisha kwa sababu imekuwa katikakati ya jiji si sawa kwa vile baada ya jiji kufika kibaha hapi mbezi itakUWA KATIKATI YA JIJI TENA. TUFIKIRIE ZAIDI. MNAONA RAHISI KUCHUKUA PESA NA KUZITUMIA BILA UCHUNGU. WAULIZE WA LONDONI WAMEFANYAJE NA MJICWAO UNA WAKAZI MILLIONI 20. ENEO LA UBUNGO LINATOSHA KWA MAGARI YOTE YA UDART NA MIKOANI KWA MIAKA ZAIDI YA 100 IJAYO. NI AFADHALI KUNUNUA ENEO LINALOZUNGUKA STENDI MAANA HAKUNA HATA MGOROFA MENGI MUONGEZEE ENEO. HIYO FLYOVER ITASAIDIA MAGARI KUINGIA NA KUTOKA NA STENDI TAYARI IPI KUBWA YA UDART

Tena UDART yenyewe imeshaanza kupooza mara magari yameharibika mengi. Mara wanaburuzana mahakamani. Siombei mabaya katikati ya mazuri tuliyotegemea but hawa UDART wanatoa huduma zilizofubaa, huduma zimezeeka na kutia kichefuchefu. Yale magari ile milango yake siku siyo nyingi wataajiri makonda wa kufunga na kufungua.

Wakazi wa Mbezi/kimara wameshapata adhabu ya kutosha kabisa kabla hata hayo magari hayajaoga mafuriko ilikuwa shida na utumbo mtupu.
 
Back
Top Bottom