Stephen Hawking's Final Book Says There's 'No Possibility' of God in Our Universe

Stephen Hawking's Final Book Says There's 'No Possibility' of God in Our Universe

"'(hivi hii inaingia akilini kweli? Unajua kabisa kuwa hii nyumba nayo jenga kesho itaungua moto halafu unaweka wanao wakae humo mpaka mwakani '" Mantiki ya ujuzi wake wa yote -upendo kwa wote iko wapi hapo. ...?"

Tukijaribu kutoa mifano sie mnasema tunalinganisha Mungu na hivyo vitu ila nyie mkitoa mifano ndio sahihi,sasa wewe hapo ulikuwa unamlinganisha Mungu na nani?wakati mwengine huwa mnafurahisha tu.
Kwanza hawa wanafahamu maana ya vifungu hivi:-MUWEZA WA YOTE NA MWENYE UPENDO KWA WOTE?.

Hivi maneno hayo yana limitation?.
 
Kuamini unaruhusiwa kuamini chochote, hilo si jambo la kuvutia mjadala.

Unaruhusiwa na katiba ya Tanzania na Universal Declaration of Human Rights kuamini unachotaka, mradi usiingilie wengine wala kuvunja sheria.

Sasa hata sielewi kwa nini unaleta habari za kuamini hapa.

Mimi najadili habari za fact. Unaweza kuthibitisha kwa fact Mungu yupo?

Na unaelewa kwamba unaposema anayesema hakuna Mungu ni mpumbavu, hilo nalo linathibitisha kwamba Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo?

Kwa sababu.

1. Mungu mwenye uwezo wote ujuzi wote na upendo wote ana uwezo wa kuumba ulimwengu ambao hauna upumbavu.
2. Mungu huyo, kwa sifa zake, angekuwa na sababu zote za kuumba ulimwengu ambao hauna upumbavu na kutoumba ulimwengu ambao una upumbavu.
3. Mimi nimesema Mungu hayupo
4. Kama kusema Mungu hayupo ni upumbavu, na mimi nimesema hivyo, ulimwengu huu una upumbavu.
5. Tumeona kwamba Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote asingeumba ulimwengu ambao nunaweza kuwa na upumbavu.
6. Zaidi, Mungu huyo asingeruhusu upumbavu uwepo popote.
7. Upumbavu upo.
8. Hivyo, Mungu huyo hayupo.
Kwani huo UPUMBAFU ni nje ya YOTE?.
 
Kila mtu yuko free kuamini anachoamini. Unaweza kuamini sukari ni chumvi na chumvi ni sukari. Unaweza kuamini nyekundu ni nyeusi na nyeusi ni nyekundu. Lakini unapashwa kujua kwamba kuamini kwako hivyo hakubadilishi maana wala uhalisia. Sukari itabaki sukari na nyeusi itabaki nyeusi.

Unaposema unataka facts za uwepo wa Mungu nikakuambia uumbaji ni fact mojawapo mbona unakataa? Unataka facts zipi labda za kisayansi, za laboratory? Hizo facts sina na sidhani kama unaweza fanya experiment ya kisayansi kutambua uwepo wa MUNGU.

Hapo no 3 unasema hakuna Mungu kwa namna ipi? Una aamini au una uhakika?

Mungu hajaumba upumbavu. Nafikiri unaelewa maana ya upumbavu au mpumbavu. Halafu no 7& 8 sijaelewa uwepo wa upumbavu unathibitisha vipi Mungu hayupo? Sijaona logic wala connection hapo.
Huyo mnadekeza tu,ni mweupe kabisaa.Ebu mwambie athibishe kama UPUMBAFU ni nje ya YOTE?.Maana,Mungu ni muweza wa YOTE.Kwa nini wapumbafu anawatoa katika YOTE?.
 
Point ni kwamba, mtu yeyote anaweza kuandika kitabu, akamuahadithia character ambaye hayupo, akamuita Mungu, akasema huyu yupo, kaumba dunia, ana nguvu zisizo mwisho, ujuzi usio mwisho na upendo usio mwisho nk.

Kuandika huko tu, hakumfanyi huyo character wa kitabu awepo.

Unaweza kuthibitisha huyo Mungu yupo kweli na si hadithi za vitabuni tu?
Si kweli,maana character ni muwakilishi wa aliyepo,yaliyopo,kilichopo.
 
Thibitisha Mungu yupo kwa njia 8nayoweza kuhakikiwa na kuonesha yupo na ambayo haina contradi tion.

Kwa mfano. Umisema "Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote yupo, kwa sababu yeye ndiye kaumba ulimwengu huu" unatakiwa.

1. Uthibitishe ulimwengu umeumbwa na Mungu na haujatokea kwa namna nyingine yoyote.
2. Uondoe contradiction ya problem of evil inayoleta swali la, kama Mungu yupo, ni mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wotw, kwa nini kaumba ulimwengu ambao mabaya yanaweza kutokea, wakati alikuwa na uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezi kutokea?
Hayo unayosema mabaya, ni nje ya UJUZI WOTE?.
Fungu hili (UJUZI WOTE) Lina limitation?.
 
Umesahau kumtaja Prof. John Lennox mtaalamu wa hesabu toka Oxford University. Very smart. Anaamini uwepo wa Mungu.

Sijui kwann wakina Kiranga wanashindwa kutupa comments za hawa wanasanyansi pia wamekomaa na Hawkins tuu
Prof John Lennox akiacha kuamini Mungu utakubali Mungu hayupo?

Yani Mungu wako hawezi kusimama mwenyewe, kusimama mpaka apate muhuri wa Prof. John Lennox?

Unaamini Mungu yupo kwa imani yako mwenyewe au kwa sababu Prof John Lennox kasema?

Akitokea Prof mkali kushinda John Lennox anasema Mungu hayupo, utaacha kuamini Mungu?
 
Napita kuangalia kama kuna mtu kathibitisha Mungu yupo tu.

Naona bado.

Mtu akiweza kuthibitisha Mungu yupo naomba nistue.
We mwenyewe umeisha thibitisha uwepo wake.Kwani umewezaje kumuita MUNGU?.
 
Mkuu mtu anayepinga uwepo wa mungu ana haki ya kutumia mifano hii kwasababu wanatoa mapungufu yake, kitu ambacho kipo duniani. Lakini kwa wewe unayemuamini huyo mungu huwezi kumlinganisha na vitu vilivyokuwa na mapungufu kwasababu unaamini mungu ni mkamilifu na mjuzi wa kila kitu na hivyo basi kufanya hivyo ni kumshushia thamani huyo mungu wako ambaye ni nyali na mjuvi wa mambo yote..
Ebu eleza maana ya maneno haya:-MJUZI WA YOTE.

Alafu niambie kama MABAYA/MAOVU ni nje ya YOTE.
 
Utakapojiongeza kidogo kwa kutumia akili na utashi wako bila kutumia maandiko ya watu wowote... including waumini wa dini mbalimbali au wapinga dini utajua ukweli na utakuwa huru

Atakuambia thibitisha kuwa Mungu yupo acha longolongo.

Ukimuambia nithibitishe kwa njia gani (maana watu wameshatoa uthibitisho) hatakuambia njia anazotaka umthibitishe huyo Mungu, au labda anataka njia za kisayansi labda umchukue Mungu umuweke kwenye bunsen burner baadaye umweke kwenye test tubes na conical flasks umchanganye na sulphuric acid kisha ikitokea rangi flani ndio akubali Mungu yupo[emoji23][emoji38][emoji38]. Sasa kwa mindset hiyo hapa hata mjadiliane vipi hamtafikia mwisho, mtakesha.

Kimsingi hawezi kukubali uthibitisho wowote atakaopewa kuhusu uwepo wa Mungu which in turns inapelekea akatae na kupinga jibu lolote atakalopewa.

Anyaways, since we are God's creation, He has put his signature in our hearts and souls na mwisho wa yote hata upingeje, bado dhamiri ndani yako inakuambia kwamba God is there.

We have an opinion to deny and reject his existence but that wont change anything bse He surely exists.
 
Atakuambia thibitisha kuwa Mungu yupo acha longolongo.

Ukimuambia nithibitishe kwa njia gani (maana watu wameshatoa uthibitisho) hatakuambia njia anazotaka umthibitishe huyo Mungu, au labda anataka njia za kisayansi labda umchukue Mungu umuweke kwenye bunsen burner baadaye umweke kwenye test tubes na conical flasks umchanganye na sulphuric acid kisha ikitokea rangi flani ndio akubali Mungu yupo[emoji23][emoji38][emoji38]. Sasa kwa mindset hiyo hapa hata mjadiliane vipi hamtafikia mwisho, mtakesha.

Kimsingi hawezi kukubali uthibitisho wowote atakaopewa kuhusu uwepo wa Mungu which in turns inapelekea akatae na kupinga jibu lolote atakalopewa.

Anyaways, since we are God's creation, He has put his signature in our hearts and souls na mwisho wa yote hata upingeje, bado dhamiri ndani yako inakuambia kwamba God is there.

We have an opinion to deny and reject his existence but that wont change anything bse He surely exists.

Kwangu nilishasema nataka uthibitisho wa Mungu uliojikamilisha kwa logical consistency na usio na contradiction.

Unaweza kutoa uthibitisho huo wa Mungu kuwepo?
 
Hujathibitisha Mungu yupo.

Hujajibu swali langu.

Kama Mungu yupo, ni mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, kwa nini hakuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani, na kaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana?

Mnasema Mungu anajua yote, ina maana kabla hajamjaribu mtu anajua uwezo wa mtu, kwamba huyu atafeli hapa na huyu atapasi.

Sasa kama anajua tayari, anatujaribisha ili iweje?

Thibitisha Mungu yupo na si hadithi tu. Ondoa contradiction ya problem ya evil. Niambie Mungu anajitekenya mwenyewe na kucheka mwenyewe kwa kutujaribisha wakati anajua majibu tayari kwa sababu gani?
Mwenyezi Mungu ni muweza wa YOTE.

Je! Mabaya ni nje ya YOTE?.
 
Naona flat earthers mnaninukuu, lakini sioni mnachoandika kwa sababu nilishawaweka kwenye ignore list.

Nawakumbusha tu mpo katika ignore list kama nilivyowaambia.

Sina muda wa kujadiliana na flat earthers.
 
Ndugu Kiranga, sio kwamba hauna hoja, unayo. Mimi naelewa hasa kinachokutatiza.
Kuna masuala kadhaa usiyo yaelewa bado. Kuna elimu hizi: saikolojia, falsafa na teolojia bado huzielewi na kwa sababu hiyo huelewi pia sayansi. Ni kutoelewa, kwasababu unawezaje kukataa wewe siyo uthibitisho wa kuwepo Mungu lakini ukakubali hadumi inathibisha uwepo wa vimelea au viumbe vingine tusivyoviona kwa macho?
Bado ni tatizo hilohilo la kutoelewa, kama sayansi inathibisha kwamba DNA hutawala maisha ya mtu daima, lakini ukakataa dini inaposema roho ndiyo hutawala maisha ya mtu. Hii ni kwa sababu huelewi kipi unakiegemea na kukifuata na kipi inakithibitisha.
Madai yako yote yanaonyesha kwamba bado hujaelewa Mungu ni nani na nini? Uliza au jielimishe! Kwa sababu huelewi na humjui Mungu ndiyo maana unalalamika kwanini alishindwa kuumba ulimwengu usiyo na matatizo badala yake akaumba ulimwengu huu wenye matatizo na kila aina ya uovu; na hivyo unaelewa hakuna uthibitisho wa Mungu kwa sababu tu ya dunia ilivyo. Yaani hata dunia yenyewe ilivyo kando na matatizo yaliyomo, bado akili yako haitambui? Sasa kama jambo dogo kama hilo huelewi, utawezaje kujijua na kuelewe wewe mwenyewe? Na kama wewe mwenyewe hujijuwi na kujielewa, unawezaje kujua na kuelewa Mungu?
Huwezi kudai matatizo hayawezi kudhibitisha jambo jema. Yaani hivi: kwa vile kuna matatizo, basi hakuna mema. Kama unashindwa kuuthibisha ukweli kwenye matatizo huwezi kuona uzuri kwenye wema.
Unaposhindwa kuelewa zaidi ni pale unapofikiri Mungu ni contradiction lakini wewe ni facts and not contradiction! Wewe huoni kama ni fact ya Mungu, lakini unaona Mungu ni contradictions wakati huohuo wewe ni facts, lakini hujioni kama ni contradiction s!
Ndugu Kiranga uthibitisho wa Mungu uko ndani yako na siyo sehemu nyingine yeyote. Hiki kilichopo nje unachokiona ni uthibitisho ya kile kidogo kilichomo ndani yako. Kama hukioni hiki kidogo kilichopo nje maana yake hauna sayansi-hauna uthibitisho hivyo, unakataa hicho kilichomo ndani yako, ambacho kwa chenyewe, hiki kinachoonekana nje kinatokana na hicho kilichomo ndani yako, ndiyo Mungu.
Katika msingi huo, sayansi kwa maana nyingine ni uthibisho unaomthibisha Mungu, ambae yuko ndani yako anaejithibisha na kujidhihirisha kwa maarifa ya sayansi kadiri ya wakati.
Sasa unaposema unataka uthibitisho wa Mungu: sijui ni uthibitisho gani zaidi ya huu wa: wewe mwenyewe ndani yako, ndiyo roho, wewe mwenyewe kama umbo la kuonekana, ndiyo mwili; dunia na vitu vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyooneka, maarifa kama tulivyonayo, ndiyo sayansi, saikolojia, falsafa na teolojia?

Perfect [emoji1488]
 
Naona flat earthers mnaninukuu, lakini sioni mnachoandika kwa sababu nilishawaweka kwenye ignore list.

Nawakumbusha tu mpo katika ignore list kama nilivyowaambia.

Sina muda wa kujadiliana na flat earthers.
Mi mwenyewe naona kuna umuhimu wa kuwa block watu wa dzain hiyo
 
Back
Top Bottom